< Kutoka 21 >

1 “Hizi ndizo sheria utakazoweka mbele ya Waisraeli:
И сия оправдания, яже да положиши пред ними:
2 “Kama ukimnunua mtumwa wa Kiebrania, atakutumikia kwa miaka sita. Lakini katika mwaka wa saba, atakuwa huru naye atakwenda zake pasipo kulipa chochote.
аще стяжеши раба Евреина, шесть лет да поработает тебе, в седмое же лето отпустиши его свободна туне:
3 Kama akija peke yake, atakwenda huru peke yake, lakini kama akija na mke, ataondoka pamoja naye.
аще сам един внидет, то един и изыдет: аще же жена внидет с ним, то и жена отидет с ним:
4 Kama bwana wake alimpatia mke naye akamzalia wana au binti, mwanamke pamoja na watoto wake watakuwa mali ya bwana wake na huyo mwanaume ataondoka peke yake.
аще же господин даст ему жену, и родит ему сыны или дщери, жена и дети да будут господину его, сам же един да отидет.
5 “Lakini kama mtumishi akisema, ‘Ninampenda bwana wangu, mke wangu pamoja na watoto na sitaki kuwa huru,’
Аще же отвещав раб речет: возлюбих господина моего и жену мою и дети моя, не отхожду свободен:
6 ndipo bwana wake atakapolazimika kumpeleka mbele ya waamuzi. Kisha atampeleka kwenye mlango au kizingiti na kutoboa sikio lake kwa shazia. Naye atamtumikia bwana wake maisha yake yote.
да приведет его господин его пред судище Божие, и тогда приведет его пред двери на праг, и да провертит ему ухо господин его шилом, и да поработает ему во веки.
7 “Kama mtu akimuuza binti yake kuwa mtumwa, hataachwa huru kama watumwa wa kiume waachiwavyo.
Аще же кто продаст свою дщерь в рабыню, да не отидет, якоже отходят рабыни:
8 Kama hakumpendeza bwana wake aliyemchagua, huyo bwana atamwacha akombolewe. Hatakuwa na haki ya kumuuza kwa wageni, kwa sababu huyo bwana atakuwa amekosa uaminifu.
аще не угодит пред очима господина своего, юже он взяти в жену обеща, да отпустит ю: языку же чуждему господин да не продаст ея, понеже отверже ю:
9 Kama akimchagua aolewe na mwanawe, ni lazima ampe haki za kuwa binti yake.
аще же сыну своему обещал ю, по обыкновению дщерей да сотворит ей:
10 Ikiwa huyo mwana aliyeozwa mtumwa mwanamke ataoa mwanamke mwingine, ni lazima aendelee kumtosheleza huyo mke wa kwanza kwa chakula, mavazi na haki zote za ndoa.
аще же другую поймет себе, потребных и одежд и союбщения ея да не лишит:
11 Iwapo hatamtosheleza kwa mambo hayo matatu, huyo mke wa kwanza ataondoka na kuwa huru bila malipo yoyote ya fedha.
аще же сих трех не сотворит ей, да отидет без сребра туне.
12 “Yeyote ampigaye mtu na kumuua ni lazima auawe hakika.
И аще кого кто ударит, и умрет, смертию да умрет (и той):
13 Hata hivyo, kama hakumuua kwa makusudi, lakini Mungu akaruhusu itendeke, basi atakimbilia mahali nitakapomchagulia.
аще же не хотя, но Бог предаде в руце его, дам тебе место, в неже убежит тамо убивый:
14 Lakini kama mtu akipanga na kumuua mwingine kwa makusudi, mwondoe katika madhabahu yangu na kumuua.
аще же кто приложит убити ближняго своего лестию и прибегнет ко олтарю, от олтаря Моего да возмеши того умертвити.
15 “Yeyote amshambuliaye baba yake au mama yake ni lazima auawe.
Иже биет отца своего или матерь свою, смертию да умрет.
16 “Yeyote amtekaye nyara mwingine akamuuza au akamweka kwake, akikamatwa ni lazima auawe.
Иже злословит отца своего или матерь свою, смертию да умрет.
17 “Yeyote atakayemlaani baba yake au mama yake ni lazima auawe.
Аще кто кого украдет от сынов Израилевых, и соодолев сему продаст его, и обрящется у него, смертию да скончается.
18 “Kama watu wakigombana na mmoja akimpiga mwingine kwa jiwe au kwa ngumi yake na hakufa bali akaugua na kulala kitandani,
Аще же сварятся два мужа, и ударит един другаго каменем или пястию, и не умрет, но сляжет на одре:
19 yule aliyempiga ngumi hatahesabiwa kuwa na hatia kama mwenzake ataamka na kujikongoja kwa fimbo yake, lakini hata hivyo, ni lazima amlipe fidia ya muda wake aliopoteza na awajibike mpaka apone kabisa.
аще востав человек походит вне о жезле, неповинен будет ударивый его: точию за неделание его да даст цену и на цельбу.
20 “Kama mtu akimpiga mtumwa wake wa kiume au wa kike kwa fimbo na mtumwa huyo akafa papo hapo, ni lazima aadhibiwe
Аще же кто ударит раба своего или рабу свою жезлом, и умрет от руки его, судом да отмстится:
21 lakini ikiwa mtumwa ataamka baada ya siku moja au mbili, hataadhibiwa, kwa sababu yule mtumwa ni mali yake.
аще же преживет день един или два, да не мстится: сребро бо его есть.
22 “Ikiwa watu wawili wanapigana na wakamuumiza mwanamke mjamzito, naye akazaa kabla ya wakati lakini hakuna majeraha makubwa, mhalifu atatozwa mali kiasi cha madai ya mume wa yule mwanamke, na jinsi mahakama itakavyoamua.
Аще же биются два мужа, и поразят жену непраздну, и изыдет младенец ея неизображен, тщетою да отщетится: якоже наложит муж жены тоя, подобающее да отдаст:
23 Lakini kukiwa na jeraha kubwa, ni lazima ulipe uhai kwa uhai,
аще же изображен будет, да даст душу за душу,
24 jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu,
око за око, зуб за зуб, руку за руку, ногу за ногу,
25 kuchomwa moto kwa kuchomwa moto, jeraha kwa jeraha, mchubuko kwa mchubuko.
жжение за жжение, язву за язву, вред за вред.
26 “Ikiwa mtu atampiga mtumwa mwanaume au mwanamke kwenye jicho na kuliharibu, ni lazima amwache huru yule mtumwa kama fidia ya hilo jicho.
Аще же кто исткнет око рабу своему или око рабыни своей и ослепит, свободны да отпустит я за око их:
27 Kama akimvunja jino mtumwa wa kiume au wa kike, ni lazima amwache huru huyo mtumwa kwa kufidia hilo jino.
аще же зуб рабу своему или зуб рабе своей избиет, свободны да отпустит я за зуб их.
28 “Kama fahali akimuua mwanaume au mwanamke kwa kumpiga kwa pembe, fahali huyo ni lazima auawe kwa kupigwa mawe, na nyama yake haitaliwa. Lakini mwenye fahali huyo hatawajibika.
Аще же вол убодет мужа или жену, и умрет, камением да побиется вол той, и да не снедят мяса его, господин же вола неповинен будет:
29 Lakini hata hivyo, ikiwa huyo fahali amekuwa na tabia ya kupiga kwa pembe, na mwenyewe ameonywa na hakutaka kumfungia naye akamuua mwanaume au mwanamke, huyo fahali ni lazima auawe kwa mawe na mwenye fahali pia auawe.
аще же вол бодлив будет прежде вчерашняго и третияго дне, и возвестят господину его, и не заключит его, и убиет мужа или жену: вол камением да побиется, и господин его купно да умрет:
30 Lakini ikiwa malipo yatatakiwa kwake, basi anaweza kulipa kinachodaiwa ili kuukomboa uhai wake.
аще же окуп наложится ему, да даст окуп за душу свою, елико наложат ему:
31 Sheria hii pia itatumika ikiwa fahali atampiga kwa pembe mwana au binti.
аще же сына или дщерь убодет, по сему же суду да сотворят ему:
32 Ikiwa fahali atampiga mtumwa wa kike au wa kiume, mwenye fahali atalipa shekeli thelathini za fedha kwa bwana mwenye mtumwa, na fahali ni lazima auawe kwa mawe.
аще же раба или рабу убодет вол, сребра тридесять дидрахм да даст господину их, и вол камением да побиется.
33 “Kama mtu akiacha shimo wazi, ama akachimba shimo kisha asilifukie, na ngʼombe au punda akatumbukia ndani yake,
Аще же кто отверзет яму или ископает яму и не покрыет ея, и впадется в ню телец или осля,
34 mwenye shimo ni lazima alipe hasara iliyotokea; ni lazima amlipe mwenye mnyama. Mnyama aliyekufa atakuwa wake.
господин ямы отдаст (цену), сребро даст господину их: умершее же ему да будет.
35 “Kama fahali wa mtu fulani atamuumiza fahali wa mtu mwingine na akafa, watamuuza yule aliye hai na wagawane sawa fedha pamoja na mnyama aliyekufa.
Аще же чий вол убодет вола ближняго, и умрет, да продадут вола живаго, и да разделят цену его, и вола умершаго да разделят:
36 Hata hivyo, kama ikifahamika kwamba fahali huyo alikuwa na tabia ya kupiga kwa pembe na mwenyewe hakumfunga, ni lazima mwenye fahali alipe mnyama kwa mnyama, na mnyama aliyekufa atakuwa wake.
аще же знаемь есть вол, яко бодлив есть прежде вчерашняго и третияго дне, и глаголаша господину его, и той не заключит его: да отдаст вола за вола, мертвый же ему да будет.

< Kutoka 21 >