< Kutoka 23 >

1 “Usieneze habari za uongo. Usimsaidie mtu mwovu kwa kuwa shahidi mwenye nia ya kudhuru wengine.
Thou schalt not resseyue a vois of leesyng, nether thou schalt ioyne thin hond, that thou seie fals witnessyng for a wickid man.
2 “Usifuate umati wa watu katika kutenda mabaya. Unapotoa ushahidi kwenye mashtaka, usipotoshe haki ukijumuika na umati wa watu,
Thou schalt not sue the cumpanye to do yuel, nether thou schalt ascente to the sentence of ful many men in doom, that thou go awey fro treuthe.
3 nawe usimpendelee mtu maskini katika mashtaka yake.
Also thou schalt not haue mercy of a pore man in a `cause, ethir doom.
4 “Kama ukikutana na maksai au punda wa adui yako anapotea, hakikisha umemrudisha kwake.
If thou meetist `the oxe of thin enemye, ethir the asse errynge, lede thou ayen to hym.
5 Ukiona punda wa mtu anayekuchukia ameanguka na mzigo wake, usimwache hapo alipoangukia; hakikisha kuwa umemsaidia.
If thou seest that the asse of hym that hatith thee liggyth vndir a burthun, thou schalt not passe, but thou schalt reise with hym.
6 “Usiwanyime haki watu wako walio maskini katika mashtaka yao.
Thou schalt not bowe in the doom of a pore man.
7 Ujiepushe na mashtaka ya uongo, wala usimuue mtu asiye na hatia au mtu mwaminifu, kwa maana sitamhesabia hana hatia yeye aliye na hatia.
Thou schalt fle a lesyng. Thou schalt not sle an innocent man, and iust; for Y am aduersarie to a wickid man.
8 “Usipokee rushwa, kwa kuwa rushwa hupofusha wale waonao, na kupinda maneno ya wenye haki.
Take thou not yiftis, that blynden also prudent men, and destryen the wordys of iust men.
9 “Usimwonee mgeni; ninyi wenyewe mnajua jinsi mgeni anavyojisikia, kwa sababu mlikuwa wageni Misri.
Thou schalt not be diseseful to a pilgrym, for ye knowen the soulis of comelyngis, for also ye weren pilgryms in the lond of Egipt.
10 “Kwa muda wa miaka sita mtapanda mashamba yenu na kuvuna mazao,
Sixe yeer thou schalt sowe thi lond, and thou schalt gadre fruytis therof;
11 lakini katika mwaka wa saba usiilime ardhi wala kuitumia, ili watu walio maskini miongoni mwenu waweze kupata chakula kutoka kwenye hayo mashamba, nao wanyama pori wapate chakula kwa yale mabaki watakayobakiza. Utafanya hivyo katika shamba lako la mizabibu na la mizeituni.
forsothe in the seuenthe yeer thou schalt leeue it, and schalt make to reste, that the pore men of thi puple ete, and what euer is residue, the beestis of the feeld ete; so thou schalt do in thi vyner, and in place of olyue trees.
12 “Kwa siku sita fanya kazi zako, lakini siku ya saba usifanye kazi, ili maksai wako na punda wako wapate kupumzika, naye mtumwa aliyezaliwa nyumbani mwako, pamoja na mgeni, wapate kustarehe.
Sixe dayes thou schalt worche, in the seuenthe dai thou schalt ceesse, that thin oxe and asse reste, and the sone of thin handmaide, and the comelyng be refreischid.
13 “Uzingatie kutenda kila kitu nilichokuambia. Usiombe kwa majina ya miungu mingine, wala usiyaruhusu kusikika kinywani mwako.
Kepe ye alle thingis, whiche Y seide to you; and ye schulen not swere bi the name of alien goddis, nether it schal be herd of youre mouth.
14 “Mara tatu kwa mwaka utanifanyia sikukuu.
In thre tymes bi alle yeeris ye schulen halewe feestis to me.
15 “Utaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu; kwa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu kama nilivyokuagiza. Fanya jambo hili kwa wakati uliopangwa katika mwezi wa Abibu, ndio mwezi wa nne, kwa sababu katika mwezi huo ulitoka Misri. “Mtu yeyote asije mbele yangu mikono mitupu.
Thou schalt kepe the solempnyte of therf looues; seuene daies thou schalt ete therf breed, as Y comaundide to thee, in the tyme of monethe of newe thingis, whanne thou yedist out of Egipt; thou schalt not appere voide in my siyt.
16 “Utaadhimisha Sikukuu ya Mavuno kwa malimbuko ya mazao yako uliyopanda katika shamba lako. “Utaadhimisha Sikukuu ya Kukusanya mavuno mwishoni mwa mwaka, unapokusanya mavuno yako toka shambani.
And thou schalt kepe the solempnete of the monethe of the firste thingis of thi werk, what euer thingis thou hast sowe in the feeld. Also thou schalt kepe the solempnyte in the goyng out of the yeer, whanne thou hast gaderid all thi fruytis of the feeld.
17 “Mara tatu kwa mwaka wanaume wote watakuja mbele za Bwana Mwenyezi.
Thries in the yeer al thi male kynde schal appere bifore thi Lord God.
18 “Msitoe damu ya dhabihu kwangu pamoja na kitu chochote kilicho na chachu. “Mafuta ya mnyama wa sadaka ya sikukuu yangu yasibakizwe mpaka asubuhi.
Thou schalt not offre the blood of thi slayn sacrifice on sour douy; nether the fatnesse of my solempnete schal dwelle til to the morewtid.
19 “Utaleta malimbuko bora ya ardhi yako katika nyumba ya Bwana Mungu wako. “Usimchemshe mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
Thou schalt bere the firste thingis of the fruytis of thi lond in to the hows of thi Lord God. Thou schalt not sethe a kide in the mylke of his modir.
20 “Tazama, ninamtuma malaika akutangulie mbele yako akulinde njiani na kukuleta mpaka mahali nilipoandaa.
Lo! Y schal sende myn aungel, that schal go bifore thee, and schal kepe in the weie, and schal lede to the place which Y haue maad redi to thee.
21 Mtamtii na kusikiliza kile anachokisema. Usiasi dhidi yake; hatakusamehe uasi wako, kwa maana Jina langu limo ndani yake.
Take thou hede to hym, and here thou his vois, nether gesse thou hym to be dispisid; for he schal not foryyue, whanne thou synnest, and my name is in him.
22 Kama ukitii kweli kweli kile asemacho na kufanya yote nisemayo, nitakuwa adui wa adui zako, na nitawapinga wale wakupingao.
For if thou herest his vois, and doist alle thingis whiche Y speke, Y schal be enemy to thin enemyes, and Y schal turment hem, that turmenten thee;
23 Malaika wangu atatangulia mbele yako na kukuleta katika nchi ya Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanaani, Wahivi na Wayebusi, nami nitawafutilia mbali.
and myn aungel schal go bifore thee, and he schal lede yn thee to Amorrei, and Ethei, and Ferezei, and Cananey, and Euey, and Jebusei, whiche Y schal breke.
24 Usiisujudie miungu yao, au kuiabudu, wala kufuata desturi yao. Utayabomoa kabisa na kuvunjavunja mawe yao ya ibada vipande vipande.
Thou schalt not onoure `the goddis of hem, nether thou schalt worschipe hem; thou schalt not do the werkis of hem, but thou schalt destrie the goddis, and thou schalt breke the ymagis of hem.
25 Utamwabudu Bwana Mungu wako, na baraka zake zitakuwa juu ya vyakula vyako na maji yako. Nami nitaondoa maradhi miongoni mwako,
And ye schulen serue to youre Lord God, that Y blesse thi looues, and watris, and do awei sikenesse fro the myddis of thee;
26 na hakuna atakayeharibu mimba wala atakayekuwa tasa katika nchi yako. Nami nitakupa maisha makamilifu.
neithir a womman vnfruytful, neither bareyn, schal be in thi lond; Y schal fille the noumbre of thi daies.
27 “Nitapeleka utisho wangu mbele yako na kufadhaisha kila taifa utakalolifikia. Nitafanya adui zako wote wakupe kisogo na kukimbia.
Y schal sende my drede in to thi biforgoyng, and Y schal sle al the puple, to which thou schalt entre, and Y schal turne the backis of alle thin enemyes bifore thee;
28 Nitatanguliza manyigu mbele yako kuwafukuza Wahivi, Wakanaani na Wahiti waondoke njiani mwako.
and Y schal sende out bifore scrabrouns, that schulen dryue awei Euey, and Cananey, and Ethei, bifore that thou entre.
29 Lakini sitawafukuza kwa mara moja, kwa sababu nchi itabaki ukiwa na wanyama pori watakuwa wengi mno kwako.
Y schal not caste hem out fro thi face in o yeer, lest the lond be turned in to wildirnesse, and beestis encreesse ayens thee;
30 Nitawafukuza kidogo kidogo mbele yako, mpaka uwe umeongezeka kiasi cha kutosha kuimiliki nchi.
litil and litil I schal caste hem out fro thi siyt, til thou be encreessid, and welde the loond.
31 “Nitaweka mipaka ya nchi yako kuanzia Bahari ya Shamu hadi Bahari ya Wafilisti, na kuanzia jangwani hadi Mto Frati. Nitawatia watu wanaoishi katika nchi hizo mikononi mwako, nawe utawafukuza watoke mbele yako.
Forsothe Y schal sette thi termys fro the reed see til to the see of Palestyns, and fro desert til to the flood. Y schal yyue to youre hondis the dwelleris of the lond, and Y schal caste hem out fro youre siyt;
32 Usifanye agano lolote nao wala na miungu yao.
thou schalt not make boond of pees with hem, nethir with `the goddis of hem.
33 Usiwaache waishi katika nchi yako, la sivyo watakusababisha utende dhambi dhidi yangu, kwa sababu ibada ya miungu yao hakika itakuwa mtego kwako.”
Dwelle thei not in thi lond, lest perauenture thei make thee to do synne ayens me, yf thou seruest her goddis, which thing certis schal be to thee in to sclaundir.

< Kutoka 23 >