< Kutoka 28 >
1 “Mtwae Aroni ndugu yako aliyeletwa kwako kutoka miongoni mwa Waisraeli, pamoja na wanawe Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
And thou shalt take thee Aaron thy brother, and his sons with him, from among the children of Israel, that he may serve me as priest — Aaron, Nadab and Abihu, Eleazar and Ithamar, Aaron's sons.
2 Mshonee Aroni ndugu yako mavazi matakatifu ili yampe ukuu na heshima.
And thou shalt make holy garments for Aaron thy brother, for glory and for ornament.
3 Waambie mafundi stadi wote niliowapa hekima katika shughuli hiyo wamtengenezee Aroni mavazi hayo, ili awekwe wakfu, anitumikie katika kazi ya ukuhani.
And thou shalt speak with all [that are] wise-hearted, whom I have filled with the spirit of wisdom, that they may make Aaron's garments to hallow him, that he may serve me as priest.
4 Haya ndiyo mavazi watakayoshona: kifuko cha kifuani, kisibau, kanzu, joho lililorembwa, kilemba na mshipi. Mavazi haya yatashonwa kwa ajili ya ndugu yako Aroni na wanawe ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
And these are the garments which they shall make: a breastplate, and an ephod, and a cloak, and a checkered vest, a turban, and a girdle; and they shall make holy garments for Aaron thy brother, and his sons, that he may serve me as priest.
5 Waambie watumie dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani safi.
And they shall take gold, and blue, and purple, and scarlet, and twined byssus,
6 “Tengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa, kazi ya fundi stadi.
and shall make the ephod of gold, blue, and purple, scarlet and twined byssus, of artistic work.
7 Kitakuwa na vipande viwili vya mabegani vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kufungia kisibau.
It shall have two shoulder-pieces joined at the two ends thereof, where it is joined together.
8 Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi utafanana nacho: utakuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao utengenezwe kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri.
And the girdle of the ephod, which is upon it, shall be of the same, according to its work of gold, blue, and purple, and scarlet and twined byssus.
9 “Chukua vito viwili vya shohamu, na uchore juu yake majina ya wana wa Israeli
And thou shalt take two onyx stones, and engrave on them the names of the children of Israel:
10 kufuatana na walivyozaliwa: majina sita katika kito kimoja, na mengine sita katika kito kingine.
six of their names on the one stone, and the six names of the rest on the other stone, according to their birth.
11 Yachore majina ya wana wa Israeli juu ya vito hivyo viwili kama vile sonara anavyochonga muhuri. Kisha uvitie vito hivyo katika vijalizo vya dhahabu,
According to the work of an engraver in stone, as the engravings of a seal, shalt thou engrave the two stones with the names of the sons of Israel; surrounded by enclosures of gold shalt thou make them.
12 na uvifungie juu ya vipande vya mabega ya kisibau yawe kama vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli. Aroni atavaa majina hayo mabegani mwake kama kumbukumbu mbele za Bwana.
And thou shalt put the two stones upon the shoulder-pieces of the ephod [as] stones of memorial for the children of Israel; and Aaron shall bear their names before Jehovah upon his two shoulders for a memorial.
13 Tengeneza vijalizo vya dhahabu
And thou shalt make enclosures of gold;
14 na mikufu miwili ya dhahabu safi iliyosokotwa kama kamba, na uifunge mikufu hiyo kwenye vijalizo.
and two chains of pure gold; of laced work shalt thou make them, of wreathen work, and fasten the wreathen chains to the enclosures.
15 “Fanyiza kifuko cha kifuani kwa ajili ya kufanya maamuzi, kazi ya fundi stadi. Kitengeneze kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
And thou shalt make the breastplate of judgment of artistic work, like the work of the ephod thou shalt make it; of gold, blue, and purple, and scarlet, and twined byssus shalt thou make it.
16 Kitakuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, na kikunjwe mara mbili.
Square shall it be, doubled; a span the length thereof, and a span the breadth thereof.
17 Kisha weka safu nne za vito vya thamani juu yake. Safu ya kwanza itakuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
And thou shalt set in it settings of stones — four rows of stones: [one] row, a sardoin, a topaz, and an emerald — the first row;
18 katika safu ya pili itakuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
and the second row, a carbuncle, a sapphire, and a diamond;
19 safu ya tatu itakuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
and the third row, an opal, an agate, and an amethyst;
20 na safu ya nne itakuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Yote yatiwe kwenye vijalizo vya dhahabu.
and the fourth row, a chrysolite, and an onyx, and a jasper; enclosed in gold shall they be in their settings.
21 Patakuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kwa jina mojawapo la wana wa Israeli, kila kimoja kichorwe kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
And the stones shall be according to the names of the children of Israel, twelve, according to their names, engraved as a seal: every one according to his name shall they be for the twelve tribes.
22 “Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani, tengeneza mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
And thou shalt make on the breastplate chains of laced work, of wreathen work, of pure gold.
23 Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili yake, uzifungie kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
And thou shalt make on the breastplate two rings of gold, and shalt put the two rings on the two ends of the breastplate.
24 Funga ile mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete zilizo katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
And thou shalt put the two wreathen [cords] of gold in the two rings on the ends of the breastplate;
25 nazo zile ncha nyingine za mkufu zifunge kwenye vile vijalizo viwili, na uzishikamanishe na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
and the two ends of the two wreathen [cords] thou shalt fasten to the two enclosures, and shalt put [them] on the shoulder-pieces of the ephod, on the front thereof.
26 Tengeneza pete mbili za dhahabu, uzishikamanishe kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
And thou shalt make two rings of gold, and shalt put them on the two ends of the breastplate, on the border thereof, which faceth the ephod inwards.
27 Tengeneza pete nyingine mbili za dhahabu, na uzishikamanishe sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
And two rings of gold shalt thou make, and shalt put them upon the two shoulder-pieces of the ephod underneath, to the front thereof just by the coupling thereof, above the girdle of the ephod.
28 Pete za kifuko cha kifuani zitafungwa kwenye pete zile za kisibau kwa kamba ya buluu, ziunganishwe na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau.
And they shall bind the breastplate with its rings to the rings of the ephod with a lace of blue, that it may be above the girdle of the ephod, and that the breastplate be not loosed from the ephod.
29 “Wakati wowote Aroni aingiapo Mahali Patakatifu, atakuwa na yale majina ya wana wa Israeli moyoni mwake juu ya kile kifuko cha kifuani cha uamuzi kama kumbukumbu ya kudumu mbele za Bwana.
And Aaron shall bear the names of the children of Israel in the breastplate of judgment on his heart, when he goes in to the sanctuary, for a memorial before Jehovah continually.
30 Pia weka Urimu na Thumimu ndani ya kifuko cha kifuani, yawe juu ya moyo wa Aroni kila mara aingiapo mbele za Bwana. Kwa hiyo siku zote Aroni atakuwa na uwezo kufanya maamuzi kwa ajili ya wana wa Israeli mbele za Bwana.
And thou shalt put into the breastplate of judgment the Urim and the Thummim, that they may be upon Aaron's heart when he goeth in before Jehovah; and Aaron shall bear the judgment of the children of Israel upon his heart before Jehovah continually.
31 “Shona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu,
And thou shalt make the cloak of the ephod all of blue.
32 na katikati uweke nafasi ya kuingizia kichwa. Kutakuwa na utepe uliofumwa, unaofanana na ukosi kuizunguka nafasi hiyo, ili isichanike.
And its opening for the head shall be in the midst thereof; there shall be a binding of woven work at its opening round about; as the opening of a coat of mail, it shall be in it — it shall not rend.
33 Tengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu kuzunguka pindo la hilo joho, na uweke pia vikengele vya dhahabu kati ya hayo makomamanga.
And on the skirts thereof thou shalt make pomegranates of blue, and purple, and scarlet, round about the skirts thereof; and bells of gold between them round about:
34 Hivyo vikengele vya dhahabu na makomamanga vitapishana kuzunguka upindo wa joho lile.
a golden bell and a pomegranate, a golden bell and a pomegranate, in the skirts of the cloak round about.
35 Ni lazima Aroni alivae anapofanya huduma. Sauti ya hivyo vikengele itasikika anapoingia na kutoka Mahali Patakatifu mbele za Bwana, ili asije akafa.
And it shall be on Aaron for service; that his sound may be heard when he goeth into the sanctuary before Jehovah, and when he cometh out, that he may not die.
36 “Tengeneza bamba la dhahabu safi na uchore juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
And thou shalt make a thin plate of pure gold, and engrave on it, as the engravings of a seal, Holiness to Jehovah!
37 Lifunge hilo bamba kwa kamba ya buluu kwenye kilemba, nalo ni lazima liwe mbele ya kilemba.
And thou shalt put it on a lace of blue, and it shall be upon the turban — upon the front of the turban shall it be.
38 Aroni alivae bamba hilo kwenye paji la uso wake, naye atachukua hatia kuhusu sadaka takatifu za Waisraeli wanazoweka wakfu, sadaka za aina yoyote. Litakuwa kwenye paji la uso wa Aroni daima ili zikubalike kwa Bwana.
And it shall be upon Aaron's forehead, and Aaron shall bear the iniquity of the holy things, which the children of Israel shall hallow in all gifts of their holy things; and it shall be continually on his forehead, that they may be accepted before Jehovah.
39 “Fuma koti la kitani safi na ufanye kilemba cha kitani safi. Mshipi uwe ni kazi ya mtarizi.
And thou shalt weave the vest of byssus; and thou shalt make a turban of byssus; and thou shalt make a girdle of embroidery.
40 Watengenezee wana wa Aroni makoti, mishipi na kofia, ili kuwapa ukuu na heshima.
And for Aaron's sons thou shalt make vests; and thou shalt make for them girdles; and high caps shalt thou make for them, for glory and for ornament.
41 Baada ya kumvika Aroni ndugu yako pamoja na wanawe nguo hizi, watie mafuta na kuwabariki. Waweke wakfu ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
And thou shalt clothe with them Aaron thy brother, and his sons with him; and shalt anoint them, and consecrate them, and hallow them, that they may serve me as priests.
42 “Watengenezee nguo za ndani za kitani zitakazofunika mwili, kutoka kiunoni hadi mapajani.
And thou shalt make them linen trousers to cover the flesh of nakedness; from the loins even to the hips shall they reach.
43 Aroni na wanawe ni lazima wavae haya kila wanapoingia katika Hema la Kukutania au wanaposogelea madhabahu wakati wa kutoa huduma katika Mahali Patakatifu, ili wasije wakafanya kosa wakafa. “Haya yawe maagizo ya kudumu kwa Aroni na vizazi vyake.
And they shall be upon Aaron and his sons when they enter into the tent of meeting, or when they come near to the altar to serve in the sanctuary; that they may not bear iniquity and die — an everlasting statute for him and his seed after him.