< Kutoka 22 >
1 “Kama mtu akiiba maksai au kondoo na kumchinja au kumuuza, ni lazima alipe ngʼombe watano badala ya maksai mmoja na kondoo wanne badala ya kondoo mmoja.
Ja kas vērsi vai avi zog un to nokauj vai pārdod, tam būs atdot piecus vēršus par vienu vērsi un četras avis par vienu avi.
2 “Kama mwizi akishikwa anavunja nyumba akapigwa hata akafa, aliyemuua hana hatia ya kumwaga damu;
Ja zaglis kur top atrasts ielauzies, un top sists, ka mirst, tad viņa asinis nebūs atriebt.
3 lakini jambo hilo likitokea wakati jua limechomoza, huyo mtu atakuwa na hatia ya kumwaga damu. “Mwizi huyo sharti alipe, lakini kama hana kitu, lazima auzwe ili alipe kwa ajili ya wizi wake.
Ja saule pār to zagli ir uzlēkusi, tad viņa asinis būs atriebt. Zaglis lai atdod. Ja tam nav, tad tam būs tapt pārdotam savas zādzības dēļ.
4 “Kama mnyama aliyeibwa akikutwa hai mikononi mwake, ikiwa ni maksai au punda au kondoo, lazima alipe mara mbili.
Ja zagtais lops viņa rokā top atrasts dzīvs, lai tas ir vērsis vai ēzelis vai avs, tad tam to būs atdot divkārtīgi.
5 “Kama mtu akichunga mifugo yake katika shamba au shamba la mizabibu, na akawaachia wajilishe katika shamba la mtu mwingine, ni lazima alipe vitu bora kutoka kwenye shamba lake mwenyewe au kutoka shamba lake la mizabibu.
Ja kas kādu tīrumu vai vīna dārzu nogana un tur palaiž savu lopu, ka ēd cita tīrumā, tam par to būs atdot to labāko no sava tīruma un to labāko no sava vīna dārza.
6 “Kama moto ukiwaka na kuenea kwenye vichaka vya miiba na kuteketeza miganda ya nafaka au nafaka ambayo haijavunwa, au kuteketeza shamba lote, mtu yule aliyewasha moto lazima alipe.
Kad uguns izceļas un aizņem ērkšķus, ka labības guba vai druva vai tīrums sadeg, tad tam, kas to uguni iededzinājis, būs pilnīgi atdot.
7 “Kama mtu akimpa jirani yake fedha au mali nyingine amtunzie, na kama vikiibwa kutoka nyumba ya huyo jirani, kama mwizi atashikwa, lazima alipe mara mbili.
Ja kas savam tuvākam dod glabāt naudu vai lietas, un tās top izzagtas no tā vīra nama, - ja tas zaglis top atrasts, tam divkārtīgi to būs atdot.
8 Lakini mwizi asipopatikana, mwenye nyumba atafika mbele ya waamuzi ili kuthibitisha kuwa hakuchukua mali ya mwenzake.
Ja tas zaglis netop atrasts, tad to nama kungu būs vest Dieva priekšā, vai tas pats nav licis savu roku pie sava tuvākā mantas.
9 Pakiwepo jambo lolote la mali isiyo halali, ikiwa ni maksai, punda, kondoo, mavazi, ama mali yoyote iliyopotea ambayo fulani atasema, ‘Hii ni mali yangu,’ pande zote mbili wataleta mashauri yao mbele ya waamuzi. Yule ambaye waamuzi watamwona kuwa na hatia atamlipa jirani yake mara mbili.
Ikviena sūdzības lieta par vērsi, par ēzeli, par avi, par drēbēm, par ikvienu pazudušu lietu, ko kurš saka savu esam, lai nāk Dieva priekšā; kuru nu Dievs notiesā, tam divkārtīgi būs atdot savam tuvākam.
10 “Kama mtu akimpa jirani yake punda, ngʼombe, kondoo au mnyama mwingine yeyote amtunzie, akifa au akijeruhiwa au akichukuliwa wakati haonekani na mtu yeyote,
Ja kas savam tuvākam dod glabāt ēzeli vai vērsi vai avi vai citu kādu lopu, un tas nosprāgst vai top ievainots vai nodzīts, ka neviens to neredz,
11 jambo hili kati yao wawili litaamuliwa kwa kuapa kiapo mbele za Bwana, kwamba huyo jirani hakuhusika na wizi wa mali ya jirani yake. Mwenye mali itampasa akubali jambo hili, na hakuna malipo yatakayohitajika.
Tad pie Tā Kunga jānozvēras abu starpā, vai tas savu roku pats nav licis pie sava tuvākā mantas, un (tā lopa) kungam būs to pieņemt un tam (glabātajam) to nebūs atmaksāt.
12 Lakini kama mnyama aliibwa kwa jirani, itampasa amlipe mwenye mnyama.
Bet ja tas (lops) tam (glabātajam) zagšus top nozagts, tad lai tā (lopa) kungam to atmaksā.
13 Kama ameraruliwa na mnyama pori, ataleta mabaki ya mnyama kama ushahidi, naye hatadaiwa kulipa mnyama aliyeraruliwa.
Ja ir saplosīts, tad būs dot liecību par to, un tad to saplosīto nebūs maksāt.
14 “Kama mtu akimwazima mnyama kutoka kwa jirani yake, na kama akiumia au akafa na mwenye mnyama hayupo, lazima amlipe huyo mnyama.
Un ja kas no sava tuvākā (lopu) aizņēmās un šis top ievainots vai nosprāgst viņa kungam klātu neesot, tad to būs atmaksāt.
15 Lakini mwenye mnyama akiwa angalipo na mnyama wake, mwazimaji hatalazimika kumlipa. Kama mnyama alikuwa amekodishwa, fedha iliyolipwa kwa kukodisha inatosha kwa kufidia hasara.
Ja viņa kungs bijis klātu, tad nebūs atmaksāt; ja tas (lops) par naudu ņemts, tad tas caur to maksu ir aizmaksāts.
16 “Kama mtu akimshawishi bikira ambaye hajaposwa na akilala naye, lazima alipe mahari, kisha atamwoa msichana huyo.
Ja kas meitu pieviļ, kas vēl nav saderēta, un pie tās guļ, tad lai viņai to kroņa naudu dod un lai viņu ņem par sievu.
17 Baba wa msichana akikataa katakata kumpa huyo mtu huyo msichana wake, bado ni lazima huyo mtu atalipa mahari kama inavyostahili malipo ya ubikira.
Bet ja viņas tēvs liedzās viņam to dot, tad lai to naudu dod, cik tai meitai kroņa naudas pienākas.
18 “Usiruhusu mwanamke mchawi aishi.
Burvi tev nebūs pamest dzīvu.
19 “Mtu yeyote aziniye na mnyama lazima auawe.
Visiem, kas ar kādu lopu jaucās, būs tapt nokautiem.
20 “Mtu awaye yote anayemtolea mungu mwingine dhabihu isipokuwa Bwana, lazima aangamizwe.
Kas upurē svešiem dieviem, un ne Tam Kungam vien, tam būs būt nolādētam.
21 “Usimtendee mgeni vibaya au kumwonea, kwa kuwa nanyi mlikuwa wageni huko Misri.
Tev arī nevienu svešinieku nebūs ne dragāt, ne spaidīt, jo jūs esat bijuši svešinieki Ēģiptes zemē.
22 “Usimdhulumu mjane wala yatima.
Tev nevienu atraitni un nevienu bāriņu nebūs apbēdināt.
23 Kama ukifanya hivyo nao wakinililia, hakika nitasikia kilio chao.
Ja tu kaut kā to apbēdināsi, un tā brēkdama uz Mani brēks, tad Es klausīt paklausīšu viņas brēkšanu.
24 Hasira yangu itawaka, nami nitawaua kwa upanga, wake zenu watakuwa wajane na watoto wenu watakuwa yatima.
Un Mana bardzība iedegsies, un Es jūs nokaušu ar zobenu, un jūsu sievām būs tapt par atraitnēm un jūsu bērniem par bāriņiem.
25 “Kama ukimkopesha mmojawapo wa watu wangu fedha ambaye ni mhitaji, usiwe kama mtu mkopesha fedha; usimtoze riba.
Ja tu Maniem ļaudīm, kas ir pie tevis par nabagiem, naudu aizdod, tad neesi pret tiem, kā kāds pagaidu plēsējs; tev par to nebūs augļus dzīt.
26 Kama ukichukua vazi la jirani kama rehani, ulirudishe kwake kabla jua kuzama,
Ja tu sava tuvākā drēbes ķīlā ņem, tad tev tās viņam būs atdot, pirms saule noiet;
27 kwa kuwa vazi lake ndilo pekee alilo nalo la kumfunika mwili wake. Ni nini kingine atajifunika nacho? Atakaponililia, nitasikia, kwa kuwa nina huruma.
Jo tās ir viņa vienīgais apsegs, tās ir tās drēbes pār viņa miesām, iekš kā viņš būtu gulējis; bet kad tas uz Mani brēks, tad Es to klausīšu, jo Es esmu žēlīgs.
28 “Usimkufuru Mungu au kumlaani mtawala wa watu wako.
Dievu tev nebūs zaimot, un savu ļaužu virsnieku tev nebūs lādēt.
29 “Usiache kutoa sadaka kutoka ghala lako au mapipa yako. “Lazima unipe mzaliwa wa kwanza wa wana wako.
Savus pirmajus augļus no labības un vīna tev nebūs aizturēt, to pirmdzimušo no saviem dēliem tev Man būs dot.
30 Ufanye vivyo hivyo kwa ngʼombe wako na kwa kondoo wako. Waache wakae na mama zao kwa siku saba, lakini siku ya nane unipe.
Tāpat tev būs darīt ar savu vērsi un ar savām avīm; septiņas dienas tiem būs būt pie savas mātes un astotā dienā tev tos Man būs atdot.
31 “Ninyi mtakuwa watu wangu watakatifu. Kwa hiyo msile nyama ya mnyama aliyeraruliwa na wanyama pori; mtupieni mbwa.
Jums būs svētiem ļaudīm būt Manā priekšā; tāpēc jums nebūs ēst tādas miesas gaļu, kas laukā ir saplosīta; jums to būs mest suņiem priekšā.