< Kutoka 25 >
Et l'Eternel parla à Moïse, en disant:
2 “Waambie Waisraeli waniletee sadaka. Utapokea sadaka kwa niaba yangu kutoka kwa kila mtu ambaye moyo wake wapenda kutoa.
Parle aux enfants d'Israël, et qu'on prenne une offrande pour moi. Vous prendrez mon offrande de tout homme, dont le cœur [me] l'offrira volontairement.
3 Hizi ndizo sadaka utakazozipokea kutoka kwao: dhahabu, fedha na shaba;
Et c'est ici l'offrande que vous prendrez d'eux, de l'or, de l'argent, de l'airain,
4 nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu, pamoja na kitani safi; singa za mbuzi;
De la pourpre, de l'écarlate, du cramoisi, du fin lin, des poils de chèvres,
5 ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
Des peaux de moutons teintes en rouge, des peaux de taissons, du bois de Sittim,
6 mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
De l'huile pour le luminaire, des odeurs aromatiques pour l'huile de l'onction, des drogues pour le parfum,
7 na vito vya shohamu na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
Des pierres d'Onyx, et des pierres de remplages pour l'Ephod et pour le Pectoral,
8 “Kisha uwaamuru wanitengenezee mahali patakatifu, nami nitakaa miongoni mwao.
Et ils me feront un Sanctuaire, et j'habiterai au milieu d'eux.
9 Tengeneza hema hili na vyombo vyake vyote sawasawa na kielelezo nitakachokuonyesha.
[Ils le feront] conformément à tout ce que je te vais montrer, selon le patron du pavillon, et [selon] le patron de tous ses ustensiles; vous le ferez donc ainsi.
10 “Nao watatengeneza Sanduku la mbao za mshita, lenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, upana wa dhiraa moja na nusu, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
Et ils feront une Arche de bois de Sittim; et sa longueur sera de deux coudées et demie, et sa largeur d'une coudée et demie, et sa hauteur d'une coudée et demie.
11 Utalifunika hilo Sanduku kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulifanyia ukingo wa dhahabu juu yake kulizunguka.
Et tu la couvriras de pur or, tu l'[en] couvriras par dehors et par-dedans; et tu feras sur elle un couronnement d'or tout autour.
12 Utalisubu kwa pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
Et tu fondras pour elle quatre anneaux d'or, que tu mettras à ses quatre coins, deux anneaux à l'un de ses côtés, et deux autres à l'autre côté.
13 Kisha utatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
Tu feras aussi des barres de bois de Sittim, et tu les couvriras d'or.
14 Utaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
Puis tu feras entrer les barres dans les anneaux aux côtés de l'Arche, pour porter l'Arche avec elles.
15 Hiyo mipiko itabakia daima katika hizo pete za hilo Sanduku; haitaondolewa.
Les barres seront dans les anneaux de l'Arche, et on ne les en tirera point.
16 Kisha weka ndani ya hilo Sanduku ule Ushuhuda nitakaokupa.
Et tu mettras dans l'Arche le Témoignage que je te donnerai.
17 “Tengeneza kifuniko cha upatanisho cha dhahabu safi, chenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, na upana wa dhiraa moja na nusu.
Tu feras aussi un Propitiatoire de pur or, dont la longueur sera de deux coudées et demie, et la largeur d'une coudée et demie.
18 Tengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
Et tu feras deux Chérubins d'or; tu les feras d'ouvrage étendu au marteau, [tiré] des deux bouts du Propitiatoire.
19 Tengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; watengeneze makerubi hao wawe kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
Fais donc un Chérubin tiré du bout de deçà, et l'autre Chérubin du bout de delà: vous ferez les Chérubins tirés du Propitiatoire sur ses deux bouts.
20 Makerubi hao watakuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, yakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao wataelekeana, wakitazama hicho kifuniko.
Et les Chérubins étendront les ailes en haut, couvrant de leurs ailes le Propitiatoire, et leurs faces seront vis-à-vis l'une de l'autre; et le regard des Chérubins sera vers le Propitiatoire.
21 Weka huo Ushuhuda nitakaokupa ndani ya hilo Sanduku la Agano, na uweke hicho kifuniko juu ya hilo Sanduku.
Et tu poseras le Propitiatoire au-dessus de l'Arche, et tu mettras dans l'Arche le Témoignage que je te donnerai.
22 Hapo juu ya hicho kifuniko, kati ya hao makerubi wawili walioko juu ya hilo Sanduku la Ushuhuda, hapo ndipo nitakapokutana nawe na kukupa maagizo yangu kwa ajili ya Waisraeli.
Et je me trouverai là avec toi, et je te dirai de dessus le Propitiatoire, d'entre les deux Chérubins qui seront sur l'Arche du Témoignage, toutes les choses que je te commanderai pour les enfants d'Israël.
23 “Tengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
Tu feras aussi une table de bois de Sittim: sa longueur sera de deux coudées, et sa largeur d'une coudée, et sa hauteur d'une coudée et demie.
24 Ifunike kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
Tu la couvriras de pur or, et tu lui feras un couronnement d'or à l’entour.
25 Kisha tengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na ufanyie ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
Tu lui feras aussi à l’entour une clôture d'une paume, et tout autour de sa clôture tu feras un couronnement d'or.
26 Tengeneza pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na uzifungie kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
Tu lui feras aussi quatre anneaux d'or, que tu mettras aux quatre coins, qui seront à ses quatre pieds.
27 Pete hizo zitakuwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko itakayotumika kuibebea hiyo meza.
Les anneaux seront à l'endroit de la clôture, afin d'y mettre les barres pour porter la table.
28 Tengeneza mipiko hiyo kwa mbao za mshita, uifunike na dhahabu, uitumie kubeba hiyo meza.
Tu feras les barres de bois de Sittim, et tu les couvriras d'or, et on portera la table avec elles.
29 Tengeneza sahani zake na masinia yake kwa dhahabu safi, pamoja na bilauri na bakuli zake kwa ajili ya kumiminia sadaka.
Tu feras aussi ses plats, ses tasses, ses gobelets, et ses bassins, avec lesquels on fera les aspersions; tu les feras de pur or.
30 Utaweka mikate ya Wonyesho juu ya meza hii iwe mbele yangu daima.
Et tu mettras sur cette table le pain de proposition, continuellement devant moi.
31 “Tengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vinavyofanana na ua, matovu yake na maua yake viwe kitu kimoja.
Tu feras aussi un chandelier de pur or; le chandelier sera étendu au marteau; sa tige et ses branches, ses plats, ses pommeaux, et ses fleurs, seront [tirés] de lui.
32 Matawi sita yatatokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
Six branches sortiront de ses côtés; trois branches d'un côté du chandelier, et trois autres de l'autre côté du chandelier.
33 Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vitakuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yanayotokeza kwenye kile kinara cha taa.
Il y aura en une des branches trois petits plats en forme d'amande, un pommeau et une fleur; en l'autre branche trois petits plats en forme d'amande, un pommeau et une fleur; [il en sera] de même des six branches procédant du chandelier.
34 Juu ya kinara chenyewe vitakuwepo vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
Il y aura aussi au chandelier quatre petits plats en forme d'amande, ses pommeaux et ses fleurs.
35 Tovu moja litakuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani matawi sita kwa jumla.
Un pommeau sous deux branches [tirées] du chandelier, un pommeau sous deux [autres] branches [tirées] de lui, et un pommeau sous deux [autres] branches tirées de lui; il [en sera] de même des six branches procédant du chandelier.
36 Matovu na matawi yote yatakuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakifuliwa kwa dhahabu safi.
Leurs pommeaux et leurs branches seront [tirés] de lui, [et] tout le chandelier sera un seul ouvrage étendu au marteau, [et] de pur or.
37 “Kisha tengeneza taa zake saba na uziweke juu ya kinara hicho ili ziangaze mbele yake.
Tu feras aussi ses sept lampes, et on les allumera, afin qu'elles éclairent vis-à-vis du chandelier.
38 Mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote zitakuwa za dhahabu safi.
Et ses mouchettes, et ses creuseaux seront de pur or.
39 Utatumia talanta moja ya dhahabu safi kutengeneza hicho kinara na vifaa vyake vyote.
On le fera avec tous ses ustensiles d'un talent de pur or.
40 Hakikisha kuwa umevitengeneza sawasawa na ule mfano ulioonyeshwa kule mlimani.
Regarde donc, et fais selon le patron qui t'est montré en la montagne.