< Kutoka 28 >

1 “Mtwae Aroni ndugu yako aliyeletwa kwako kutoka miongoni mwa Waisraeli, pamoja na wanawe Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
Also applie thou to thee Aaron, thi brother, with hise sones, fro the myddis of the sones of Israel, that Aaron, Nadab, and Abyu, Eleazar, and Ythamar, be set in preesthod to me.
2 Mshonee Aroni ndugu yako mavazi matakatifu ili yampe ukuu na heshima.
And thou schalt make an hooli clooth to Aaron, thi brother, in to glorie and fairenesse.
3 Waambie mafundi stadi wote niliowapa hekima katika shughuli hiyo wamtengenezee Aroni mavazi hayo, ili awekwe wakfu, anitumikie katika kazi ya ukuhani.
And thou schalt speke to alle wise men in herte, whiche Y haue fillid with the spirit of prudence, that thei make clothis to Aaron, in whiche he schal be halewid, and schal mynystre to me.
4 Haya ndiyo mavazi watakayoshona: kifuko cha kifuani, kisibau, kanzu, joho lililorembwa, kilemba na mshipi. Mavazi haya yatashonwa kwa ajili ya ndugu yako Aroni na wanawe ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
Forsothe these schulen be the clothis, whiche thei schulen make; `thei schulen make racional, and a clooth on the schuldris, a coote, and a streyt lynnun clooth, a mytre, and a girdil; hooli cloothis to Aaron, thi brother, and to hise sones, that thei be set in preesthod to me.
5 Waambie watumie dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani safi.
And thei schulen take gold, and iacynt, and purpur, and `reed selk twies died, and bijs;
6 “Tengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa, kazi ya fundi stadi.
forsothe thei schulen make the clooth on the schuldris of gold, and of iacynt, and purpur, and of `reed selk twies died, and of bijs foldid ayen, bi broyderi werk of dyuerse colours.
7 Kitakuwa na vipande viwili vya mabegani vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kufungia kisibau.
It schal haue twey hemmes ioyned in euer either side of hiynessis, that tho go ayen in to oon.
8 Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi utafanana nacho: utakuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao utengenezwe kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri.
Thilke weuyng, and al dyuersite of the werk schal be of gold, and iacynt, and purpur, and of `reed selk twies died, and bijs foldis ayen.
9 “Chukua vito viwili vya shohamu, na uchore juu yake majina ya wana wa Israeli
And thou schalt take twei stoonys of onychym, and thou schalt graue in tho the names of the sones of Israel,
10 kufuatana na walivyozaliwa: majina sita katika kito kimoja, na mengine sita katika kito kingine.
sixe names in o stoon, and sixe othere in the tother stoon, bi the ordre of her birthe;
11 Yachore majina ya wana wa Israeli juu ya vito hivyo viwili kama vile sonara anavyochonga muhuri. Kisha uvitie vito hivyo katika vijalizo vya dhahabu,
bi the werk of a grauere, and bi the peyntyng of a man that ourneth with gemmes thou schalt graue tho stoonys, with the names of the sones of Israel; and thou schalt enclose and cumpasse in gold.
12 na uvifungie juu ya vipande vya mabega ya kisibau yawe kama vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli. Aroni atavaa majina hayo mabegani mwake kama kumbukumbu mbele za Bwana.
And thou schalt sette tho stoonus in euer either side of the cloth on the schuldris, a memorial to the sones of Israel; and Aaron schal bere the names of hem bifor the Lord on euer either schuldre, for remembryng.
13 Tengeneza vijalizo vya dhahabu
And thou schalt make hookis of gold,
14 na mikufu miwili ya dhahabu safi iliyosokotwa kama kamba, na uifunge mikufu hiyo kwenye vijalizo.
and twey litil chaynes of clenneste gold, cleuynge to hem silf togidere, whiche litil chaynes thou schalt sette in the hookis.
15 “Fanyiza kifuko cha kifuani kwa ajili ya kufanya maamuzi, kazi ya fundi stadi. Kitengeneze kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
Also thou schalt make the racional of doom by werk of dyuerse colours, bi the weuyng of the cloth on the schuldre, of gold, iacynt, and purpur, of `reed silk twies died, and of bijs foldid ayen.
16 Kitakuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, na kikunjwe mara mbili.
It schal be foure cornerid, and double; it schal haue the mesure of a pawme of the hond, as wel in lengthe, as in breede.
17 Kisha weka safu nne za vito vya thamani juu yake. Safu ya kwanza itakuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
And thou schalt sette ther ynne foure ordris of stoonys; in the firste ordre schal be the stoon sardius, and topazyus, and smaragdus;
18 katika safu ya pili itakuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
in the secunde ordre schal be charbuncle, safir, and iaspis; in the thridde ordre schal be ligurie,
19 safu ya tatu itakuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
achates, and ametiste;
20 na safu ya nne itakuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Yote yatiwe kwenye vijalizo vya dhahabu.
in the fourthe ordre schal be crisolitus, onochyn, and berille; tho schulen be closid in gold, bi her ordris,
21 Patakuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kwa jina mojawapo la wana wa Israeli, kila kimoja kichorwe kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
and schulen haue the names of the sones of Israel: tho schulen be graven with twelue names; al stonus bi hem silf, with the names of the sones `of Israel bi hem silf, bi twelue lynagis.
22 “Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani, tengeneza mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
Thou schalt make in the racional chaynes cleuynge to hem silf togidere of pureste gold,
23 Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili yake, uzifungie kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
and thou schalt make twei goldun ryngis, whiche thou schalt sette in euer either hiynesse of racional.
24 Funga ile mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete zilizo katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
And thou schalt ioyne the goldun chaynes with the ryngis that ben in the brynkis therof,
25 nazo zile ncha nyingine za mkufu zifunge kwenye vile vijalizo viwili, na uzishikamanishe na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
and thou schalt couple the `last thingis of tho chaynes to twey hookis in euer either side of the `cloth on the schuldur, that biholdith the racional.
26 Tengeneza pete mbili za dhahabu, uzishikamanishe kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
And thou schalt make twei goldun ryngis, whiche thou schalt sette in the hiynesses of the racional, and in the hemmes of the cloth on the schuldur, that ben euene ayens, and biholden the lattere thingis therof.
27 Tengeneza pete nyingine mbili za dhahabu, na uzishikamanishe sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
Also and thou schalt make tweyne othere goldun ryngis, that schulen be set in euer either side of the clooth on the schuldur bynethe, that biholdith ayens the face of the lowere ioynyng, that it may be set couenabli with the `cloth on the schuldre.
28 Pete za kifuko cha kifuani zitafungwa kwenye pete zile za kisibau kwa kamba ya buluu, ziunganishwe na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau.
And the racional be boundun bi hise ryngis with the ryngis of the `cloth on the schuldre, with a lace of iacynt, that the ioyning maad craftili dwelle, and that the racional and `cloth on the schuldre moun not be departid ech fro other.
29 “Wakati wowote Aroni aingiapo Mahali Patakatifu, atakuwa na yale majina ya wana wa Israeli moyoni mwake juu ya kile kifuko cha kifuani cha uamuzi kama kumbukumbu ya kudumu mbele za Bwana.
And Aaron schal bere the names of the sones of Israel in the racional of doom on his brest, whanne he entrith in to the seyntuarie, a memorial bifor the Lord with outen ende.
30 Pia weka Urimu na Thumimu ndani ya kifuko cha kifuani, yawe juu ya moyo wa Aroni kila mara aingiapo mbele za Bwana. Kwa hiyo siku zote Aroni atakuwa na uwezo kufanya maamuzi kwa ajili ya wana wa Israeli mbele za Bwana.
Forsothe thou schalt sette in the racional of doom, techyng, and treuthe, whiche schulen be in the brest of Aaron, whanne he entrith bifor the Lord, and he schal bere the doom of the sones of Israel in his brest in the siyt of the Lord euere.
31 “Shona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu,
And thou schalt make the coote of the `cloth on the schuldre al of iacynt,
32 na katikati uweke nafasi ya kuingizia kichwa. Kutakuwa na utepe uliofumwa, unaofanana na ukosi kuizunguka nafasi hiyo, ili isichanike.
in whos myddil aboue schal be an hood, and a wouun hemme `bi cumpas therof, as it is wont to be don in the hemmes of clothis, lest it be brokun liytli.
33 Tengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu kuzunguka pindo la hilo joho, na uweke pia vikengele vya dhahabu kati ya hayo makomamanga.
Forsothe bynethe at the feet of the same coote, bi cumpas, thou schalt make as `piyn applis, of iacynt, and purpur, of `reed selk twies died, and of biis foldid ayen; while smale bellis ben medlid in the myddis,
34 Hivyo vikengele vya dhahabu na makomamanga vitapishana kuzunguka upindo wa joho lile.
so that a litil `belle of gold be and a `piyn appil, and eft another litel belle of gold and a `pyn appil.
35 Ni lazima Aroni alivae anapofanya huduma. Sauti ya hivyo vikengele itasikika anapoingia na kutoka Mahali Patakatifu mbele za Bwana, ili asije akafa.
And Aaron schal be clothid with that coote in the office of seruyce, that sown be herd, whanne he entrith in to the seyntuarie, and goith out, in the siyt of the Lord; and that he die not.
36 “Tengeneza bamba la dhahabu safi na uchore juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
And thou schalt make a plate of pureste gold, in which thou schalt graue bi the werk of a grauere, the holi to the Lord.
37 Lifunge hilo bamba kwa kamba ya buluu kwenye kilemba, nalo ni lazima liwe mbele ya kilemba.
And thou schalt bynde that plate with a lace of iacynt, and it schal be on the mytre,
38 Aroni alivae bamba hilo kwenye paji la uso wake, naye atachukua hatia kuhusu sadaka takatifu za Waisraeli wanazoweka wakfu, sadaka za aina yoyote. Litakuwa kwenye paji la uso wa Aroni daima ili zikubalike kwa Bwana.
and schal neiye the forheed of the bischop. And Aaron schal bere the wickidnessis of hem whiche the sones of Israel `offeriden, and halewiden in alle her yiftis and fre yiftis; forsothe the plate schal euere be in `his forhed, that the Lord be plesid to him.
39 “Fuma koti la kitani safi na ufanye kilemba cha kitani safi. Mshipi uwe ni kazi ya mtarizi.
And thou schalt bynde the coot of biis, and the myter of bijs, and thou schalt make also a girdil, `bi werk of broiderye.
40 Watengenezee wana wa Aroni makoti, mishipi na kofia, ili kuwapa ukuu na heshima.
Forsothe thou schalt make redi to `the sones of Aaron linnun cootis, and girdlis, and mytris, in to glorie and fairnesse.
41 Baada ya kumvika Aroni ndugu yako pamoja na wanawe nguo hizi, watie mafuta na kuwabariki. Waweke wakfu ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
And thou schalt clothe Aaron, thi brother, with alle these, and hise sones with hym. And thou schalt sacre the hondis of alle; and thou schalt halewe hem, that thei be set in preesthood to me.
42 “Watengenezee nguo za ndani za kitani zitakazofunika mwili, kutoka kiunoni hadi mapajani.
Also thou schalt make lynnun brechis, that thei hile the fleisch of her filthe fro the reynes `til to the hipis.
43 Aroni na wanawe ni lazima wavae haya kila wanapoingia katika Hema la Kukutania au wanaposogelea madhabahu wakati wa kutoa huduma katika Mahali Patakatifu, ili wasije wakafanya kosa wakafa. “Haya yawe maagizo ya kudumu kwa Aroni na vizazi vyake.
And Aaron and hise sones schulen vse tho, whanne thei schulen entre in to the tabernacle of witnessyng, ether whanne thei neiyen to the auter, that thei mynystren in the seyntuarie, lest thei ben gilti of wickidnesse, and dien; it schal be a lawful thing euerlastynge to Aaron, and to his seed after hym.

< Kutoka 28 >