< Kutoka 25 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Yahweh parla à Moïse, en disant:
2 “Waambie Waisraeli waniletee sadaka. Utapokea sadaka kwa niaba yangu kutoka kwa kila mtu ambaye moyo wake wapenda kutoa.
" Dis aux enfants d'Israël de prélever pour moi une offrande; de tout homme qui la donnera de bon cœur vous recevrez pour moi l'offrande.
3 Hizi ndizo sadaka utakazozipokea kutoka kwao: dhahabu, fedha na shaba;
Voici l'offrande que vous recevrez d'eux: de l'or, de l'argent et de l'airain;
4 nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu, pamoja na kitani safi; singa za mbuzi;
de la pourpre violette, de la pourpre écarlate, du cramoisi, du fin lin et du poil de chèvre;
5 ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
des peaux de béliers teintes en rouge, des peaux de veaux marins et du bois d'acacia;
6 mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
de l'huile pour le chandelier, des aromates pour l'huile d'onction et pour le parfum d'encensement;
7 na vito vya shohamu na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
des pierres d'onyx et d'autres pierres à enchâsser pour l'éphod et le pectoral.
8 “Kisha uwaamuru wanitengenezee mahali patakatifu, nami nitakaa miongoni mwao.
Ils me feront un sanctuaire, et j'habiterai au milieu d'eux.
9 Tengeneza hema hili na vyombo vyake vyote sawasawa na kielelezo nitakachokuonyesha.
Vous vous conformerez à tout ce que je vais vous montrer, au modèle du tabernacle, et au modèle de tous ses ustensiles. "
10 “Nao watatengeneza Sanduku la mbao za mshita, lenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, upana wa dhiraa moja na nusu, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
" Ils feront une arche de bois d'acacia; sa longueur sera de deux coudées et demie, sa largeur d'une coudée et demie, et sa hauteur d'une coudée et demie.
11 Utalifunika hilo Sanduku kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulifanyia ukingo wa dhahabu juu yake kulizunguka.
Tu la revêtiras d'or pur, en dedans et en dehors, et tu y feras une guirlande d'or tout autour.
12 Utalisubu kwa pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
Tu fondras pour elle quatre anneaux d'or, que tu mettras à ses quatre pieds, deux anneaux d'un côté et deux anneaux de l'autre.
13 Kisha utatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
Tu feras des barres de bois d'acacia, et tu les revêtiras d'or.
14 Utaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
Tu passeras les barres dans les anneaux sur les côtés de l'arche, pour qu'elles servent à porter l'arche.
15 Hiyo mipiko itabakia daima katika hizo pete za hilo Sanduku; haitaondolewa.
Les barres resteront dans les anneaux de l'arche, et n'en seront point retirées.
16 Kisha weka ndani ya hilo Sanduku ule Ushuhuda nitakaokupa.
Tu mettras dans l'arche le témoignage que je te donnerai.
17 “Tengeneza kifuniko cha upatanisho cha dhahabu safi, chenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, na upana wa dhiraa moja na nusu.
Tu feras un propitiatoire d'or pur; sa longueur sera de deux coudées et demie, et sa largeur d'une coudée et demie.
18 Tengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
Tu feras deux chérubins d'or; tu les feras d'or battu, aux deux extrémités du propitiatoire.
19 Tengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; watengeneze makerubi hao wawe kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
Fais un chérubin à l'une des extrémités et un chérubin à l'autre extrémité; vous ferez les chérubins sortant du propitiatoire à ses deux extrémités.
20 Makerubi hao watakuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, yakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao wataelekeana, wakitazama hicho kifuniko.
Les chérubins auront leurs ailes déployées vers le haut, couvrant de leurs ailes le propitiatoire, et se faisant face l'un à l'autre; les faces des chérubins seront tournées vers le propitiatoire.
21 Weka huo Ushuhuda nitakaokupa ndani ya hilo Sanduku la Agano, na uweke hicho kifuniko juu ya hilo Sanduku.
Tu mettras le propitiatoire au-dessus de l'arche, et tu mettras dans l'arche le témoignage que je te donnerai.
22 Hapo juu ya hicho kifuniko, kati ya hao makerubi wawili walioko juu ya hilo Sanduku la Ushuhuda, hapo ndipo nitakapokutana nawe na kukupa maagizo yangu kwa ajili ya Waisraeli.
Là je me rencontrerai avec toi et je te communiquerai, de dessus le propitiatoire, du milieu des deux chérubins qui sont sur l'arche du témoignage, tous les ordres que je te donnerai pour les enfants d'Israël.
23 “Tengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
Tu feras une table de bois d'acacia; sa longueur sera de deux coudées, sa largeur d'une coudée, et sa hauteur d'une coudée et demie.
24 Ifunike kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
Tu la revêtiras d'or pur, et tu y mettras une guirlande d'or tout autour.
25 Kisha tengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na ufanyie ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
Tu lui feras à l'entour un châssis d'une palme, et tu feras une guirlande d'or au châssis, tout autour.
26 Tengeneza pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na uzifungie kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
Tu feras pour la table quatre anneaux d'or; et tu mettras les anneaux aux quatre coins, qui seront à ses quatre pieds.
27 Pete hizo zitakuwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko itakayotumika kuibebea hiyo meza.
Les anneaux seront près du châssis, pour recevoir les barres qui doivent porter la table.
28 Tengeneza mipiko hiyo kwa mbao za mshita, uifunike na dhahabu, uitumie kubeba hiyo meza.
Tu feras les barres de bois d'acacia, et tu les revêtiras d'or; elles serviront à porter la table.
29 Tengeneza sahani zake na masinia yake kwa dhahabu safi, pamoja na bilauri na bakuli zake kwa ajili ya kumiminia sadaka.
Tu feras ses plats, ses cassolettes, ses coupes et ses tasses servant aux libations; tu les feras d'or pur.
30 Utaweka mikate ya Wonyesho juu ya meza hii iwe mbele yangu daima.
Tu placeras sur la table les pains de proposition, perpétuellement devant ma face.
31 “Tengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vinavyofanana na ua, matovu yake na maua yake viwe kitu kimoja.
Tu feras un chandelier d'or pur; le chandelier, avec son pied et sa tige, sera fait d'or battu; ses calices, ses boutons et ses fleurs seront d'une même pièce.
32 Matawi sita yatatokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
Six branches sortiront de ses côtés; trois branches du chandelier de l'un de ses côtés, et trois branches du chandelier du second de ses côtés.
33 Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vitakuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yanayotokeza kwenye kile kinara cha taa.
Il y aura sur la première branche trois calices en fleurs d'amandier, bouton et fleur, et sur la seconde branche trois calices en fleurs d'amandier, bouton et fleur; il en sera de même pour les six branches partant du chandelier.
34 Juu ya kinara chenyewe vitakuwepo vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
A la tige du chandelier, il y aura quatre calices en fleurs d'amandier, leurs boutons et leurs fleurs.
35 Tovu moja litakuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani matawi sita kwa jumla.
Il y aura un bouton sous les deux premières branches partant de la tige du chandelier, un bouton sous les deux branches suivantes partant de la tige du chandelier, et un bouton sous les deux dernières branches partant de la tige du chandelier, selon les six branches sortant de la tige du chandelier.
36 Matovu na matawi yote yatakuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakifuliwa kwa dhahabu safi.
Ces boutons et ces branches seront d'une même pièce avec le chandelier; le tout sera une masse d'or battu, d'or pur.
37 “Kisha tengeneza taa zake saba na uziweke juu ya kinara hicho ili ziangaze mbele yake.
Tu feras ses lampes, au nombre de sept, et on placera ses lampes sur les branches, de manière à éclairer en face.
38 Mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote zitakuwa za dhahabu safi.
Ses mouchettes et ses vases à cendre seront en or pur.
39 Utatumia talanta moja ya dhahabu safi kutengeneza hicho kinara na vifaa vyake vyote.
On emploiera un talent d'or pur pour faire le chandelier avec tous ses ustensiles.
40 Hakikisha kuwa umevitengeneza sawasawa na ule mfano ulioonyeshwa kule mlimani.
Regarde, et fais selon le modèle qui t'est montré sur la montagne. "

< Kutoka 25 >