< Kutoka 25 >

1 Bwana akamwambia Mose,
The Lord told Moses,
2 “Waambie Waisraeli waniletee sadaka. Utapokea sadaka kwa niaba yangu kutoka kwa kila mtu ambaye moyo wake wapenda kutoa.
“Instruct the Israelites to bring me an offering. You are to receive my offering from everyone who willingly wants to give.
3 Hizi ndizo sadaka utakazozipokea kutoka kwao: dhahabu, fedha na shaba;
These are the items you are to accept from them as contributions: gold, silver, and bronze;
4 nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu, pamoja na kitani safi; singa za mbuzi;
blue, purple, and crimson thread; finely-spun linen and goat hair;
5 ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
ram skins that have been tanned, and fine leather; acacia wood;
6 mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
olive oil for the lamps; spices for the olive oil used in anointing and for the fragrant incense;
7 na vito vya shohamu na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
and onyx stones and other gemstones to be used in making the ephod and breastpiece.
8 “Kisha uwaamuru wanitengenezee mahali patakatifu, nami nitakaa miongoni mwao.
They are to make me a sanctuary so I can live among them.
9 Tengeneza hema hili na vyombo vyake vyote sawasawa na kielelezo nitakachokuonyesha.
You must make the Tabernacle and all its furnishings according to design I'm going to show you.
10 “Nao watatengeneza Sanduku la mbao za mshita, lenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, upana wa dhiraa moja na nusu, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
They are to make an Ark of acacia wood that measures two and a half cubits long by a cubit and a half wide by one and a half cubits high.
11 Utalifunika hilo Sanduku kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulifanyia ukingo wa dhahabu juu yake kulizunguka.
Cover it with pure gold on the inside and the outside, and make a gold trim to go around it.
12 Utalisubu kwa pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
Cast four gold rings and attach them to its four feet, two on one side and two on the other.
13 Kisha utatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
Make poles of acacia wood and cover them with gold.
14 Utaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
Place the poles into the rings on the sides of the Ark, so it can be carried.
15 Hiyo mipiko itabakia daima katika hizo pete za hilo Sanduku; haitaondolewa.
The poles are to stay in the rings of the Ark; don't take them out.
16 Kisha weka ndani ya hilo Sanduku ule Ushuhuda nitakaokupa.
Place inside the Ark the Testimony which I'm going to give you.
17 “Tengeneza kifuniko cha upatanisho cha dhahabu safi, chenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, na upana wa dhiraa moja na nusu.
You are to make an atonement cover of pure gold, two and a half cubits long by a cubit and a half wide.
18 Tengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
Make two cherubim of hammered gold for the ends of the atonement cover,
19 Tengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; watengeneze makerubi hao wawe kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
and put one cherub on each end. All of this is to be made from one piece of gold.
20 Makerubi hao watakuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, yakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao wataelekeana, wakitazama hicho kifuniko.
The cherubim are to be designed with spread wings pointing upward, covering the atonement cover. The cherubim are to be placed facing each another, looking down towards the atonement cover.
21 Weka huo Ushuhuda nitakaokupa ndani ya hilo Sanduku la Agano, na uweke hicho kifuniko juu ya hilo Sanduku.
Place the atonement cover on top of the Ark, and put the Testimony that I'm going to give you inside the Ark.
22 Hapo juu ya hicho kifuniko, kati ya hao makerubi wawili walioko juu ya hilo Sanduku la Ushuhuda, hapo ndipo nitakapokutana nawe na kukupa maagizo yangu kwa ajili ya Waisraeli.
I will meet with you there as arranged above the atonement cover, between the two cherubim that stand over the Ark of the Testimony, and I will talk with you about all the commands I will give the Israelites.
23 “Tengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
Then you are to make a table of acacia wood two cubits long by a cubit wide by a cubit and a half high.
24 Ifunike kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
Cover it with pure gold and make a gold trim to go around it.
25 Kisha tengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na ufanyie ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
Make a border around it the width of a hand and put a gold trim on the border.
26 Tengeneza pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na uzifungie kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
Make four gold rings for the table and attach them to the four corners of the table by the legs.
27 Pete hizo zitakuwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko itakayotumika kuibebea hiyo meza.
The rings are to be close to the border to hold the poles used to carry the table.
28 Tengeneza mipiko hiyo kwa mbao za mshita, uifunike na dhahabu, uitumie kubeba hiyo meza.
Make the poles of acacia wood for carrying the table and cover them with gold.
29 Tengeneza sahani zake na masinia yake kwa dhahabu safi, pamoja na bilauri na bakuli zake kwa ajili ya kumiminia sadaka.
Make plates and dishes for the table, as well as pitchers and bowls for pouring out drink offerings. Make all of them out of pure gold.
30 Utaweka mikate ya Wonyesho juu ya meza hii iwe mbele yangu daima.
Place the Bread of the Presence on the table so it is always in my presence.
31 “Tengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vinavyofanana na ua, matovu yake na maua yake viwe kitu kimoja.
Make a lampstand of pure, hammered gold. The whole of it is to be made of one piece—its base, shaft, cups, buds, and flowers.
32 Matawi sita yatatokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
It is to have six branches coming out of the sides of the lampstand, three on each side.
33 Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vitakuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yanayotokeza kwenye kile kinara cha taa.
Have three cups shaped like almond flowers on the first branch, each with buds and petals, three on the next branch. Each of six branches that come out will have three cups shaped like almond flowers, all complete with buds and petals.
34 Juu ya kinara chenyewe vitakuwepo vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
On the main shaft of the lampstand make four cups shaped like almond flowers, complete with buds and petals.
35 Tovu moja litakuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani matawi sita kwa jumla.
On the six branches that come out from the lampstand, place a bud under the first pair of branches, a bud under the second pair, and a bud under the third pair.
36 Matovu na matawi yote yatakuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakifuliwa kwa dhahabu safi.
The buds and branches are to be made with the lampstand as one piece, hammered out of pure gold.
37 “Kisha tengeneza taa zake saba na uziweke juu ya kinara hicho ili ziangaze mbele yake.
Make seven lamps and place them on the lampstand so they can light up the area in front of it.
38 Mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote zitakuwa za dhahabu safi.
The wick tongs and their trays are to be made of pure gold.
39 Utatumia talanta moja ya dhahabu safi kutengeneza hicho kinara na vifaa vyake vyote.
The lampstand and all these utensils will require a talent of pure gold.
40 Hakikisha kuwa umevitengeneza sawasawa na ule mfano ulioonyeshwa kule mlimani.
Be sure to make everything according to the design you were shown on the mountain.”

< Kutoka 25 >