< Kutoka 22 >

1 “Kama mtu akiiba maksai au kondoo na kumchinja au kumuuza, ni lazima alipe ngʼombe watano badala ya maksai mmoja na kondoo wanne badala ya kondoo mmoja.
for to steal man: anyone cattle or sheep and to slaughter him or to sell him five cattle to complete underneath: instead [the] cattle and four flock underneath: instead [the] sheep
2 “Kama mwizi akishikwa anavunja nyumba akapigwa hata akafa, aliyemuua hana hatia ya kumwaga damu;
if in/on/with breaking to find [the] thief and to smite and to die nothing to/for him blood
3 lakini jambo hilo likitokea wakati jua limechomoza, huyo mtu atakuwa na hatia ya kumwaga damu. “Mwizi huyo sharti alipe, lakini kama hana kitu, lazima auzwe ili alipe kwa ajili ya wizi wake.
if to rise [the] sun upon him blood to/for him to complete to complete if nothing to/for him and to sell in/on/with theft his
4 “Kama mnyama aliyeibwa akikutwa hai mikononi mwake, ikiwa ni maksai au punda au kondoo, lazima alipe mara mbili.
if to find to find in/on/with hand: power his [the] theft from cattle till donkey till sheep alive two to complete
5 “Kama mtu akichunga mifugo yake katika shamba au shamba la mizabibu, na akawaachia wajilishe katika shamba la mtu mwingine, ni lazima alipe vitu bora kutoka kwenye shamba lake mwenyewe au kutoka shamba lake la mizabibu.
for be brutish man: anyone land: country or vineyard and to send: let go [obj] (cattle his *Q(K)*) and be brutish in/on/with land: country another best land: country his and best vineyard his to complete
6 “Kama moto ukiwaka na kuenea kwenye vichaka vya miiba na kuteketeza miganda ya nafaka au nafaka ambayo haijavunwa, au kuteketeza shamba lote, mtu yule aliyewasha moto lazima alipe.
for to come out: issue fire and to find thorn and to eat stack or [the] standing grain or [the] land: country to complete to complete [the] to burn: burn [obj] [the] fire
7 “Kama mtu akimpa jirani yake fedha au mali nyingine amtunzie, na kama vikiibwa kutoka nyumba ya huyo jirani, kama mwizi atashikwa, lazima alipe mara mbili.
for to give: give man: anyone to(wards) neighbor his silver: money or article/utensil to/for to keep: guard and to steal from house: home [the] man if to find [the] thief to complete two
8 Lakini mwizi asipopatikana, mwenye nyumba atafika mbele ya waamuzi ili kuthibitisha kuwa hakuchukua mali ya mwenzake.
if not to find [the] thief and to present: come master [the] house: home to(wards) [the] God if not to send: reach hand his in/on/with work neighbor his
9 Pakiwepo jambo lolote la mali isiyo halali, ikiwa ni maksai, punda, kondoo, mavazi, ama mali yoyote iliyopotea ambayo fulani atasema, ‘Hii ni mali yangu,’ pande zote mbili wataleta mashauri yao mbele ya waamuzi. Yule ambaye waamuzi watamwona kuwa na hatia atamlipa jirani yake mara mbili.
upon all word: case transgression upon cattle upon donkey upon sheep upon garment upon all something lost which to say for he/she/it this till [the] God to come (in): come word: case two their which be wicked [emph?] God to complete two to/for neighbor his
10 “Kama mtu akimpa jirani yake punda, ngʼombe, kondoo au mnyama mwingine yeyote amtunzie, akifa au akijeruhiwa au akichukuliwa wakati haonekani na mtu yeyote,
for to give: give man: anyone to(wards) neighbor his donkey or cattle or sheep and all animal to/for to keep: guard and to die or to break or to take captive nothing to see: see
11 jambo hili kati yao wawili litaamuliwa kwa kuapa kiapo mbele za Bwana, kwamba huyo jirani hakuhusika na wizi wa mali ya jirani yake. Mwenye mali itampasa akubali jambo hili, na hakuna malipo yatakayohitajika.
oath LORD to be between two their if not to send: reach hand his in/on/with work neighbor his and to take: recieve master his and not to complete
12 Lakini kama mnyama aliibwa kwa jirani, itampasa amlipe mwenye mnyama.
and if to steal to steal from from with him to complete to/for master his
13 Kama ameraruliwa na mnyama pori, ataleta mabaki ya mnyama kama ushahidi, naye hatadaiwa kulipa mnyama aliyeraruliwa.
if to tear to tear to come (in): bring him witness [the] torn animal not to complete
14 “Kama mtu akimwazima mnyama kutoka kwa jirani yake, na kama akiumia au akafa na mwenye mnyama hayupo, lazima amlipe huyo mnyama.
and for to ask man: anyone from from with neighbor his and to break or to die master his nothing with him to complete to complete
15 Lakini mwenye mnyama akiwa angalipo na mnyama wake, mwazimaji hatalazimika kumlipa. Kama mnyama alikuwa amekodishwa, fedha iliyolipwa kwa kukodisha inatosha kwa kufidia hasara.
if master his with him not to complete if hired he/she/it to come (in): come in/on/with wages his
16 “Kama mtu akimshawishi bikira ambaye hajaposwa na akilala naye, lazima alipe mahari, kisha atamwoa msichana huyo.
and for to entice man virgin which not to betroth and to lie down: have sex with her to pay brideprice to pay brideprice her to/for him to/for woman: wife
17 Baba wa msichana akikataa katakata kumpa huyo mtu huyo msichana wake, bado ni lazima huyo mtu atalipa mahari kama inavyostahili malipo ya ubikira.
if to refuse to refuse father her to/for to give: give her to/for him silver: money to weigh like/as brideprice [the] virgin
18 “Usiruhusu mwanamke mchawi aishi.
to practice sorcery not to live
19 “Mtu yeyote aziniye na mnyama lazima auawe.
all to lie down: have sex with animal to die to die
20 “Mtu awaye yote anayemtolea mungu mwingine dhabihu isipokuwa Bwana, lazima aangamizwe.
to sacrifice to/for God to devote/destroy lest to/for LORD to/for alone him
21 “Usimtendee mgeni vibaya au kumwonea, kwa kuwa nanyi mlikuwa wageni huko Misri.
and sojourner not to oppress and not to oppress him for sojourner to be in/on/with land: country/planet Egypt
22 “Usimdhulumu mjane wala yatima.
all widow and orphan not to afflict [emph?]
23 Kama ukifanya hivyo nao wakinililia, hakika nitasikia kilio chao.
if to afflict to afflict [obj] him that if: except if: except to cry to cry to(wards) me to hear: hear to hear: hear cry his
24 Hasira yangu itawaka, nami nitawaua kwa upanga, wake zenu watakuwa wajane na watoto wenu watakuwa yatima.
and to be incensed face: anger my and to kill [obj] you in/on/with sword and to be woman: wife your widow and son: child your orphan
25 “Kama ukimkopesha mmojawapo wa watu wangu fedha ambaye ni mhitaji, usiwe kama mtu mkopesha fedha; usimtoze riba.
if silver: money to borrow [obj] people my [obj] [the] afflicted with you not to be to/for him like/as to lend not to set: take [emph?] upon him interest
26 Kama ukichukua vazi la jirani kama rehani, ulirudishe kwake kabla jua kuzama,
if to pledge to pledge garment neighbor your till to come (in): come [the] sun to return: return him to/for him
27 kwa kuwa vazi lake ndilo pekee alilo nalo la kumfunika mwili wake. Ni nini kingine atajifunika nacho? Atakaponililia, nitasikia, kwa kuwa nina huruma.
for he/she/it (covering his *Q(k)*) to/for alone her he/she/it mantle his to/for skin his in/on/with what? to lie down: sleep and to be for to cry to(wards) me and to hear: hear for gracious I
28 “Usimkufuru Mungu au kumlaani mtawala wa watu wako.
God not to lighten and leader in/on/with people your not to curse
29 “Usiache kutoa sadaka kutoka ghala lako au mapipa yako. “Lazima unipe mzaliwa wa kwanza wa wana wako.
fruit your and juice your not to delay firstborn son: child your to give: give to/for me
30 Ufanye vivyo hivyo kwa ngʼombe wako na kwa kondoo wako. Waache wakae na mama zao kwa siku saba, lakini siku ya nane unipe.
so to make: do to/for cattle your to/for flock your seven day to be with mother his in/on/with day [the] eighth to give: give him to/for me
31 “Ninyi mtakuwa watu wangu watakatifu. Kwa hiyo msile nyama ya mnyama aliyeraruliwa na wanyama pori; mtupieni mbwa.
and human holiness to be [emph?] to/for me and flesh in/on/with land: country torn animal not to eat to/for dog to throw [emph?] [obj] him

< Kutoka 22 >