< Kutoka 28 >

1 “Mtwae Aroni ndugu yako aliyeletwa kwako kutoka miongoni mwa Waisraeli, pamoja na wanawe Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
And you bring near to yourself Aaron brother your and sons his with him from among [the] people of Israel to serve as priest he to me Aaron Nadab and Abihu Eleazar and Ithamar [the] sons of Aaron.
2 Mshonee Aroni ndugu yako mavazi matakatifu ili yampe ukuu na heshima.
And you will make garments of holiness for Aaron brother your for glory and for beauty.
3 Waambie mafundi stadi wote niliowapa hekima katika shughuli hiyo wamtengenezee Aroni mavazi hayo, ili awekwe wakfu, anitumikie katika kazi ya ukuhani.
And you you will speak to all [people] skillful of heart which I have filled it a spirit of wisdom and they will make [the] garments of Aaron to consecrate him to serve as priest he to me.
4 Haya ndiyo mavazi watakayoshona: kifuko cha kifuani, kisibau, kanzu, joho lililorembwa, kilemba na mshipi. Mavazi haya yatashonwa kwa ajili ya ndugu yako Aroni na wanawe ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
And these [are] the garments which they will make a breastpiece and an ephod and a robe and a tunic of checkered work a turban and a sash and they will make garments of holiness for Aaron brother your and for sons his to serve as priest he to me.
5 Waambie watumie dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani safi.
And they they will take the gold and the violet stuff and the purple and [the] scarlet stuff of the scarlet and the fine linen.
6 “Tengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa, kazi ya fundi stadi.
And they will make the ephod gold violet stuff and purple scarlet stuff of scarlet and fine linen twisted [the] work of a skillful worker.
7 Kitakuwa na vipande viwili vya mabegani vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kufungia kisibau.
Two shoulder-pieces joined it will be[long] to it to [the] two ends its and it will be joined together.
8 Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi utafanana nacho: utakuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao utengenezwe kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri.
And [the] girdle of ephod its which [will be] on it [will be] like workmanship its from it it will be gold violet stuff and purple and scarlet stuff of scarlet and fine linen twisted.
9 “Chukua vito viwili vya shohamu, na uchore juu yake majina ya wana wa Israeli
And you will take two stones of onyx and you will engrave on them [the] names of [the] sons of Israel.
10 kufuatana na walivyozaliwa: majina sita katika kito kimoja, na mengine sita katika kito kingine.
Six of names their [will be] on the stone one and [the] names of the six which remain over [will be] on the stone second according to genealogies their.
11 Yachore majina ya wana wa Israeli juu ya vito hivyo viwili kama vile sonara anavyochonga muhuri. Kisha uvitie vito hivyo katika vijalizo vya dhahabu,
[the] work of An engraver of stone [the] engravings of a seal you will engrave [the] two the stones on [the] names of [the] sons of Israel surrounded filigree settings of gold you will make them.
12 na uvifungie juu ya vipande vya mabega ya kisibau yawe kama vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli. Aroni atavaa majina hayo mabegani mwake kama kumbukumbu mbele za Bwana.
And you will put [the] two the stones on [the] shoulder-pieces of the ephod stones of reminder for [the] sons of Israel and he will bear Aaron names their before Yahweh on [the] two shoulder-pieces his to a reminder.
13 Tengeneza vijalizo vya dhahabu
And you will make filigree settings of gold.
14 na mikufu miwili ya dhahabu safi iliyosokotwa kama kamba, na uifunge mikufu hiyo kwenye vijalizo.
And two chains of gold pure twisted cords you will make them a work of cordage and you will put [the] chains of the cords on the filigree settings.
15 “Fanyiza kifuko cha kifuani kwa ajili ya kufanya maamuzi, kazi ya fundi stadi. Kitengeneze kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
And you will make a breastpiece of judgment [the] work of a skillful worker like [the] work of [the] ephod you will make it gold violet stuff and purple and scarlet stuff of scarlet and fine linen twisted you will make it.
16 Kitakuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, na kikunjwe mara mbili.
Square it will be folded double [will be] a span length its and [will be] a span breadth its.
17 Kisha weka safu nne za vito vya thamani juu yake. Safu ya kwanza itakuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
And you will fill in it a setting of stone[s] four rows stone [will be] a row of a ruby a topaz and a beryl the row one.
18 katika safu ya pili itakuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
And the row second [will be] a turquoise a sapphire and an emerald.
19 safu ya tatu itakuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
And the row third [will be] a jacinth an agate and an amethyst.
20 na safu ya nne itakuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Yote yatiwe kwenye vijalizo vya dhahabu.
And the row fourth [will be] a chrysolite and an onyx and a jasper set gold they will be in settings their.
21 Patakuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kwa jina mojawapo la wana wa Israeli, kila kimoja kichorwe kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
And the stones they will be on [the] names of [the] sons of Israel two [plus] ten on names their [the] engravings of a seal each one on name its they will be for [the] two [plus] ten tribe[s].
22 “Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani, tengeneza mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
And you will make on the breastpiece chains of twisting a work of cordage gold pure.
23 Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili yake, uzifungie kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
And you will make on the breastpiece two rings of gold and you will put [the] two the rings on [the] two [the] ends of the breastpiece.
24 Funga ile mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete zilizo katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
And you will put [the] two [the] cords of gold on [the] two the rings to [the] ends of the breastpiece.
25 nazo zile ncha nyingine za mkufu zifunge kwenye vile vijalizo viwili, na uzishikamanishe na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
And [the] two [the] ends of [the] two the cords you will put on [the] two the filigree settings and you will put [them] on [the] shoulder-pieces of the ephod to [the] front of face its.
26 Tengeneza pete mbili za dhahabu, uzishikamanishe kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
And you will make two rings of gold and you will put them on [the] two [the] ends of the breastpiece on edge its which [is] to [the] side of the ephod [the] inside towards.
27 Tengeneza pete nyingine mbili za dhahabu, na uzishikamanishe sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
And you will make two rings of gold and you will put them on [the] two [the] shoulder-pieces of the ephod from to downwards from in front of face its close to joining its from above [the] girdle of the ephod.
28 Pete za kifuko cha kifuani zitafungwa kwenye pete zile za kisibau kwa kamba ya buluu, ziunganishwe na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau.
So they may bind the breastpiece (from rings its *Q(K)*) to [the] rings of the ephod with a cord of violet stuff to be on [the] girdle of the ephod and not it will be displaced the breastpiece from on the ephod.
29 “Wakati wowote Aroni aingiapo Mahali Patakatifu, atakuwa na yale majina ya wana wa Israeli moyoni mwake juu ya kile kifuko cha kifuani cha uamuzi kama kumbukumbu ya kudumu mbele za Bwana.
And he will bear Aaron [the] names of [the] sons of Israel on [the] breastpiece of judgment over heart his when goes he into the holy place to a memorial before Yahweh continually.
30 Pia weka Urimu na Thumimu ndani ya kifuko cha kifuani, yawe juu ya moyo wa Aroni kila mara aingiapo mbele za Bwana. Kwa hiyo siku zote Aroni atakuwa na uwezo kufanya maamuzi kwa ajili ya wana wa Israeli mbele za Bwana.
And you will put into [the] breastpiece of judgment the Urim and the Thummim and they will be over [the] heart of Aaron when goes he before Yahweh and he will bear Aaron [the] judgment of [the] people of Israel over heart his before Yahweh continually.
31 “Shona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu,
And you will make [the] robe of the ephod an entirety of violet stuff.
32 na katikati uweke nafasi ya kuingizia kichwa. Kutakuwa na utepe uliofumwa, unaofanana na ukosi kuizunguka nafasi hiyo, ili isichanike.
And it will be [the] opening of top its in [the] middle of it an edge it will be[long] to opening its all around [the] work a weaver like [the] opening of a collar it will be[long] to it not it will be torn.
33 Tengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu kuzunguka pindo la hilo joho, na uweke pia vikengele vya dhahabu kati ya hayo makomamanga.
And you will make on skirt its pomegranates of violet stuff and purple and scarlet stuff of scarlet on skirt its all around and bells of gold [will be] in between them all around.
34 Hivyo vikengele vya dhahabu na makomamanga vitapishana kuzunguka upindo wa joho lile.
A bell of gold and a pomegranate a bell of gold and a pomegranate [will be] on [the] skirts of the robe all around.
35 Ni lazima Aroni alivae anapofanya huduma. Sauti ya hivyo vikengele itasikika anapoingia na kutoka Mahali Patakatifu mbele za Bwana, ili asije akafa.
And it will be on Aaron to serve and it will be heard sound its when goes he into the holy place before Yahweh and when comes out he and not he will die.
36 “Tengeneza bamba la dhahabu safi na uchore juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
And you will make a plate of gold pure and you will engrave on it [the] engravings of a seal holiness to Yahweh.
37 Lifunge hilo bamba kwa kamba ya buluu kwenye kilemba, nalo ni lazima liwe mbele ya kilemba.
And you will put it on a cord of violet stuff and it will be on the turban to [the] front of [the] face of the turban it will be.
38 Aroni alivae bamba hilo kwenye paji la uso wake, naye atachukua hatia kuhusu sadaka takatifu za Waisraeli wanazoweka wakfu, sadaka za aina yoyote. Litakuwa kwenye paji la uso wa Aroni daima ili zikubalike kwa Bwana.
And it will be on [the] forehead of Aaron and he will bear Aaron [the] guilt of the holy things which they will consecrate [the] people of Israel to all [the] gifts of holiness their and it will be on forehead his continually for acceptance to them before Yahweh.
39 “Fuma koti la kitani safi na ufanye kilemba cha kitani safi. Mshipi uwe ni kazi ya mtarizi.
And you will weave the tunic fine linen and you will make a turban of fine linen and a sash you will make [the] work of a worker in colors.
40 Watengenezee wana wa Aroni makoti, mishipi na kofia, ili kuwapa ukuu na heshima.
And for [the] sons of Aaron you will make tunics and you will make for them sashes and headdresses you will make for them for glory and for beauty.
41 Baada ya kumvika Aroni ndugu yako pamoja na wanawe nguo hizi, watie mafuta na kuwabariki. Waweke wakfu ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
And you will clothe them Aaron brother your and sons his with him and you will anoint them and you will fill hand their and you will consecrate them and they will serve as priests me.
42 “Watengenezee nguo za ndani za kitani zitakazofunika mwili, kutoka kiunoni hadi mapajani.
And make for them undergarments of linen to cover [the] flesh of nakedness from [the] hips and to [the] thighs they will be.
43 Aroni na wanawe ni lazima wavae haya kila wanapoingia katika Hema la Kukutania au wanaposogelea madhabahu wakati wa kutoa huduma katika Mahali Patakatifu, ili wasije wakafanya kosa wakafa. “Haya yawe maagizo ya kudumu kwa Aroni na vizazi vyake.
And they will be on Aaron and on sons his when go they - into [the] tent of meeting or when draw near they to the altar to serve in the holy place and not they will bear guilt and they will die [it will be] a statute of perpetuity for him and for offspring his after him.

< Kutoka 28 >