< Kutoka 29 >
1 “Hili ndilo utakalofanya ili kuwaweka wakfu makuhani ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani: Chukua fahali mchanga mmoja na kondoo dume wawili wasio na dosari.
Now this is how you are to proceed to dedicate them to serve me as priests. Take a young bull and two rams with no defects.
2 Kutokana na unga laini wa ngano usiotiwa chachu, tengeneza mikate na maandazi yaliyokandwa kwa mafuta, pamoja na mikate midogo myembamba.
Then using the best wheat flour, make the following without yeast: bread, cakes mixed with olive oil, and wafers sprinkled with olive oil.
3 Viwekwe vyote ndani ya kikapu na kuvitoa pamoja na yule fahali na wale kondoo dume wawili.
Put them all in a basket, and bring them as an offering, along with the bull and the two rams.
4 Kisha mlete Aroni na wanawe kwenye lango la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
Then bring Aaron and his sons to the entrance of the Tent of Meeting, and wash them with water.
5 Chukua yale mavazi na umvike Aroni koti, joho la kisibau na kisibau chenyewe pamoja na kile kifuko cha kifuani. Mfungie hicho kisibau kwa ule mshipi wa kiunoni uliosukwa kwa ustadi.
Take the clothes and put them on Aaron: the tunic, the robe of the ephod, the ephod itself, and the breastpiece. Tie the ephod on him with its waistband.
6 Weka kilemba kichwani mwake na kuweka taji takatifu ishikamane na hicho kilemba.
Wrap the turban on his head and attach the holy crown to the turban.
7 Chukua yale mafuta ya upako umimine juu ya kichwa chake.
Then use the anointing oil to anoint him by pouring it over his head.
8 Walete wanawe na uwavike makoti,
Then have his sons come and put the tunics on them.
9 pia uwavike zile tepe za kichwani. Ndipo uwafunge Aroni na wanawe mishipi. Ukuhani ni wao kwa agizo la kudumu. Kwa njia hii utamweka wakfu Aroni na wanawe.
Tie the sashes around Aaron and his sons and put headdresses on them. The priesthood belongs to them forever. This is how you are to ordain Aaron and his sons.
10 “Mlete yule fahali mbele ya Hema la Kukutania, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
Take the bull to the front of the Tent of Meeting, and Aaron and his sons are to place their hands on its head.
11 Mchinje huyo fahali mbele za Bwana kwenye mlango wa Hema la Kukutania.
Then slaughter the bull in the Lord's presence at the entrance to the Tent of Meeting.
12 Chukua sehemu ya damu ya huyo fahali na kuipaka kwenye pembe za hayo madhabahu kwa kidole chako, na damu iliyobaki uimwage sehemu ya chini ya madhabahu.
Take some of the bull's blood and smear it on the horns of the altar with your finger. Then pour out the rest of the blood at the base of the altar.
13 Kisha chukua mafuta yote ya huyo mnyama ya sehemu za ndani, yale yanayofunika ini, figo zote mbili pamoja na mafuta yake, uviteketeze juu ya madhabahu.
Take all the fat that covers the intestines, the best parts of the liver, and the two kidneys with their fat, and burn them on the altar.
14 Lakini nyama ya huyo fahali na ngozi yake na matumbo yake utavichoma nje ya kambi. Hii ni sadaka ya dhambi.
But burn the bull's meat, its hide, and its excrement outside the camp—it is an offering for sin.
15 “Chukua mmoja wa wale kondoo dume, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake.
Next have Aaron and his sons place their hands on the head of one of the rams.
16 Mchinje huyo kondoo dume, chukua damu yake na uinyunyize pande zote za hayo madhabahu.
Slaughter the ram, take its blood, and splash it all around the altar.
17 Mkate huyo kondoo dume vipande vipande na usafishe sehemu za ndani pamoja na miguu, ukiviweka pamoja na kichwa na vipande vingine.
Cut the ram in pieces, wash the intestines and legs, and put them with the other pieces and the head.
18 Kisha mteketeze huyo kondoo dume mzima juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
Then burn all of the ram on the altar. It is a burnt offering to the Lord to be accepted by him.
19 “Mchukue yule kondoo dume mwingine, naye Aroni na wanawe waweke mikono yao juu ya kichwa chake.
Then have Aaron and his sons place their hands the head of the other ram.
20 Mchinje, uchukue sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye masikio ya Aroni na wanawe, kwenye vidole gumba vya mikono yao ya kuume, pia kwenye vidole gumba vya miguu yao ya kuume. Kisha nyunyiza hiyo damu pande zote za madhabahu.
Slaughter the ram, and put some of its blood on the right earlobes of Aaron and his sons, and on the thumbs of their right hands, and on the big toes of their right feet. Splash the rest of its blood all around the altar.
21 Pia chukua sehemu ya damu iliyo juu ya madhabahu na sehemu ya mafuta ya upako, umnyunyizie Aroni na mavazi yake, pia wanawe na mavazi yao. Ndipo Aroni na wanawe pamoja na mavazi yao watakuwa wamewekwa wakfu.
Take some of the blood from the altar and some of the anointing oil and sprinkle it on Aaron and his clothes, and on his sons and their clothes. Then he and his clothes will be made holy, likewise his sons and their clothes.
22 “Chukua mafuta ya huyu kondoo dume, mafuta ya mkia, mafuta ya sehemu za ndani yale yanayofunika ini, figo zote mbili na mafuta yake, pamoja na paja la kulia. (Huyo ndiye kondoo dume kwa ajili ya kuwaweka wakfu.)
Take the fat from the ram, including the fat of its broad tail, the fat covering the intestines, the best parts of the liver, the two kidneys with their fat, as well as the right thigh (because this is a ram for ordination).
23 Kutoka kwenye kile kikapu chenye mikate iliyotengenezwa bila chachu, kilichoko mbele za Bwana, chukua mkate, andazi lililokandwa kwa mafuta na mkate mdogo mwembamba.
Also take one loaf of bread, one cake of bread made with olive oil, and one wafer from the basket of bread made without yeast that is in the Lord's presence.
24 Viweke vitu hivi vyote mikononi mwa Aroni na wanawe na uviinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
Give all of them to Aaron and his sons to wave before the Lord as a wave offering.
25 Kisha vichukue vitu hivyo kutoka mikononi mwao, uviteketeze juu ya madhabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kupendeza kwa Bwana, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
Then take the different breads back and burn them on the altar on top of the burnt offering to the Lord to be accepted by him.
26 Baada ya kuchukua kidari cha huyo kondoo dume wa kuwekwa wakfu kwa Aroni, kiinue mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, nayo itakuwa fungu lako.
Take the breast of the ram of Aaron's ordination and wave it before the Lord as a wave offering. This is the part you can keep.
27 “Weka wakfu zile sehemu za kondoo dume aliyetumika kwa kumweka wakfu Aroni na wanawe: kidari kile kilichoinuliwa na lile paja lililotolewa.
Set apart for Aaron and his sons the breast of the wave offering and the thigh of the offering that is lifted up, both taken from the ram of ordination.
28 Siku zote hili litakuwa fungu la kawaida kutoka kwa Waisraeli kwa ajili ya Aroni na wanawe. Hili ni toleo la Waisraeli watakalotoa kwa Bwana kutoka sadaka zao za amani.
From now on whenever the Israelites lift up peace offerings to the Lord, these parts will belong to Aaron and his sons forever as a regular share from the Israelites.
29 “Mavazi matakatifu ya Aroni yatakuwa ya wazao wake ili kwamba waweze kutiwa mafuta na kuwekwa wakfu wakiwa wameyavaa.
The holy garments that Aaron has will be passed down to his descendants, so they can wear them when they're anointed and ordained.
30 Mwana atakayeingia mahali pake kuwa kuhani na kuja kwenye Hema la Kukutania kuhudumu katika Mahali Patakatifu atayavaa kwa siku saba.
The descendant who succeeds him as priest and enters the Tent of Meeting to serve in the Holy Place must wear them for the seven days of his ordination.
31 “Chukua nyama ya huyo kondoo dume wa kuwaweka wakfu uipike katika Mahali Patakatifu.
Take the ram of ordination and boil its meat in a holy place.
32 Aroni na wanawe wataila ile nyama ya huyo kondoo dume pamoja na ile mikate iliyo kwenye hicho kikapu wakiwa hapo ingilio la Hema la Kukutania.
Aaron and his sons are to eat the ram's meat, and the bread that is in the basket, at the entrance to the Tent of Meeting,
33 Watakula sadaka hizi ambazo upatanisho ulifanywa kwazo kwa ajili ya kuwaweka wakfu na kuwatakasa. Lakini hakuna mtu mwingine yeyote anayeruhusiwa kuvila, kwa sababu ni vitakatifu.
They are to eat the meat and the bread that were part of the offerings that symbolized the forgiveness required for their ordination and dedication. No one else may eat them, because they are holy.
34 Ikiwa nyama yoyote ya huyo kondoo dume iliyotumika kwa kuwaweka wakfu au mkate wowote umebaki mpaka asubuhi, vichomwe. Kamwe visiliwe, kwa sababu ni vitakatifu.
If any of the meat of ordination or any bread remains until the morning, burn what's left. It must not be eaten, because it's holy.
35 “Hivyo utamfanyia Aroni na wanawe kila kitu kama vile nilivyokuamuru: Utachukua muda wa siku saba kuwaweka wakfu.
This is the process you are to follow for Aaron and his sons, observing all the instructions I have given you. It will take seven days to ordain them.
36 Utatoa dhabihu ya fahali kila siku kuwa sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho. Takasa madhabahu kwa kufanya upatanisho kwa ajili yake, nayo uitie mafuta na kuiweka wakfu.
Every day you are to sacrifice a bull as a sin offering for forgiveness. When you do this the altar needs to be purified. Anoint it to make it holy.
37 Kwa muda wa siku saba fanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu na kuiweka wakfu. Ndipo madhabahu itakuwa takatifu sana na chochote kitakachoigusa kitakuwa kitakatifu.
For seven days you shall purify the altar and consecrate it. Then the altar will become completely holy, and everything that touches the altar will become holy.
38 “Kwa kawaida hiki ndicho utakachotoa juu ya madhabahu kila siku: wana-kondoo wawili wenye umri wa mwaka mmoja.
You are to offer two lambs that are a year old on the altar, daily and continually.
39 Utamtoa mmoja asubuhi na huyo mwingine jioni.
In the morning offer one lamb, and offer the other one in the evening before it gets dark.
40 Pamoja na mwana-kondoo wa kwanza utatoa efa moja ya unga wa ngano laini uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta yaliyokamuliwa, pamoja na robo ya hini ya divai kuwa sadaka ya kinywaji.
With the first lamb also offer a tenth of an ephah of best quality flour, mixed with a quarter of a hin of olive oil, and a drink offering of a quarter of a hin of wine.
41 Huyo mwana-kondoo mwingine mtoe dhabihu wakati wa machweo pamoja na sadaka za unga na za kinywaji kama vile ulivyofanya asubuhi, kuwa harufu ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
Then offer the second lamb in the evening, with the same grain and drink offerings as in the morning, a burnt offering to the Lord and accepted by him.
42 “Kwa vizazi vijavyo itakuwa kawaida kutoa sadaka hii ya kuteketezwa kila mara kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana. Hapo ndipo nitakapokutana na ninyi na kusema nanyi,
These burnt offerings will be made continually for all generations at the entrance to the Tent of Meeting in the Lord's presence. I will meet you there to speak with you.
43 Huko ndipo nitakapokutana na Waisraeli, nalo Hema la Kukutania litatakaswa na utukufu wangu.
I will meet with the Israelites there, and that place will be made holy by my glory.
44 “Kwa hiyo nitaliweka wakfu Hema la Kukutania pamoja na madhabahu, nami nitamweka wakfu Aroni na wanawe ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani.
In this way I will dedicate the Tent of Meeting and the altar, and I will dedicate Aaron and his sons to serve me as priests.
45 Ndipo nitakapofanya makao miongoni mwa Waisraeli na kuwa Mungu wao.
Then I will live with the Israelites and be their God.
46 Nao watajua kuwa Mimi Ndimi Bwana Mungu wao, aliyewatoa Misri ili nipate kufanya makao miongoni mwao. Mimi Ndimi Bwana Mungu wao.
They will know that I am the Lord their God, who led them out of Egypt, so that I could live with them. I am the Lord their God.