< Kutoka 26 >

1 “Tengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi atatarizi makerubi kwenye mapazia hayo.
Make ten curtains for the Tabernacle of finely-spun linen, using blue, purple, and crimson threads. Have them embroidered with cherubim by someone who is skilled.
2 Mapazia yote yatatoshana kwa ukubwa: kila moja litakuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane, na upana wa dhiraa nne
Each curtain is to measure twenty-eight cubits long by four cubits wide, and all the curtains are to be the same size.
3 Unganisha mapazia matano pamoja; fanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano.
Join five of the curtains together, and then do the same to the other five.
4 Tengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, na ufanye vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho.
Use blue material to make loops on the edge of the last curtain of both sets.
5 Fanya vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vielekeane.
Make fifty loops on one curtain and fifty loops on the last curtain of the second set, lining up the loops with each another.
6 Kisha tengeneza vifungo hamsini vya dhahabu ili vitumike kufunga na kuunganisha mapazia pamoja kufanya Hema liwe kitu kimoja.
Then make fifty gold clips and join the curtains together with the clips, so that the Tabernacle will be a single structure.
7 “Tengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani.
Make eleven curtains of goat hair as a tent to cover the Tabernacle.
8 Mapazia hayo kumi na moja yatakuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini, na upana wa dhiraa nne.
Each of the eleven curtains is to be the same size—thirty cubits long by four cubits wide.
9 Unganisha hayo mapazia matano yawe fungu moja, na hayo mengine sita yawe fungu lingine. Kunja hilo pazia la sita mara mbili mbele ya maskani.
Join five of the curtains together as one set and the other six as another set. Then fold the sixth curtain in two at the front of the tent.
10 Tengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine.
Make fifty loops on the edge of the last curtain in the first set, and fifty loops along the edge of the last curtain in the second set.
11 Kisha tengeneza vifungo hamsini vya shaba, uviingize katika vile vitanzi ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja.
Make fifty bronze clips and put them in the loops to join the tent together as a single cover.
12 Kuhusu kile kipande cha ziada cha pazia la Hema, nusu ya hilo pazia lililobaki litaningʼinizwa upande wa nyuma wa Hema.
The extra half-curtain of this tent covering will be left to hang over the back of the Tabernacle.
13 Mapazia ya hema yatakuwa na urefu wa dhiraa moja zaidi pande zote, sehemu itakayobaki itaningʼinia pande zote za Hema ili kuifunika.
The tent curtains will be a cubit longer on every side, and the extra length will hang over the sides of the Tabernacle so it is all covered.
14 Tengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
Make a covering for the goat hair tent from tanned ram skins, and place an extra covering of fine leather over that.
15 “Tengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.
Make an upright framework of acacia wood for the Tabernacle.
16 Kila mhimili uwe na urefu wa dhiraa kumi na upana wa dhiraa moja na nusu,
Each frame is to be ten cubits long by one and a half cubits wide.
17 zikiwa na ndimi mbili zilizo sambamba kila mmoja na mwingine. Tengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.
Each frame will have two pegs so the frames can be connected to each other. Make all the frames of the Tabernacle like this.
18 Tengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,
Make twenty frames for the south side of the Tabernacle.
19 kisha tengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.
Make forty silver stands as supports for the twenty frames using two stands per frame, one under every frame peg.
20 Kuhusu upande wa kaskazini wa maskani, tengeneza mihimili ishirini
Similarly for the north side of the Tabernacle, make twenty frames
21 na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
and forty silver stands, two stands per frame.
22 Kisha tengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,
Make six frames for the back (west side) of the Tabernacle,
23 na pia utengeneze mihimili miwili ya pembe za upande ulio mbali.
along with two frames for its two back corners.
24 Katika pembe hizi mbili ni lazima mihimili yake iwe miwili kuanzia chini mpaka juu, na iingizwe kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili itafanana.
Join these corner frames at the bottom and at the top near to the first ring. This is how you are to make the two corner frames.
25 Kwa hiyo itakuwepo mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
In total there will be eight frames and sixteen silver stands, two under each frame.
26 “Pia tengeneza mataruma ya mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,
Make five crossbars of acacia wood to hold together the frames on the south side of the Tabernacle,
27 matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili ya mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.
five for those on the north, and five for those at the back of the Tabernacle, to the west.
28 Taruma la katikati litapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.
The central crossbar which is placed halfway up the frames will run from one end to the other.
29 Funika hiyo mihimili kwa dhahabu, kisha tengeneza pete za dhahabu ambazo zitashikilia hayo mataruma. Pia funika hayo mataruma kwa dhahabu.
Cover the frames with gold, and make gold rings to hold the crossbars in place. Cover the crossbars with gold too.
30 “Simamisha Hema sawasawa na mfano ulioonyeshwa kule mlimani.
Assemble the Tabernacle following to the design you were shown on the mountain.
31 “Tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi atirizi makerubi kwenye hilo pazia.
Make a veil out of blue, purple, and crimson thread, and finely-spun linen, embroidered with cherubim by someone who is skilled.
32 Litundike kwa kulabu za dhahabu kwenye nguzo nne za mti wa mshita ambazo zimefunikwa kwa dhahabu, zikiwa zimesimamishwa kwenye vitako vinne vya fedha.
Using gold hooks hang it from four posts of acacia wood covered with gold, held up by four silver stands.
33 Ningʼiniza pazia hilo kwenye vifungo, kisha weka Sanduku la Ushuhuda nyuma ya pazia. Pazia litatenganisha Mahali Patakatifu kutoka Patakatifu pa Patakatifu.
Place the veil under the clips and take the Ark of the Testimony inside behind the veil. The veil will separate the Holy Place from the Most Holy Place.
34 Weka kifuniko cha kiti cha rehema juu ya Sanduku la Ushuhuda ndani ya Patakatifu pa Patakatifu.
Put the atonement cover on the Ark of the Testimony in the Most Holy Place.
35 Weka meza nje ya pazia upande wa kaskazini wa Hema, kisha weka kinara cha taa upande wa kusini wa Hema.
Place the table outside the veil on the north side of the Tabernacle and put the lampstand opposite it on the south side.
36 “Kwa ajili ya ingilio la hema, tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi.
Make a screen for the entrance to the tent using blue, purple, and crimson thread, and finely-spun linen. Have it embroidered.
37 Tengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya hilo pazia, na nguzo tano za mshita zilizofunikwa kwa dhahabu. Kisha mimina vitako vitano vya shaba kwa ajili yake.
Make five posts of acacia wood with gold hooks to hang the screen, and cast five bronze stands to hold them.

< Kutoka 26 >