< Kutoka 28 >
1 “Mtwae Aroni ndugu yako aliyeletwa kwako kutoka miongoni mwa Waisraeli, pamoja na wanawe Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
Call to yourself Aaron your brother and his sons—Nadab, Abihu, Eleazar, and Ithamar—from among the Israelites so that they may serve me as priests.
2 Mshonee Aroni ndugu yako mavazi matakatifu ili yampe ukuu na heshima.
You must make for Aaron, your brother, garments that are set apart to me. These garments will be for his honor and splendor.
3 Waambie mafundi stadi wote niliowapa hekima katika shughuli hiyo wamtengenezee Aroni mavazi hayo, ili awekwe wakfu, anitumikie katika kazi ya ukuhani.
You must speak to all people who are wise in heart, those whom I have filled with the spirit of wisdom, so that they may make Aaron's garments to set him apart to serve me as my priest.
4 Haya ndiyo mavazi watakayoshona: kifuko cha kifuani, kisibau, kanzu, joho lililorembwa, kilemba na mshipi. Mavazi haya yatashonwa kwa ajili ya ndugu yako Aroni na wanawe ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
The garments that they must make are a breastpiece, an ephod, a robe, a coat of woven work, a turban, and a sash. They must make these garments that are set them apart to me. They will be for your brother Aaron and his sons so that they may serve me as priests.
5 Waambie watumie dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani safi.
Craftsmen must use fine linen that is gold, blue, purple, and scarlet.
6 “Tengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa, kazi ya fundi stadi.
They must make the ephod of gold, of blue, purple, and scarlet wool, and of fine-twined linen. It must be the work of a skillful craftsman.
7 Kitakuwa na vipande viwili vya mabegani vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kufungia kisibau.
It must have two shoulder pieces attached to its two upper corners.
8 Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi utafanana nacho: utakuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao utengenezwe kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri.
Its finely-woven waistband must be like the ephod; it must be made of one piece with the ephod, made of fine twined linen that is gold, blue, purple, and scarlet.
9 “Chukua vito viwili vya shohamu, na uchore juu yake majina ya wana wa Israeli
You must take two onyx stones and engrave on them the names of Israel's twelve sons.
10 kufuatana na walivyozaliwa: majina sita katika kito kimoja, na mengine sita katika kito kingine.
Six of their names must be on one stone, and six names must be on the other stone, in order of the sons' birth.
11 Yachore majina ya wana wa Israeli juu ya vito hivyo viwili kama vile sonara anavyochonga muhuri. Kisha uvitie vito hivyo katika vijalizo vya dhahabu,
With the work of an engraver in stone, like the engraving on a signet, you must engrave the two stones with the names of Israel's twelve sons. You must mount the stones in settings of gold.
12 na uvifungie juu ya vipande vya mabega ya kisibau yawe kama vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli. Aroni atavaa majina hayo mabegani mwake kama kumbukumbu mbele za Bwana.
You must put the two stones on the shoulder pieces of the ephod, to be stones to remind Yahweh of Israel's sons. Aaron will carry their names before Yahweh on his two shoulders as a reminder to him.
13 Tengeneza vijalizo vya dhahabu
You must make settings of gold
14 na mikufu miwili ya dhahabu safi iliyosokotwa kama kamba, na uifunge mikufu hiyo kwenye vijalizo.
and two braided chains of pure gold like cords, and you must attach the chains to the settings.
15 “Fanyiza kifuko cha kifuani kwa ajili ya kufanya maamuzi, kazi ya fundi stadi. Kitengeneze kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
You must make a breastpiece for decision making, the work of a skillful workman, fashioned like the ephod. Make it of gold, of blue, purple, and scarlet wool, and of fine linen.
16 Kitakuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, na kikunjwe mara mbili.
It is to be square. You must fold the breastpiece double. It must be one span long and one span wide.
17 Kisha weka safu nne za vito vya thamani juu yake. Safu ya kwanza itakuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
You must place in it four rows of precious stones. The first row must have a ruby, a topaz, and a garnet.
18 katika safu ya pili itakuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
The second row must have an emerald, a sapphire, and a diamond.
19 safu ya tatu itakuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
The third row must have a jacinth, an agate, and an amethyst.
20 na safu ya nne itakuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Yote yatiwe kwenye vijalizo vya dhahabu.
The fourth row must have a beryl, and an onyx, and a jasper. They must be mounted in gold settings.
21 Patakuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kwa jina mojawapo la wana wa Israeli, kila kimoja kichorwe kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
The stones must be arranged by the names of Israel's twelve sons, each in order by name. They must be like the engraving on a signet ring, each name standing for one of the twelve tribes.
22 “Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani, tengeneza mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
You must make on the breastpiece chains like cords, braided work of pure gold.
23 Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili yake, uzifungie kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
You must make two rings of gold for the breastpiece and must attach them to the two ends of the breastpiece.
24 Funga ile mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete zilizo katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
You must attach the two golden chains to the two corners of the breastpiece.
25 nazo zile ncha nyingine za mkufu zifunge kwenye vile vijalizo viwili, na uzishikamanishe na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
You must attach the other ends of the two braided chains to the two settings. Then you must attach those to the shoulder pieces of the ephod at its front.
26 Tengeneza pete mbili za dhahabu, uzishikamanishe kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
You must make two rings of gold, and you must put them on the other two corners of the breastpiece, on the edge next to the inner border.
27 Tengeneza pete nyingine mbili za dhahabu, na uzishikamanishe sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
You must make two more gold rings, and you must attach them to the bottom of the two shoulder pieces of the front of the ephod, close to its seam above the finely-woven waistband of the ephod.
28 Pete za kifuko cha kifuani zitafungwa kwenye pete zile za kisibau kwa kamba ya buluu, ziunganishwe na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau.
They must tie the breastpiece by its rings to the ephod's rings with a blue cord, so that it might be attached just above the ephod's woven waistband. This is so that the breastpiece might not become unattached from the ephod.
29 “Wakati wowote Aroni aingiapo Mahali Patakatifu, atakuwa na yale majina ya wana wa Israeli moyoni mwake juu ya kile kifuko cha kifuani cha uamuzi kama kumbukumbu ya kudumu mbele za Bwana.
When Aaron goes into the holy place, he must carry the names of the people of Israel over his heart in the breastpiece for decision making, as a continuing memorial before Yahweh.
30 Pia weka Urimu na Thumimu ndani ya kifuko cha kifuani, yawe juu ya moyo wa Aroni kila mara aingiapo mbele za Bwana. Kwa hiyo siku zote Aroni atakuwa na uwezo kufanya maamuzi kwa ajili ya wana wa Israeli mbele za Bwana.
You are to put the Urim and the Thummim in the breastpiece for decision making, so they may be over Aaron's heart when he goes in before Yahweh. Thus Aaron will always carry the means for making decisions for the people of Israel over his heart before Yahweh.
31 “Shona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu,
You will make the robe of the ephod entirely of blue fabric.
32 na katikati uweke nafasi ya kuingizia kichwa. Kutakuwa na utepe uliofumwa, unaofanana na ukosi kuizunguka nafasi hiyo, ili isichanike.
It must have an opening for the head in the middle. The opening must have a woven edge round about so that it does not tear. This must be the work of a weaver.
33 Tengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu kuzunguka pindo la hilo joho, na uweke pia vikengele vya dhahabu kati ya hayo makomamanga.
On the bottom hem, you must make pomegranates of blue, purple, and scarlet yarn all around. Gold bells must be between them all around.
34 Hivyo vikengele vya dhahabu na makomamanga vitapishana kuzunguka upindo wa joho lile.
There must be a golden bell and a pomegranate, a golden bell and a pomegranate—and so on—all around the hem of the robe.
35 Ni lazima Aroni alivae anapofanya huduma. Sauti ya hivyo vikengele itasikika anapoingia na kutoka Mahali Patakatifu mbele za Bwana, ili asije akafa.
The robe is to be on Aaron when he serves, so that its sound can be heard when he goes into the holy place before Yahweh and when he leaves. This is so that he does not die.
36 “Tengeneza bamba la dhahabu safi na uchore juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
You must make a plate of pure gold and engrave on it, like the engraving on a signet, “Holy to Yahweh.”
37 Lifunge hilo bamba kwa kamba ya buluu kwenye kilemba, nalo ni lazima liwe mbele ya kilemba.
You must attach this plate by a blue cord to the front of the turban.
38 Aroni alivae bamba hilo kwenye paji la uso wake, naye atachukua hatia kuhusu sadaka takatifu za Waisraeli wanazoweka wakfu, sadaka za aina yoyote. Litakuwa kwenye paji la uso wa Aroni daima ili zikubalike kwa Bwana.
It must be on Aaron's forehead; he must always bear any guilt that might attach to the offering of the holy gifts that the Israelites set apart to Yahweh. The turban must be always on his forehead so that Yahweh may accept their gifts.
39 “Fuma koti la kitani safi na ufanye kilemba cha kitani safi. Mshipi uwe ni kazi ya mtarizi.
You must make the coat with fine linen, and you must make a turban of fine linen. You must also make a sash, the work of an embroiderer.
40 Watengenezee wana wa Aroni makoti, mishipi na kofia, ili kuwapa ukuu na heshima.
For Aaron's sons you must make coats, sashes, and headbands for their honor and splendor.
41 Baada ya kumvika Aroni ndugu yako pamoja na wanawe nguo hizi, watie mafuta na kuwabariki. Waweke wakfu ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
You must clothe Aaron your brother, and his sons with him. You must anoint them, ordain them, and set them apart to me, so that they may serve me as priests.
42 “Watengenezee nguo za ndani za kitani zitakazofunika mwili, kutoka kiunoni hadi mapajani.
You must make for them linen undergarments to cover their naked flesh, that will cover them from the waist to the thighs.
43 Aroni na wanawe ni lazima wavae haya kila wanapoingia katika Hema la Kukutania au wanaposogelea madhabahu wakati wa kutoa huduma katika Mahali Patakatifu, ili wasije wakafanya kosa wakafa. “Haya yawe maagizo ya kudumu kwa Aroni na vizazi vyake.
Aaron and his sons must wear these garments when they enter the tent of meeting or when they approach the altar to serve in the holy place. They must do this so they would not be guilty or else they would die. This is a permanent law for Aaron and his descendants after him.