< Kutoka 21 >

1 “Hizi ndizo sheria utakazoweka mbele ya Waisraeli:
And these are the judgments which thou shalt set before them.
2 “Kama ukimnunua mtumwa wa Kiebrania, atakutumikia kwa miaka sita. Lakini katika mwaka wa saba, atakuwa huru naye atakwenda zake pasipo kulipa chochote.
If thou buy a Hebrew bondman, six years shall he serve; and in the seventh he shall go out free for nothing.
3 Kama akija peke yake, atakwenda huru peke yake, lakini kama akija na mke, ataondoka pamoja naye.
If he came in alone, he shall go out alone: if he had a wife, then his wife shall go out with him.
4 Kama bwana wake alimpatia mke naye akamzalia wana au binti, mwanamke pamoja na watoto wake watakuwa mali ya bwana wake na huyo mwanaume ataondoka peke yake.
If his master have given him a wife, and she have borne him sons or daughters, the wife and her children shall be her master's, and he shall go out alone.
5 “Lakini kama mtumishi akisema, ‘Ninampenda bwana wangu, mke wangu pamoja na watoto na sitaki kuwa huru,’
But if the bondman shall say distinctly, I love my master, my wife, and my children, I will not go free;
6 ndipo bwana wake atakapolazimika kumpeleka mbele ya waamuzi. Kisha atampeleka kwenye mlango au kizingiti na kutoboa sikio lake kwa shazia. Naye atamtumikia bwana wake maisha yake yote.
then his master shall bring him before the judges, and shall bring him to the door, or to the door-post; and his master shall bore his ear through with an awl; and he shall be his bondman for ever.
7 “Kama mtu akimuuza binti yake kuwa mtumwa, hataachwa huru kama watumwa wa kiume waachiwavyo.
And if a man shall sell his daughter as a handmaid, she shall not go out as the bondmen go out.
8 Kama hakumpendeza bwana wake aliyemchagua, huyo bwana atamwacha akombolewe. Hatakuwa na haki ya kumuuza kwa wageni, kwa sababu huyo bwana atakuwa amekosa uaminifu.
If she is unacceptable in the eyes of her master, who had taken her for himself, then shall he let her be ransomed: to sell her unto a foreign people he hath no power, after having dealt unfaithfully with her.
9 Kama akimchagua aolewe na mwanawe, ni lazima ampe haki za kuwa binti yake.
And if he have appointed her unto his son, he shall deal with her after the law of daughters.
10 Ikiwa huyo mwana aliyeozwa mtumwa mwanamke ataoa mwanamke mwingine, ni lazima aendelee kumtosheleza huyo mke wa kwanza kwa chakula, mavazi na haki zote za ndoa.
If he take himself another, her food, her clothing, and her conjugal rights he shall not diminish.
11 Iwapo hatamtosheleza kwa mambo hayo matatu, huyo mke wa kwanza ataondoka na kuwa huru bila malipo yoyote ya fedha.
And if he do not these three things unto her, then shall she go out free without money.
12 “Yeyote ampigaye mtu na kumuua ni lazima auawe hakika.
He that striketh a man, so that he die, shall certainly be put to death.
13 Hata hivyo, kama hakumuua kwa makusudi, lakini Mungu akaruhusu itendeke, basi atakimbilia mahali nitakapomchagulia.
But if he have not lain in wait, and God have delivered [him] into his hand, I will appoint thee a place to which he shall flee.
14 Lakini kama mtu akipanga na kumuua mwingine kwa makusudi, mwondoe katika madhabahu yangu na kumuua.
But if a man act wantonly toward his neighbour, and slay him with guile, thou shalt take him from mine altar, that he may die.
15 “Yeyote amshambuliaye baba yake au mama yake ni lazima auawe.
And he that striketh his father, or his mother, shall certainly be put to death.
16 “Yeyote amtekaye nyara mwingine akamuuza au akamweka kwake, akikamatwa ni lazima auawe.
And he that stealeth a man, and selleth him, or if he be found in his hand, he shall certainly be put to death.
17 “Yeyote atakayemlaani baba yake au mama yake ni lazima auawe.
And he that curseth his father, or his mother, shall certainly be put to death.
18 “Kama watu wakigombana na mmoja akimpiga mwingine kwa jiwe au kwa ngumi yake na hakufa bali akaugua na kulala kitandani,
And if men dispute, and one strike the other with a stone, or with the fist, and he die not, but take to [his] bed,
19 yule aliyempiga ngumi hatahesabiwa kuwa na hatia kama mwenzake ataamka na kujikongoja kwa fimbo yake, lakini hata hivyo, ni lazima amlipe fidia ya muda wake aliopoteza na awajibike mpaka apone kabisa.
— if he rise, and walk abroad upon his staff, then shall he that struck [him] be guiltless; only he shall pay [for] the loss of his time, and shall cause [him] to be thoroughly healed.
20 “Kama mtu akimpiga mtumwa wake wa kiume au wa kike kwa fimbo na mtumwa huyo akafa papo hapo, ni lazima aadhibiwe
And if a man strike his bondman or his handmaid with a staff, and he die under his hand, he shall certainly be avenged.
21 lakini ikiwa mtumwa ataamka baada ya siku moja au mbili, hataadhibiwa, kwa sababu yule mtumwa ni mali yake.
Only, if he continue [to live] a day or two days, he shall not be avenged; for he is his money.
22 “Ikiwa watu wawili wanapigana na wakamuumiza mwanamke mjamzito, naye akazaa kabla ya wakati lakini hakuna majeraha makubwa, mhalifu atatozwa mali kiasi cha madai ya mume wa yule mwanamke, na jinsi mahakama itakavyoamua.
And if men strive together, and strike a woman with child, so that she be delivered, and no mischief happen, he shall in any case be fined, according as the woman's husband shall impose on him, and shall give it as the judges estimate.
23 Lakini kukiwa na jeraha kubwa, ni lazima ulipe uhai kwa uhai,
But if mischief happen, then thou shalt give life for life,
24 jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu,
eye for eye, tooth for tooth, hand for hand, foot for foot,
25 kuchomwa moto kwa kuchomwa moto, jeraha kwa jeraha, mchubuko kwa mchubuko.
branding for branding, wound for wound, stripe for stripe.
26 “Ikiwa mtu atampiga mtumwa mwanaume au mwanamke kwenye jicho na kuliharibu, ni lazima amwache huru yule mtumwa kama fidia ya hilo jicho.
And if a man strike the eye of his bondman or the eye of his handmaid, and it be marred, he shall let him go for his eye.
27 Kama akimvunja jino mtumwa wa kiume au wa kike, ni lazima amwache huru huyo mtumwa kwa kufidia hilo jino.
And if he knock out his bondman's tooth or his handmaid's tooth, he shall let him go free for his tooth.
28 “Kama fahali akimuua mwanaume au mwanamke kwa kumpiga kwa pembe, fahali huyo ni lazima auawe kwa kupigwa mawe, na nyama yake haitaliwa. Lakini mwenye fahali huyo hatawajibika.
And if an ox gore a man or a woman, so that they die, then the ox shall certainly be stoned, and its flesh shall not be eaten; but the owner of the ox shall be guiltless.
29 Lakini hata hivyo, ikiwa huyo fahali amekuwa na tabia ya kupiga kwa pembe, na mwenyewe ameonywa na hakutaka kumfungia naye akamuua mwanaume au mwanamke, huyo fahali ni lazima auawe kwa mawe na mwenye fahali pia auawe.
But if the ox have gored heretofore, and it have been testified to its owner, and he have not kept it in, and it kill a man or a woman, — the ox shall be stoned, and its owner also shall be put to death.
30 Lakini ikiwa malipo yatatakiwa kwake, basi anaweza kulipa kinachodaiwa ili kuukomboa uhai wake.
If there be imposed on him a satisfaction, then he shall give the ransom of his life, according to what is imposed on him.
31 Sheria hii pia itatumika ikiwa fahali atampiga kwa pembe mwana au binti.
Whether it gore a son or gore a daughter, according to this judgment shall it be done to him.
32 Ikiwa fahali atampiga mtumwa wa kike au wa kiume, mwenye fahali atalipa shekeli thelathini za fedha kwa bwana mwenye mtumwa, na fahali ni lazima auawe kwa mawe.
If the ox gore a bondman or a handmaid, he shall give to their master thirty shekels of silver, and the ox shall be stoned.
33 “Kama mtu akiacha shimo wazi, ama akachimba shimo kisha asilifukie, na ngʼombe au punda akatumbukia ndani yake,
— And if a man open a pit, or if a man dig a pit, and do not cover it, and an ox or an ass fall into it,
34 mwenye shimo ni lazima alipe hasara iliyotokea; ni lazima amlipe mwenye mnyama. Mnyama aliyekufa atakuwa wake.
the owner of the pit shall make it good, shall give money to the owner of them; and the dead [ox] shall be his.
35 “Kama fahali wa mtu fulani atamuumiza fahali wa mtu mwingine na akafa, watamuuza yule aliye hai na wagawane sawa fedha pamoja na mnyama aliyekufa.
— And if one man's ox gore his neighbour's ox, and it die, then they shall sell the live ox, and divide the money thereof, and divide the dead also.
36 Hata hivyo, kama ikifahamika kwamba fahali huyo alikuwa na tabia ya kupiga kwa pembe na mwenyewe hakumfunga, ni lazima mwenye fahali alipe mnyama kwa mnyama, na mnyama aliyekufa atakuwa wake.
Or if it be known that the ox have gored heretofore, and its owner have not kept him in, he shall in any case restore ox for ox; and the dead shall be his.

< Kutoka 21 >