< Kutoka 22 >

1 “Kama mtu akiiba maksai au kondoo na kumchinja au kumuuza, ni lazima alipe ngʼombe watano badala ya maksai mmoja na kondoo wanne badala ya kondoo mmoja.
Si quelqu’un vole un bœuf ou une brebis, et qu’il les tue ou les vende, il restituera cinq bœufs pour un bœuf et quatre brebis pour une brebis.
2 “Kama mwizi akishikwa anavunja nyumba akapigwa hata akafa, aliyemuua hana hatia ya kumwaga damu;
Si le voleur est trouvé forçant une maison ou la minant, et qu’il meure d’une blessure reçue, celui qui l’a frappé ne sera pas coupable de son sang.
3 lakini jambo hilo likitokea wakati jua limechomoza, huyo mtu atakuwa na hatia ya kumwaga damu. “Mwizi huyo sharti alipe, lakini kama hana kitu, lazima auzwe ili alipe kwa ajili ya wizi wake.
Que s’il a fait cela, le soleil levé, il a commis un homicide, et il mourra lui-même. S’il n’a pas de quoi rendre pour le larcin, il sera vendu lui-même.
4 “Kama mnyama aliyeibwa akikutwa hai mikononi mwake, ikiwa ni maksai au punda au kondoo, lazima alipe mara mbili.
Si ce qu’il a volé est trouvé chez lui, vivant, soit un bœuf, soit un âne, soit une brebis, il restituera le double.
5 “Kama mtu akichunga mifugo yake katika shamba au shamba la mizabibu, na akawaachia wajilishe katika shamba la mtu mwingine, ni lazima alipe vitu bora kutoka kwenye shamba lake mwenyewe au kutoka shamba lake la mizabibu.
Si quelqu’un endommage un champ ou une vigne, et qu’il laisse aller sa bête, pour qu’elle paisse ce qui est à autrui, il rendra tout ce qu’il aura de meilleur dans son champ, ou dans sa vigne, selon l’estimation du dommage.
6 “Kama moto ukiwaka na kuenea kwenye vichaka vya miiba na kuteketeza miganda ya nafaka au nafaka ambayo haijavunwa, au kuteketeza shamba lote, mtu yule aliyewasha moto lazima alipe.
Si un feu qui s’élève trouve des épines et gagne un tas de gerbes, ou bien les blés sur pied dans les champs, celui qui a allumé le feu réparera le dommage.
7 “Kama mtu akimpa jirani yake fedha au mali nyingine amtunzie, na kama vikiibwa kutoka nyumba ya huyo jirani, kama mwizi atashikwa, lazima alipe mara mbili.
Si quelqu’un confie en garde à son ami de l’argent ou un objet quelconque, et qu’il soit volé à celui qui l’a reçu, si le voleur est trouvé, il rendra le double.
8 Lakini mwizi asipopatikana, mwenye nyumba atafika mbele ya waamuzi ili kuthibitisha kuwa hakuchukua mali ya mwenzake.
Si le voleur reste inconnu, le maître de la maison sera conduit aux dieux, et il jurera qu’il n’a pas étendu sa main sur le bien de son prochain,
9 Pakiwepo jambo lolote la mali isiyo halali, ikiwa ni maksai, punda, kondoo, mavazi, ama mali yoyote iliyopotea ambayo fulani atasema, ‘Hii ni mali yangu,’ pande zote mbili wataleta mashauri yao mbele ya waamuzi. Yule ambaye waamuzi watamwona kuwa na hatia atamlipa jirani yake mara mbili.
Pour commettre le vol, soit d’un bœuf, soit d’un âne, d’une brebis, d’un vêtement et de tout ce qui peut porter dommage; c’est devant les dieux que viendra la cause de l’un et de l’autre; et si ceux-ci le condamnent, il restituera le double à son prochain.
10 “Kama mtu akimpa jirani yake punda, ngʼombe, kondoo au mnyama mwingine yeyote amtunzie, akifa au akijeruhiwa au akichukuliwa wakati haonekani na mtu yeyote,
Si quelqu’un confie en garde à son prochain un âne, un bœuf, une brebis, ou toute autre bête, et qu’elle meure, ou dépérisse, ou bien soit prise par les ennemis, et que personne ne l’ait vu,
11 jambo hili kati yao wawili litaamuliwa kwa kuapa kiapo mbele za Bwana, kwamba huyo jirani hakuhusika na wizi wa mali ya jirani yake. Mwenye mali itampasa akubali jambo hili, na hakuna malipo yatakayohitajika.
Interviendra le serment qu’il n’a pas étendu sa main sur le bien de son prochain, et le maître recevra le serment, et celui-là ne sera pas contraint de rendre.
12 Lakini kama mnyama aliibwa kwa jirani, itampasa amlipe mwenye mnyama.
Que si c’est par un vol que la bête a été enlevée, il réparera le dommage envers le maître.
13 Kama ameraruliwa na mnyama pori, ataleta mabaki ya mnyama kama ushahidi, naye hatadaiwa kulipa mnyama aliyeraruliwa.
Si elle a été mangée par une bête sauvage, qu’il lui apporte ce qui sera resté, et il ne restituera pas.
14 “Kama mtu akimwazima mnyama kutoka kwa jirani yake, na kama akiumia au akafa na mwenye mnyama hayupo, lazima amlipe huyo mnyama.
Si quelqu’un demande en prêt à son prochain quelqu’une de ses bêtes, et qu’elle dépérisse ou meure, le maître n’étant pas présent, il sera forcé de la rendre.
15 Lakini mwenye mnyama akiwa angalipo na mnyama wake, mwazimaji hatalazimika kumlipa. Kama mnyama alikuwa amekodishwa, fedha iliyolipwa kwa kukodisha inatosha kwa kufidia hasara.
Que si le maître se trouve présent, il ne restituera pas, surtout s’il était venu la louer, pour le prix de son travail.
16 “Kama mtu akimshawishi bikira ambaye hajaposwa na akilala naye, lazima alipe mahari, kisha atamwoa msichana huyo.
Si quelqu’un séduit une vierge non encore fiancée, et dort avec elle, il la dotera et la prendra pour femme.
17 Baba wa msichana akikataa katakata kumpa huyo mtu huyo msichana wake, bado ni lazima huyo mtu atalipa mahari kama inavyostahili malipo ya ubikira.
Si le père de la vierge ne veut pas la donner, il rendra de l’argent selon la dot que les vierges ont coutume de recevoir.
18 “Usiruhusu mwanamke mchawi aishi.
Tu ne laisseras pas vivre ceux qui usent de maléfices.
19 “Mtu yeyote aziniye na mnyama lazima auawe.
Que celui qui commet un crime avec une bête, meure de mort.
20 “Mtu awaye yote anayemtolea mungu mwingine dhabihu isipokuwa Bwana, lazima aangamizwe.
Celui qui sacrifie à d’autres dieux qu’au Seigneur seul sera mis à mort.
21 “Usimtendee mgeni vibaya au kumwonea, kwa kuwa nanyi mlikuwa wageni huko Misri.
Tu ne contristeras point l’étranger, et tu ne l’affligeras point; car vous avez été étrangers vous-mêmes dans la terre d’Egypte.
22 “Usimdhulumu mjane wala yatima.
Vous ne nuirez point à la veuve et à l’orphelin.
23 Kama ukifanya hivyo nao wakinililia, hakika nitasikia kilio chao.
Si vous les offensez, ils crieront fortement vers moi, et j’entendrai leur clameur;
24 Hasira yangu itawaka, nami nitawaua kwa upanga, wake zenu watakuwa wajane na watoto wenu watakuwa yatima.
Et ma fureur s’indignera, puis je vous frapperai du glaive, et vos femmes seront veuves et vos fils orphelins.
25 “Kama ukimkopesha mmojawapo wa watu wangu fedha ambaye ni mhitaji, usiwe kama mtu mkopesha fedha; usimtoze riba.
Si tu prêtes de l’argent à mon peuple pauvre qui habite avec toi, tu ne le presseras point comme un exacteur, et tu ne l’accableras point d’usures.
26 Kama ukichukua vazi la jirani kama rehani, ulirudishe kwake kabla jua kuzama,
Si tu prends en gage de ton prochain un vêtement, tu lui rendras avant le coucher du soleil.
27 kwa kuwa vazi lake ndilo pekee alilo nalo la kumfunika mwili wake. Ni nini kingine atajifunika nacho? Atakaponililia, nitasikia, kwa kuwa nina huruma.
Car c’est le seul dont il se couvre, le seul vêtement de sa chair, et il n’en a pas un autre dans lequel il dorme: s’il crie vers moi, je l’exaucerai, parce que je suis miséricordieux.
28 “Usimkufuru Mungu au kumlaani mtawala wa watu wako.
Tu ne parleras point mal des dieux, et tu ne maudiras point le prince de ton peuple.
29 “Usiache kutoa sadaka kutoka ghala lako au mapipa yako. “Lazima unipe mzaliwa wa kwanza wa wana wako.
Tu ne différeras point à rendre tes dîmes et tes prémices: tu me donneras le premier-né de tes fils.
30 Ufanye vivyo hivyo kwa ngʼombe wako na kwa kondoo wako. Waache wakae na mama zao kwa siku saba, lakini siku ya nane unipe.
Pour tes bœufs aussi et tes brebis tu feras de même: que pendant sept jours le premier-né soit avec sa mère, et au huitième jour tu me le rendras.
31 “Ninyi mtakuwa watu wangu watakatifu. Kwa hiyo msile nyama ya mnyama aliyeraruliwa na wanyama pori; mtupieni mbwa.
Vous me serez des hommes consacrés; vous ne mangerez point de la chair dont les bêtes sauvages auront déjà goûté, mais vous la jetterez aux chiens.

< Kutoka 22 >