< Kutoka 28 >

1 “Mtwae Aroni ndugu yako aliyeletwa kwako kutoka miongoni mwa Waisraeli, pamoja na wanawe Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
Fais aussi approcher de toi Aaron ton frère avec ses fils du milieu des enfants d’Israël, afin qu’ils exercent les fonctions du sacerdoce pour moi: Aaron, Nadab et Abiu, Eléazar et Ithamar.
2 Mshonee Aroni ndugu yako mavazi matakatifu ili yampe ukuu na heshima.
Et tu feras un vêtement saint à Aaron ton frère pour la gloire et l’ornement.
3 Waambie mafundi stadi wote niliowapa hekima katika shughuli hiyo wamtengenezee Aroni mavazi hayo, ili awekwe wakfu, anitumikie katika kazi ya ukuhani.
Et tu parleras à tous les sages de cœur, que j’ai remplis de l’esprit de prudence, pour qu’ils fassent à Aaron des vêtements, par lesquels étant sanctifié, il me servira.
4 Haya ndiyo mavazi watakayoshona: kifuko cha kifuani, kisibau, kanzu, joho lililorembwa, kilemba na mshipi. Mavazi haya yatashonwa kwa ajili ya ndugu yako Aroni na wanawe ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
Or voici les vêtements qu’ils feront: Un rational, un éphod, une robe et une tunique de lin étroite, une tiare, et une ceinture. Ainsi, ils feront des vêtements saints à ton frère Aaron et à ses fils, afin qu’ils exercent les fonctions du sacerdoce, pour moi.
5 Waambie watumie dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani safi.
Et ils prendront l’or, l’hyacinthe, la pourpre, l’écarlate deux fois teinte et le fin lin.
6 “Tengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa, kazi ya fundi stadi.
Or ils feront l’éphod d’or, d’hyacinthe, de pourpre, d’écarlate deux fois teinte, et de fin lin retors, d’un ouvrage en tissu de diverses couleurs.
7 Kitakuwa na vipande viwili vya mabegani vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kufungia kisibau.
Il aura aux deux côtés de ses sommités deux bandes jointes, de manière à former une seule pièce.
8 Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi utafanana nacho: utakuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao utengenezwe kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri.
Le tissu lui-même et tous les ouvrages divers seront d’or, d’hyacinthe, de pourpre, d’écarlate deux fois teinte et de fin lin retors.
9 “Chukua vito viwili vya shohamu, na uchore juu yake majina ya wana wa Israeli
Et tu prendras deux pierres d’onyx, et tu graveras sur elles les noms des fils d’Israël:
10 kufuatana na walivyozaliwa: majina sita katika kito kimoja, na mengine sita katika kito kingine.
Six noms sur une pierre, et les six autres sur une autre, selon l’ordre de leur naissance.
11 Yachore majina ya wana wa Israeli juu ya vito hivyo viwili kama vile sonara anavyochonga muhuri. Kisha uvitie vito hivyo katika vijalizo vya dhahabu,
Au moyen d’un travail de sculpteur et de la taille d’un lapidaire, tu graveras sur les pierres les noms des fils d’Israël, après les avoir enchâssées dans l’or et les en avoir environnées;
12 na uvifungie juu ya vipande vya mabega ya kisibau yawe kama vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli. Aroni atavaa majina hayo mabegani mwake kama kumbukumbu mbele za Bwana.
Et tu les mettras sur les deux côtés de l’éphod, souvenir pour les enfants d’Israël. Et Aaron portera sur ses épaules leur nom devant le Seigneur, pour souvenir.
13 Tengeneza vijalizo vya dhahabu
Tu feras encore des agrafes d’or.
14 na mikufu miwili ya dhahabu safi iliyosokotwa kama kamba, na uifunge mikufu hiyo kwenye vijalizo.
Et deux chaînettes d’un or très pur, se tenant l’une à l’autre, que tu attacheras aux agrafes.
15 “Fanyiza kifuko cha kifuani kwa ajili ya kufanya maamuzi, kazi ya fundi stadi. Kitengeneze kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
Tu feras aussi le rational du jugement, d’un ouvrage en tissu de diverses couleurs, selon la tissure de l’éphod, d’or, d’hyacinthe, de pourpre, d’écarlate deux teinte et de fin lin retors.
16 Kitakuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, na kikunjwe mara mbili.
Il sera carré et double, et il aura la mesure d’une palme, tant en longueur qu’en largeur.
17 Kisha weka safu nne za vito vya thamani juu yake. Safu ya kwanza itakuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
Tu y mettras quatre rangs de pierres: à la première rangée il y aura une sardoine, une topaze et une émeraude;
18 katika safu ya pili itakuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
À la seconde, une escarboucle, un saphir et un jaspe;
19 safu ya tatu itakuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
À la troisième, un ligure, une agate et une améthyste;
20 na safu ya nne itakuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Yote yatiwe kwenye vijalizo vya dhahabu.
À la quatrième, un chrysolite, un onyx, et un béryl; ils seront enchâssés dans de l’or, selon leurs rangs.
21 Patakuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kwa jina mojawapo la wana wa Israeli, kila kimoja kichorwe kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
Et ils porteront les noms des fils d’Israël: leurs douze noms seront gravés, chaque nom sur chaque pierre, selon les douze tribus.
22 “Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani, tengeneza mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
Tu feras pour le rational des chaînes se tenant l’une à l’autre, d’un or très pur,
23 Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili yake, uzifungie kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
Et deux anneaux d’or que tu mettras aux deux sommités du rational;
24 Funga ile mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete zilizo katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
Puis tu joindras les deux chaînes d’or par les anneaux qui sont aux bords du rational;
25 nazo zile ncha nyingine za mkufu zifunge kwenye vile vijalizo viwili, na uzishikamanishe na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
Et tu attacheras les extrémités des chaînes elles-mêmes aux agrafes aux deux côtés de l’éphod qui regarde le rational.
26 Tengeneza pete mbili za dhahabu, uzishikamanishe kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
Tu feras aussi deux anneaux d’or que tu mettras aux sommités du rational sur les bords qui sont vis-à-vis de l’éphod, et regardent sa partie de derrière.
27 Tengeneza pete nyingine mbili za dhahabu, na uzishikamanishe sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
Tu feras de plus deux autres anneaux d’or qui devront être posés aux deux côtés de l’éphod par en bas; côtés qui regardent en face de la jonction inférieure, afin que le rational puisse s’adapter à l’éphod.
28 Pete za kifuko cha kifuani zitafungwa kwenye pete zile za kisibau kwa kamba ya buluu, ziunganishwe na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau.
Et que le rational soit attaché par ses anneaux aux anneaux de l’éphod au moyen d’un ruban d’hyacinthe, afin que la jonction habilement faite se maintienne, et que le rational et l’éphod ne puissent être séparés l’un de l’autre.
29 “Wakati wowote Aroni aingiapo Mahali Patakatifu, atakuwa na yale majina ya wana wa Israeli moyoni mwake juu ya kile kifuko cha kifuani cha uamuzi kama kumbukumbu ya kudumu mbele za Bwana.
Et Aaron portera les noms des fils d’Israël dans le rational du jugement sur sa poitrine, lorsqu’ils entrera dans le sanctuaire, souvenir en présence du Seigneur pour toujours.
30 Pia weka Urimu na Thumimu ndani ya kifuko cha kifuani, yawe juu ya moyo wa Aroni kila mara aingiapo mbele za Bwana. Kwa hiyo siku zote Aroni atakuwa na uwezo kufanya maamuzi kwa ajili ya wana wa Israeli mbele za Bwana.
Or tu mettras sur le rational du jugement: La Doctrine et la Vérité, qui seront sur la poitrine d’Aaron, lorsqu’il entrera devant le Seigneur; ainsi il portera toujours le jugement des fils d’Israël sur sa poitrine en la présence du Seigneur.
31 “Shona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu,
Tu feras encore, toute de couleur d’hyacinthe, la tunique de l’éphod.
32 na katikati uweke nafasi ya kuingizia kichwa. Kutakuwa na utepe uliofumwa, unaofanana na ukosi kuizunguka nafasi hiyo, ili isichanike.
Au milieu de laquelle il y aura dans le haut une ouverture, et autour d’elle un bord tissu, comme on a coutume d’en faire aux extrémités des vêtements, pour ne pas qu’il se déchire facilement.
33 Tengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu kuzunguka pindo la hilo joho, na uweke pia vikengele vya dhahabu kati ya hayo makomamanga.
Mais en bas, aux pieds de la même tunique, tu feras tout autour comme des grenades d’hyacinthe, de pourpre, d’écarlate deux fois teinte, en entremêlant des sonnettes,
34 Hivyo vikengele vya dhahabu na makomamanga vitapishana kuzunguka upindo wa joho lile.
En sorte qu’il y ait une sonnette d’or et une grenade, et de nouveau, une autre sonnette d’or et une grenade.
35 Ni lazima Aroni alivae anapofanya huduma. Sauti ya hivyo vikengele itasikika anapoingia na kutoka Mahali Patakatifu mbele za Bwana, ili asije akafa.
Aaron en sera revêtu dans les fonctions du ministère, afin qu’on entende le son, quand il entrera dans le sanctuaire en la présence du Seigneur, et qu’il en sortira, et qu’il ne meure point.
36 “Tengeneza bamba la dhahabu safi na uchore juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
Tu feras encore une lame d’un or très pur, sur laquelle tu graveras, en ouvrage de ciseleur: La sainteté est au Seigneur.
37 Lifunge hilo bamba kwa kamba ya buluu kwenye kilemba, nalo ni lazima liwe mbele ya kilemba.
Et tu la lieras avec un ruban d’hyacinthe, et elle sera sur la tiare,
38 Aroni alivae bamba hilo kwenye paji la uso wake, naye atachukua hatia kuhusu sadaka takatifu za Waisraeli wanazoweka wakfu, sadaka za aina yoyote. Litakuwa kwenye paji la uso wa Aroni daima ili zikubalike kwa Bwana.
Dominant le front du pontife. Et Aaron portera les iniquités de ce que les enfants d’Israël auront offert et consacré dans tous leurs dons et présents. Or cette lame sera toujours sur son front, afin que le Seigneur leur soit propice.
39 “Fuma koti la kitani safi na ufanye kilemba cha kitani safi. Mshipi uwe ni kazi ya mtarizi.
Et tu feras la tunique étroite de fin lin; tu feras aussi une tiare de fin lin, et une ceinture, en ouvrage de brodeur.
40 Watengenezee wana wa Aroni makoti, mishipi na kofia, ili kuwapa ukuu na heshima.
Mais aux fils d’Aaron, tu prépareras des tuniques de lin, des ceintures et des tiares pour la gloire et l’ornement;
41 Baada ya kumvika Aroni ndugu yako pamoja na wanawe nguo hizi, watie mafuta na kuwabariki. Waweke wakfu ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
Et tu revêtiras de tous ces vêtements Aaron ton frère, et ses fils avec lui. Et tu consacreras les mains de tous, et tu les sanctifieras afin qu’ils exercent les fonctions du sacerdoce pour moi.
42 “Watengenezee nguo za ndani za kitani zitakazofunika mwili, kutoka kiunoni hadi mapajani.
Tu feras aussi des caleçons de lin, afin qu’ils couvrent la chair de leur nudité, depuis les reins jusqu’aux cuisses;
43 Aroni na wanawe ni lazima wavae haya kila wanapoingia katika Hema la Kukutania au wanaposogelea madhabahu wakati wa kutoa huduma katika Mahali Patakatifu, ili wasije wakafanya kosa wakafa. “Haya yawe maagizo ya kudumu kwa Aroni na vizazi vyake.
Et Aaron et ses fils s’en serviront, quand ils entreront dans le tabernacle de témoignage, ou quand ils approcheront de l’autel pour servir dans le sanctuaire, afin qu’ils ne meurent point coupables d’iniquité. Ce sera une loi perpétuelle pour Aaron et pour sa postérité après lui.

< Kutoka 28 >