< Kutoka 25 >
And he spoke Yahweh to Moses saying.
2 “Waambie Waisraeli waniletee sadaka. Utapokea sadaka kwa niaba yangu kutoka kwa kila mtu ambaye moyo wake wapenda kutoa.
Speak to [the] people of Israel so they may take for me a contribution from with every person whom it will impel him heart his you will take contribution my.
3 Hizi ndizo sadaka utakazozipokea kutoka kwao: dhahabu, fedha na shaba;
And this [is] the contribution which you will take from with them gold and silver and bronze.
4 nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu, pamoja na kitani safi; singa za mbuzi;
And violet stuff and purple and scarlet stuff of scarlet and fine linen and goat hair.
5 ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
And hides of rams dyed red and hides of dolphins and wood of acacia.
6 mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
Oil for the light spices for [the] oil of the anointing and for [the] incense of the perfume.
7 na vito vya shohamu na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
Stones of onyx and stones of setting for the ephod and for the breastpiece.
8 “Kisha uwaamuru wanitengenezee mahali patakatifu, nami nitakaa miongoni mwao.
And they will make for me a sanctuary and I will dwell in midst of them.
9 Tengeneza hema hili na vyombo vyake vyote sawasawa na kielelezo nitakachokuonyesha.
According to all that I [am] about to show you [the] pattern of the tabernacle and [the] pattern of all articles its thus you will make [it].
10 “Nao watatengeneza Sanduku la mbao za mshita, lenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, upana wa dhiraa moja na nusu, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
And they will make an ark of wood of acacia [will be] two cubits and a half length its and [will be] a cubit and a half breadth its and [will be] a cubit and a half height its.
11 Utalifunika hilo Sanduku kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulifanyia ukingo wa dhahabu juu yake kulizunguka.
And you will overlay it gold pure from inside and from outside you will overlay it and you will make on it a molding gold all around.
12 Utalisubu kwa pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
And you will cast for it four rings of gold and you will put [them] on [the] four feet its and two rings [will be] on side its one and two rings [will be] on side its second.
13 Kisha utatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
And you will make poles of wood of acacia and you will overlay them gold.
14 Utaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
And you will put the poles in the rings on [the] sides of the ark to carry the ark by them.
15 Hiyo mipiko itabakia daima katika hizo pete za hilo Sanduku; haitaondolewa.
In [the] rings of the ark they will be the poles not they will be removed from it.
16 Kisha weka ndani ya hilo Sanduku ule Ushuhuda nitakaokupa.
And you will put into the ark the testimony which I will give to you.
17 “Tengeneza kifuniko cha upatanisho cha dhahabu safi, chenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, na upana wa dhiraa moja na nusu.
And you will make an atonement cover gold pure [will be] two cubits and a half length its and [will be] a cubit and a half breadth its.
18 Tengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
And you will make two cherubim gold hammered work you will make them from [the] two [the] ends of the atonement cover.
19 Tengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; watengeneze makerubi hao wawe kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
And make a cherub one from an end from this and a cherub one from an end from this from the atonement cover you will make the cherubim on [the] two ends its.
20 Makerubi hao watakuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, yakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao wataelekeana, wakitazama hicho kifuniko.
And they will be the cherubim spreading out wings upwards covering with wings their over the atonement cover and faces their each [will be] to brother its to the atonement cover they will be [the] faces of the cherubim.
21 Weka huo Ushuhuda nitakaokupa ndani ya hilo Sanduku la Agano, na uweke hicho kifuniko juu ya hilo Sanduku.
And you will put the atonement cover on the ark from to above and into the ark you will put the testimony which I will give to you.
22 Hapo juu ya hicho kifuniko, kati ya hao makerubi wawili walioko juu ya hilo Sanduku la Ushuhuda, hapo ndipo nitakapokutana nawe na kukupa maagizo yangu kwa ajili ya Waisraeli.
And I will meet you there and I will speak with you from above the atonement cover from between [the] two the cherubim which [will be] above [the] ark of the testimony all that I will command you to [the] people of Israel.
23 “Tengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
And you will make a table wood of acacia [will be] two cubits length its and [will be] a cubit breadth its and [will be] a cubit and a half height its.
24 Ifunike kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
And you will overlay it gold pure and you will make for it a molding of gold all around.
25 Kisha tengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na ufanyie ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
And you will make for it a rim of a hand breadth all around and you will make a molding of gold for rim its all around.
26 Tengeneza pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na uzifungie kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
And you will make for it four rings of gold and you will put the rings on [the] four the corners which [belong] to [the] four feet its.
27 Pete hizo zitakuwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko itakayotumika kuibebea hiyo meza.
Close to the rim they will become the rings holders for poles to carry the table.
28 Tengeneza mipiko hiyo kwa mbao za mshita, uifunike na dhahabu, uitumie kubeba hiyo meza.
And you will make the poles wood of acacia and you will overlay them gold and it will be carried by them the table.
29 Tengeneza sahani zake na masinia yake kwa dhahabu safi, pamoja na bilauri na bakuli zake kwa ajili ya kumiminia sadaka.
And you will make dishes its and pans its and jugs its and bowls its which it will be poured out with them gold pure you will make them.
30 Utaweka mikate ya Wonyesho juu ya meza hii iwe mbele yangu daima.
And you will put on the table bread of presence before me continually.
31 “Tengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vinavyofanana na ua, matovu yake na maua yake viwe kitu kimoja.
And you will make a lampstand of gold pure hammered work it will be made the lampstand base its and shaft its cups its bulbs its and blossoms its from it they will be.
32 Matawi sita yatatokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
And six branches [will be] coming out from sides its three - branches of lampstand [will be] from side its one and three branches of lampstand [will be] from side its second.
33 Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vitakuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yanayotokeza kwenye kile kinara cha taa.
Three cups shaped like almond blossoms [will be] on the branch one a bulb and a blossom and three cups shaped like almond blossoms [will be] on the branch one a bulb and a blossom thus for [the] six the branches which come out from the lampstand.
34 Juu ya kinara chenyewe vitakuwepo vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
And [will be] on the lampstand four cups shaped like almond blossoms bulbs its and blossoms its.
35 Tovu moja litakuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani matawi sita kwa jumla.
And a bulb [will be] under [the] two the branches from it and a bulb [will be] under [the] two the branches from it and a bulb [will be] under [the] two the branches from it for [the] six the branches which come out from the lampstand.
36 Matovu na matawi yote yatakuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakifuliwa kwa dhahabu safi.
Bulbs their and branches their from it they will be all of it [will be] hammered work one gold pure.
37 “Kisha tengeneza taa zake saba na uziweke juu ya kinara hicho ili ziangaze mbele yake.
And you will make lamps its seven and it will lift up lamps its and it will give light on [the] side of face its.
38 Mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote zitakuwa za dhahabu safi.
And tongs its and fire-pans its [will be] gold pure.
39 Utatumia talanta moja ya dhahabu safi kutengeneza hicho kinara na vifaa vyake vyote.
A talent gold pure someone will make it all the articles these.
40 Hakikisha kuwa umevitengeneza sawasawa na ule mfano ulioonyeshwa kule mlimani.
And see and make [them] in pattern their which you [are] being shown on the mountain.