< Kutoka 23 >
1 “Usieneze habari za uongo. Usimsaidie mtu mwovu kwa kuwa shahidi mwenye nia ya kudhuru wengine.
Thou shalt not accept a false report; extend not thy hand to the wicked, to be an unrighteous witness.
2 “Usifuate umati wa watu katika kutenda mabaya. Unapotoa ushahidi kwenye mashtaka, usipotoshe haki ukijumuika na umati wa watu,
Thou shalt not follow the multitude for evil; neither shalt thou answer in a cause, to go after the multitude to pervert [judgment].
3 nawe usimpendelee mtu maskini katika mashtaka yake.
Neither shalt thou favour a poor man in his cause.
4 “Kama ukikutana na maksai au punda wa adui yako anapotea, hakikisha umemrudisha kwake.
— If thou meet thine enemy's ox or his ass going astray, thou shalt certainly bring it back to him.
5 Ukiona punda wa mtu anayekuchukia ameanguka na mzigo wake, usimwache hapo alipoangukia; hakikisha kuwa umemsaidia.
If thou see the ass of him that hateth thee lying under its burden, beware of leaving [it] to him: thou shalt certainly loosen [it] with him.
6 “Usiwanyime haki watu wako walio maskini katika mashtaka yao.
Thou shalt not pervert the judgment of thy poor in his cause.
7 Ujiepushe na mashtaka ya uongo, wala usimuue mtu asiye na hatia au mtu mwaminifu, kwa maana sitamhesabia hana hatia yeye aliye na hatia.
Thou shalt keep far from the cause of falsehood; and the innocent and righteous slay not; for I will not justify the wicked.
8 “Usipokee rushwa, kwa kuwa rushwa hupofusha wale waonao, na kupinda maneno ya wenye haki.
And thou shalt take no bribe; for the bribe blindeth those whose eyes are open, and perverteth the words of the righteous.
9 “Usimwonee mgeni; ninyi wenyewe mnajua jinsi mgeni anavyojisikia, kwa sababu mlikuwa wageni Misri.
And the stranger thou shalt not oppress; for ye know the spirit of the stranger, for ye have been strangers in the land of Egypt.
10 “Kwa muda wa miaka sita mtapanda mashamba yenu na kuvuna mazao,
And six years thou shalt sow thy land, and gather in its produce;
11 lakini katika mwaka wa saba usiilime ardhi wala kuitumia, ili watu walio maskini miongoni mwenu waweze kupata chakula kutoka kwenye hayo mashamba, nao wanyama pori wapate chakula kwa yale mabaki watakayobakiza. Utafanya hivyo katika shamba lako la mizabibu na la mizeituni.
but in the seventh thou shalt let it rest and lie [fallow], that the poor of thy people may eat [of it]; and what they leave, the beasts of the field shall eat. In like manner thou shalt deal with thy vineyard, and with thine olive-tree.
12 “Kwa siku sita fanya kazi zako, lakini siku ya saba usifanye kazi, ili maksai wako na punda wako wapate kupumzika, naye mtumwa aliyezaliwa nyumbani mwako, pamoja na mgeni, wapate kustarehe.
— Six days thou shalt do thy work, but on the seventh day thou shalt rest; that thine ox and thine ass may rest, and the son of thy handmaid, and the stranger may be refreshed.
13 “Uzingatie kutenda kila kitu nilichokuambia. Usiombe kwa majina ya miungu mingine, wala usiyaruhusu kusikika kinywani mwako.
And ye shall be on your guard as to everything that I have said unto you; and shall make no mention of the name of other gods — it shall not be heard in thy mouth.
14 “Mara tatu kwa mwaka utanifanyia sikukuu.
Thrice in the year thou shalt celebrate a feast to me.
15 “Utaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu; kwa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu kama nilivyokuagiza. Fanya jambo hili kwa wakati uliopangwa katika mwezi wa Abibu, ndio mwezi wa nne, kwa sababu katika mwezi huo ulitoka Misri. “Mtu yeyote asije mbele yangu mikono mitupu.
Thou shalt keep the feast of unleavened bread, (thou shalt eat unleavened bread seven days, as I have commanded thee, in the time appointed of the month Abib; for in it thou camest out from Egypt; and none shall appear in my presence empty; )
16 “Utaadhimisha Sikukuu ya Mavuno kwa malimbuko ya mazao yako uliyopanda katika shamba lako. “Utaadhimisha Sikukuu ya Kukusanya mavuno mwishoni mwa mwaka, unapokusanya mavuno yako toka shambani.
and the feast of harvest, the first-fruits of thy labours which thou hast sown in the field, and the feast of in-gathering, at the end of the year, when thou gatherest in thy labours out of the field.
17 “Mara tatu kwa mwaka wanaume wote watakuja mbele za Bwana Mwenyezi.
Three times in the year all thy males shall appear in the presence of the Lord Jehovah.
18 “Msitoe damu ya dhabihu kwangu pamoja na kitu chochote kilicho na chachu. “Mafuta ya mnyama wa sadaka ya sikukuu yangu yasibakizwe mpaka asubuhi.
Thou shalt not offer the blood of my sacrifice with leavened bread; neither shall the fat of my feast remain all night until the morning.
19 “Utaleta malimbuko bora ya ardhi yako katika nyumba ya Bwana Mungu wako. “Usimchemshe mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
The first of the first-fruits of thy land thou shalt bring into the house of Jehovah thy God. Thou shalt not boil a kid in its mother's milk.
20 “Tazama, ninamtuma malaika akutangulie mbele yako akulinde njiani na kukuleta mpaka mahali nilipoandaa.
Behold, I send an Angel before thee, to keep thee in the way, and to bring thee to the place that I have prepared.
21 Mtamtii na kusikiliza kile anachokisema. Usiasi dhidi yake; hatakusamehe uasi wako, kwa maana Jina langu limo ndani yake.
Be careful in his presence, and hearken unto his voice: do not provoke him, for he will not forgive your transgressions; for my name is in him.
22 Kama ukitii kweli kweli kile asemacho na kufanya yote nisemayo, nitakuwa adui wa adui zako, na nitawapinga wale wakupingao.
But if thou shalt diligently hearken unto his voice, and do all that I shall say, then I will be an enemy to thine enemies, and an adversary to thine adversaries.
23 Malaika wangu atatangulia mbele yako na kukuleta katika nchi ya Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanaani, Wahivi na Wayebusi, nami nitawafutilia mbali.
For mine Angel shall go before thee, and bring thee in unto the Amorites and the Hittites and the Perizzites and the Canaanites, the Hivites and the Jebusites; and I will cut them off.
24 Usiisujudie miungu yao, au kuiabudu, wala kufuata desturi yao. Utayabomoa kabisa na kuvunjavunja mawe yao ya ibada vipande vipande.
Thou shalt not bow down to their gods, nor serve them, nor do after their deeds; but thou shalt utterly destroy them, and utterly shatter their statues.
25 Utamwabudu Bwana Mungu wako, na baraka zake zitakuwa juu ya vyakula vyako na maji yako. Nami nitaondoa maradhi miongoni mwako,
And ye shall serve Jehovah your God; and he shall bless thy bread and thy water; and I will take sickness away from thy midst.
26 na hakuna atakayeharibu mimba wala atakayekuwa tasa katika nchi yako. Nami nitakupa maisha makamilifu.
There shall nothing cast their young, nor be barren, in thy land; the number of thy days will I fulfil.
27 “Nitapeleka utisho wangu mbele yako na kufadhaisha kila taifa utakalolifikia. Nitafanya adui zako wote wakupe kisogo na kukimbia.
I will send my fear before thee, and confound every people to which thou comest, and will make all thine enemies turn their back to thee.
28 Nitatanguliza manyigu mbele yako kuwafukuza Wahivi, Wakanaani na Wahiti waondoke njiani mwako.
And I will send hornets before thee, which shall drive out the Hivite, the Canaanite, and the Hittite, from before thee.
29 Lakini sitawafukuza kwa mara moja, kwa sababu nchi itabaki ukiwa na wanyama pori watakuwa wengi mno kwako.
I will not drive them out from before thee in one year: lest the land become desolate, and the beast of the field multiply against thee.
30 Nitawafukuza kidogo kidogo mbele yako, mpaka uwe umeongezeka kiasi cha kutosha kuimiliki nchi.
By little and little I will drive them out from before thee, until thou art fruitful, and possess the land.
31 “Nitaweka mipaka ya nchi yako kuanzia Bahari ya Shamu hadi Bahari ya Wafilisti, na kuanzia jangwani hadi Mto Frati. Nitawatia watu wanaoishi katika nchi hizo mikononi mwako, nawe utawafukuza watoke mbele yako.
And I will set thy bounds from the Red Sea even unto the sea of the Philistines, and from the wilderness unto the river; for I will give the inhabitants of the land into your hand, that thou mayest dispossess them from before thee.
32 Usifanye agano lolote nao wala na miungu yao.
Thou shalt make no covenant with them, nor with their gods.
33 Usiwaache waishi katika nchi yako, la sivyo watakusababisha utende dhambi dhidi yangu, kwa sababu ibada ya miungu yao hakika itakuwa mtego kwako.”
They shall not dwell in thy land, lest they make thee sin against me; for if thou serve their gods, it is sure to be a snare unto thee.