< Kutoka 27 >

1 “Jenga madhabahu ya mbao za mti wa mshita, kimo chake kiwe dhiraa tatu; itakuwa mraba, urefu wake dhiraa tano, na upana wake dhiraa tano.
“And you have made the altar of shittim wood, five cubits the length, and five cubits the breadth—the altar is square—and three cubits [is] its height.
2 Tengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu ziwe zimeungana, na ufunike madhabahu kwa shaba.
And you have made its horns on its four corners, its horns are of the same, and you have overlaid it [with] bronze.
3 Tengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama, na vyombo vya kuchukulia moto.
And you have made its pots to remove its ashes, and its shovels, and its bowls, and its forks, and its fire-pans, even all its vessels you make of bronze.
4 Kisha tengenezea hayo madhabahu wavu wa shaba, na utengeneze pete za shaba kwenye kila moja ya hizo pembe nne za huo wavu.
And you have made a grate of network of bronze for it, and have made four rings of bronze on the net on its four extremities,
5 Weka wavu huo chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu.
and have put it under the rim of the altar beneath, and the net has been up to the middle of the altar.
6 Tengeneza mipiko ya mti wa mshita kwa ajili ya madhabahu, na uifunike kwa shaba.
And you have made poles for the altar, poles of shittim wood, and have overlaid them [with] bronze.
7 Hiyo mipiko itaingizwa kwenye zile pete ili iwe pande mbili za madhabahu inapobebwa.
And the poles have been brought into the rings, and the poles have been on the two sides of the altar in carrying it.
8 Tengeneza madhabahu yawe na uvungu ndani yake ukitumia mbao. Utaitengeneza sawasawa na vile ulivyoonyeshwa mlimani.
You make it hollow [with] boards; as it has been showed [to] you on the mountain, so do they make [it].
9 “Tengeneza ua kwa ajili ya Hema la Kukutania. Upande wa kusini utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja, na utakuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri,
And you have made the court of the Dwelling Place: for the south side southward, hangings for the court of twined linen, the length of the first side [is] one hundred by the cubit,
10 pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
and its twenty pillars and their twenty sockets [are] of bronze, the pegs of the pillars and their fillets [are] of silver;
11 Upande wa kaskazini utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja, nao utakuwa na mapazia, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
and so for the north side in length, hangings of one hundred [cubits] in length, and its twenty pillars and their twenty sockets [are] of bronze, the pegs of the pillars and their fillets [are] of silver.
12 “Upande wa magharibi wa ua utakuwa na upana wa dhiraa hamsini, nao utakuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi.
And [for] the breadth of the court at the west side [are] hangings of fifty cubits, their pillars ten, and their sockets ten.
13 Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, ua pia utakuwa na upana wa dhiraa hamsini.
And the breadth of the court at the east side, eastward, [is] fifty cubits.
14 Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yatakuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
And the hangings at the side [are] fifteen cubits, their pillars three, and their sockets three.
15 Kutakuwepo tena na mapazia ya dhiraa kumi na tano kwa upande mwingine wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
And at the second side [are] hangings of fifteen [cubits], their pillars three, and their sockets three.
16 “Kuhusu ingilio la ua, weka pazia lenye urefu wa dhiraa ishirini la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo litashikiliwa na nguzo nne na vitako vinne.
And for the gate of the court [is] a covering of twenty cubits of blue, and purple, and scarlet, and twined linen, the work of an embroiderer; their pillars four, their sockets four.
17 Nguzo zote zinazozunguka ua zitakuwa na tepe na kulabu za fedha, na vitako vya shaba.
All the pillars of the court all around [are] filleted [with] silver, their pegs [are] silver, and their sockets bronze.
18 Ua wa kukutania utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja na upana wa dhiraa hamsini, ukiwa na mapazia ya kitani yaliyosokotwa vizuri yenye urefu wa dhiraa tano kwenda juu na vitako vya shaba.
The length of the court [is] one hundred by the cubit, and the breadth fifty by fifty, and the height five cubits, of twined linen, and their sockets [are] bronze;
19 Vyombo vingine vyote vinavyotumika katika maskani kwa shughuli yoyote, pamoja na vigingi vyote na hata vile vya ua, vitakuwa vya shaba.
for all the vessels of the Dwelling Place, in all its service, and all its pins, and all the pins of the court, [are] bronze.
20 “Utawaamuru Waisraeli wakuletee mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa kwa ajili ya mwanga ili zile taa ziwake mfululizo.
And you command the sons of Israel, and they bring pure oil of beaten olive to you for the light, to cause the lamp to go up continually.
21 Katika Hema la Kukutania, nje ya pazia lililo mbele ya Sanduku la Ushuhuda, Aroni na wanawe watahakikisha kuwa taa hizo zinawaka kuanzia jioni mpaka asubuhi mbele za Bwana. Hili litakuwa agizo la milele miongoni mwa Waisraeli kwa vizazi vyote vijavyo.
In the Tent of Meeting, at the outside of the veil, which [is] over the Testimony, Aaron—his sons also—arrange it from evening until morning before YHWH. [It is] a continuous statute for their generations, from the sons of Israel.”

< Kutoka 27 >