< Kutoka 28 >

1 “Mtwae Aroni ndugu yako aliyeletwa kwako kutoka miongoni mwa Waisraeli, pamoja na wanawe Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
И ты приведи к себе Аарона, брата твоего, и сыны его от сынов Израилевых, да священнодействуют Мне Аарон и Надав, и Авиуд и Елеазар и Ифамар, сынове Аарони.
2 Mshonee Aroni ndugu yako mavazi matakatifu ili yampe ukuu na heshima.
И да сотвориши ризу святу Аарону брату твоему в честь и славу.
3 Waambie mafundi stadi wote niliowapa hekima katika shughuli hiyo wamtengenezee Aroni mavazi hayo, ili awekwe wakfu, anitumikie katika kazi ya ukuhani.
И ты возглаголи ко всем премудрым умом, ихже наполних духа мудрости и смышления: и да сотворят ризу святу Аарону, в нейже имать священнодействовати Мне во святилищи.
4 Haya ndiyo mavazi watakayoshona: kifuko cha kifuani, kisibau, kanzu, joho lililorembwa, kilemba na mshipi. Mavazi haya yatashonwa kwa ajili ya ndugu yako Aroni na wanawe ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
И сия суть ризы, ихже сотворят: наперсник и ризу верхнюю, и долгую ризу и ризу тресновиту, и наглавие и пояс: и да сотворят ризы святы Аарону и сыном его, во еже священнодействовати Мне.
5 Waambie watumie dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani safi.
И сии да возмут злато и синету, и багряницу и червленицу и виссон,
6 “Tengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa, kazi ya fundi stadi.
и да сотворят ризу верхнюю от виссона сканаго, дело тканно пестрящаго.
7 Kitakuwa na vipande viwili vya mabegani vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kufungia kisibau.
Две ризы верхния да будут ему придержащяся едина друзей, на обе стране связаныя.
8 Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi utafanana nacho: utakuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao utengenezwe kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri.
И ткание риз верхних, еже есть на них, по сотворению их да будет от злата чиста и синеты, и багряницы и червленицы пряденыя и виссона сканаго.
9 “Chukua vito viwili vya shohamu, na uchore juu yake majina ya wana wa Israeli
И возмеши два каменя, камене смарагда, и изваяеши на них имена сынов Израилевых:
10 kufuatana na walivyozaliwa: majina sita katika kito kimoja, na mengine sita katika kito kingine.
шесть имен на камени единем и шесть имен прочиих на камени друзем по родом их,
11 Yachore majina ya wana wa Israeli juu ya vito hivyo viwili kama vile sonara anavyochonga muhuri. Kisha uvitie vito hivyo katika vijalizo vya dhahabu,
дело каменныя хитрости: ваянием печати изваяеши оба каменя имены сынов Израилевых.
12 na uvifungie juu ya vipande vya mabega ya kisibau yawe kama vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli. Aroni atavaa majina hayo mabegani mwake kama kumbukumbu mbele za Bwana.
И положиши оба каменя на раменах верхния ризы: камени в память суть сыном Израилевым: и воздвигнет Аарон имена сынов Израилевых пред Господем на оба рамена своя в память о них.
13 Tengeneza vijalizo vya dhahabu
И да сотвориши щитцы от злата чиста,
14 na mikufu miwili ya dhahabu safi iliyosokotwa kama kamba, na uifunge mikufu hiyo kwenye vijalizo.
и да сотвориши две тресновицы от злата чиста, смешены цветами, дело плетения: и возложиши тресновицы сплетеныя на щитцы по нарамником их сопреди.
15 “Fanyiza kifuko cha kifuani kwa ajili ya kufanya maamuzi, kazi ya fundi stadi. Kitengeneze kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
И да сотвориши слово судное, дело пестрящаго: по составу ризы верхния да сотвориши сие от злата и синеты, и багряницы и червленицы пряденыя и виссона сканаго:
16 Kitakuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, na kikunjwe mara mbili.
сотвориши е четвероуголно: да будет сугубо, пяди долгота его и пяди широта,
17 Kisha weka safu nne za vito vya thamani juu yake. Safu ya kwanza itakuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
и нашиеши на нем швение каменное в четыри ряда. Ряд камений да будет: сардий, топазий и смарагд, ряд един:
18 katika safu ya pili itakuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
и ряд вторый, анфракс и сапфир и иаспис:
19 safu ya tatu itakuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
и ряд третий, лигирий и ахат и амефист:
20 na safu ya nne itakuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Yote yatiwe kwenye vijalizo vya dhahabu.
и ряд четвертый, хрисолиф и вириллий и онихий: объяты златом, исплетены в злате да будут по ряду своему.
21 Patakuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kwa jina mojawapo la wana wa Israeli, kila kimoja kichorwe kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
И камение да будут от имен двунадесяти сынов Израилевых пред Господем: на дву раменах его дванадесять по именам их и по родом их, изваяни печатми, коегождо по имени да будут в дванадесять племен.
22 “Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani, tengeneza mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
И да сотвориши на слове тресны сплетены, делом верижным, от злата чиста.
23 Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili yake, uzifungie kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
И да сотвориши на словеси два колца злата: и возложиши два колца злата на оба края словесе.
24 Funga ile mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete zilizo katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
И возложиши тресны и чепи златы на два колца от обоих краев словесе.
25 nazo zile ncha nyingine za mkufu zifunge kwenye vile vijalizo viwili, na uzishikamanishe na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
И два края двух тресн наложиши на две чепочки, и возложиши на рамена верхних риз лицем ко другъдругу.
26 Tengeneza pete mbili za dhahabu, uzishikamanishe kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
И сотвориши два колца злата, и возложиши на обе страны словесе на край от края задняго верхних риз, отвнутрь.
27 Tengeneza pete nyingine mbili za dhahabu, na uzishikamanishe sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
И сотвориши два колца злата, и возложиши на оба рамена верхния ризы снизу его, лицем по согбению свыше соткания верхних риз.
28 Pete za kifuko cha kifuani zitafungwa kwenye pete zile za kisibau kwa kamba ya buluu, ziunganishwe na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau.
И стягнеши слово колцами, яже на нем, с колцами верхних риз сложеными, из синеты плетеными во ткание верхних риз, да не низпускается слово с верхних риз.
29 “Wakati wowote Aroni aingiapo Mahali Patakatifu, atakuwa na yale majina ya wana wa Israeli moyoni mwake juu ya kile kifuko cha kifuani cha uamuzi kama kumbukumbu ya kudumu mbele za Bwana.
И да возмет Аарон имена сынов Израилевых на слове суднем на персех, входящь во святое на память пред Богом. И да положиши на словеси суднем тресны: плетения на оба края словесе возложиши, и оба щита возложиши на обе раме нарамника на лице.
30 Pia weka Urimu na Thumimu ndani ya kifuko cha kifuani, yawe juu ya moyo wa Aroni kila mara aingiapo mbele za Bwana. Kwa hiyo siku zote Aroni atakuwa na uwezo kufanya maamuzi kwa ajili ya wana wa Israeli mbele za Bwana.
И да возложиши на слово судное явление и истину: и да будет на персех Аарону, егда внидет в святое пред Господа: и да носит Аарон суды сынов Израилевых на персех пред Господем всегда.
31 “Shona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu,
И да сотвориши ризу внутреннюю подир всю синю.
32 na katikati uweke nafasi ya kuingizia kichwa. Kutakuwa na utepe uliofumwa, unaofanana na ukosi kuizunguka nafasi hiyo, ili isichanike.
И да будет устие посреде его, ожерелие имущо кругом устия делом тканым, сгиб сошвен от него, да не раздерется.
33 Tengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu kuzunguka pindo la hilo joho, na uweke pia vikengele vya dhahabu kati ya hayo makomamanga.
И да сотвориши на омете ризнем снизу, аки шипка цветущаго, пугвицы из синеты и багряницы, и червленицы пряденыя и виссона сканаго, на омете ризы кругом: в тойже образ пугвицы златы, и звонцы между сими окрест.
34 Hivyo vikengele vya dhahabu na makomamanga vitapishana kuzunguka upindo wa joho lile.
При пугвице злат звонец, и цвет на омете ризнем, кругом.
35 Ni lazima Aroni alivae anapofanya huduma. Sauti ya hivyo vikengele itasikika anapoingia na kutoka Mahali Patakatifu mbele za Bwana, ili asije akafa.
И да будет Аарону, егда служит, слышан глас его, входящу во святое пред Господа, и исходящу, да не умрет.
36 “Tengeneza bamba la dhahabu safi na uchore juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
И да сотвориши дщицу злату чисту: и изобразиши на ней образ печати, Святыня Господня,
37 Lifunge hilo bamba kwa kamba ya buluu kwenye kilemba, nalo ni lazima liwe mbele ya kilemba.
и да возложиши ю на синету сканую, и да будет на увясле, спреди увясла да будет,
38 Aroni alivae bamba hilo kwenye paji la uso wake, naye atachukua hatia kuhusu sadaka takatifu za Waisraeli wanazoweka wakfu, sadaka za aina yoyote. Litakuwa kwenye paji la uso wa Aroni daima ili zikubalike kwa Bwana.
и да будет на челе Аарони: и отимет Аарон согрешения святых, елика освятят сынове Израилевы от всякаго даяния святых своих, и да будет на челе Аарони всегда приято ими пред Господем.
39 “Fuma koti la kitani safi na ufanye kilemba cha kitani safi. Mshipi uwe ni kazi ya mtarizi.
И тресны риз от виссона: и сотвориши клобук виссонный, и пояс да сотвориши дело пестрящаго.
40 Watengenezee wana wa Aroni makoti, mishipi na kofia, ili kuwapa ukuu na heshima.
И сыном Аароновым да сотвориши ризы и поясы, и клобуки да сотвориши им в честь и славу:
41 Baada ya kumvika Aroni ndugu yako pamoja na wanawe nguo hizi, watie mafuta na kuwabariki. Waweke wakfu ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
и облечеши в ня Аарона брата твоего и сыны его с ним, и да помажеши их, и исполниши руце их и освятиши их, да Ми священнодействуют.
42 “Watengenezee nguo za ndani za kitani zitakazofunika mwili, kutoka kiunoni hadi mapajani.
И да сотвориши им надраги льняны покрывати стыдения плоти их, от бедр даже до стегн будут,
43 Aroni na wanawe ni lazima wavae haya kila wanapoingia katika Hema la Kukutania au wanaposogelea madhabahu wakati wa kutoa huduma katika Mahali Patakatifu, ili wasije wakafanya kosa wakafa. “Haya yawe maagizo ya kudumu kwa Aroni na vizazi vyake.
и да имать Аарон и сынове его, егда входят в скинию свидения, или егда приходят служити к жертвеннику святыни: и да не наведут на ся греха, да не умрут: законное вечное (да будет) ему и семени его по нем.

< Kutoka 28 >