< Kutoka 22 >

1 “Kama mtu akiiba maksai au kondoo na kumchinja au kumuuza, ni lazima alipe ngʼombe watano badala ya maksai mmoja na kondoo wanne badala ya kondoo mmoja.
« Si un homme vole un bœuf ou une brebis, et le tue ou le vend, il paiera cinq bœufs pour un bœuf, et quatre brebis pour une brebis.
2 “Kama mwizi akishikwa anavunja nyumba akapigwa hata akafa, aliyemuua hana hatia ya kumwaga damu;
Si le voleur est trouvé en train d'entrer par effraction, et qu'il soit frappé de telle sorte qu'il meure, il ne sera pas coupable d'effusion de sang pour lui.
3 lakini jambo hilo likitokea wakati jua limechomoza, huyo mtu atakuwa na hatia ya kumwaga damu. “Mwizi huyo sharti alipe, lakini kama hana kitu, lazima auzwe ili alipe kwa ajili ya wizi wake.
Si le soleil s'est levé sur lui, il est coupable d'effusion de sang. Il devra le restituer. S'il n'a rien, il sera vendu pour son vol.
4 “Kama mnyama aliyeibwa akikutwa hai mikononi mwake, ikiwa ni maksai au punda au kondoo, lazima alipe mara mbili.
Si le bien volé est trouvé vivant entre ses mains, qu'il s'agisse d'un bœuf, d'un âne ou d'un mouton, il paiera le double.
5 “Kama mtu akichunga mifugo yake katika shamba au shamba la mizabibu, na akawaachia wajilishe katika shamba la mtu mwingine, ni lazima alipe vitu bora kutoka kwenye shamba lake mwenyewe au kutoka shamba lake la mizabibu.
« Si un homme fait paître un champ ou une vigne en laissant son animal en liberté, et que celui-ci paisse dans le champ d'un autre homme, il devra le restituer sur le meilleur de son champ et sur le meilleur de sa vigne.
6 “Kama moto ukiwaka na kuenea kwenye vichaka vya miiba na kuteketeza miganda ya nafaka au nafaka ambayo haijavunwa, au kuteketeza shamba lote, mtu yule aliyewasha moto lazima alipe.
« Si un feu éclate et s'accroche à des épines, de sorte que les chocs du grain, le grain sur pied ou le champ soient consumés, celui qui a allumé le feu devra le restituer.
7 “Kama mtu akimpa jirani yake fedha au mali nyingine amtunzie, na kama vikiibwa kutoka nyumba ya huyo jirani, kama mwizi atashikwa, lazima alipe mara mbili.
« Si un homme livre à son prochain de l'argent ou des objets à garder, et qu'on les vole dans la maison de cet homme, si le voleur est trouvé, il paiera le double.
8 Lakini mwizi asipopatikana, mwenye nyumba atafika mbele ya waamuzi ili kuthibitisha kuwa hakuchukua mali ya mwenzake.
Si le voleur n'est pas trouvé, le maître de la maison s'approchera de Dieu, pour savoir s'il a mis la main sur les biens de son prochain.
9 Pakiwepo jambo lolote la mali isiyo halali, ikiwa ni maksai, punda, kondoo, mavazi, ama mali yoyote iliyopotea ambayo fulani atasema, ‘Hii ni mali yangu,’ pande zote mbili wataleta mashauri yao mbele ya waamuzi. Yule ambaye waamuzi watamwona kuwa na hatia atamlipa jirani yake mara mbili.
Pour toute affaire de dépouillement, qu'il s'agisse d'un bœuf, d'un âne, d'un mouton, d'un vêtement, ou de toute autre chose perdue, au sujet de laquelle quelqu'un dit: « Ceci est à moi », la cause des deux parties sera portée devant Dieu. Celui que Dieu condamne devra payer le double à son prochain.
10 “Kama mtu akimpa jirani yake punda, ngʼombe, kondoo au mnyama mwingine yeyote amtunzie, akifa au akijeruhiwa au akichukuliwa wakati haonekani na mtu yeyote,
« Si un homme livre à son prochain un âne, un bœuf, un mouton, ou tout autre animal à garder, et qu'il meure, soit blessé, soit chassé, sans que personne ne le voie,
11 jambo hili kati yao wawili litaamuliwa kwa kuapa kiapo mbele za Bwana, kwamba huyo jirani hakuhusika na wizi wa mali ya jirani yake. Mwenye mali itampasa akubali jambo hili, na hakuna malipo yatakayohitajika.
le serment de Yahvé sera entre eux deux: il n'a pas mis la main sur le bien de son prochain; son propriétaire l'acceptera, et il ne le restituera pas.
12 Lakini kama mnyama aliibwa kwa jirani, itampasa amlipe mwenye mnyama.
Mais s'il lui est volé, celui qui a volé devra le restituer à son propriétaire.
13 Kama ameraruliwa na mnyama pori, ataleta mabaki ya mnyama kama ushahidi, naye hatadaiwa kulipa mnyama aliyeraruliwa.
S'il est déchiré en morceaux, qu'il l'apporte comme preuve. Il ne restituera pas ce qui a été déchiré.
14 “Kama mtu akimwazima mnyama kutoka kwa jirani yake, na kama akiumia au akafa na mwenye mnyama hayupo, lazima amlipe huyo mnyama.
Si un homme emprunte un objet à son prochain, et que cet objet se blesse ou meurt sans que son propriétaire soit avec lui, il devra le restituer.
15 Lakini mwenye mnyama akiwa angalipo na mnyama wake, mwazimaji hatalazimika kumlipa. Kama mnyama alikuwa amekodishwa, fedha iliyolipwa kwa kukodisha inatosha kwa kufidia hasara.
Si son propriétaire est avec elle, il ne la restituera pas. Si c'est un objet loué, il est venu pour son bail.
16 “Kama mtu akimshawishi bikira ambaye hajaposwa na akilala naye, lazima alipe mahari, kisha atamwoa msichana huyo.
Si un homme séduit une vierge qui n'est pas promise au mariage et couche avec elle, il paiera une dot pour qu'elle devienne sa femme.
17 Baba wa msichana akikataa katakata kumpa huyo mtu huyo msichana wake, bado ni lazima huyo mtu atalipa mahari kama inavyostahili malipo ya ubikira.
Si son père refuse catégoriquement de la lui donner, il paiera une somme d'argent correspondant à la dot des vierges.
18 “Usiruhusu mwanamke mchawi aishi.
« Tu ne permettras pas à une sorcière de vivre.
19 “Mtu yeyote aziniye na mnyama lazima auawe.
« Celui qui aura des rapports sexuels avec un animal sera puni de mort.
20 “Mtu awaye yote anayemtolea mungu mwingine dhabihu isipokuwa Bwana, lazima aangamizwe.
« Celui qui sacrifie à un dieu quelconque, sauf à Yahvé seul, sera anéanti.
21 “Usimtendee mgeni vibaya au kumwonea, kwa kuwa nanyi mlikuwa wageni huko Misri.
« Tu ne feras pas tort à un étranger et tu ne l'opprimeras pas, car vous étiez des étrangers dans le pays d'Égypte.
22 “Usimdhulumu mjane wala yatima.
« Vous ne profiterez d'aucune veuve ni d'aucun orphelin.
23 Kama ukifanya hivyo nao wakinililia, hakika nitasikia kilio chao.
Si tu en profites, et qu'ils crient vers moi, j'entendrai leur cri;
24 Hasira yangu itawaka, nami nitawaua kwa upanga, wake zenu watakuwa wajane na watoto wenu watakuwa yatima.
ma colère s'enflammera, et je vous tuerai par l'épée; vos femmes seront veuves, et vos enfants orphelins.
25 “Kama ukimkopesha mmojawapo wa watu wangu fedha ambaye ni mhitaji, usiwe kama mtu mkopesha fedha; usimtoze riba.
« Si tu prêtes de l'argent à un pauvre de mon peuple qui est avec toi, tu ne seras pas pour lui un créancier. Tu ne lui demanderas pas d'intérêt.
26 Kama ukichukua vazi la jirani kama rehani, ulirudishe kwake kabla jua kuzama,
Si tu prends en gage le vêtement de ton prochain, tu le lui rendras avant le coucher du soleil,
27 kwa kuwa vazi lake ndilo pekee alilo nalo la kumfunika mwili wake. Ni nini kingine atajifunika nacho? Atakaponililia, nitasikia, kwa kuwa nina huruma.
car c'est sa seule couverture, c'est son vêtement pour sa peau. Dans quoi dormira-t-il? S'il crie vers moi, j'entendrai, car je suis miséricordieux.
28 “Usimkufuru Mungu au kumlaani mtawala wa watu wako.
« Tu ne blasphémeras pas Dieu et tu ne maudiras pas un chef de ton peuple.
29 “Usiache kutoa sadaka kutoka ghala lako au mapipa yako. “Lazima unipe mzaliwa wa kwanza wa wana wako.
« Tu ne tarderas pas à offrir de ta récolte et de l'écoulement de tes presses. « Vous me donnerez le premier-né de vos fils.
30 Ufanye vivyo hivyo kwa ngʼombe wako na kwa kondoo wako. Waache wakae na mama zao kwa siku saba, lakini siku ya nane unipe.
Tu feras de même avec ton bétail et avec tes brebis. Il restera sept jours avec sa mère, puis le huitième jour, vous me le donnerez.
31 “Ninyi mtakuwa watu wangu watakatifu. Kwa hiyo msile nyama ya mnyama aliyeraruliwa na wanyama pori; mtupieni mbwa.
« Vous serez pour moi des hommes saints, c'est pourquoi vous ne mangerez pas de viande déchirée par les animaux dans les champs. Vous la jetterez aux chiens.

< Kutoka 22 >