< Kutoka 25 >
2 “Waambie Waisraeli waniletee sadaka. Utapokea sadaka kwa niaba yangu kutoka kwa kila mtu ambaye moyo wake wapenda kutoa.
“Tell the Israelites to take an offering for me from every person who is motivated by a willing heart. You must receive these offerings for me.
3 Hizi ndizo sadaka utakazozipokea kutoka kwao: dhahabu, fedha na shaba;
These are the offerings that you must receive from them: gold, silver, and bronze;
4 nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu, pamoja na kitani safi; singa za mbuzi;
blue, purple, and scarlet material; fine linen; goats' hair;
5 ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
ram skins dyed red and sea cow hides; acacia wood;
6 mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
oil for the sanctuary lamps; spices for the anointing oil and the fragrant incense;
7 na vito vya shohamu na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
onyx stones and other precious stones to be set for the ephod and breastpiece.
8 “Kisha uwaamuru wanitengenezee mahali patakatifu, nami nitakaa miongoni mwao.
Let them make me a sanctuary so that I may live among them.
9 Tengeneza hema hili na vyombo vyake vyote sawasawa na kielelezo nitakachokuonyesha.
You must make it exactly as I will show you in the plans for the tabernacle and for all its equipment.
10 “Nao watatengeneza Sanduku la mbao za mshita, lenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, upana wa dhiraa moja na nusu, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
They are to make an ark of acacia wood. Its length must be two and a half cubits; its width will be one cubit and a half; and its height will be one cubit and a half.
11 Utalifunika hilo Sanduku kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulifanyia ukingo wa dhahabu juu yake kulizunguka.
You must cover it inside and out with pure gold, and you must make on it a border of gold around its top.
12 Utalisubu kwa pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
You must cast four rings of gold for it, and put them on the ark's four feet, with two rings on one side of it, and two rings on the other side.
13 Kisha utatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
You must make poles of acacia wood and cover them with gold.
14 Utaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
You must put the poles into the rings on the ark's sides, in order to carry the ark.
15 Hiyo mipiko itabakia daima katika hizo pete za hilo Sanduku; haitaondolewa.
The poles must remain in the rings of the ark; they must not be taken from it.
16 Kisha weka ndani ya hilo Sanduku ule Ushuhuda nitakaokupa.
You must put into the ark the covenant decrees that I will give you.
17 “Tengeneza kifuniko cha upatanisho cha dhahabu safi, chenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, na upana wa dhiraa moja na nusu.
You must make an atonement lid of pure gold. Its length must be two and a half cubits, and its width must be a cubit and a half.
18 Tengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
You must make two cherubim of hammered gold for the two ends of the atonement lid.
19 Tengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; watengeneze makerubi hao wawe kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
Make one cherub for one end of the atonement lid, and the other cherub for the other end. They must be made as one piece with the atonement lid.
20 Makerubi hao watakuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, yakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao wataelekeana, wakitazama hicho kifuniko.
The cherubim must spread out their wings upward and overshadow the atonement lid with them. The cherubim must face one another and look toward the center of the atonement lid.
21 Weka huo Ushuhuda nitakaokupa ndani ya hilo Sanduku la Agano, na uweke hicho kifuniko juu ya hilo Sanduku.
You must put the atonement lid on top of the ark, and you must put into the ark the covenant decrees that I am giving you.
22 Hapo juu ya hicho kifuniko, kati ya hao makerubi wawili walioko juu ya hilo Sanduku la Ushuhuda, hapo ndipo nitakapokutana nawe na kukupa maagizo yangu kwa ajili ya Waisraeli.
It is at the ark that I will meet with you. I will speak with you from my position above the atonement lid. It will be from between the two cherubim over the ark of the testimony that I will speak to you about all the commands I will give you for the Israelites.
23 “Tengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
You must make a table of acacia wood. Its length must be two cubits; its width must be one cubit, and its height must be a cubit and a half.
24 Ifunike kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
You must cover it with pure gold and put a border of gold around the top.
25 Kisha tengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na ufanyie ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
You must make a surrounding frame for it one handbreadth wide, with a surrounding border of gold for the frame.
26 Tengeneza pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na uzifungie kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
You must make for it four rings of gold and attach the rings to the four corners, where the four feet were.
27 Pete hizo zitakuwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko itakayotumika kuibebea hiyo meza.
The rings must be attached to the frame to provide places for the poles, in order to carry the table.
28 Tengeneza mipiko hiyo kwa mbao za mshita, uifunike na dhahabu, uitumie kubeba hiyo meza.
You must make the poles out of acacia wood and cover them with gold so that the table may be carried with them.
29 Tengeneza sahani zake na masinia yake kwa dhahabu safi, pamoja na bilauri na bakuli zake kwa ajili ya kumiminia sadaka.
You must make the dishes, spoons, pitchers, and bowls to be used to pour out drink offerings. You must make them of pure gold.
30 Utaweka mikate ya Wonyesho juu ya meza hii iwe mbele yangu daima.
You must regularly set the bread of the presence on the table before me.
31 “Tengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vinavyofanana na ua, matovu yake na maua yake viwe kitu kimoja.
You must make a lampstand of pure hammered gold. The lampstand is to be made with its base and shaft. Its cups, its leafy bases, and its flowers are to be all made of one piece with it.
32 Matawi sita yatatokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
Six branches must extend out from its sides—three branches must extend from one side, and three branches of the lampstand must extend from the other side.
33 Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vitakuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yanayotokeza kwenye kile kinara cha taa.
The first branch must have three cups made like almond blossoms, with a leafy base and a flower, and three cups made like almond blossoms in the other branch, with a leafy base and a flower. It must be the same for all six branches extending out from the lampstand.
34 Juu ya kinara chenyewe vitakuwepo vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
On the lampstand itself, the central shaft, there must be four cups made like almond blossoms, with their leafy bases and the flowers.
35 Tovu moja litakuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani matawi sita kwa jumla.
There must be a leafy base under the first pair of branches—made as one piece with it, and a leafy base under the second pair of branches—also made as one piece with it. In the same way there must be a leafy base under the third pair of branches, made as one piece with it. It must be the same for all six branches extending out from the lampstand.
36 Matovu na matawi yote yatakuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakifuliwa kwa dhahabu safi.
Their leafy bases and branches must all be one piece with it, one beaten piece of work of pure gold.
37 “Kisha tengeneza taa zake saba na uziweke juu ya kinara hicho ili ziangaze mbele yake.
You must make the lampstand and its seven lamps, and set up its lamps for them to give light from it.
38 Mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote zitakuwa za dhahabu safi.
The tongs and their trays must be made of pure gold.
39 Utatumia talanta moja ya dhahabu safi kutengeneza hicho kinara na vifaa vyake vyote.
Use one talent of pure gold to make the lampstand and its accessories.
40 Hakikisha kuwa umevitengeneza sawasawa na ule mfano ulioonyeshwa kule mlimani.
Be sure to make them after the pattern that you are being shown on the mountain.