< Kutoka 21 >
1 “Hizi ndizo sheria utakazoweka mbele ya Waisraeli:
Šīs nu ir tās tiesas, ko tev viņiem būs likt priekšā.
2 “Kama ukimnunua mtumwa wa Kiebrania, atakutumikia kwa miaka sita. Lakini katika mwaka wa saba, atakuwa huru naye atakwenda zake pasipo kulipa chochote.
Ja tu pirksi Ebreju kalpu, tad tam būs sešus gadus kalpot, bet septītā tam par velti būs iziet svabadam.
3 Kama akija peke yake, atakwenda huru peke yake, lakini kama akija na mke, ataondoka pamoja naye.
Ja tas viens pats ir nācis, tad tam būs vienam pašam iziet, ja viņš bijis laulāts vīrs, tad viņa sievai būs iziet līdz ar viņu.
4 Kama bwana wake alimpatia mke naye akamzalia wana au binti, mwanamke pamoja na watoto wake watakuwa mali ya bwana wake na huyo mwanaume ataondoka peke yake.
Ja viņa kungs viņam sievu devis, un tā viņam dzemdējusi dēlus vai meitas, tad tai sievai un viņas bērniem būs palikt kungam, un viņam būs iziet vienam pašam.
5 “Lakini kama mtumishi akisema, ‘Ninampenda bwana wangu, mke wangu pamoja na watoto na sitaki kuwa huru,’
Bet ja tas kalps pats sacīs: es mīlēju savu kungu, savu sievu un savus bērnus, es negribu svabads iziet,
6 ndipo bwana wake atakapolazimika kumpeleka mbele ya waamuzi. Kisha atampeleka kwenye mlango au kizingiti na kutoboa sikio lake kwa shazia. Naye atamtumikia bwana wake maisha yake yote.
Tad lai viņa kungs to ved Dieva priekšā, un tad lai to ved pie durvīm vai pie stenderes, un lai viņa kungs tam ausi izdur ar īlenu, un lai tas viņam kalpo mūžam.
7 “Kama mtu akimuuza binti yake kuwa mtumwa, hataachwa huru kama watumwa wa kiume waachiwavyo.
Un kad kas savu meitu pārdevis par kalponi, tad tai nebūs iziet, kā tie kalpi iziet.
8 Kama hakumpendeza bwana wake aliyemchagua, huyo bwana atamwacha akombolewe. Hatakuwa na haki ya kumuuza kwa wageni, kwa sababu huyo bwana atakuwa amekosa uaminifu.
Ja viņa savam kungam nepatīk, ka viņš to neņem par sievu, tad viņam būs ļaut, lai to izpērk; viņš viltīgi ar to darīdams to nevar pārdot svešai tautai.
9 Kama akimchagua aolewe na mwanawe, ni lazima ampe haki za kuwa binti yake.
Bet ja viņš to savam dēlam dod par sievu, tad lai viņai ir meitas tiesa.
10 Ikiwa huyo mwana aliyeozwa mtumwa mwanamke ataoa mwanamke mwingine, ni lazima aendelee kumtosheleza huyo mke wa kwanza kwa chakula, mavazi na haki zote za ndoa.
Ja viņš tam citu ved, tad lai viņai nekā neatrauj no viņas barības, no viņas apsega un piedzīvošanas.
11 Iwapo hatamtosheleza kwa mambo hayo matatu, huyo mke wa kwanza ataondoka na kuwa huru bila malipo yoyote ya fedha.
Un ja viņš šās trīs lietas nedarīs, tad viņai būs velti(brīvai) iziet bez naudas.
12 “Yeyote ampigaye mtu na kumuua ni lazima auawe hakika.
Kas cilvēku sit, ka tas mirst, tam būs tapt nokautam.
13 Hata hivyo, kama hakumuua kwa makusudi, lakini Mungu akaruhusu itendeke, basi atakimbilia mahali nitakapomchagulia.
Bet kad viņš ar viltu uz to nav glūnējis, bet Dievs ļāvis caur viņa roku tā notikt, tad es tev nosacīšu kādu vietu, kurp tam būs bēgt.
14 Lakini kama mtu akipanga na kumuua mwingine kwa makusudi, mwondoe katika madhabahu yangu na kumuua.
Bet ja kas blēdīgi darījis pret savu tuvāko, viņu viltīgi nokaudams, tad arī no mana altāra tev to būs ņemt, ka tas tiek nokauts.
15 “Yeyote amshambuliaye baba yake au mama yake ni lazima auawe.
Ja kas savu tēvu vai savu māti sit, tam būs tapt nokautam.
16 “Yeyote amtekaye nyara mwingine akamuuza au akamweka kwake, akikamatwa ni lazima auawe.
Ja kas cilvēku zog un viņu pārdod, un tas pie viņa top atrasts, tam būs tapt nokautam.
17 “Yeyote atakayemlaani baba yake au mama yake ni lazima auawe.
Arī kas savu tēvu vai savu māti lād, tam būs tapt nokautam.
18 “Kama watu wakigombana na mmoja akimpiga mwingine kwa jiwe au kwa ngumi yake na hakufa bali akaugua na kulala kitandani,
Un ja vīri baras, un viens otru sit ar akmeni vai ar dūri, ka tas nemirst, bet tam uz gultas jāguļ;
19 yule aliyempiga ngumi hatahesabiwa kuwa na hatia kama mwenzake ataamka na kujikongoja kwa fimbo yake, lakini hata hivyo, ni lazima amlipe fidia ya muda wake aliopoteza na awajibike mpaka apone kabisa.
Ja tas atkal uzceļas un iet ārā ar savu spieķi, tad tam, kas viņu sita, būs būt nenoziedzīgam; viņam tikai būs maksāt, ko tas ir aizkavējis un būs to it labi likt dziedināt.
20 “Kama mtu akimpiga mtumwa wake wa kiume au wa kike kwa fimbo na mtumwa huyo akafa papo hapo, ni lazima aadhibiwe
Un ja kas savu kalpu vai kalponi ar koku sit, ka tas apakš viņa rokas mirst, pie tā to it tiešām būs atriebt.
21 lakini ikiwa mtumwa ataamka baada ya siku moja au mbili, hataadhibiwa, kwa sababu yule mtumwa ni mali yake.
Bet ja viņš vienu vai divas dienas paliek pie dzīvības, tad to nebūs atriebt, jo tas ir ar viņa naudu pirkts.
22 “Ikiwa watu wawili wanapigana na wakamuumiza mwanamke mjamzito, naye akazaa kabla ya wakati lakini hakuna majeraha makubwa, mhalifu atatozwa mali kiasi cha madai ya mume wa yule mwanamke, na jinsi mahakama itakavyoamua.
Un kad vīri baras un sit grūtu sievu, ka viņas auglis noiet, bet tomēr viņai pašai nekāda vaina nenotiek, tad to ar naudu būs sodīt, cik tās sievas vīrs viņam noprasa un tam to būs dot pēc soģu sprieduma.
23 Lakini kukiwa na jeraha kubwa, ni lazima ulipe uhai kwa uhai,
Bet ja tai kāda nelaime būs, tad tam būs dot dvēseli pret dvēseli,
24 jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu,
Aci pret aci, zobu pret zobu, roku pret roku,
25 kuchomwa moto kwa kuchomwa moto, jeraha kwa jeraha, mchubuko kwa mchubuko.
Kāju pret kāju, degunu pret degunu, vāti pret vāti, trumu(rētu) pret trumu.
26 “Ikiwa mtu atampiga mtumwa mwanaume au mwanamke kwenye jicho na kuliharibu, ni lazima amwache huru yule mtumwa kama fidia ya hilo jicho.
Un ja kas savu kalpu vai savu kalponi acī sit un to samaitā, tam būs viņu svabadu atlaist tās acs labad.
27 Kama akimvunja jino mtumwa wa kiume au wa kike, ni lazima amwache huru huyo mtumwa kwa kufidia hilo jino.
Un ja viņš sava kalpa vai savas kalpones zobu izsit, tad tam viņu būs atlaist tā zoba labad.
28 “Kama fahali akimuua mwanaume au mwanamke kwa kumpiga kwa pembe, fahali huyo ni lazima auawe kwa kupigwa mawe, na nyama yake haitaliwa. Lakini mwenye fahali huyo hatawajibika.
Un ja kāds vērsis vai vīru vai sievu sabada, ka mirst, tad to vērsi akmeņiem būs nomētāt un viņa gaļu nebūs ēst, bet tā vērša kungam būs būt nenoziedzīgam.
29 Lakini hata hivyo, ikiwa huyo fahali amekuwa na tabia ya kupiga kwa pembe, na mwenyewe ameonywa na hakutaka kumfungia naye akamuua mwanaume au mwanamke, huyo fahali ni lazima auawe kwa mawe na mwenye fahali pia auawe.
Bet ja tas vērsis jau papriekš bijis badīgs, un tas viņa kungam ir teikts, un viņš to nav sargājis, un tas nobada vai vīru vai sievu, tad tam vērsim akmeņiem būs tapt nomētātam un viņa kungam arīdzan būs tapt nokautam.
30 Lakini ikiwa malipo yatatakiwa kwake, basi anaweza kulipa kinachodaiwa ili kuukomboa uhai wake.
Ja viņam top nospriesta izpirkšana, tad tam par savas dvēseles izglābšanu būs dot visu, kas viņam top nospriests.
31 Sheria hii pia itatumika ikiwa fahali atampiga kwa pembe mwana au binti.
Ja tas (vērsis) dēlu vai meitu ir badījis, tad tam būs darīt pēc šīs tiesas.
32 Ikiwa fahali atampiga mtumwa wa kike au wa kiume, mwenye fahali atalipa shekeli thelathini za fedha kwa bwana mwenye mtumwa, na fahali ni lazima auawe kwa mawe.
Ja tas vērsis kalpu vai kalponi bada, tad lai viņa kungs dod trīsdesmit sudraba sēķeļus, un to vērsi akmeņiem lai nomētā.
33 “Kama mtu akiacha shimo wazi, ama akachimba shimo kisha asilifukie, na ngʼombe au punda akatumbukia ndani yake,
Un ja kas aku attaisa, vai ja kas aku rok un neapsedz, un tur kāds vērsis vai ēzelis krīt iekšā,
34 mwenye shimo ni lazima alipe hasara iliyotokea; ni lazima amlipe mwenye mnyama. Mnyama aliyekufa atakuwa wake.
Tad lai tās akas kungs to maksā, lai atdod (tā lopa) kungam to naudu, bet to maitu lai patur.
35 “Kama fahali wa mtu fulani atamuumiza fahali wa mtu mwingine na akafa, watamuuza yule aliye hai na wagawane sawa fedha pamoja na mnyama aliyekufa.
Un ja kaut kāda vērsis bada sava tuvākā vērsi, ka tas mirst, tad to dzīvo vērsi būs pārdot un to naudu dalīt, un to maitu būs arī dalīt.
36 Hata hivyo, kama ikifahamika kwamba fahali huyo alikuwa na tabia ya kupiga kwa pembe na mwenyewe hakumfunga, ni lazima mwenye fahali alipe mnyama kwa mnyama, na mnyama aliyekufa atakuwa wake.
Bet ja tas bijis zināms, ka tas vērsis papriekš bijis badīgs, un viņa kungs to nav sargājis, tad lai vērsi pret vērsi atdod, bet to maitu lai patur.