< Kutoka 28 >

1 “Mtwae Aroni ndugu yako aliyeletwa kwako kutoka miongoni mwa Waisraeli, pamoja na wanawe Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
'And thou, bring thou near unto thee Aaron thy brother, and his sons with him, from the midst of the sons of Israel, for his being priest to Me, [even] Aaron, Nadab, and Abihu, Eleazar and Ithamar, sons of Aaron;
2 Mshonee Aroni ndugu yako mavazi matakatifu ili yampe ukuu na heshima.
and thou hast made holy garments for Aaron thy brother, for honour and for beauty;
3 Waambie mafundi stadi wote niliowapa hekima katika shughuli hiyo wamtengenezee Aroni mavazi hayo, ili awekwe wakfu, anitumikie katika kazi ya ukuhani.
and thou — thou dost speak unto all the wise of heart, whom I have filled [with] a spirit of wisdom, and they have made the garments of Aaron to sanctify him for his being priest to Me.
4 Haya ndiyo mavazi watakayoshona: kifuko cha kifuani, kisibau, kanzu, joho lililorembwa, kilemba na mshipi. Mavazi haya yatashonwa kwa ajili ya ndugu yako Aroni na wanawe ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
'And these [are] the garments which they make: a breastplate, and an ephod, and an upper robe, and an embroidered coat, a mitre, and a girdle; yea, they have made holy garments for Aaron thy brother, and for his sons, for his being priest to Me.
5 Waambie watumie dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani safi.
'And they take the gold, and the blue, and the purple, and the scarlet, and the linen,
6 “Tengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa, kazi ya fundi stadi.
and have made the ephod of gold, blue, and purple, and scarlet, and twined linen, work of a designer;
7 Kitakuwa na vipande viwili vya mabegani vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kufungia kisibau.
it hath two shoulders joining at its two ends, and it is joined.
8 Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi utafanana nacho: utakuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao utengenezwe kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri.
'And the girdle of his ephod which [is] on him, according to its work, is of the same, of gold, blue, and purple, and scarlet, and twined linen.
9 “Chukua vito viwili vya shohamu, na uchore juu yake majina ya wana wa Israeli
'And thou hast taken the two shoham stones, and hast opened on them the names of the sons of Israel;
10 kufuatana na walivyozaliwa: majina sita katika kito kimoja, na mengine sita katika kito kingine.
six of their names on the one stone, and the names of the remaining six on the second stone, according to their births;
11 Yachore majina ya wana wa Israeli juu ya vito hivyo viwili kama vile sonara anavyochonga muhuri. Kisha uvitie vito hivyo katika vijalizo vya dhahabu,
the work of an engraver in stone, openings of a signet, thou dost open the two stones by the names of the sons of Israel; turned round, embroidered [with] gold, thou dost make them.
12 na uvifungie juu ya vipande vya mabega ya kisibau yawe kama vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli. Aroni atavaa majina hayo mabegani mwake kama kumbukumbu mbele za Bwana.
'And thou hast set the two stones on the shoulders of the ephod — stones of memorial to the sons of Israel — and Aaron hath borne their names before Jehovah, on his two shoulders, for a memorial.
13 Tengeneza vijalizo vya dhahabu
'And thou hast made embroidered things of gold,
14 na mikufu miwili ya dhahabu safi iliyosokotwa kama kamba, na uifunge mikufu hiyo kwenye vijalizo.
and two chains of pure gold, wreathed work thou dost make them, work of thick bands, and thou hast put the thick chains on the embroidered things.
15 “Fanyiza kifuko cha kifuani kwa ajili ya kufanya maamuzi, kazi ya fundi stadi. Kitengeneze kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
'And thou hast made a breastplate of judgment, work of a designer; according to the work of the ephod thou dost make it; of gold, blue, and purple, and scarlet, and twined linen thou dost make it;
16 Kitakuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, na kikunjwe mara mbili.
it is square, doubled, a span its length, and a span its breadth.
17 Kisha weka safu nne za vito vya thamani juu yake. Safu ya kwanza itakuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
'And thou hast set in it settings of stone, four rows of stone; a row of sardius, topaz, and carbuncle [is] the first row;
18 katika safu ya pili itakuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
and the second row [is] emerald, sapphire, and diamond;
19 safu ya tatu itakuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
and the third row [is] opal, agate, and amethyst;
20 na safu ya nne itakuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Yote yatiwe kwenye vijalizo vya dhahabu.
and the fourth row [is] beryl, and onyx, and jasper; embroidered with gold are they in their settings,
21 Patakuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kwa jina mojawapo la wana wa Israeli, kila kimoja kichorwe kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
and the stones are according to the names of the sons of Israel, twelve, according to their names, openings of a signet, each by his name are they for the twelve tribes.
22 “Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani, tengeneza mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
'And thou hast made on the breastplate wreathed chains, work of thick bands, of pure gold;
23 Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili yake, uzifungie kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
and thou hast made on the breastplate two rings of gold, and hast put the two rings on the two ends of the breastplate;
24 Funga ile mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete zilizo katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
and thou hast put the two thick bands of gold on the two rings at the ends of the breastplate;
25 nazo zile ncha nyingine za mkufu zifunge kwenye vile vijalizo viwili, na uzishikamanishe na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
and the two ends of the two thick bands thou dost put on the two embroidered things, and thou hast put [them] on the shoulders of the ephod over-against its face.
26 Tengeneza pete mbili za dhahabu, uzishikamanishe kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
'And thou hast made two rings of gold, and hast set them on the two ends of the breastplate, on its border, which [is] over-against the ephod within;
27 Tengeneza pete nyingine mbili za dhahabu, na uzishikamanishe sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
and thou hast made two rings of gold, and hast put them on the two shoulders of the ephod, beneath, over-against its front, over-against its joining, above the girdle of the ephod,
28 Pete za kifuko cha kifuani zitafungwa kwenye pete zile za kisibau kwa kamba ya buluu, ziunganishwe na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau.
and they bind the breastplate by its rings unto the rings of the ephod with a ribbon of blue, to be above the girdle of the ephod, and the breastplate is not loosed from the ephod.
29 “Wakati wowote Aroni aingiapo Mahali Patakatifu, atakuwa na yale majina ya wana wa Israeli moyoni mwake juu ya kile kifuko cha kifuani cha uamuzi kama kumbukumbu ya kudumu mbele za Bwana.
'And Aaron hath borne the names of the sons of Israel in the breastplate of judgment, on his heart, in his going in unto the sanctuary, for a memorial before Jehovah continually.
30 Pia weka Urimu na Thumimu ndani ya kifuko cha kifuani, yawe juu ya moyo wa Aroni kila mara aingiapo mbele za Bwana. Kwa hiyo siku zote Aroni atakuwa na uwezo kufanya maamuzi kwa ajili ya wana wa Israeli mbele za Bwana.
'And thou hast put unto the breastplate of judgment the Lights and the Perfections, and they have been on the heart of Aaron, in his going in before Jehovah, and Aaron hath borne the judgment of the sons of Israel on his heart before Jehovah continually.
31 “Shona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu,
'And thou hast made the upper robe of the ephod completely of blue,
32 na katikati uweke nafasi ya kuingizia kichwa. Kutakuwa na utepe uliofumwa, unaofanana na ukosi kuizunguka nafasi hiyo, ili isichanike.
and the opening for its head hath been in its midst, a border is to its opening round about, work of a weaver, as the opening of a habergeon there is to it; it is not rent.
33 Tengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu kuzunguka pindo la hilo joho, na uweke pia vikengele vya dhahabu kati ya hayo makomamanga.
'And thou hast made on its hem pomegranates of blue, and purple, and scarlet, on its hem round about, and bells of gold in their midst round about;
34 Hivyo vikengele vya dhahabu na makomamanga vitapishana kuzunguka upindo wa joho lile.
a bell of gold and a pomegranate, a bell of gold and a pomegranate [are] on the hems of the upper robe round about.
35 Ni lazima Aroni alivae anapofanya huduma. Sauti ya hivyo vikengele itasikika anapoingia na kutoka Mahali Patakatifu mbele za Bwana, ili asije akafa.
'And it hath been on Aaron to minister in, and its sound hath been heard in his coming in unto the sanctuary before Jehovah, and in his going out, and he doth not die.
36 “Tengeneza bamba la dhahabu safi na uchore juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
'And thou hast made a flower of pure gold, and hast opened on it — openings of a signet — 'Holy to Jehovah;'
37 Lifunge hilo bamba kwa kamba ya buluu kwenye kilemba, nalo ni lazima liwe mbele ya kilemba.
and thou hast put it on a blue ribbon, and it hath been on the mitre — over-against the front of the mitre it is;
38 Aroni alivae bamba hilo kwenye paji la uso wake, naye atachukua hatia kuhusu sadaka takatifu za Waisraeli wanazoweka wakfu, sadaka za aina yoyote. Litakuwa kwenye paji la uso wa Aroni daima ili zikubalike kwa Bwana.
and it hath been on the forehead of Aaron, and Aaron hath borne the iniquity of the holy things which the sons of Israel do hallow, even all their holy gifts; and it hath been on his forehead continually for a pleasing thing for them before Jehovah.
39 “Fuma koti la kitani safi na ufanye kilemba cha kitani safi. Mshipi uwe ni kazi ya mtarizi.
'And thou hast embroidered the coat of linen, and hast made a mitre of linen, and a girdle thou dost make — work of an embroiderer.
40 Watengenezee wana wa Aroni makoti, mishipi na kofia, ili kuwapa ukuu na heshima.
'And for the sons of Aaron thou dost make coats, and thou hast made for them girdles, yea, bonnets thou dost make for them, for honour and for beauty;
41 Baada ya kumvika Aroni ndugu yako pamoja na wanawe nguo hizi, watie mafuta na kuwabariki. Waweke wakfu ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
and thou hast clothed Aaron thy brother with them, and his sons with him, and hast anointed them, and hast consecrated their hand, and hast sanctified them, and they have been priests to Me.
42 “Watengenezee nguo za ndani za kitani zitakazofunika mwili, kutoka kiunoni hadi mapajani.
'And make thou for them linen trousers to cover the naked flesh: they are from the loins even unto the thighs;
43 Aroni na wanawe ni lazima wavae haya kila wanapoingia katika Hema la Kukutania au wanaposogelea madhabahu wakati wa kutoa huduma katika Mahali Patakatifu, ili wasije wakafanya kosa wakafa. “Haya yawe maagizo ya kudumu kwa Aroni na vizazi vyake.
and they have been on Aaron and on his sons, in their going in unto the tent of meeting, or in their drawing nigh unto the altar to minister in the sanctuary, and they do not bear iniquity nor have they died; a statute age-during to him, and to his seed after him.

< Kutoka 28 >