< Kutoka 27 >
1 “Jenga madhabahu ya mbao za mti wa mshita, kimo chake kiwe dhiraa tatu; itakuwa mraba, urefu wake dhiraa tano, na upana wake dhiraa tano.
“Você deve fazer o altar de madeira de acácia, cinco côvados de comprimento e cinco côvados de largura. O altar deve ser quadrado. Sua altura deve ser de três côvados.
2 Tengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu ziwe zimeungana, na ufunike madhabahu kwa shaba.
Você fará seus chifres em seus quatro cantos. Seus chifres serão de uma só peça com ele. Você o cobrirá com bronze.
3 Tengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama, na vyombo vya kuchukulia moto.
Você fará suas panelas para tirar suas cinzas; e suas pás, suas bacias, seus ganchos de carne, e suas panelas de fogo. Você deve fazer todos os seus recipientes de bronze.
4 Kisha tengenezea hayo madhabahu wavu wa shaba, na utengeneze pete za shaba kwenye kila moja ya hizo pembe nne za huo wavu.
Você deve fazer uma grade para ele de rede de bronze. Na rede, você fará quatro anéis de bronze em seus quatro cantos.
5 Weka wavu huo chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu.
Debaixo do parapeito ao redor do altar, para que a rede possa chegar à metade do altar.
6 Tengeneza mipiko ya mti wa mshita kwa ajili ya madhabahu, na uifunike kwa shaba.
Você fará postes para o altar, postes de madeira de acácia, e os cobrirá com bronze.
7 Hiyo mipiko itaingizwa kwenye zile pete ili iwe pande mbili za madhabahu inapobebwa.
Seus mastros serão colocados nos anéis, e os mastros estarão nos dois lados do altar ao carregá-lo.
8 Tengeneza madhabahu yawe na uvungu ndani yake ukitumia mbao. Utaitengeneza sawasawa na vile ulivyoonyeshwa mlimani.
Você deve torná-lo oco com tábuas. Fá-lo-ão como lhe foi mostrado na montanha.
9 “Tengeneza ua kwa ajili ya Hema la Kukutania. Upande wa kusini utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja, na utakuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri,
“Você fará o pátio do tabernáculo: para o lado sul, haverá enforcamentos para o pátio de linho fino torcido de cem côvados de comprimento para um lado.
10 pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
Its os pilares serão vinte, e suas bases vinte, de bronze. Os ganchos dos pilares e seus filetes devem ser de prata.
11 Upande wa kaskazini utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja, nao utakuwa na mapazia, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
Da mesma forma, para o comprimento do lado norte, haverá penduras de cem côvados de comprimento, e seus pilares vinte, e suas bases vinte, de bronze; os ganchos dos pilares, e seus filetes, de prata.
12 “Upande wa magharibi wa ua utakuwa na upana wa dhiraa hamsini, nao utakuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi.
For a largura da quadra do lado oeste será de cinqüenta côvados; seus pilares dez, e suas bases dez.
13 Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, ua pia utakuwa na upana wa dhiraa hamsini.
a largura da quadra do lado leste será de cinqüenta côvados.
14 Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yatakuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
As pendurações para um lado do portão serão de quinze côvados; seus pilares três, e suas bases três.
15 Kutakuwepo tena na mapazia ya dhiraa kumi na tano kwa upande mwingine wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
Para o outro lado serão penduras de quinze côvados; suas colunas três, e suas bases três.
16 “Kuhusu ingilio la ua, weka pazia lenye urefu wa dhiraa ishirini la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo litashikiliwa na nguzo nne na vitako vinne.
Para a porta do pátio será uma tela de vinte côvados, de azul, e roxo, e escarlate, e linho fino torcido, o trabalho do bordador; seus pilares quatro, e suas bases quatro.
17 Nguzo zote zinazozunguka ua zitakuwa na tepe na kulabu za fedha, na vitako vya shaba.
Todos os pilares da quadra ao redor devem ser preenchidos com prata; seus ganchos de prata e suas soquetes de bronze.
18 Ua wa kukutania utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja na upana wa dhiraa hamsini, ukiwa na mapazia ya kitani yaliyosokotwa vizuri yenye urefu wa dhiraa tano kwenda juu na vitako vya shaba.
O comprimento da quadra deve ser de cem côvados, e a largura de cinqüenta por toda a largura, e a altura de cinco côvados, de linho fino torcido, e suas bases de bronze.
19 Vyombo vingine vyote vinavyotumika katika maskani kwa shughuli yoyote, pamoja na vigingi vyote na hata vile vya ua, vitakuwa vya shaba.
Todos os instrumentos do tabernáculo em todos os seus serviços, e todos os seus pinos, e todos os pinos da quadra, devem ser de bronze.
20 “Utawaamuru Waisraeli wakuletee mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa kwa ajili ya mwanga ili zile taa ziwake mfululizo.
“Você ordenará aos filhos de Israel, que lhe tragam azeite de oliva puro batido para a luz, para fazer com que uma lâmpada arda continuamente.
21 Katika Hema la Kukutania, nje ya pazia lililo mbele ya Sanduku la Ushuhuda, Aroni na wanawe watahakikisha kuwa taa hizo zinawaka kuanzia jioni mpaka asubuhi mbele za Bwana. Hili litakuwa agizo la milele miongoni mwa Waisraeli kwa vizazi vyote vijavyo.
Na Tenda da Reunião, fora do véu que está diante do pacto, Aarão e seus filhos a manterão em ordem de noite a manhã antes de Yahweh: será um estatuto para sempre através de suas gerações em nome dos filhos de Israel.