< Kutoka 27 >

1 “Jenga madhabahu ya mbao za mti wa mshita, kimo chake kiwe dhiraa tatu; itakuwa mraba, urefu wake dhiraa tano, na upana wake dhiraa tano.
“You shall also make an altar of setim wood, which will have five cubits in length, and the same in width, that is, four equal sides, and three cubits in height.
2 Tengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu ziwe zimeungana, na ufunike madhabahu kwa shaba.
Now there shall be horns at the four corners of it, and you shall cover it with brass.
3 Tengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama, na vyombo vya kuchukulia moto.
And you shall make, for its uses, pans to receive the ashes, and tongs as well as small hooks, and receptacles for fire. You shall fabricate all of its vessels from brass,
4 Kisha tengenezea hayo madhabahu wavu wa shaba, na utengeneze pete za shaba kwenye kila moja ya hizo pembe nne za huo wavu.
along with a grating of brass in the manner of a net. At its four corners there shall be four rings of brass,
5 Weka wavu huo chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu.
which you shall place under the base of the altar. And the grating will extend even to the middle of the altar.
6 Tengeneza mipiko ya mti wa mshita kwa ajili ya madhabahu, na uifunike kwa shaba.
You shall also make, for the altar, two bars of setim wood, which you shall cover with layers of brass.
7 Hiyo mipiko itaingizwa kwenye zile pete ili iwe pande mbili za madhabahu inapobebwa.
And you shall lead them through the rings, and they will be on both sides of the altar to carry it.
8 Tengeneza madhabahu yawe na uvungu ndani yake ukitumia mbao. Utaitengeneza sawasawa na vile ulivyoonyeshwa mlimani.
You shall not make it solid, but empty and hollow at the interior, just as it was shown to you on the mountain.
9 “Tengeneza ua kwa ajili ya Hema la Kukutania. Upande wa kusini utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja, na utakuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri,
You shall also make the atrium of the tabernacle, at the southern part of which, opposite the meridian, there shall be hangings of fine twisted linen: one side extending for one hundred cubits in length.
10 pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
And you shall make twenty columns with the same number of bases of brass, the heads of which, with their engravings, shall be made of silver.
11 Upande wa kaskazini utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja, nao utakuwa na mapazia, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.
In like manner also, throughout the length of the north side, there shall be hangings of one hundred cubits, and twenty columns, and the same number of bases of brass, and their heads with their engravings of silver.
12 “Upande wa magharibi wa ua utakuwa na upana wa dhiraa hamsini, nao utakuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi.
Yet truly, along the width of the atrium that looks out toward the west, there shall be hangings of fifty cubits, and ten columns, and the same number of bases.
13 Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, ua pia utakuwa na upana wa dhiraa hamsini.
Likewise, along the width of the atrium that looks out toward the east, there shall be fifty cubits,
14 Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yatakuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
along which there shall be assigned hangings of fifteen cubits for one side, and three columns, and the same number of bases.
15 Kutakuwepo tena na mapazia ya dhiraa kumi na tano kwa upande mwingine wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.
And, along the other side, there shall be hangings occupying fifteen cubits, with three columns and the same number of bases.
16 “Kuhusu ingilio la ua, weka pazia lenye urefu wa dhiraa ishirini la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo litashikiliwa na nguzo nne na vitako vinne.
Yet truly, at the entrance of the atrium, there shall be made a hanging of twenty cubits, of hyacinth and purple, and twice-dyed scarlet, and fine twisted linen, wrought with embroidery. It shall have four columns, with the same number of bases.
17 Nguzo zote zinazozunguka ua zitakuwa na tepe na kulabu za fedha, na vitako vya shaba.
All the columns surrounding the atrium shall be clothed with layers of silver, with silver heads, and with bases of brass.
18 Ua wa kukutania utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja na upana wa dhiraa hamsini, ukiwa na mapazia ya kitani yaliyosokotwa vizuri yenye urefu wa dhiraa tano kwenda juu na vitako vya shaba.
In length, the atrium shall occupy one hundred cubits, in width, fifty; the height shall be of five cubits. And it shall be made of fine twisted linen, and it shall have bases of brass.
19 Vyombo vingine vyote vinavyotumika katika maskani kwa shughuli yoyote, pamoja na vigingi vyote na hata vile vya ua, vitakuwa vya shaba.
All the vessels of the tabernacle, for all uses and ceremonies, even to the tent pegs for its atrium, you shall make of brass.
20 “Utawaamuru Waisraeli wakuletee mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa kwa ajili ya mwanga ili zile taa ziwake mfululizo.
Instruct the sons of Israel so that they may bring you the purest oil of the olive trees, crushed with a pestle, so that a lamp may always burn
21 Katika Hema la Kukutania, nje ya pazia lililo mbele ya Sanduku la Ushuhuda, Aroni na wanawe watahakikisha kuwa taa hizo zinawaka kuanzia jioni mpaka asubuhi mbele za Bwana. Hili litakuwa agizo la milele miongoni mwa Waisraeli kwa vizazi vyote vijavyo.
in the tabernacle of the testimony, outside of the veil that enshrouds the testimony. And Aaron and his sons shall arrange it, so that it may give light in the presence of the Lord, until morning. This shall be a perpetual observance among the sons of Israel, throughout their successions.”

< Kutoka 27 >