< Kutoka 27 >

1 “Jenga madhabahu ya mbao za mti wa mshita, kimo chake kiwe dhiraa tatu; itakuwa mraba, urefu wake dhiraa tano, na upana wake dhiraa tano.
“Tell them to make an altar from acacia wood. It is to be square, (7-1/2 feet/2.2 meters) on each side, and make it (4-1/2 feet/1.3 meters) high.
2 Tengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu ziwe zimeungana, na ufunike madhabahu kwa shaba.
[They] must make [a projection that looks like] a horn on each of the top corners. The projections must be carved from the same block of wood as the altar. [Tell them to] cover the whole altar with gold.
3 Tengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama, na vyombo vya kuchukulia moto.
[They must] make pans in which to put the [greasy] ashes [from the animal sacrifices]. Also [they must] make shovels for cleaning out the ashes, basins and forks for turning the meat as it cooks, and buckets for carrying hot coals/ashes. All of these things must be made from bronze.
4 Kisha tengenezea hayo madhabahu wavu wa shaba, na utengeneze pete za shaba kwenye kila moja ya hizo pembe nne za huo wavu.
Also [tell them to] make a bronze grating to hold the wood and burning coals. They must fasten to each of the corners of the altar a bronze ring for carrying the altar.
5 Weka wavu huo chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu.
[They must] put the grating under the rim that is around the altar. [They must] make it so that it is [inside the altar], halfway down.
6 Tengeneza mipiko ya mti wa mshita kwa ajili ya madhabahu, na uifunike kwa shaba.
For [carrying] the altar, [they must] make poles from acacia wood and cover them with bronze.
7 Hiyo mipiko itaingizwa kwenye zile pete ili iwe pande mbili za madhabahu inapobebwa.
[They must] put the poles through the rings on each side of the altar. The poles are for carrying the altar.
8 Tengeneza madhabahu yawe na uvungu ndani yake ukitumia mbao. Utaitengeneza sawasawa na vile ulivyoonyeshwa mlimani.
The altar will be like a box, made from boards [of acacia wood]. [They must] make it according to these instructions that I am giving you [here] on [this] mountain.”
9 “Tengeneza ua kwa ajili ya Hema la Kukutania. Upande wa kusini utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja, na utakuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri,
“Around the Sacred Tent there is to be a courtyard. To form the courtyard, [tell them to] make curtains of fine linen. On the south side, the curtain is to be (50 yards/44 meters) long.
10 pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
[To support/hang the curtain], [tell them to] make twenty bronze posts, and one bronze base for each post. To fasten the curtains to the posts, [they must] make silver hooks, and [metal] rods [covered with] silver [to fasten the curtains to the hooks].
11 Upande wa kaskazini utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja, nao utakuwa na mapazia, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
[They must] make the same kind of curtains for the north side of the courtyard.
12 “Upande wa magharibi wa ua utakuwa na upana wa dhiraa hamsini, nao utakuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi.
On the west side [of the courtyard] they must make a curtain (25 yards/22 meters) long. The curtains are to be supported by ten posts, with a base under [each] post.
13 Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, ua pia utakuwa na upana wa dhiraa hamsini.
On the east side, [where the entrance is], the courtyard must also be (25 yards/22 meters) wide.
14 Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yatakuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
[Tell them to] make a curtain (22-1/2 feet/6.6 meters) wide for each side of the entrance [to the courtyard].
15 Kutakuwepo tena na mapazia ya dhiraa kumi na tano kwa upande mwingine wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
16 “Kuhusu ingilio la ua, weka pazia lenye urefu wa dhiraa ishirini la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo litashikiliwa na nguzo nne na vitako vinne.
They must make a curtain (30 feet/9 meters) long for the entrance. A skilled weaver must embroider it with blue, purple, and red yarn/thread. It must be (supported by/hung from) four posts, each one with a base under it.
17 Nguzo zote zinazozunguka ua zitakuwa na tepe na kulabu za fedha, na vitako vya shaba.
All the posts around the courtyard must be connected with metal rods covered with silver. The clasps/fasteners must be made of silver, and the bases must be made of bronze.
18 Ua wa kukutania utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja na upana wa dhiraa hamsini, ukiwa na mapazia ya kitani yaliyosokotwa vizuri yenye urefu wa dhiraa tano kwenda juu na vitako vya shaba.
The whole courtyard, [from the east entrance to the west end], must be (50 yards/44 meters) long, and the curtains that enclose it must be (7-1/2 feet/2.3 meters) high. All the curtains must be made of fine linen, and all the bases [under the posts] must be made of bronze.
19 Vyombo vingine vyote vinavyotumika katika maskani kwa shughuli yoyote, pamoja na vigingi vyote na hata vile vya ua, vitakuwa vya shaba.
All the things [that are not made of gold] that are to be used inside the Sacred Tent and in the courtyard, and all the tent pegs to support the Sacred Tent and the curtains, must be made of bronze.
20 “Utawaamuru Waisraeli wakuletee mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa kwa ajili ya mwanga ili zile taa ziwake mfululizo.
“Command the Israeli people that they must bring to you the best kind of olive oil to [burn in] the lamps. [They must bring this oil to you continually], in order that the lamps can burn continually.
21 Katika Hema la Kukutania, nje ya pazia lililo mbele ya Sanduku la Ushuhuda, Aroni na wanawe watahakikisha kuwa taa hizo zinawaka kuanzia jioni mpaka asubuhi mbele za Bwana. Hili litakuwa agizo la milele miongoni mwa Waisraeli kwa vizazi vyote vijavyo.
They must put the lampstand outside of the curtain which is in front of [the sacred chest which contains the stone slabs on which I have written] my commandments. Aaron must take care of the lamps. [After he dies], his descendants must do this work. The lamps are to burn every night, from evening until morning. The Israeli people must obey this regulation throughout all future generations.”

< Kutoka 27 >