< Kutoka 22 >

1 “Kama mtu akiiba maksai au kondoo na kumchinja au kumuuza, ni lazima alipe ngʼombe watano badala ya maksai mmoja na kondoo wanne badala ya kondoo mmoja.
If a man shall steal an ox, or a sheep, and kill it, or sell it; he shall restore five oxen for an ox, and four sheep for a sheep.
2 “Kama mwizi akishikwa anavunja nyumba akapigwa hata akafa, aliyemuua hana hatia ya kumwaga damu;
If a thief be found breaking up, and be smitten that he die, there shall no blood be shed for him.
3 lakini jambo hilo likitokea wakati jua limechomoza, huyo mtu atakuwa na hatia ya kumwaga damu. “Mwizi huyo sharti alipe, lakini kama hana kitu, lazima auzwe ili alipe kwa ajili ya wizi wake.
If the sun be risen on him, there shall be blood shed for him; for he should make full restitution; if he have nothing, then he shall be sold for his theft.
4 “Kama mnyama aliyeibwa akikutwa hai mikononi mwake, ikiwa ni maksai au punda au kondoo, lazima alipe mara mbili.
If the theft be certainly found in his hand alive, whether it be ox, or ass, or sheep; he shall restore double.
5 “Kama mtu akichunga mifugo yake katika shamba au shamba la mizabibu, na akawaachia wajilishe katika shamba la mtu mwingine, ni lazima alipe vitu bora kutoka kwenye shamba lake mwenyewe au kutoka shamba lake la mizabibu.
If a man shall cause a field or vineyard to be eaten, and shall put in his beast, and shall feed in another man’s field; of the best of his own field, and of the best of his own vineyard, shall he make restitution.
6 “Kama moto ukiwaka na kuenea kwenye vichaka vya miiba na kuteketeza miganda ya nafaka au nafaka ambayo haijavunwa, au kuteketeza shamba lote, mtu yule aliyewasha moto lazima alipe.
If fire break out, and catch in thorns, so that the stacks of corn, or the standing corn, or the field, be consumed therewith; he that kindled the fire shall surely make restitution.
7 “Kama mtu akimpa jirani yake fedha au mali nyingine amtunzie, na kama vikiibwa kutoka nyumba ya huyo jirani, kama mwizi atashikwa, lazima alipe mara mbili.
If a man shall deliver to his neighbor money or stuff to keep, and it be stolen out of the man’s house; if the thief be found, let him pay double.
8 Lakini mwizi asipopatikana, mwenye nyumba atafika mbele ya waamuzi ili kuthibitisha kuwa hakuchukua mali ya mwenzake.
If the thief be not found, then the master of the house shall be brought to the judges, to see whether he have put his hand to his neighbor’s goods.
9 Pakiwepo jambo lolote la mali isiyo halali, ikiwa ni maksai, punda, kondoo, mavazi, ama mali yoyote iliyopotea ambayo fulani atasema, ‘Hii ni mali yangu,’ pande zote mbili wataleta mashauri yao mbele ya waamuzi. Yule ambaye waamuzi watamwona kuwa na hatia atamlipa jirani yake mara mbili.
For all manner of trespass, whether it be for ox, for ass, for sheep, for raiment, or for any manner of lost thing which another challenges to be his, the cause of both parties shall come before the judges; and whom the judges shall condemn, he shall pay double to his neighbor.
10 “Kama mtu akimpa jirani yake punda, ngʼombe, kondoo au mnyama mwingine yeyote amtunzie, akifa au akijeruhiwa au akichukuliwa wakati haonekani na mtu yeyote,
If a man deliver to his neighbor an ass, or an ox, or a sheep, or any beast, to keep; and it die, or be hurt, or driven away, no man seeing it:
11 jambo hili kati yao wawili litaamuliwa kwa kuapa kiapo mbele za Bwana, kwamba huyo jirani hakuhusika na wizi wa mali ya jirani yake. Mwenye mali itampasa akubali jambo hili, na hakuna malipo yatakayohitajika.
Then shall an oath of the LORD be between them both, that he has not put his hand to his neighbor’s goods; and the owner of it shall accept thereof, and he shall not make it good.
12 Lakini kama mnyama aliibwa kwa jirani, itampasa amlipe mwenye mnyama.
And if it be stolen from him, he shall make restitution to the owner thereof.
13 Kama ameraruliwa na mnyama pori, ataleta mabaki ya mnyama kama ushahidi, naye hatadaiwa kulipa mnyama aliyeraruliwa.
If it be torn in pieces, then let him bring it for witness, and he shall not make good that which was torn.
14 “Kama mtu akimwazima mnyama kutoka kwa jirani yake, na kama akiumia au akafa na mwenye mnyama hayupo, lazima amlipe huyo mnyama.
And if a man borrow something of his neighbor, and it be hurt, or die, the owner thereof being not with it, he shall surely make it good.
15 Lakini mwenye mnyama akiwa angalipo na mnyama wake, mwazimaji hatalazimika kumlipa. Kama mnyama alikuwa amekodishwa, fedha iliyolipwa kwa kukodisha inatosha kwa kufidia hasara.
But if the owner thereof be with it, he shall not make it good: if it be an hired thing, it came for his hire.
16 “Kama mtu akimshawishi bikira ambaye hajaposwa na akilala naye, lazima alipe mahari, kisha atamwoa msichana huyo.
And if a man entice a maid that is not betrothed, and lie with her, he shall surely endow her to be his wife.
17 Baba wa msichana akikataa katakata kumpa huyo mtu huyo msichana wake, bado ni lazima huyo mtu atalipa mahari kama inavyostahili malipo ya ubikira.
If her father utterly refuse to give her to him, he shall pay money according to the dowry of virgins.
18 “Usiruhusu mwanamke mchawi aishi.
You shall not suffer a witch to live.
19 “Mtu yeyote aziniye na mnyama lazima auawe.
Whoever lies with a beast shall surely be put to death.
20 “Mtu awaye yote anayemtolea mungu mwingine dhabihu isipokuwa Bwana, lazima aangamizwe.
He that sacrifices to any god, save to the LORD only, he shall be utterly destroyed.
21 “Usimtendee mgeni vibaya au kumwonea, kwa kuwa nanyi mlikuwa wageni huko Misri.
You shall neither vex a stranger, nor oppress him: for you were strangers in the land of Egypt.
22 “Usimdhulumu mjane wala yatima.
You shall not afflict any widow, or fatherless child.
23 Kama ukifanya hivyo nao wakinililia, hakika nitasikia kilio chao.
If you afflict them in any wise, and they cry at all to me, I will surely hear their cry;
24 Hasira yangu itawaka, nami nitawaua kwa upanga, wake zenu watakuwa wajane na watoto wenu watakuwa yatima.
And my wrath shall wax hot, and I will kill you with the sword; and your wives shall be widows, and your children fatherless.
25 “Kama ukimkopesha mmojawapo wa watu wangu fedha ambaye ni mhitaji, usiwe kama mtu mkopesha fedha; usimtoze riba.
If you lend money to any of my people that is poor by you, you shall not be to him as an usurer, neither shall you lay on him usury.
26 Kama ukichukua vazi la jirani kama rehani, ulirudishe kwake kabla jua kuzama,
If you at all take your neighbor’s raiment to pledge, you shall deliver it to him by that the sun goes down:
27 kwa kuwa vazi lake ndilo pekee alilo nalo la kumfunika mwili wake. Ni nini kingine atajifunika nacho? Atakaponililia, nitasikia, kwa kuwa nina huruma.
For that is his covering only, it is his raiment for his skin: wherein shall he sleep? and it shall come to pass, when he cries to me, that I will hear; for I am gracious.
28 “Usimkufuru Mungu au kumlaani mtawala wa watu wako.
You shall not revile the gods, nor curse the ruler of your people.
29 “Usiache kutoa sadaka kutoka ghala lako au mapipa yako. “Lazima unipe mzaliwa wa kwanza wa wana wako.
You shall not delay to offer the first of your ripe fruits, and of your liquors: the firstborn of your sons shall you give to me.
30 Ufanye vivyo hivyo kwa ngʼombe wako na kwa kondoo wako. Waache wakae na mama zao kwa siku saba, lakini siku ya nane unipe.
Likewise shall you do with your oxen, and with your sheep: seven days it shall be with his dam; on the eighth day you shall give it me.
31 “Ninyi mtakuwa watu wangu watakatifu. Kwa hiyo msile nyama ya mnyama aliyeraruliwa na wanyama pori; mtupieni mbwa.
And you shall be holy men to me: neither shall you eat any flesh that is torn of beasts in the field; you shall cast it to the dogs.

< Kutoka 22 >