< Kutoka 29 >

1 “Hili ndilo utakalofanya ili kuwaweka wakfu makuhani ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani: Chukua fahali mchanga mmoja na kondoo dume wawili wasio na dosari.
And this [is] the thing which you will do to them to consecrate them to serve as priests me take a young bull one a son of [the] herd and rams two unblemished.
2 Kutokana na unga laini wa ngano usiotiwa chachu, tengeneza mikate na maandazi yaliyokandwa kwa mafuta, pamoja na mikate midogo myembamba.
And bread of unleavened bread and cakes of unleavened bread mixed with oil and wafers of unleavened bread smeared with oil fine flour of wheat you will make them.
3 Viwekwe vyote ndani ya kikapu na kuvitoa pamoja na yule fahali na wale kondoo dume wawili.
And you will put them on a basket one and you will bring near them in the basket and the young bull and [the] two the rams.
4 Kisha mlete Aroni na wanawe kwenye lango la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
And Aaron and sons his you will bring near to [the] entrance of [the] tent of meeting and you will wash them with water.
5 Chukua yale mavazi na umvike Aroni koti, joho la kisibau na kisibau chenyewe pamoja na kile kifuko cha kifuani. Mfungie hicho kisibau kwa ule mshipi wa kiunoni uliosukwa kwa ustadi.
And you will take the garments and you will clothe Aaron the tunic and [the] robe of the ephod and the ephod and the breastpiece and you will gird [the] ephod to him with [the] girdle of the ephod.
6 Weka kilemba kichwani mwake na kuweka taji takatifu ishikamane na hicho kilemba.
And you will put the turban on head his and you will put [the] crown of holiness on the turban.
7 Chukua yale mafuta ya upako umimine juu ya kichwa chake.
And you will take [the] oil of anointing and you will pour [it] on head his and you will anoint him.
8 Walete wanawe na uwavike makoti,
And sons his you will bring near and you will clothe them tunics.
9 pia uwavike zile tepe za kichwani. Ndipo uwafunge Aroni na wanawe mishipi. Ukuhani ni wao kwa agizo la kudumu. Kwa njia hii utamweka wakfu Aroni na wanawe.
And you will gird them a sash Aaron and sons his and you will bind on to them headdresses and it will be[long] to them priesthood to a statute of perpetuity and you will fill [the] hand of Aaron and [the] hand of sons his.
10 “Mlete yule fahali mbele ya Hema la Kukutania, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
And you will bring near the young bull before [the] tent of meeting and he will lay Aaron and sons his hands their on [the] head of the young bull.
11 Mchinje huyo fahali mbele za Bwana kwenye mlango wa Hema la Kukutania.
And you will slaughter the young bull before Yahweh [the] entrance of [the] tent of meeting.
12 Chukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuipaka kwenye pembe za hayo madhabahu kwa kidole chako, na damu iliyobaki uimwage sehemu ya chini ya madhabahu.
And you will take some of [the] blood of the young bull and you will put [it] on [the] horns of the altar with finger your and all the blood you will pour out to [the] base of the altar.
13 Kisha chukua mafuta yote ya huyo mnyama ya sehemu za ndani, yale yanayofunika ini, figo zote mbili pamoja na mafuta yake, uviteketeze juu ya madhabahu.
And you will take all the fat which covers the entrails and the lobe on the liver and [the] two the kidneys and the fat which [is] on them and you will make [them] smoke the altar towards.
14 Lakini nyama ya huyo fahali na ngozi yake na matumbo yake utavichoma nje ya kambi. Hii ni sadaka ya dhambi.
And [the] flesh of the young bull and hide its and offal its you will burn with fire from [the] outside of the camp [is] a sin offering it.
15 “Chukua mmoja wa wale kondoo dume, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
And the ram one you will take and they will lay Aaron and sons his hands their on [the] head of the ram.
16 Mchinje huyo kondoo dume, chukua damu yake na uinyunyize pande zote za hayo madhabahu.
And you will slaughter the ram and you will take blood its and you will sprinkle [it] on the altar all around.
17 Mkate huyo kondoo dume vipande vipande na usafishe sehemu za ndani pamoja na miguu, ukiviweka pamoja na kichwa na vipande vingine.
And the ram you will cut in pieces into pieces its and you will wash entrails its and legs its and you will put [them] with pieces its and with head its.
18 Kisha mteketeze huyo kondoo dume mzima juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
And you will make smoke all the ram the altar towards [is] a burnt offering it to Yahweh [is] an odor of soothing a fire offering to Yahweh it.
19 “Mchukue yule kondoo dume mwingine, naye Aroni na wanawe waweke mikono yao juu ya kichwa chake.
And you will take the ram second and he will lay Aaron and sons his hands their on [the] head of the ram.
20 Mchinje, uchukue sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye masikio ya Aroni na wanawe, kwenye vidole gumba vya mikono yao ya kuume, pia kwenye vidole gumba vya miguu yao ya kuume. Kisha nyunyiza hiyo damu pande zote za madhabahu.
And you will slaughter the ram and you will take some of blood its and you will put [it] on [the] lobe of [the] ear of Aaron and on [the] lobe of [the] ear of sons his right and on [the] thumb of hand their right and on [the] big toe of foot their right and you will sprinkle the blood on the altar all around.
21 Pia chukua sehemu ya damu iliyo juu ya madhabahu na sehemu ya mafuta ya upako, umnyunyizie Aroni na mavazi yake, pia wanawe na mavazi yao. Ndipo Aroni na wanawe pamoja na mavazi yao watakuwa wamewekwa wakfu.
And you will take some of the blood which [is] on the altar and some of [the] oil of anointing and you will spatter [it] on Aaron and on garments his and on sons his and on [the] garments of sons his with him and he will be holy he and garments his and sons his and [the] garments of sons his with him.
22 “Chukua mafuta ya huyu kondoo dume, mafuta ya mkia, mafuta ya sehemu za ndani yale yanayofunika ini, figo zote mbili na mafuta yake, pamoja na paja la kulia. (Huyo ndiye kondoo dume kwa ajili ya kuwaweka wakfu.)
And you will take from the ram the fat and the fat tail and the fat - which covers the entrails and [the] lobe of the liver and - [the] two the kidneys and the fat which [is] on them and [the] thigh of the right for [is] a ram of installation offering it.
23 Kutoka kwenye kile kikapu chenye mikate iliyotengenezwa bila chachu, kilichoko mbele za Bwana, chukua mkate, andazi lililokandwa kwa mafuta na mkate mdogo mwembamba.
And a round loaf of bread one and a cake of bread of oil one and a wafer one from [the] basket of the unleavened bread which [will be] before Yahweh.
24 Viweke vitu hivi vyote mikononi mwa Aroni na wanawe na uviinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
And you will put everything on [the] hands of Aaron and on [the] hands of sons his and you will wave them a wave-offering before Yahweh.
25 Kisha vichukue vitu hivyo kutoka mikononi mwao, uviteketeze juu ya madhabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kupendeza kwa Bwana, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
And you will take them from hand their and you will make [them] smoke the altar towards on the burnt offering to an odor of soothing before Yahweh [is] a fire offering it to Yahweh.
26 Baada ya kuchukua kidari cha huyo kondoo dume wa kuwekwa wakfu kwa Aroni, kiinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, nayo itakuwa fungu lako.
And you will take the breast from [the] ram of installation offering which [belongs] to Aaron and you will wave it a wave-offering before Yahweh and it will be[long] to you to a portion.
27 “Weka wakfu zile sehemu za kondoo dume aliyetumika kwa kumweka wakfu Aroni na wanawe: kidari kile kilichoinuliwa na lile paja lililotolewa.
And you will consecrate - [the] breast of the wave-offering and [the] thigh of the contribution which it was waved and which it was raised from [the] ram of installation offering from [that] which [belongs] to Aaron from [that] which [belongs] to sons his.
28 Siku zote hili litakuwa fungu la kawaida kutoka kwa Waisraeli kwa ajili ya Aroni na wanawe. Hili ni toleo la Waisraeli watakalotoa kwa Bwana kutoka sadaka zao za amani.
And it will belong to Aaron and to sons his to a prescribed portion of perpetuity from with [the] people of Israel for [is] a contribution it and a contribution it will be from with [the] people of Israel from [the] sacrifices of peace offerings their contribution their to Yahweh.
29 “Mavazi matakatifu ya Aroni yatakuwa ya wazao wake ili kwamba waweze kutiwa mafuta na kuwekwa wakfu wakiwa wameyavaa.
And [the] garments of holiness which [belong] to Aaron they will belong to sons his after him for anointing in them and to fill in them hand their.
30 Mwana atakayeingia mahali pake kuwa kuhani na kuja kwenye Hema la Kukutania kuhudumu katika Mahali Patakatifu atayavaa kwa siku saba.
Seven days he will wear them the priest in place of him one of sons his who he will come into [the] tent of meeting to serve in the holy place.
31 “Chukua nyama ya huyo kondoo dume wa kuwaweka wakfu uipike katika Mahali Patakatifu.
And [the] ram of installation offering you will take and you will boil meat its in a place holy.
32 Aroni na wanawe wataila ile nyama ya huyo kondoo dume pamoja na ile mikate iliyo kwenye hicho kikapu wakiwa hapo ingilio la Hema la Kukutania.
And he will eat Aaron and sons his [the] meat of the ram and the bread which [is] in the basket [the] entrance of [the] tent of meeting.
33 Watakula sadaka hizi ambazo upatanisho ulifanywa kwazo kwa ajili ya kuwaweka wakfu na kuwatakasa. Lakini hakuna mtu mwingine yeyote anayeruhusiwa kuvila, kwa sababu ni vitakatifu.
And they will eat them which it was atoned by them to fill hand their to consecrate them and a stranger not he will eat [them] for [are] a holy thing they.
34 Ikiwa nyama yoyote ya huyo kondoo dume iliyotumika kwa kuwaweka wakfu au mkate wowote umebaki mpaka asubuhi, vichomwe. Kamwe visiliwe, kwa sababu ni vitakatifu.
And if it will be left over some of [the] meat of installation offering and some of the bread until the morning and you will burn what is left over with fire not it will be eaten for [is] a holy thing it.
35 “Hivyo utamfanyia Aroni na wanawe kila kitu kama vile nilivyokuamuru: Utachukua muda wa siku saba kuwaweka wakfu.
And you will do to Aaron and to sons his thus according to all that I have commanded you seven days you will fill hand their.
36 Utatoa dhabihu ya fahali kila siku kuwa sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho. Takasa madhabahu kwa kufanya upatanisho kwa ajili yake, nayo uitie mafuta na kuiweka wakfu.
And a young bull of a sin offering you will offer to the day on atonement and you will make a sin offering on the altar when making atonement you on it and you will anoint it to consecrate it.
37 Kwa muda wa siku saba fanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuiweka wakfu. Ndipo madhabahu itakuwa takatifu sana na chochote kitakachoigusa kitakuwa kitakatifu.
Seven days you will make atonement on the altar and you will consecrate it and it will be the altar holiness of holiness every [thing which] touches the altar it will be holy.
38 “Kwa kawaida hiki ndicho utakachotoa juu ya madhabahu kila siku: wana-kondoo wawili wenye umri wa mwaka mmoja.
And this [is that] which you will offer on the altar lambs sons of a year two to the day continually.
39 Utamtoa mmoja asubuhi na huyo mwingine jioni.
The lamb one you will offer in the morning and the lamb second you will offer between the evenings.
40 Pamoja na mwana-kondoo wa kwanza utatoa efa moja ya unga wa ngano laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta yaliyokamuliwa, pamoja na robo ya hini ya divai kuwa sadaka ya kinywaji.
And a tenth of fine flour mixed with oil pressed fourth part of hin and a drink offering fourth of hin wine for the lamb one.
41 Huyo mwana-kondoo mwingine mtoe dhabihu wakati wa machweo pamoja na sadaka za unga na za kinywaji kama vile ulivyofanya asubuhi, kuwa harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
And the lamb second you will offer between the evenings like [the] grain offering of the morning and like drink offering its you will offer it to an odor of soothing a fire offering to Yahweh.
42 “Kwa vizazi vijavyo itakuwa kawaida kutoa sadaka hii ya kuteketezwa kila mara kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Hapo ndipo nitakapokutana na ninyi na kusema nanyi,
A burnt offering of continuity to generations your [the] entrance of [the] tent of meeting before Yahweh where I will meet you there to speak to you there.
43 Huko ndipo nitakapokutana na Waisraeli, nalo Hema la Kukutania litatakaswa na utukufu wangu.
And I will meet there [the] people of Israel and it will be shown as holy by glory my.
44 “Kwa hiyo nitaliweka wakfu Hema la Kukutania pamoja na madhabahu, nami nitamweka wakfu Aroni na wanawe ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani.
And I will consecrate [the] tent of meeting and the altar and Aaron and sons his I will consecrate to serve as priests me.
45 Ndipo nitakapofanya makao miongoni mwa Waisraeli na kuwa Mungu wao.
And I will dwell in among [the] people of Israel and I will become for them God.
46 Nao watajua kuwa Mimi Ndimi Bwana Mungu wao, aliyewatoa Misri ili nipate kufanya makao miongoni mwao. Mimi Ndimi Bwana Mungu wao.
And they will know that I [am] Yahweh God their who I brought out them from [the] land of Egypt to dwell I in midst of them I [am] Yahweh God their.

< Kutoka 29 >