< Kutoka 26 >

1 “Tengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi atatarizi makerubi kwenye mapazia hayo.
Moreover you shall make the tabernacle with ten curtains of fine twined linen, and blue, and purple, and scarlet: with cherubim of cunning work shall you make them.
2 Mapazia yote yatatoshana kwa ukubwa: kila moja litakuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane, na upana wa dhiraa nne
The length of one curtain shall be eight and twenty cubits, and the breadth of one curtain four cubits: and every one of the curtains shall have one measure.
3 Unganisha mapazia matano pamoja; fanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano.
The five curtains shall be coupled together one to another; and other five curtains shall be coupled one to another.
4 Tengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, na ufanye vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho.
And you shall make loops of blue on the edge of the one curtain from the selvedge in the coupling; and likewise shall you make in the uttermost edge of another curtain, in the coupling of the second.
5 Fanya vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vielekeane.
Fifty loops shall you make in the one curtain, and fifty loops shall you make in the edge of the curtain that is in the coupling of the second; that the loops may take hold one of another.
6 Kisha tengeneza vifungo hamsini vya dhahabu ili vitumike kufunga na kuunganisha mapazia pamoja kufanya Hema liwe kitu kimoja.
And you shall make fifty clasps of gold, and couple the curtains together with the clasps: and it shall be one tabernacle.
7 “Tengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani.
And you shall make curtains of goats’ hair to be a covering on the tabernacle: eleven curtains shall you make.
8 Mapazia hayo kumi na moja yatakuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini, na upana wa dhiraa nne.
The length of one curtain shall be thirty cubits, and the breadth of one curtain four cubits: and the eleven curtains shall be all of one measure.
9 Unganisha hayo mapazia matano yawe fungu moja, na hayo mengine sita yawe fungu lingine. Kunja hilo pazia la sita mara mbili mbele ya maskani.
And you shall couple five curtains by themselves, and six curtains by themselves, and shall double the sixth curtain in the forefront of the tabernacle.
10 Tengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine.
And you shall make fifty loops on the edge of the one curtain that is outmost in the coupling, and fifty loops in the edge of the curtain which couples the second.
11 Kisha tengeneza vifungo hamsini vya shaba, uviingize katika vile vitanzi ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja.
And you shall make fifty clasps of brass, and put the clasps into the loops, and couple the tent together, that it may be one.
12 Kuhusu kile kipande cha ziada cha pazia la Hema, nusu ya hilo pazia lililobaki litaningʼinizwa upande wa nyuma wa Hema.
And the remnant that remains of the curtains of the tent, the half curtain that remains, shall hang over the backside of the tabernacle.
13 Mapazia ya hema yatakuwa na urefu wa dhiraa moja zaidi pande zote, sehemu itakayobaki itaningʼinia pande zote za Hema ili kuifunika.
And a cubit on the one side, and a cubit on the other side of that which remains in the length of the curtains of the tent, it shall hang over the sides of the tabernacle on this side and on that side, to cover it.
14 Tengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
And you shall make a covering for the tent of rams’ skins dyed red, and a covering above of badgers’ skins.
15 “Tengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.
And you shall make boards for the tabernacle of shittim wood standing up.
16 Kila mhimili uwe na urefu wa dhiraa kumi na upana wa dhiraa moja na nusu,
Ten cubits shall be the length of a board, and a cubit and a half shall be the breadth of one board.
17 zikiwa na ndimi mbili zilizo sambamba kila mmoja na mwingine. Tengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.
Two tenons shall there be in one board, set in order one against another: thus shall you make for all the boards of the tabernacle.
18 Tengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,
And you shall make the boards for the tabernacle, twenty boards on the south side southward.
19 kisha tengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.
And you shall make forty sockets of silver under the twenty boards; two sockets under one board for his two tenons, and two sockets under another board for his two tenons.
20 Kuhusu upande wa kaskazini wa maskani, tengeneza mihimili ishirini
And for the second side of the tabernacle on the north side there shall be twenty boards:
21 na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
And their forty sockets of silver; two sockets under one board, and two sockets under another board.
22 Kisha tengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,
And for the sides of the tabernacle westward you shall make six boards.
23 na pia utengeneze mihimili miwili ya pembe za upande ulio mbali.
And two boards shall you make for the corners of the tabernacle in the two sides.
24 Katika pembe hizi mbili ni lazima mihimili yake iwe miwili kuanzia chini mpaka juu, na iingizwe kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili itafanana.
And they shall be coupled together beneath, and they shall be coupled together above the head of it to one ring: thus shall it be for them both; they shall be for the two corners.
25 Kwa hiyo itakuwepo mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
And they shall be eight boards, and their sockets of silver, sixteen sockets; two sockets under one board, and two sockets under another board.
26 “Pia tengeneza mataruma ya mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,
And you shall make bars of shittim wood; five for the boards of the one side of the tabernacle,
27 matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili ya mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.
And five bars for the boards of the other side of the tabernacle, and five bars for the boards of the side of the tabernacle, for the two sides westward.
28 Taruma la katikati litapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.
And the middle bar in the middle of the boards shall reach from end to end.
29 Funika hiyo mihimili kwa dhahabu, kisha tengeneza pete za dhahabu ambazo zitashikilia hayo mataruma. Pia funika hayo mataruma kwa dhahabu.
And you shall overlay the boards with gold, and make their rings of gold for places for the bars: and you shall overlay the bars with gold.
30 “Simamisha Hema sawasawa na mfano ulioonyeshwa kule mlimani.
And you shall raise up the tabernacle according to the fashion thereof which was showed you in the mount.
31 “Tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi atirizi makerubi kwenye hilo pazia.
And you shall make a veil of blue, and purple, and scarlet, and fine twined linen of cunning work: with cherubim shall it be made:
32 Litundike kwa kulabu za dhahabu kwenye nguzo nne za mti wa mshita ambazo zimefunikwa kwa dhahabu, zikiwa zimesimamishwa kwenye vitako vinne vya fedha.
And you shall hang it on four pillars of shittim wood overlaid with gold: their hooks shall be of gold, on the four sockets of silver.
33 Ningʼiniza pazia hilo kwenye vifungo, kisha weka Sanduku la Ushuhuda nyuma ya pazia. Pazia litatenganisha Mahali Patakatifu kutoka Patakatifu pa Patakatifu.
And you shall hang up the veil under the clasps, that you may bring in thither within the veil the ark of the testimony: and the veil shall divide to you between the holy place and the most holy.
34 Weka kifuniko cha kiti cha rehema juu ya Sanduku la Ushuhuda ndani ya Patakatifu pa Patakatifu.
And you shall put the mercy seat on the ark of the testimony in the most holy place.
35 Weka meza nje ya pazia upande wa kaskazini wa Hema, kisha weka kinara cha taa upande wa kusini wa Hema.
And you shall set the table without the veil, and the candlestick over against the table on the side of the tabernacle toward the south: and you shall put the table on the north side.
36 “Kwa ajili ya ingilio la hema, tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi.
And you shall make an hanging for the door of the tent, of blue, and purple, and scarlet, and fine twined linen, worked with needlework.
37 Tengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya hilo pazia, na nguzo tano za mshita zilizofunikwa kwa dhahabu. Kisha mimina vitako vitano vya shaba kwa ajili yake.
And you shall make for the hanging five pillars of shittim wood, and overlay them with gold, and their hooks shall be of gold: and you shall cast five sockets of brass for them.

< Kutoka 26 >