< Kutoka 28 >
1 “Mtwae Aroni ndugu yako aliyeletwa kwako kutoka miongoni mwa Waisraeli, pamoja na wanawe Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
“Trae a Aarón, tu hermano, y a sus hijos con él, cerca de ti, de entre los hijos de Israel, para que me sirva en el oficio de sacerdote: Aarón, con Nadab, Abiú, Eleazar e Itamar, hijos de Aarón.
2 Mshonee Aroni ndugu yako mavazi matakatifu ili yampe ukuu na heshima.
Harás vestiduras sagradas para Aarón, tu hermano, para gloria y belleza.
3 Waambie mafundi stadi wote niliowapa hekima katika shughuli hiyo wamtengenezee Aroni mavazi hayo, ili awekwe wakfu, anitumikie katika kazi ya ukuhani.
Hablarás a todos los sabios de corazón, a quienes he llenado de espíritu de sabiduría, para que hagan las vestiduras de Aarón para santificarlo, a fin de que me sirva en el oficio de sacerdote.
4 Haya ndiyo mavazi watakayoshona: kifuko cha kifuani, kisibau, kanzu, joho lililorembwa, kilemba na mshipi. Mavazi haya yatashonwa kwa ajili ya ndugu yako Aroni na wanawe ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
Estas son las vestimentas que harán: un pectoral, un efod, un manto, una túnica ajustada, un turbante y un fajín. Harán las vestiduras sagradas para Aarón tu hermano y sus hijos, para que me sirvan en el oficio sacerdotal.
5 Waambie watumie dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani safi.
Usarán el oro, el azul, la púrpura, la escarlata y el lino fino.
6 “Tengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa, kazi ya fundi stadi.
“Harán el efod de oro, azul, púrpura, escarlata y lino torcido, obra del obrero hábil.
7 Kitakuwa na vipande viwili vya mabegani vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kufungia kisibau.
Tendrá dos correas para los hombros, unidas a los dos extremos del mismo, para que se pueda unir.
8 Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi utafanana nacho: utakuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao utengenezwe kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri.
La banda tejida con destreza, que está sobre él, será como su obra y de la misma pieza; de oro, azul, púrpura, escarlata y lino fino torcido.
9 “Chukua vito viwili vya shohamu, na uchore juu yake majina ya wana wa Israeli
Tomarás dos piedras de ónice y grabarás en ellas los nombres de los hijos de Israel.
10 kufuatana na walivyozaliwa: majina sita katika kito kimoja, na mengine sita katika kito kingine.
Seis de sus nombres en una piedra, y los nombres de los seis que quedan en la otra piedra, en el orden de su nacimiento.
11 Yachore majina ya wana wa Israeli juu ya vito hivyo viwili kama vile sonara anavyochonga muhuri. Kisha uvitie vito hivyo katika vijalizo vya dhahabu,
Con el trabajo de un grabador en piedra, como los grabados de un sello, grabarás las dos piedras, según los nombres de los hijos de Israel. Las harás encerrar en engastes de oro.
12 na uvifungie juu ya vipande vya mabega ya kisibau yawe kama vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli. Aroni atavaa majina hayo mabegani mwake kama kumbukumbu mbele za Bwana.
Pondrás las dos piedras en los tirantes del efod, para que sean piedras conmemorativas de los hijos de Israel. Aarón llevará sus nombres ante el Señor en sus dos hombros como recuerdo.
13 Tengeneza vijalizo vya dhahabu
Harás engastes de oro,
14 na mikufu miwili ya dhahabu safi iliyosokotwa kama kamba, na uifunge mikufu hiyo kwenye vijalizo.
y dos cadenas de oro puro; las harás como cordones trenzados. Pondrás las cadenas trenzadas en los engastes.
15 “Fanyiza kifuko cha kifuani kwa ajili ya kufanya maamuzi, kazi ya fundi stadi. Kitengeneze kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
“Harás un pectoral de juicio, obra de obrero experto; como la obra del efod lo harás; de oro, de azul, de púrpura, de carmesí y de lino torcido, lo harás.
16 Kitakuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, na kikunjwe mara mbili.
Será cuadrado y con doble pliegue; un palmo será su longitud, y un palmo su anchura.
17 Kisha weka safu nne za vito vya thamani juu yake. Safu ya kwanza itakuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
Pondrás en él engastes de piedras, cuatro hileras de piedras: una hilera de rubíes, topacios y berilos será la primera hilera;
18 katika safu ya pili itakuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
y la segunda hilera una turquesa, un zafiro, y una esmeralda;
19 safu ya tatu itakuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
y la tercera hilera un jacinto, un ágata y una amatista;
20 na safu ya nne itakuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Yote yatiwe kwenye vijalizo vya dhahabu.
y la cuarta hilera un crisolito, un ónice y un jaspe. Estarán encerrados en oro en sus engastes.
21 Patakuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kwa jina mojawapo la wana wa Israeli, kila kimoja kichorwe kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
Las piedras serán según los nombres de los hijos de Israel, doce, según sus nombres; como los grabados de un sello, cada uno según su nombre, serán para las doce tribus.
22 “Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani, tengeneza mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
Harás en el pectoral cadenas como cordones, de oro puro trenzado.
23 Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili yake, uzifungie kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
Harás en el pectoral dos anillos de oro, y pondrás los dos anillos en los dos extremos del pectoral.
24 Funga ile mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete zilizo katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
Pondrás las dos cadenas trenzadas de oro en los dos anillos de los extremos del pectoral.
25 nazo zile ncha nyingine za mkufu zifunge kwenye vile vijalizo viwili, na uzishikamanishe na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
Los otros dos extremos de las dos cadenas trenzadas los pondrás en los dos engastes, y los pondrás en los tirantes del efod en su parte delantera.
26 Tengeneza pete mbili za dhahabu, uzishikamanishe kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
Harás dos anillos de oro y los pondrás en los dos extremos del pectoral, en su borde, que está hacia el lado del efod, hacia adentro.
27 Tengeneza pete nyingine mbili za dhahabu, na uzishikamanishe sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
Harás dos anillos de oro y los pondrás en los dos tirantes del efod por debajo, en su parte delantera, cerca de su acoplamiento, por encima de la banda hábilmente tejida del efod.
28 Pete za kifuko cha kifuani zitafungwa kwenye pete zile za kisibau kwa kamba ya buluu, ziunganishwe na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau.
El pectoral lo unirán por sus anillos a los anillos del efod con un cordón de color azul, para que quede sobre la banda hábilmente tejida del efod, y para que el pectoral no se salga del efod.
29 “Wakati wowote Aroni aingiapo Mahali Patakatifu, atakuwa na yale majina ya wana wa Israeli moyoni mwake juu ya kile kifuko cha kifuani cha uamuzi kama kumbukumbu ya kudumu mbele za Bwana.
Aarón llevará los nombres de los hijos de Israel en el pectoral del juicio sobre su corazón, cuando entre en el lugar santo, como recuerdo ante Yahvé siempre.
30 Pia weka Urimu na Thumimu ndani ya kifuko cha kifuani, yawe juu ya moyo wa Aroni kila mara aingiapo mbele za Bwana. Kwa hiyo siku zote Aroni atakuwa na uwezo kufanya maamuzi kwa ajili ya wana wa Israeli mbele za Bwana.
En el pectoral del juicio pondrás el Urim y el Tumim, y estarán en el corazón de Aarón cuando entre delante de Yahvé. Aarón llevará el juicio de los hijos de Israel en su corazón ante el Señor continuamente.
31 “Shona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu,
“Harás el manto del efod todo de color azul.
32 na katikati uweke nafasi ya kuingizia kichwa. Kutakuwa na utepe uliofumwa, unaofanana na ukosi kuizunguka nafasi hiyo, ili isichanike.
Tendrá un orificio para la cabeza en el centro. Tendrá un cordón de tejido alrededor de su orificio, como el orificio de una cota de malla, para que no se rompa.
33 Tengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu kuzunguka pindo la hilo joho, na uweke pia vikengele vya dhahabu kati ya hayo makomamanga.
En su dobladillo harás granadas de azul, de púrpura y de escarlata, alrededor de su dobladillo; con campanillas de oro entre ellas y alrededor de ellas:
34 Hivyo vikengele vya dhahabu na makomamanga vitapishana kuzunguka upindo wa joho lile.
una campanilla de oro y una granada, una campanilla de oro y una granada, alrededor del dobladillo del manto.
35 Ni lazima Aroni alivae anapofanya huduma. Sauti ya hivyo vikengele itasikika anapoingia na kutoka Mahali Patakatifu mbele za Bwana, ili asije akafa.
Estará sobre Aarón para ministrar; y su sonido se oirá cuando entre al lugar santo delante de Yahvé, y cuando salga, para que no muera.
36 “Tengeneza bamba la dhahabu safi na uchore juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
“Harás una placa de oro puro y grabarás en ella, como los grabados de un sello, ‘SANTO A YAHWEH’.
37 Lifunge hilo bamba kwa kamba ya buluu kwenye kilemba, nalo ni lazima liwe mbele ya kilemba.
La pondrás sobre un cordón de color azul, y estará en el fajín. Estará en la parte delantera del fajín.
38 Aroni alivae bamba hilo kwenye paji la uso wake, naye atachukua hatia kuhusu sadaka takatifu za Waisraeli wanazoweka wakfu, sadaka za aina yoyote. Litakuwa kwenye paji la uso wa Aroni daima ili zikubalike kwa Bwana.
Estará en la frente de Aarón, y Aarón llevará la iniquidad de las cosas sagradas que los hijos de Israel santifican en todos sus dones sagrados; y estará siempre en su frente, para que sean aceptados ante Yahvé.
39 “Fuma koti la kitani safi na ufanye kilemba cha kitani safi. Mshipi uwe ni kazi ya mtarizi.
Tejerás la túnica con lino fino. Harás un turbante de lino fino. Harás un fajín, obra del bordador.
40 Watengenezee wana wa Aroni makoti, mishipi na kofia, ili kuwapa ukuu na heshima.
“Harás túnicas para los hijos de Aarón. Les harás fajas. Les harás cintillos, para gloria y belleza.
41 Baada ya kumvika Aroni ndugu yako pamoja na wanawe nguo hizi, watie mafuta na kuwabariki. Waweke wakfu ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
Se las pondrás a Aarón, tu hermano, y a sus hijos con él, y los ungirás, los consagrarás y los santificarás, para que me sirvan en el oficio de sacerdote.
42 “Watengenezee nguo za ndani za kitani zitakazofunika mwili, kutoka kiunoni hadi mapajani.
Les harás pantalones de lino para cubrir su carne desnuda. Llegarán desde la cintura hasta los muslos.
43 Aroni na wanawe ni lazima wavae haya kila wanapoingia katika Hema la Kukutania au wanaposogelea madhabahu wakati wa kutoa huduma katika Mahali Patakatifu, ili wasije wakafanya kosa wakafa. “Haya yawe maagizo ya kudumu kwa Aroni na vizazi vyake.
Estarán sobre Aarón y sobre sus hijos, cuando entren en la Tienda de Reunión, o cuando se acerquen al altar para ministrar en el lugar santo, para que no lleven iniquidad y mueran. Esto será un estatuto para siempre para él y para su descendencia después de él.