< Kutoka 29 >

1 “Hili ndilo utakalofanya ili kuwaweka wakfu makuhani ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani: Chukua fahali mchanga mmoja na kondoo dume wawili wasio na dosari.
Now this is what you must do to set them apart to me so that they may serve me as priests. Take one young bull and two rams without blemish,
2 Kutokana na unga laini wa ngano usiotiwa chachu, tengeneza mikate na maandazi yaliyokandwa kwa mafuta, pamoja na mikate midogo myembamba.
bread without yeast, and cakes without yeast mixed with oil. Also take wafers without yeast rubbed with oil. Make the wafers using fine wheat flour.
3 Viwekwe vyote ndani ya kikapu na kuvitoa pamoja na yule fahali na wale kondoo dume wawili.
You must put them into a single basket, bring them in the basket, and present them with the bull and the two rams.
4 Kisha mlete Aroni na wanawe kwenye lango la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
You must present Aaron and his sons at the entrance to the tent of meeting. You must wash Aaron and his sons in water.
5 Chukua yale mavazi na umvike Aroni koti, joho la kisibau na kisibau chenyewe pamoja na kile kifuko cha kifuani. Mfungie hicho kisibau kwa ule mshipi wa kiunoni uliosukwa kwa ustadi.
You must take the garments and clothe Aaron with the coat, the robe of the ephod, the ephod, and the breastpiece, fastening the finely-woven waistband of the ephod around him.
6 Weka kilemba kichwani mwake na kuweka taji takatifu ishikamane na hicho kilemba.
You must set the turban on his head and put the holy crown on the turban.
7 Chukua yale mafuta ya upako umimine juu ya kichwa chake.
Then take the anointing oil and pour it on his head, and in this way anoint him.
8 Walete wanawe na uwavike makoti,
You must bring his sons and put coats on them.
9 pia uwavike zile tepe za kichwani. Ndipo uwafunge Aroni na wanawe mishipi. Ukuhani ni wao kwa agizo la kudumu. Kwa njia hii utamweka wakfu Aroni na wanawe.
You must clothe Aaron and his sons with sashes and put headbands on them. The work of the priesthood will belong to them by permanent law. In this way you must consecrate Aaron and his sons for them to serve me.
10 “Mlete yule fahali mbele ya Hema la Kukutania, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
You must all bring the bull before the tent of meeting, and Aaron and his sons must lay their hands on its head.
11 Mchinje huyo fahali mbele za Bwana kwenye mlango wa Hema la Kukutania.
You must kill the bull before Yahweh at the entrance to the tent of meeting.
12 Chukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuipaka kwenye pembe za hayo madhabahu kwa kidole chako, na damu iliyobaki uimwage sehemu ya chini ya madhabahu.
You must take some of the bull's blood and put it on the horns of the altar with your finger, and you must pour out the rest of the blood at the base of the altar.
13 Kisha chukua mafuta yote ya huyo mnyama ya sehemu za ndani, yale yanayofunika ini, figo zote mbili pamoja na mafuta yake, uviteketeze juu ya madhabahu.
You must take all the fat that covers the inner parts, and also take the covering of the liver and the two kidneys with the fat that is on them; burn it all on the altar.
14 Lakini nyama ya huyo fahali na ngozi yake na matumbo yake utavichoma nje ya kambi. Hii ni sadaka ya dhambi.
But as for the bull's flesh, as well as its skin and dung, you must burn it up outside the camp. It will be a sin offering.
15 “Chukua mmoja wa wale kondoo dume, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
You must also take the one ram, and Aaron and his sons must lay their hands on its head.
16 Mchinje huyo kondoo dume, chukua damu yake na uinyunyize pande zote za hayo madhabahu.
You must kill the ram, then take its blood and sprinkle it on all sides of the altar.
17 Mkate huyo kondoo dume vipande vipande na usafishe sehemu za ndani pamoja na miguu, ukiviweka pamoja na kichwa na vipande vingine.
You must cut the ram into pieces and wash its inner parts and its legs, and you must put the inner parts, together with its pieces and with its head,
18 Kisha mteketeze huyo kondoo dume mzima juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
on the altar. Then burn the whole ram. It will be a burnt offering to Yahweh, a sweet aroma, an offering made to Yahweh by fire.
19 “Mchukue yule kondoo dume mwingine, naye Aroni na wanawe waweke mikono yao juu ya kichwa chake.
You must then take the other ram, and Aaron and his sons must lay their hands on its head.
20 Mchinje, uchukue sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye masikio ya Aroni na wanawe, kwenye vidole gumba vya mikono yao ya kuume, pia kwenye vidole gumba vya miguu yao ya kuume. Kisha nyunyiza hiyo damu pande zote za madhabahu.
Then you must kill the ram and take some of its blood. Put it on the tip of Aaron's right ear, and on the tip of his sons' right ears, on the thumb of their right hands, and on the great toe of their right feet. Then you must sprinkle the blood against the altar on every side.
21 Pia chukua sehemu ya damu iliyo juu ya madhabahu na sehemu ya mafuta ya upako, umnyunyizie Aroni na mavazi yake, pia wanawe na mavazi yao. Ndipo Aroni na wanawe pamoja na mavazi yao watakuwa wamewekwa wakfu.
You must take some of the blood that is on the altar and some of the anointing oil, and sprinkle it all on Aaron and on his garments, and also on his sons and on their garments. Aaron will then be set apart for me, as well as his garments, his sons and his sons' garments with him.
22 “Chukua mafuta ya huyu kondoo dume, mafuta ya mkia, mafuta ya sehemu za ndani yale yanayofunika ini, figo zote mbili na mafuta yake, pamoja na paja la kulia. (Huyo ndiye kondoo dume kwa ajili ya kuwaweka wakfu.)
You must take the ram's fat, the fat tail, the fat that covers the inner parts, the covering of the liver, the two kidneys and the fat on them, and the right thigh—for this ram is for the priests' consecration to me.
23 Kutoka kwenye kile kikapu chenye mikate iliyotengenezwa bila chachu, kilichoko mbele za Bwana, chukua mkate, andazi lililokandwa kwa mafuta na mkate mdogo mwembamba.
Take one loaf of bread, one cake of bread made with oil, and one wafer out of the basket of bread without yeast that is before Yahweh.
24 Viweke vitu hivi vyote mikononi mwa Aroni na wanawe na uviinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
You must put these in Aaron's hands and in the hands of his sons and wave them before me for a wave offering before Yahweh.
25 Kisha vichukue vitu hivyo kutoka mikononi mwao, uviteketeze juu ya madhabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kupendeza kwa Bwana, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
You must then take the food from their hands and burn it on the altar with the burnt offering. It will produce a sweet aroma for me; it will be an offering made to me by fire.
26 Baada ya kuchukua kidari cha huyo kondoo dume wa kuwekwa wakfu kwa Aroni, kiinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, nayo itakuwa fungu lako.
You must take the breast of Aaron's ram of dedication and wave it for a wave offering before Yahweh, and it will be your share.
27 “Weka wakfu zile sehemu za kondoo dume aliyetumika kwa kumweka wakfu Aroni na wanawe: kidari kile kilichoinuliwa na lile paja lililotolewa.
You must set apart to me the breast of the wave offering that is waved, and the thigh that is the contribution for the priests—both the breast that was waved and the thigh that was contributed for Aaron and his sons.
28 Siku zote hili litakuwa fungu la kawaida kutoka kwa Waisraeli kwa ajili ya Aroni na wanawe. Hili ni toleo la Waisraeli watakalotoa kwa Bwana kutoka sadaka zao za amani.
This will be a perpetual ordinance for Aaron and his sons. It will be a contribution from the people of Israel to give to Yahweh from their peace offerings.
29 “Mavazi matakatifu ya Aroni yatakuwa ya wazao wake ili kwamba waweze kutiwa mafuta na kuwekwa wakfu wakiwa wameyavaa.
The holy garments of Aaron must also be reserved for his sons after him. They are to be anointed in them and ordained to me in them.
30 Mwana atakayeingia mahali pake kuwa kuhani na kuja kwenye Hema la Kukutania kuhudumu katika Mahali Patakatifu atayavaa kwa siku saba.
The priest who succeeds him from among his sons, who comes into the tent of meeting to serve me in the holy place, is to wear those garments for seven days.
31 “Chukua nyama ya huyo kondoo dume wa kuwaweka wakfu uipike katika Mahali Patakatifu.
You must take the ram for the installation of the priests to me and boil its meat in a holy place.
32 Aroni na wanawe wataila ile nyama ya huyo kondoo dume pamoja na ile mikate iliyo kwenye hicho kikapu wakiwa hapo ingilio la Hema la Kukutania.
Aaron and his sons must eat the ram's meat and the bread that is in the basket at the entrance to the tent of meeting.
33 Watakula sadaka hizi ambazo upatanisho ulifanywa kwazo kwa ajili ya kuwaweka wakfu na kuwatakasa. Lakini hakuna mtu mwingine yeyote anayeruhusiwa kuvila, kwa sababu ni vitakatifu.
They must eat the meat and bread that were given to atone for them and to ordain them, to be set apart to me. No one else may eat that food, because they must treat it as consecrated to me, reserved for me.
34 Ikiwa nyama yoyote ya huyo kondoo dume iliyotumika kwa kuwaweka wakfu au mkate wowote umebaki mpaka asubuhi, vichomwe. Kamwe visiliwe, kwa sababu ni vitakatifu.
If any of the meat of the ordination offering, or any of the bread, remains to the next morning, then you must burn it. It must not be eaten because it has been set apart to me.
35 “Hivyo utamfanyia Aroni na wanawe kila kitu kama vile nilivyokuamuru: Utachukua muda wa siku saba kuwaweka wakfu.
In this way, by following all that I have commanded you to do, you must treat Aaron and his sons. For seven days you must prepare them.
36 Utatoa dhabihu ya fahali kila siku kuwa sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho. Takasa madhabahu kwa kufanya upatanisho kwa ajili yake, nayo uitie mafuta na kuiweka wakfu.
Every day you must offer a bull as a sin offering for atonement. You must purify the altar by making atonement for it, and you must anoint it in order to set it apart to me.
37 Kwa muda wa siku saba fanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuiweka wakfu. Ndipo madhabahu itakuwa takatifu sana na chochote kitakachoigusa kitakuwa kitakatifu.
For seven days you must make atonement for the altar and set it apart it to Yahweh. Then the altar will be completely set apart to me. Whatever touches the altar will be set apart to Yahweh.
38 “Kwa kawaida hiki ndicho utakachotoa juu ya madhabahu kila siku: wana-kondoo wawili wenye umri wa mwaka mmoja.
You must regularly offer on the altar every day two lambs a year old.
39 Utamtoa mmoja asubuhi na huyo mwingine jioni.
One lamb you must offer in the morning, and the other lamb you must offer about sundown.
40 Pamoja na mwana-kondoo wa kwanza utatoa efa moja ya unga wa ngano laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta yaliyokamuliwa, pamoja na robo ya hini ya divai kuwa sadaka ya kinywaji.
With the first lamb, offer a tenth of an ephah of fine flour mixed with the fourth part of a hin of oil from pressed olives, and the fourth part of a hin of wine as a drink offering.
41 Huyo mwana-kondoo mwingine mtoe dhabihu wakati wa machweo pamoja na sadaka za unga na za kinywaji kama vile ulivyofanya asubuhi, kuwa harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
You must offer the second lamb about sunset. You must offer the same grain offering as in the morning, and the same drink offering. These will produce a sweet aroma for me; it will be an offering made to me by fire.
42 “Kwa vizazi vijavyo itakuwa kawaida kutoa sadaka hii ya kuteketezwa kila mara kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Hapo ndipo nitakapokutana na ninyi na kusema nanyi,
These must be regular burnt offerings throughout your generations, at the entrance to the tent of meeting before Yahweh, where I will meet with you to speak to you there.
43 Huko ndipo nitakapokutana na Waisraeli, nalo Hema la Kukutania litatakaswa na utukufu wangu.
That is where I will meet with the Israelites; the tent will be set apart for me by my glory.
44 “Kwa hiyo nitaliweka wakfu Hema la Kukutania pamoja na madhabahu, nami nitamweka wakfu Aroni na wanawe ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani.
I will set apart the tent of meeting and the altar for these to belong to me alone. I will also set apart Aaron and his sons to serve me as priests.
45 Ndipo nitakapofanya makao miongoni mwa Waisraeli na kuwa Mungu wao.
I will live among the Israelites and will be their God.
46 Nao watajua kuwa Mimi Ndimi Bwana Mungu wao, aliyewatoa Misri ili nipate kufanya makao miongoni mwao. Mimi Ndimi Bwana Mungu wao.
They will know that I am Yahweh, their God, who brought them out from the land of Egypt so that I might live among them. I am Yahweh, their God.

< Kutoka 29 >