< Kutoka 24 >
1 Kisha Mungu akamwambia Mose, “Njooni huku juu kwa Bwana, wewe na Aroni, Nadabu na Abihu, pamoja na wazee sabini wa Israeli. Mniabudu kwa mbali,
Dieu dit aussi à Moïse: Monte vers le Seigneur, toi et Aaron, Nadab et Abiu, et les soixante dix anciens d’Israël, et vous adorerez de loin.
2 lakini Mose peke yake ndiye atakayemkaribia Bwana; wengine wasije karibu. Nao watu wasije wakapanda pamoja naye.”
Et Moïse seul montera vers le Seigneur, et eux ne s’approcheront pas, et le peuple ne montera pas avec lui.
3 Mose alipokwenda na kuwaambia watu maneno yote na sheria zote za Bwana, wakaitikia kwa sauti moja, “Kila kitu alichosema Bwana tutakifanya.”
Moïse vint donc et raconta au peuple toutes les paroles du Seigneur et ses ordonnances, et tout le peuple répondit d’une seule voix: Nous accomplirons toutes les paroles que le Seigneur a dites.
4 Ndipo Mose akaandika kila kitu Bwana alichokuwa amesema. Akaamka kesho yake asubuhi na mapema na kujenga madhabahu chini ya mlima na kusimamisha nguzo kumi na mbili za mawe kuwakilisha makabila kumi na mawili ya Israeli.
Or Moïse écrivit tous les discours du Seigneur, et le matin, se levant, il bâtit un autel au pied de la montagne et douze monuments selon les douze tribus d’Israël.
5 Kisha akawatuma vijana wanaume wa Kiisraeli, nao wakatoa sadaka za kuteketezwa na dhabihu za mafahali wachanga kuwa sadaka za amani kwa Bwana.
Et il envoya les jeunes gens d’entre les enfants d’Israël, et ils offrirent des holocaustes, et ils immolèrent des victimes pacifiques au Seigneur, des veaux.
6 Mose akachukua nusu ya damu ya wale wanyama na kuiweka kwenye mabakuli na nusu nyingine akainyunyiza juu ya madhabahu.
C’est pourquoi Moïse prit la moitié du sang et la mit dans des coupes; mais la partie qui restait, il la répandit sur l’autel.
7 Kisha akachukua kile Kitabu cha Agano na kuwasomea watu. Nao wakajibu, “Tutafanya kila kitu alichosema Bwana, nasi tutatii.”
Prenant ensuite le livre de l’alliance, il lut, le peuple écoutant, lequel dit: Tout ce que le Seigneur a dit, nous le ferons, et nous serons obéissants.
8 Ndipo Mose akachukua ile damu, akawanyunyizia wale watu, akasema, “Hii ni damu ya agano ambalo Bwana amelifanya nanyi kufuatana na maneno haya yote.”
Or Moïse ayant pris le sang, le répandit sur le peuple, et dit: Voici le sang de l’alliance que le Seigneur a faite avec vous selon toutes ces paroles.
9 Mose na Aroni, Nadabu na Abihu, pamoja na wazee sabini wa Israeli wakapanda mlimani,
Alors montèrent, Moïse et Aaron, Nadab et Abiu, et les soixante-dix anciens d’israël;
10 nao wakamwona Mungu wa Israeli. Chini ya miguu yake kulikuwa na kitu kama sakafu ya mawe ya yakuti samawi, iliyo safi kama anga angavu.
Et ils virent le Dieu d’Israël, et sous ses pieds comme un ouvrage de pierre de saphir, et comme le ciel, lorsqu’il est serein.
11 Lakini Mungu hakuinua mkono wake dhidi ya hawa viongozi wa Waisraeli; walimwona Mungu, nao wakala na kunywa.
Et Dieu ne lança pas sa main sur ceux des enfants d’Israël qui s’étaient retirés au loin; et ils virent Dieu, puis ils mangèrent et ils burent.
12 Bwana akamwambia Mose, “Panda uje kwangu huku mlimani na ukae hapa, nami nitakupa vibao vya mawe, vyenye sheria na amri ambazo nimeziandika ziwe mwongozo wao.”
Or le Seigneur dit à Moïse: Monte vers moi sur la montagne, et sois là: je te donnerai les tables de pierre, et la loi et les commandements que j’ai écrits, afin que tu les enseignes.
13 Basi Mose akaondoka na Yoshua mtumishi wake, naye Mose akapanda juu kwenye mlima wa Mungu.
Moïse et Josué son serviteur se levèrent; et Moïse montant sur la montagne de Dieu,
14 Mose akawaambia wazee wa Israeli, “Tungojeni hapa mpaka tutakapowarudia. Aroni na Huri wako pamoja nanyi, na kila aliye na neno aweza kuwaendea wao.”
Dit aux anciens; Attendez ici jusqu’à ce que nous retournions à vous. Vous avez Aaron et Hur avec vous; s’il naît quelque question, vous leur en ferez le rapport.
15 Mose alipopanda juu mlimani, wingu liliufunika huo mlima,
Et lorsque Moïse fut monté, la nuée couvrit la montagne.
16 nao utukufu wa Bwana ukatua juu ya Mlima Sinai. Kwa muda wa siku sita wingu lilifunika mlima, na siku ya saba Bwana akamwita Mose kutoka katikati ya lile wingu.
Et la gloire du Seigneur reposa sur Sinaï, le couvrant de la nuée pendant six jours; mais au septième jour il appela Moïse du milieu de l’obscurité.
17 Kwa Waisraeli utukufu wa Bwana ulionekana kama moto uteketezao juu ya mlima.
Or l’aspect de la gloire du Seigneur était comme un feu ardent sur le sommet de la montagne, en la présence des enfants d’Israël.
18 Kisha Mose akaingia ndani ya lile wingu alivyokuwa akipanda mlimani. Naye akakaa huko mlimani kwa muda wa siku arobaini, usiku na mchana.
Et Moïse étant entré au milieu de la nuée, monta sur la montagne, et il fut là quarante jours et quarante nuits.