< Kutoka 25 >

1 Bwana akamwambia Mose,
The LORD spoke to Moses, saying,
2 “Waambie Waisraeli waniletee sadaka. Utapokea sadaka kwa niaba yangu kutoka kwa kila mtu ambaye moyo wake wapenda kutoa.
“Speak to the children of Israel, that they take an offering for me. From everyone whose heart makes him willing you shall take my offering.
3 Hizi ndizo sadaka utakazozipokea kutoka kwao: dhahabu, fedha na shaba;
This is the offering which you shall take from them: gold, silver, bronze,
4 nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu, pamoja na kitani safi; singa za mbuzi;
blue, purple, scarlet, fine linen, goats’ hair,
5 ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
rams’ skins dyed red, sea cow hides, acacia wood,
6 mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
oil for the light, spices for the anointing oil and for the sweet incense,
7 na vito vya shohamu na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
onyx stones, and stones to be set for the ephod and for the breastplate.
8 “Kisha uwaamuru wanitengenezee mahali patakatifu, nami nitakaa miongoni mwao.
Let them make me a sanctuary, that I may dwell among them.
9 Tengeneza hema hili na vyombo vyake vyote sawasawa na kielelezo nitakachokuonyesha.
According to all that I show you, the pattern of the tabernacle, and the pattern of all of its furniture, even so you shall make it.
10 “Nao watatengeneza Sanduku la mbao za mshita, lenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, upana wa dhiraa moja na nusu, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
“They shall make an ark of acacia wood. Its length shall be two and a half cubits, its width a cubit and a half, and a cubit and a half its height.
11 Utalifunika hilo Sanduku kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulifanyia ukingo wa dhahabu juu yake kulizunguka.
You shall overlay it with pure gold. You shall overlay it inside and outside, and you shall make a gold molding around it.
12 Utalisubu kwa pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
You shall cast four rings of gold for it, and put them in its four feet. Two rings shall be on the one side of it, and two rings on the other side of it.
13 Kisha utatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
You shall make poles of acacia wood, and overlay them with gold.
14 Utaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
You shall put the poles into the rings on the sides of the ark to carry the ark.
15 Hiyo mipiko itabakia daima katika hizo pete za hilo Sanduku; haitaondolewa.
The poles shall be in the rings of the ark. They shall not be taken from it.
16 Kisha weka ndani ya hilo Sanduku ule Ushuhuda nitakaokupa.
You shall put the covenant which I shall give you into the ark.
17 “Tengeneza kifuniko cha upatanisho cha dhahabu safi, chenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, na upana wa dhiraa moja na nusu.
You shall make a mercy seat of pure gold. Two and a half cubits shall be its length, and a cubit and a half its width.
18 Tengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
You shall make two cherubim of hammered gold. You shall make them at the two ends of the mercy seat.
19 Tengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; watengeneze makerubi hao wawe kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
Make one cherub at the one end, and one cherub at the other end. You shall make the cherubim on its two ends of one piece with the mercy seat.
20 Makerubi hao watakuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, yakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao wataelekeana, wakitazama hicho kifuniko.
The cherubim shall spread out their wings upward, covering the mercy seat with their wings, with their faces toward one another. The faces of the cherubim shall be toward the mercy seat.
21 Weka huo Ushuhuda nitakaokupa ndani ya hilo Sanduku la Agano, na uweke hicho kifuniko juu ya hilo Sanduku.
You shall put the mercy seat on top of the ark, and in the ark you shall put the covenant that I will give you.
22 Hapo juu ya hicho kifuniko, kati ya hao makerubi wawili walioko juu ya hilo Sanduku la Ushuhuda, hapo ndipo nitakapokutana nawe na kukupa maagizo yangu kwa ajili ya Waisraeli.
There I will meet with you, and I will tell you from above the mercy seat, from between the two cherubim which are on the ark of the covenant, all that I command you for the children of Israel.
23 “Tengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
“You shall make a table of acacia wood. Its length shall be two cubits, and its width a cubit, and its height one and a half cubits.
24 Ifunike kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
You shall overlay it with pure gold, and make a gold molding around it.
25 Kisha tengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na ufanyie ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
You shall make a rim of a hand width around it. You shall make a golden molding on its rim around it.
26 Tengeneza pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na uzifungie kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
You shall make four rings of gold for it, and put the rings in the four corners that are on its four feet.
27 Pete hizo zitakuwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko itakayotumika kuibebea hiyo meza.
The rings shall be close to the rim, for places for the poles to carry the table.
28 Tengeneza mipiko hiyo kwa mbao za mshita, uifunike na dhahabu, uitumie kubeba hiyo meza.
You shall make the poles of acacia wood, and overlay them with gold, that the table may be carried with them.
29 Tengeneza sahani zake na masinia yake kwa dhahabu safi, pamoja na bilauri na bakuli zake kwa ajili ya kumiminia sadaka.
You shall make its dishes, its spoons, its ladles, and its bowls with which to pour out offerings. You shall make them of pure gold.
30 Utaweka mikate ya Wonyesho juu ya meza hii iwe mbele yangu daima.
You shall set bread of the presence on the table before me always.
31 “Tengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vinavyofanana na ua, matovu yake na maua yake viwe kitu kimoja.
“You shall make a lamp stand of pure gold. The lamp stand shall be made of hammered work. Its base, its shaft, its cups, its buds, and its flowers shall be of one piece with it.
32 Matawi sita yatatokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
There shall be six branches going out of its sides: three branches of the lamp stand out of its one side, and three branches of the lamp stand out of its other side;
33 Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vitakuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yanayotokeza kwenye kile kinara cha taa.
three cups made like almond blossoms in one branch, a bud and a flower; and three cups made like almond blossoms in the other branch, a bud and a flower, so for the six branches going out of the lamp stand;
34 Juu ya kinara chenyewe vitakuwepo vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
and in the lamp stand four cups made like almond blossoms, its buds and its flowers;
35 Tovu moja litakuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani matawi sita kwa jumla.
and a bud under two branches of one piece with it, and a bud under two branches of one piece with it, and a bud under two branches of one piece with it, for the six branches going out of the lamp stand.
36 Matovu na matawi yote yatakuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakifuliwa kwa dhahabu safi.
Their buds and their branches shall be of one piece with it, all of it one beaten work of pure gold.
37 “Kisha tengeneza taa zake saba na uziweke juu ya kinara hicho ili ziangaze mbele yake.
You shall make its lamps seven, and they shall light its lamps to give light to the space in front of it.
38 Mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote zitakuwa za dhahabu safi.
Its snuffers and its snuff dishes shall be of pure gold.
39 Utatumia talanta moja ya dhahabu safi kutengeneza hicho kinara na vifaa vyake vyote.
It shall be made of a talent of pure gold, with all these accessories.
40 Hakikisha kuwa umevitengeneza sawasawa na ule mfano ulioonyeshwa kule mlimani.
See that you make them after their pattern, which has been shown to you on the mountain.

< Kutoka 25 >