< Kutoka 21 >
1 “Hizi ndizo sheria utakazoweka mbele ya Waisraeli:
And these [are] the judgments which you will set before them.
2 “Kama ukimnunua mtumwa wa Kiebrania, atakutumikia kwa miaka sita. Lakini katika mwaka wa saba, atakuwa huru naye atakwenda zake pasipo kulipa chochote.
For you will buy a slave Hebrew six years he will serve and in the seventh [year] he will go out to free [person] without paying.
3 Kama akija peke yake, atakwenda huru peke yake, lakini kama akija na mke, ataondoka pamoja naye.
If with body his he will come with body his he will go out if [is the] husband of a wife he and she will go out wife his with him.
4 Kama bwana wake alimpatia mke naye akamzalia wana au binti, mwanamke pamoja na watoto wake watakuwa mali ya bwana wake na huyo mwanaume ataondoka peke yake.
If master his he will give to him a wife and she will bear to him sons or daughters the woman and children her she will belong to master her and he he will go out with body his.
5 “Lakini kama mtumishi akisema, ‘Ninampenda bwana wangu, mke wangu pamoja na watoto na sitaki kuwa huru,’
And if carefully he will say the slave I love master my wife my and children my not I will go out a free [person].
6 ndipo bwana wake atakapolazimika kumpeleka mbele ya waamuzi. Kisha atampeleka kwenye mlango au kizingiti na kutoboa sikio lake kwa shazia. Naye atamtumikia bwana wake maisha yake yote.
And he will bring near him master his to God and he will bring near him to the door or to the doorpost and he will pierce master his ear his with the awl and he will serve him for ever.
7 “Kama mtu akimuuza binti yake kuwa mtumwa, hataachwa huru kama watumwa wa kiume waachiwavyo.
And if he will sell a man daughter his to a female slave not she will go out when go out the [male] slaves.
8 Kama hakumpendeza bwana wake aliyemchagua, huyo bwana atamwacha akombolewe. Hatakuwa na haki ya kumuuza kwa wageni, kwa sababu huyo bwana atakuwa amekosa uaminifu.
If she is bad in [the] eyes of master her who (for himself *Q(K)*) he designated her and he will let be ransomed her to a people foreign not he will have dominion to sell her because has dealt treacherously he with her.
9 Kama akimchagua aolewe na mwanawe, ni lazima ampe haki za kuwa binti yake.
And if for son his he will designate her according to [the] custom of daughters he will do to her.
10 Ikiwa huyo mwana aliyeozwa mtumwa mwanamke ataoa mwanamke mwingine, ni lazima aendelee kumtosheleza huyo mke wa kwanza kwa chakula, mavazi na haki zote za ndoa.
If another [woman] he will take for himself food her covering her and right to intercourse her not he will reduce.
11 Iwapo hatamtosheleza kwa mambo hayo matatu, huyo mke wa kwanza ataondoka na kuwa huru bila malipo yoyote ya fedha.
And if three [things] these not he will do for her and she will go out without paying not money.
12 “Yeyote ampigaye mtu na kumuua ni lazima auawe hakika.
[one who] will strike anyone And he will die certainly he will be put to death.
13 Hata hivyo, kama hakumuua kwa makusudi, lakini Mungu akaruhusu itendeke, basi atakimbilia mahali nitakapomchagulia.
And that not he was lying in wait and God he allowed to happen to hand his and I will designate for you a place where he will flee there.
14 Lakini kama mtu akipanga na kumuua mwingine kwa makusudi, mwondoe katika madhabahu yangu na kumuua.
And if he will act presumptuously anyone on neighbor his to kill him with cunning from with altar my you will take him to die.
15 “Yeyote amshambuliaye baba yake au mama yake ni lazima auawe.
And [one who] will strike father his and mother his certainly he will be put to death.
16 “Yeyote amtekaye nyara mwingine akamuuza au akamweka kwake, akikamatwa ni lazima auawe.
And [one who] will steal anyone and he will sell him and he will be found in hand his certainly he will be put to death.
17 “Yeyote atakayemlaani baba yake au mama yake ni lazima auawe.
And [one who] will curse father his and mother his certainly he will be put to death.
18 “Kama watu wakigombana na mmoja akimpiga mwingine kwa jiwe au kwa ngumi yake na hakufa bali akaugua na kulala kitandani,
And if they will quarrel! men and he will strike anyone neighbor his with a stone or with a fist and not he will die and he will fall to a bed.
19 yule aliyempiga ngumi hatahesabiwa kuwa na hatia kama mwenzake ataamka na kujikongoja kwa fimbo yake, lakini hata hivyo, ni lazima amlipe fidia ya muda wake aliopoteza na awajibike mpaka apone kabisa.
If he will arise and he will walk about on the outside on staff his and he will be free from guilt the [one who] struck only sitting still his he will pay for and certainly he will have [him] healed.
20 “Kama mtu akimpiga mtumwa wake wa kiume au wa kike kwa fimbo na mtumwa huyo akafa papo hapo, ni lazima aadhibiwe
And if he will strike anyone [male] slave his or female slave his with the rod and he will die under hand his certainly he will be avenged.
21 lakini ikiwa mtumwa ataamka baada ya siku moja au mbili, hataadhibiwa, kwa sababu yule mtumwa ni mali yake.
Nevertheless if a day or two days he will remain not he will be avenged for [is] money his he.
22 “Ikiwa watu wawili wanapigana na wakamuumiza mwanamke mjamzito, naye akazaa kabla ya wakati lakini hakuna majeraha makubwa, mhalifu atatozwa mali kiasi cha madai ya mume wa yule mwanamke, na jinsi mahakama itakavyoamua.
And if they will struggle together men and they will strike a woman pregnant and they will come out children her and not it will be harm certainly he will be fined just as he will impose on him [the] husband of the woman and he will give for [the] estimate.
23 Lakini kukiwa na jeraha kubwa, ni lazima ulipe uhai kwa uhai,
And if harm it will be and you will give a life in place of a life.
24 jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu,
An eye in place of an eye a tooth in place of a tooth a hand in place of a hand a foot in place of a foot.
25 kuchomwa moto kwa kuchomwa moto, jeraha kwa jeraha, mchubuko kwa mchubuko.
Burning in place of burning bruise in place of bruise wound in place of wound.
26 “Ikiwa mtu atampiga mtumwa mwanaume au mwanamke kwenye jicho na kuliharibu, ni lazima amwache huru yule mtumwa kama fidia ya hilo jicho.
And if he will strike anyone [the] eye of [male] slave his or [the] eye of female slave his and he will destroy it to free [person] he will set free him in place of eye his.
27 Kama akimvunja jino mtumwa wa kiume au wa kike, ni lazima amwache huru huyo mtumwa kwa kufidia hilo jino.
And if [the] tooth of [male] slave his or [the] tooth of female slave his he will knock out to free [person] he will set free him in place of tooth his.
28 “Kama fahali akimuua mwanaume au mwanamke kwa kumpiga kwa pembe, fahali huyo ni lazima auawe kwa kupigwa mawe, na nyama yake haitaliwa. Lakini mwenye fahali huyo hatawajibika.
And if it will gore an ox a man or a woman and he will die certainly it will be stoned to death the ox and not it will be eaten meat its and [the] owner of the ox [will be] free from guilt.
29 Lakini hata hivyo, ikiwa huyo fahali amekuwa na tabia ya kupiga kwa pembe, na mwenyewe ameonywa na hakutaka kumfungia naye akamuua mwanaume au mwanamke, huyo fahali ni lazima auawe kwa mawe na mwenye fahali pia auawe.
And if [will be] an ox prone to gore it from yesterday three days ago and it has been protested on owner its and not he will guard it and it will kill a man or a woman the ox it will be stoned to death and also owner its he will be put to death.
30 Lakini ikiwa malipo yatatakiwa kwake, basi anaweza kulipa kinachodaiwa ili kuukomboa uhai wake.
If a ransom it will be imposed on him and he will give [the] ransom of life his according to all that it will be imposed on him.
31 Sheria hii pia itatumika ikiwa fahali atampiga kwa pembe mwana au binti.
Or a son it will gore or a daughter it will gore according to the judgment this it will be done to him.
32 Ikiwa fahali atampiga mtumwa wa kike au wa kiume, mwenye fahali atalipa shekeli thelathini za fedha kwa bwana mwenye mtumwa, na fahali ni lazima auawe kwa mawe.
If a [male] slave it will gore the ox or a female slave silver - thirty shekels he will give to master his and the ox it will be stoned to death.
33 “Kama mtu akiacha shimo wazi, ama akachimba shimo kisha asilifukie, na ngʼombe au punda akatumbukia ndani yake,
And if he will open anyone a pit or for he will dig anyone a pit and not he will cover it and it will fall there an ox or a donkey.
34 mwenye shimo ni lazima alipe hasara iliyotokea; ni lazima amlipe mwenye mnyama. Mnyama aliyekufa atakuwa wake.
[the] owner of The pit he will make compensation silver he will repay to owner its and the dead [animal] it will be[long] to him.
35 “Kama fahali wa mtu fulani atamuumiza fahali wa mtu mwingine na akafa, watamuuza yule aliye hai na wagawane sawa fedha pamoja na mnyama aliyekufa.
And if it will strike [the] ox of anyone [the] ox of neighbor his and it will die and they will sell the ox living and they will divide silver its and also the dead [animal] they will divide!
36 Hata hivyo, kama ikifahamika kwamba fahali huyo alikuwa na tabia ya kupiga kwa pembe na mwenyewe hakumfunga, ni lazima mwenye fahali alipe mnyama kwa mnyama, na mnyama aliyekufa atakuwa wake.
Or it is known that [is] an ox prone to gore it from yesterday three days ago and not he guarded it owner its certainly he will make compensation an ox in place of the ox and the dead [animal] it will be[long] to him.