< Kutoka 26 >

1 “Tengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi atatarizi makerubi kwenye mapazia hayo.
Mais le tabernacle, c’est ainsi que tu le feras: Tu feras dix rideaux de fin lin retors, d’hyacinthe, de pourpre et d’écarlate deux fois teinte, parsemés en ouvrage de broderie.
2 Mapazia yote yatatoshana kwa ukubwa: kila moja litakuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane, na upana wa dhiraa nne
La longueur d’un rideau aura vingt-huit coudées: la largeur sera de quatre coudées. Tous les rideaux seront faits d’une seule mesure.
3 Unganisha mapazia matano pamoja; fanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano.
Cinq rideaux seront joints ensemble, l’un à l’autre, et les autres cinq seront attachés de la même manière.
4 Tengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, na ufanye vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho.
Tu feras de petits lacs d’hyacinthe aux côtés et aux sommités des rideaux, afin qu’ils puissent s’unir l’un à l’autre.
5 Fanya vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vielekeane.
Un rideau aura cinquante petits lacs de chaque côté, disposés de telle sorte qu’un lacs vienne contre un lacs, et que l’un puisse s’ajuster à l’autre.
6 Kisha tengeneza vifungo hamsini vya dhahabu ili vitumike kufunga na kuunganisha mapazia pamoja kufanya Hema liwe kitu kimoja.
Tu feras aussi cinquante anneaux d’or par lesquels les voiles des rideaux doivent être joints, afin qu’il se fasse un seul tabernacle.
7 “Tengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani.
Tu feras encore onze couvertures de poils de chèvres pour couvrir le dessus du tabernacle.
8 Mapazia hayo kumi na moja yatakuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini, na upana wa dhiraa nne.
La longueur d’une couverture aura trente coudées, et la largeur quatre. La mesure de toutes les couvertures sera égale.
9 Unganisha hayo mapazia matano yawe fungu moja, na hayo mengine sita yawe fungu lingine. Kunja hilo pazia la sita mara mbili mbele ya maskani.
Tu en joindras cinq à part, et tu en uniras six l’une à l’autre, en sorte que tu replies la sixième couverture sur le devant du toit.
10 Tengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine.
Tu feras de plus cinquante lacs au bord d’une couverture, afin qu’elle puisse être jointe à l’autre; et cinquante lacs au bord de cette autre, afin qu’elle puisse être unie à une autre.
11 Kisha tengeneza vifungo hamsini vya shaba, uviingize katika vile vitanzi ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja.
Tu feras aussi cinquante boucles d’airain, par lesquelles les lacs doivent être joints, afin que du tout il se fasse une seule couverture.
12 Kuhusu kile kipande cha ziada cha pazia la Hema, nusu ya hilo pazia lililobaki litaningʼinizwa upande wa nyuma wa Hema.
Pour ce qui sera de trop dans les couvertures que l’on disposera pour le toit, c’est-à-dire une couverture qui sera de surplus, tu couvriras avec sa moitié le derrière du tabernacle.
13 Mapazia ya hema yatakuwa na urefu wa dhiraa moja zaidi pande zote, sehemu itakayobaki itaningʼinia pande zote za Hema ili kuifunika.
Et une coudée pendra d’un côté et une autre de l’autre; ce qui sera de surplus dans la longueur des couvertures couvrira les deux côtés du tabernacle.
14 Tengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
Tu feras aussi au toit une autre couverture de peaux de béliers teintes en rouge, et sur celle-ci tu mettras encore une autre couverture de peaux violettes.
15 “Tengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.
Tu feras aussi de bois de sétim les ais du tabernacle, qui se tiendront debout,
16 Kila mhimili uwe na urefu wa dhiraa kumi na upana wa dhiraa moja na nusu,
Qui auront chacun dix coudées en longueur, et en largeur une coudée et demie.
17 zikiwa na ndimi mbili zilizo sambamba kila mmoja na mwingine. Tengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.
Aux côtés d’un ais on fera deux emboîtements, par lesquels un ais s’enchâssera dans un autre ais; et c’est de cette manière que tous les ais seront disposés.
18 Tengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,
Il y en aura vingt du côté méridional qui regarde le vent du midi.
19 kisha tengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.
Pour ces ais, tu fondras quarante soubassements d’argent, de manière que deux soubassements soient posés au-dessous de chaque ais aux deux angles.
20 Kuhusu upande wa kaskazini wa maskani, tengeneza mihimili ishirini
Et aussi au second côté du tabernacle, qui regarde l’aquilon, il y aura vingt ais,
21 na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
Ayant quarante soubassements d’argent; deux soubassements seront posés sous chaque ais.
22 Kisha tengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,
Et pour le côté occidental du tabernacle, tu feras six
23 na pia utengeneze mihimili miwili ya pembe za upande ulio mbali.
Et encore deux autres qui seront dressés aux angles du derrière du tabernacle.
24 Katika pembe hizi mbili ni lazima mihimili yake iwe miwili kuanzia chini mpaka juu, na iingizwe kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili itafanana.
Et ils seront joints depuis le bas jusqu’au haut, et un seul joint les retiendra tous. De même pour les deux ais qui doivent être posés aux angles, on conservera une semblable jointure.
25 Kwa hiyo itakuwepo mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
Or il y aura en tout huit ais, et leurs soubassements d’argent seront au nombre de seize, en comptant deux soubassements pour un seul ais.
26 “Pia tengeneza mataruma ya mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,
Tu feras aussi des leviers de bois de sétim, cinq pour maintenir les ais à un côté du tabernacle,
27 matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili ya mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.
Et cinq autres à l’autre, et le même nombre pour le côté occidental.
28 Taruma la katikati litapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.
Et ils seront posés en travers au milieu des ais depuis une extrémité jusqu’à l’autre extrémité.
29 Funika hiyo mihimili kwa dhahabu, kisha tengeneza pete za dhahabu ambazo zitashikilia hayo mataruma. Pia funika hayo mataruma kwa dhahabu.
Tu doreras aussi les ais eux-mêmes, et tu fondras, pour les y mettre, des anneaux d’or au moyen desquels des barres maintiendront les ais; barres que tu couvriras de lames d’or.
30 “Simamisha Hema sawasawa na mfano ulioonyeshwa kule mlimani.
Ainsi, tu dresseras le tabernacle selon le modèle qui t’a été montré sur la montagne.
31 “Tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi atirizi makerubi kwenye hilo pazia.
Tu feras aussi un voile d’hyacinthe, de pourpre, d’écarlate deux fois teinte et de fin lin retors, d’un ouvrage en broderie, et tissu avec une belle variété.
32 Litundike kwa kulabu za dhahabu kwenye nguzo nne za mti wa mshita ambazo zimefunikwa kwa dhahabu, zikiwa zimesimamishwa kwenye vitako vinne vya fedha.
Tu le suspendras à quatre colonnes de bois de sétim, lesquelles seront aussi elles-mêmes dorées, et auront des chapiteaux d’or, mais des soubassements d’argent.
33 Ningʼiniza pazia hilo kwenye vifungo, kisha weka Sanduku la Ushuhuda nyuma ya pazia. Pazia litatenganisha Mahali Patakatifu kutoka Patakatifu pa Patakatifu.
Or, c’est par des anneaux que sera attaché le voile, au-dedans duquel tu placeras l’arche du témoignage, par lequel le Saint et le Saint des Saints seront divisés.
34 Weka kifuniko cha kiti cha rehema juu ya Sanduku la Ushuhuda ndani ya Patakatifu pa Patakatifu.
Tu placeras aussi le propitiatoire sur l’arche du témoignage dans le Saint des Saints,
35 Weka meza nje ya pazia upande wa kaskazini wa Hema, kisha weka kinara cha taa upande wa kusini wa Hema.
Et la table en dehors du voile, et vis-à-vis de la table le chandelier du côté méridional du tabernacle; car la table sera du côté de l’aquilon.
36 “Kwa ajili ya ingilio la hema, tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi.
Tu feras aussi à l’entrée du tabernacle un voile d’hyacinthe, de pourpre, d’écarlate deux fois teinte, et de fin lin retors, en ouvrage de brodeur.
37 Tengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya hilo pazia, na nguzo tano za mshita zilizofunikwa kwa dhahabu. Kisha mimina vitako vitano vya shaba kwa ajili yake.
Et tu doreras cinq colonnes de bois de sétim, auxquelles sera suspendu le voile, dont les chapiteaux seront d’or et les soubassements d’airain.

< Kutoka 26 >