< Kutoka 27 >

1 “Jenga madhabahu ya mbao za mti wa mshita, kimo chake kiwe dhiraa tatu; itakuwa mraba, urefu wake dhiraa tano, na upana wake dhiraa tano.
Tu feras encore un autel de bois de sétim, qui aura cinq coudées en longueur et autant en largeur, c’est-à-dire carré, et trois coudées en hauteur.
2 Tengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu ziwe zimeungana, na ufunike madhabahu kwa shaba.
Mais les cornes en sortiront aux quatre angles; et tu le couvriras d’airain.
3 Tengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama, na vyombo vya kuchukulia moto.
Et tu feras à son usage des chaudières pour recevoir les cendres, des pincettes, des fourchettes et des brasiers; tu feras tous ces instruments en airain.
4 Kisha tengenezea hayo madhabahu wavu wa shaba, na utengeneze pete za shaba kwenye kila moja ya hizo pembe nne za huo wavu.
Tu feras encore une grille d’airain en forme de rets: à ses quatre angles seront des anneaux d’airain,
5 Weka wavu huo chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu.
Que tu mettras au-dessous du foyer de l’autel: et la grille viendra jusqu’au milieu de l’autel.
6 Tengeneza mipiko ya mti wa mshita kwa ajili ya madhabahu, na uifunike kwa shaba.
Tu feras aussi deux leviers d’autel de bois de sétim, que tu couvriras de lames d’airain:
7 Hiyo mipiko itaingizwa kwenye zile pete ili iwe pande mbili za madhabahu inapobebwa.
Et tu les passeras dans les anneaux; et ils seront des deux côtés de l’autel pour le porter.
8 Tengeneza madhabahu yawe na uvungu ndani yake ukitumia mbao. Utaitengeneza sawasawa na vile ulivyoonyeshwa mlimani.
Tu ne feras point l’autel solide, mais vide et creux au dedans, comme il t’a été montré sur la montagne.
9 “Tengeneza ua kwa ajili ya Hema la Kukutania. Upande wa kusini utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja, na utakuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri,
Tu feras aussi le parvis du tabernacle au côté austral duquel seront contre le midi des rideaux de fin lin retors: un seul côté tiendra cent coudées en longueur.
10 pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
Et tu y poseras vingt colonnes avec autant de soubassements d’airain, lesquelles auront leurs chapiteaux avec leurs ornements d’argent.
11 Upande wa kaskazini utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja, nao utakuwa na mapazia, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
De même aussi du côté de l’aquilon il y aura des rideaux de cent coudées de long, vingt colonnes et des soubassements d’airain de même nombre; leurs chapiteaux avec leurs ornements seront d’argent.
12 “Upande wa magharibi wa ua utakuwa na upana wa dhiraa hamsini, nao utakuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi.
Mais dans la largeur du parvis qui regarde l’occident il y aura dans l’espace de cinquante coudées des rideaux, dix colonnes et autant de soubassements.
13 Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, ua pia utakuwa na upana wa dhiraa hamsini.
De même, dans la largeur du parvis, laquelle regarde l’orient, il y aura cinquante coudées,
14 Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yatakuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
Dans lesquelles seront affectés à un côté des rideaux de quinze coudées, trois colonnes et autant de soubassements:
15 Kutakuwepo tena na mapazia ya dhiraa kumi na tano kwa upande mwingine wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
Et de l’autre côté seront des rideaux ayant quinze coudées, trois colonnes et autant de soubassements.
16 “Kuhusu ingilio la ua, weka pazia lenye urefu wa dhiraa ishirini la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo litashikiliwa na nguzo nne na vitako vinne.
Mais à l’entrée du parvis on fera un rideau de vingt coudées d’hyacinthe, de pourpre, d’écarlate deux fois teinte et d’un fin lin retors, en ouvrage de brodeur: cette entrée aura quatre colonnes et autant de soubassements.
17 Nguzo zote zinazozunguka ua zitakuwa na tepe na kulabu za fedha, na vitako vya shaba.
Toutes les colonnes du parvis seront revêtues tout autour de lames d’argent; elles auront des chapiteaux d’argent et des soubassements d’airain.
18 Ua wa kukutania utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja na upana wa dhiraa hamsini, ukiwa na mapazia ya kitani yaliyosokotwa vizuri yenye urefu wa dhiraa tano kwenda juu na vitako vya shaba.
En longueur le parvis aura cent coudées, en largeur cinquante; sa hauteur sera de cinq coudées; et il sera fait de fin lin retors, et il aura des soubassements d’airain.
19 Vyombo vingine vyote vinavyotumika katika maskani kwa shughuli yoyote, pamoja na vigingi vyote na hata vile vya ua, vitakuwa vya shaba.
Tous les vases du tabernacle destinés à tous les usages et à toutes les cérémonies, tant ses pieux que ceux du parvis, tu les feras d’airain.
20 “Utawaamuru Waisraeli wakuletee mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa kwa ajili ya mwanga ili zile taa ziwake mfululizo.
Ordonne aux enfants d’Israël qu’ils t’apportent de l’huile d’oliviers très pure, et pilée au mortier, afin qu’une lampe brûle toujours.
21 Katika Hema la Kukutania, nje ya pazia lililo mbele ya Sanduku la Ushuhuda, Aroni na wanawe watahakikisha kuwa taa hizo zinawaka kuanzia jioni mpaka asubuhi mbele za Bwana. Hili litakuwa agizo la milele miongoni mwa Waisraeli kwa vizazi vyote vijavyo.
Dans le tabernacle de témoignage en dehors du voile qui est suspendu devant le témoignage. Et Aaron et ses fils la placeront, afin qu’elle éclaire jusqu’au matin devant le Seigneur. Ce sera un culte perpétuel durant leurs successions parmi les enfants d’Israël.

< Kutoka 27 >