< Kutoka 29 >
1 “Hili ndilo utakalofanya ili kuwaweka wakfu makuhani ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani: Chukua fahali mchanga mmoja na kondoo dume wawili wasio na dosari.
“And this [is] the thing which you do to them, to hallow them, for being priests to Me: take one bullock, a son of the herd, and two rams, perfect ones,
2 Kutokana na unga laini wa ngano usiotiwa chachu, tengeneza mikate na maandazi yaliyokandwa kwa mafuta, pamoja na mikate midogo myembamba.
and unleavened bread, and unleavened cakes anointed with oil; you make them of fine wheat flour,
3 Viwekwe vyote ndani ya kikapu na kuvitoa pamoja na yule fahali na wale kondoo dume wawili.
and you have put them on one basket, and have brought them near in the basket, also the bullock and the two rams.
4 Kisha mlete Aroni na wanawe kwenye lango la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
And you bring Aaron and his sons near to the opening of the Tent of Meeting, and have bathed them with water;
5 Chukua yale mavazi na umvike Aroni koti, joho la kisibau na kisibau chenyewe pamoja na kile kifuko cha kifuani. Mfungie hicho kisibau kwa ule mshipi wa kiunoni uliosukwa kwa ustadi.
and you have taken the garments, and have clothed Aaron with the coat, and the upper robe of the ephod, and the ephod, and the breastplate, and have girded him with the girdle of the ephod,
6 Weka kilemba kichwani mwake na kuweka taji takatifu ishikamane na hicho kilemba.
and have set the turban on his head, and have put the holy crown on the turban,
7 Chukua yale mafuta ya upako umimine juu ya kichwa chake.
and have taken the anointing oil, and have poured [it] on his head, and have anointed him.
8 Walete wanawe na uwavike makoti,
And you bring his sons near, and have clothed them [with] coats,
9 pia uwavike zile tepe za kichwani. Ndipo uwafunge Aroni na wanawe mishipi. Ukuhani ni wao kwa agizo la kudumu. Kwa njia hii utamweka wakfu Aroni na wanawe.
and have girded them [with] a girdle (Aaron and his sons), and have bound caps on them; and the priesthood has been theirs by a continuous statute, and you have consecrated the hand of Aaron, and the hand of his sons,
10 “Mlete yule fahali mbele ya Hema la Kukutania, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
and have brought the bullock near before the Tent of Meeting, and Aaron has laid—his sons also—their hands on the head of the bullock.
11 Mchinje huyo fahali mbele za Bwana kwenye mlango wa Hema la Kukutania.
And you have slaughtered the bullock before YHWH, at the opening of the Tent of Meeting,
12 Chukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuipaka kwenye pembe za hayo madhabahu kwa kidole chako, na damu iliyobaki uimwage sehemu ya chini ya madhabahu.
and have taken of the blood of the bullock, and have put [it] on the horns of the altar with your finger, and you pour out all the blood at the foundation of the altar;
13 Kisha chukua mafuta yote ya huyo mnyama ya sehemu za ndani, yale yanayofunika ini, figo zote mbili pamoja na mafuta yake, uviteketeze juu ya madhabahu.
and you have taken all the fat which is covering the innards, and the redundance on the liver, and the two kidneys, and the fat which [is] on them, and have made incense on the altar;
14 Lakini nyama ya huyo fahali na ngozi yake na matumbo yake utavichoma nje ya kambi. Hii ni sadaka ya dhambi.
and the flesh of the bullock, and his skin, and his dung, you burn with fire at the outside of the camp; it [is] a sin-offering.
15 “Chukua mmoja wa wale kondoo dume, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
And you take the first ram, and Aaron and his sons have laid their hands on the head of the ram,
16 Mchinje huyo kondoo dume, chukua damu yake na uinyunyize pande zote za hayo madhabahu.
and you have slaughtered the ram, and have taken its blood, and have sprinkled [it] around the altar,
17 Mkate huyo kondoo dume vipande vipande na usafishe sehemu za ndani pamoja na miguu, ukiviweka pamoja na kichwa na vipande vingine.
and you cut the ram into its pieces, and have washed its innards, and its legs, and have put [them] on its pieces, and on its head;
18 Kisha mteketeze huyo kondoo dume mzima juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
and you have made incense with the whole ram on the altar. It [is] a burnt-offering to YHWH, a refreshing fragrance; it [is] a fire-offering to YHWH.
19 “Mchukue yule kondoo dume mwingine, naye Aroni na wanawe waweke mikono yao juu ya kichwa chake.
And you have taken the second ram, and Aaron has laid—his sons also—their hands on the head of the ram,
20 Mchinje, uchukue sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye masikio ya Aroni na wanawe, kwenye vidole gumba vya mikono yao ya kuume, pia kwenye vidole gumba vya miguu yao ya kuume. Kisha nyunyiza hiyo damu pande zote za madhabahu.
and you have slaughtered the ram, and have taken of its blood, and have put [it] on the tip of the right ear of Aaron, and on the tip of the right ear of his sons, and on the thumb of their right hand, and on the great toe of their right foot, and have sprinkled the blood around the altar;
21 Pia chukua sehemu ya damu iliyo juu ya madhabahu na sehemu ya mafuta ya upako, umnyunyizie Aroni na mavazi yake, pia wanawe na mavazi yao. Ndipo Aroni na wanawe pamoja na mavazi yao watakuwa wamewekwa wakfu.
and you have taken of the blood which [is] on the altar, and of the anointing oil, and have sprinkled [it] on Aaron, and on his garments, and on his sons, and on the garments of his sons with him, and he has been hallowed, he and his garments, and his sons, and the garments of his sons with him.
22 “Chukua mafuta ya huyu kondoo dume, mafuta ya mkia, mafuta ya sehemu za ndani yale yanayofunika ini, figo zote mbili na mafuta yake, pamoja na paja la kulia. (Huyo ndiye kondoo dume kwa ajili ya kuwaweka wakfu.)
And you have taken from the ram the fat, and the fat tail, and the fat which is covering the innards, and the redundance on the liver, and the two kidneys, and the fat which [is] on them, and the right leg, for it [is] a ram of consecration,
23 Kutoka kwenye kile kikapu chenye mikate iliyotengenezwa bila chachu, kilichoko mbele za Bwana, chukua mkate, andazi lililokandwa kwa mafuta na mkate mdogo mwembamba.
and one round cake of bread, and one cake of oiled bread, and one thin cake out of the basket of the unleavened things which [is] before YHWH;
24 Viweke vitu hivi vyote mikononi mwa Aroni na wanawe na uviinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
and you have set the whole on the hands of Aaron, and on the hands of his sons, and have waved them [for] a wave-offering before YHWH;
25 Kisha vichukue vitu hivyo kutoka mikononi mwao, uviteketeze juu ya madhabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kupendeza kwa Bwana, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
and you have taken them out of their hand, and have made incense on the altar beside the burnt-offering, for refreshing fragrance before YHWH; it [is] a fire-offering to YHWH.
26 Baada ya kuchukua kidari cha huyo kondoo dume wa kuwekwa wakfu kwa Aroni, kiinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, nayo itakuwa fungu lako.
And you have taken the breast from the ram of the consecration which [is] for Aaron, and have waved it [for] a wave-offering before YHWH, and it has become your portion;
27 “Weka wakfu zile sehemu za kondoo dume aliyetumika kwa kumweka wakfu Aroni na wanawe: kidari kile kilichoinuliwa na lile paja lililotolewa.
and you have sanctified the breast of the wave-offering, and the leg of the raised-offering, which has been waved, and which has been lifted up from the ram of the consecration, of that which [is] for Aaron, and of that which [is] for his sons;
28 Siku zote hili litakuwa fungu la kawaida kutoka kwa Waisraeli kwa ajili ya Aroni na wanawe. Hili ni toleo la Waisraeli watakalotoa kwa Bwana kutoka sadaka zao za amani.
and it has been for Aaron and for his sons, by a continuous statute from the sons of Israel, for it [is] a raised-offering; and it is a raised-offering from the sons of Israel, from the sacrifices of their peace-offerings—their raised-offering to YHWH.
29 “Mavazi matakatifu ya Aroni yatakuwa ya wazao wake ili kwamba waweze kutiwa mafuta na kuwekwa wakfu wakiwa wameyavaa.
And the holy garments which are Aaron’s are for his sons after him, to be anointed in them and to consecrate their hand in them;
30 Mwana atakayeingia mahali pake kuwa kuhani na kuja kwenye Hema la Kukutania kuhudumu katika Mahali Patakatifu atayavaa kwa siku saba.
[for] seven days the priest in his stead (of his sons) puts them on when he goes into the Tent of Meeting to minister in the holy place.
31 “Chukua nyama ya huyo kondoo dume wa kuwaweka wakfu uipike katika Mahali Patakatifu.
And you take the ram of the consecration and have boiled its flesh in the holy place;
32 Aroni na wanawe wataila ile nyama ya huyo kondoo dume pamoja na ile mikate iliyo kwenye hicho kikapu wakiwa hapo ingilio la Hema la Kukutania.
and Aaron has eaten—his sons also—the flesh of the ram, and the bread which [is] in the basket, at the opening of the Tent of Meeting;
33 Watakula sadaka hizi ambazo upatanisho ulifanywa kwazo kwa ajili ya kuwaweka wakfu na kuwatakasa. Lakini hakuna mtu mwingine yeyote anayeruhusiwa kuvila, kwa sababu ni vitakatifu.
and they have eaten those things by which there is atonement to consecrate their hand, to sanctify them; and a stranger does not eat [them], for they [are] holy;
34 Ikiwa nyama yoyote ya huyo kondoo dume iliyotumika kwa kuwaweka wakfu au mkate wowote umebaki mpaka asubuhi, vichomwe. Kamwe visiliwe, kwa sababu ni vitakatifu.
and if there is left of the flesh of the consecration or of the bread until the morning, then you have burned that which is left with fire; it is not eaten, for it [is] holy.
35 “Hivyo utamfanyia Aroni na wanawe kila kitu kama vile nilivyokuamuru: Utachukua muda wa siku saba kuwaweka wakfu.
And you have done thus to Aaron and to his sons, according to all that I have commanded you; [for] seven days you consecrate their hand;
36 Utatoa dhabihu ya fahali kila siku kuwa sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho. Takasa madhabahu kwa kufanya upatanisho kwa ajili yake, nayo uitie mafuta na kuiweka wakfu.
and a bullock, a sin-offering, you prepare daily for the atonements, and you have atoned for the altar in your making atonement on it, and have anointed it to sanctify it;
37 Kwa muda wa siku saba fanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuiweka wakfu. Ndipo madhabahu itakuwa takatifu sana na chochote kitakachoigusa kitakuwa kitakatifu.
[for] seven days you make atonement for the altar, and have sanctified it, and the altar has been most holy; all that is coming against the altar is holy.
38 “Kwa kawaida hiki ndicho utakachotoa juu ya madhabahu kila siku: wana-kondoo wawili wenye umri wa mwaka mmoja.
And this [is] that which you prepare on the altar: two lambs, sons of a year, daily continually;
39 Utamtoa mmoja asubuhi na huyo mwingine jioni.
you prepare the first lamb in the morning, and you prepare the second lamb between the evenings;
40 Pamoja na mwana-kondoo wa kwanza utatoa efa moja ya unga wa ngano laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta yaliyokamuliwa, pamoja na robo ya hini ya divai kuwa sadaka ya kinywaji.
and a tenth part of fine flour mixed with a fourth part of a hin of beaten oil, and a fourth part of a hin of wine [for] a drink-offering, [is] for the first lamb.
41 Huyo mwana-kondoo mwingine mtoe dhabihu wakati wa machweo pamoja na sadaka za unga na za kinywaji kama vile ulivyofanya asubuhi, kuwa harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
And you prepare the second lamb between the evenings; according to the present of the morning, and according to its drink-offering, you prepare for it, for refreshing fragrance, a fire-offering to YHWH—
42 “Kwa vizazi vijavyo itakuwa kawaida kutoa sadaka hii ya kuteketezwa kila mara kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Hapo ndipo nitakapokutana na ninyi na kusema nanyi,
a continual burnt-offering for your generations [at] the opening of the Tent of Meeting before YHWH, to where I meet with you to speak to you there,
43 Huko ndipo nitakapokutana na Waisraeli, nalo Hema la Kukutania litatakaswa na utukufu wangu.
and I have met with the sons of Israel there, and it has been sanctified by My glory.
44 “Kwa hiyo nitaliweka wakfu Hema la Kukutania pamoja na madhabahu, nami nitamweka wakfu Aroni na wanawe ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani.
And I have sanctified the Tent of Meeting and the altar, and I sanctify Aaron and his sons for being priests to Me,
45 Ndipo nitakapofanya makao miongoni mwa Waisraeli na kuwa Mungu wao.
and I have dwelt in the midst of the sons of Israel, and have become their God,
46 Nao watajua kuwa Mimi Ndimi Bwana Mungu wao, aliyewatoa Misri ili nipate kufanya makao miongoni mwao. Mimi Ndimi Bwana Mungu wao.
and they have known that I [am] their God YHWH, who has brought them out of the land of Egypt, that I may dwell in their midst; I [am] their God YHWH.”