< Kutoka 21 >

1 “Hizi ndizo sheria utakazoweka mbele ya Waisraeli:
“These are the judgments which you shall place before them:
2 “Kama ukimnunua mtumwa wa Kiebrania, atakutumikia kwa miaka sita. Lakini katika mwaka wa saba, atakuwa huru naye atakwenda zake pasipo kulipa chochote.
If you buy a Hebrew servant, six years shall he serve you; in the seventh, he shall depart freely, without charge.
3 Kama akija peke yake, atakwenda huru peke yake, lakini kama akija na mke, ataondoka pamoja naye.
With whatever clothing he arrived, with the like let him depart. If he has a wife, his wife also shall depart, at the same time.
4 Kama bwana wake alimpatia mke naye akamzalia wana au binti, mwanamke pamoja na watoto wake watakuwa mali ya bwana wake na huyo mwanaume ataondoka peke yake.
But if his lord gave him a wife, and she has borne sons and daughters, the woman and her children shall belong to her lord. Yet still, he himself will go out with his clothing.
5 “Lakini kama mtumishi akisema, ‘Ninampenda bwana wangu, mke wangu pamoja na watoto na sitaki kuwa huru,’
And if the servant will say, ‘I love my lord, and my wife and children, I will not depart freely,’
6 ndipo bwana wake atakapolazimika kumpeleka mbele ya waamuzi. Kisha atampeleka kwenye mlango au kizingiti na kutoboa sikio lake kwa shazia. Naye atamtumikia bwana wake maisha yake yote.
then his lord shall make an offering for him to the heavens, and it shall be applied to the door and the posts, and he will pierce his ear with an awl. And he shall be his servant in perpetuity.
7 “Kama mtu akimuuza binti yake kuwa mtumwa, hataachwa huru kama watumwa wa kiume waachiwavyo.
If anyone sells his daughter to be a servant, she shall not depart as a female servant is accustomed to go out.
8 Kama hakumpendeza bwana wake aliyemchagua, huyo bwana atamwacha akombolewe. Hatakuwa na haki ya kumuuza kwa wageni, kwa sababu huyo bwana atakuwa amekosa uaminifu.
If she displeases the eyes of her lord, to whom she had been delivered, he shall dismiss her. But he shall have no authority to sell her to a foreign people, even if he despises her.
9 Kama akimchagua aolewe na mwanawe, ni lazima ampe haki za kuwa binti yake.
But if he has betrothed her to his son, he shall treat her according to the custom with daughters.
10 Ikiwa huyo mwana aliyeozwa mtumwa mwanamke ataoa mwanamke mwingine, ni lazima aendelee kumtosheleza huyo mke wa kwanza kwa chakula, mavazi na haki zote za ndoa.
And if he takes another for him, he shall provide to the maiden a marriage, and clothing, and he shall not refuse the price of her chastity.
11 Iwapo hatamtosheleza kwa mambo hayo matatu, huyo mke wa kwanza ataondoka na kuwa huru bila malipo yoyote ya fedha.
If he does not do these three things, she shall depart freely, without money.
12 “Yeyote ampigaye mtu na kumuua ni lazima auawe hakika.
Whoever strikes a man, intending to murder, shall be put to death.
13 Hata hivyo, kama hakumuua kwa makusudi, lakini Mungu akaruhusu itendeke, basi atakimbilia mahali nitakapomchagulia.
But if he did not lie in wait for him, but God delivered him into his hands, then I will appoint for you a place to which he must flee.
14 Lakini kama mtu akipanga na kumuua mwingine kwa makusudi, mwondoe katika madhabahu yangu na kumuua.
If someone murders his neighbor with deliberation, by lying in wait, you shall tear him away from my altar, so that he may die.
15 “Yeyote amshambuliaye baba yake au mama yake ni lazima auawe.
Whoever strikes his father or mother shall die a death.
16 “Yeyote amtekaye nyara mwingine akamuuza au akamweka kwake, akikamatwa ni lazima auawe.
Whoever will have stolen a man and sold him, having been convicted of the crime, shall be put to death.
17 “Yeyote atakayemlaani baba yake au mama yake ni lazima auawe.
Whoever speaks evil of his father or mother shall die a death.
18 “Kama watu wakigombana na mmoja akimpiga mwingine kwa jiwe au kwa ngumi yake na hakufa bali akaugua na kulala kitandani,
If men will have quarreled, and one of them has struck his neighbor with a stone or a fist, and he does not die, but lies in bed,
19 yule aliyempiga ngumi hatahesabiwa kuwa na hatia kama mwenzake ataamka na kujikongoja kwa fimbo yake, lakini hata hivyo, ni lazima amlipe fidia ya muda wake aliopoteza na awajibike mpaka apone kabisa.
if he gets up again and can walk outside on his staff, he who struck him will be innocent, but only if he makes sufficient restitution for his deeds and for the cost of the physicians.
20 “Kama mtu akimpiga mtumwa wake wa kiume au wa kike kwa fimbo na mtumwa huyo akafa papo hapo, ni lazima aadhibiwe
Whoever strikes his male or female servant with a staff, and if they have died by his hands, he shall be guilty of a crime.
21 lakini ikiwa mtumwa ataamka baada ya siku moja au mbili, hataadhibiwa, kwa sababu yule mtumwa ni mali yake.
But if he survives for one day or two, he shall not be subject to punishment, because it is his money.
22 “Ikiwa watu wawili wanapigana na wakamuumiza mwanamke mjamzito, naye akazaa kabla ya wakati lakini hakuna majeraha makubwa, mhalifu atatozwa mali kiasi cha madai ya mume wa yule mwanamke, na jinsi mahakama itakavyoamua.
If men will have quarreled, and one of them has struck a pregnant woman, and as a result she miscarries, but she herself survives, he shall be subject to as much damage as the husband of the woman shall petition from him, or as arbitrators shall judge.
23 Lakini kukiwa na jeraha kubwa, ni lazima ulipe uhai kwa uhai,
But if her death will have followed, he will repay a life for a life,
24 jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu,
an eye for an eye, a tooth for a tooth, a hand for a hand, a foot for a foot,
25 kuchomwa moto kwa kuchomwa moto, jeraha kwa jeraha, mchubuko kwa mchubuko.
a scrape for a scrape, a wound for a wound, a bruise for a bruise.
26 “Ikiwa mtu atampiga mtumwa mwanaume au mwanamke kwenye jicho na kuliharibu, ni lazima amwache huru yule mtumwa kama fidia ya hilo jicho.
If anyone will have struck the eye of his male or female servant, having left them with one eye, he shall release them freely, because of the eye that he has put out.
27 Kama akimvunja jino mtumwa wa kiume au wa kike, ni lazima amwache huru huyo mtumwa kwa kufidia hilo jino.
Likewise, if he knocks out a tooth of his male or female servant, he shall similarly release them freely.
28 “Kama fahali akimuua mwanaume au mwanamke kwa kumpiga kwa pembe, fahali huyo ni lazima auawe kwa kupigwa mawe, na nyama yake haitaliwa. Lakini mwenye fahali huyo hatawajibika.
If an ox has struck a man or a woman with his horn, and if they die, it shall be stoned. And its flesh shall not be eaten; also, the owner of the ox will be innocent.
29 Lakini hata hivyo, ikiwa huyo fahali amekuwa na tabia ya kupiga kwa pembe, na mwenyewe ameonywa na hakutaka kumfungia naye akamuua mwanaume au mwanamke, huyo fahali ni lazima auawe kwa mawe na mwenye fahali pia auawe.
But if the ox had been pushing with his horn, from yesterday and the day before, and they warned his owner, but he did not confine it, and it will have killed a man or a woman, then the ox shall be stoned, and his owner shall be killed.
30 Lakini ikiwa malipo yatatakiwa kwake, basi anaweza kulipa kinachodaiwa ili kuukomboa uhai wake.
But if they have imposed a price on him, he shall give, in exchange for his life, whatever is asked.
31 Sheria hii pia itatumika ikiwa fahali atampiga kwa pembe mwana au binti.
Likewise, if it has struck a son or a daughter with its horns, it shall be subject to a similar verdict.
32 Ikiwa fahali atampiga mtumwa wa kike au wa kiume, mwenye fahali atalipa shekeli thelathini za fedha kwa bwana mwenye mtumwa, na fahali ni lazima auawe kwa mawe.
If it attacks a male or female servant, he shall give thirty shekels of silver to their lord, yet truly the ox shall be stoned.
33 “Kama mtu akiacha shimo wazi, ama akachimba shimo kisha asilifukie, na ngʼombe au punda akatumbukia ndani yake,
If a man digs or opens a cistern, and does not cover it, and an ox or a donkey falls into it,
34 mwenye shimo ni lazima alipe hasara iliyotokea; ni lazima amlipe mwenye mnyama. Mnyama aliyekufa atakuwa wake.
then the owner of the cistern shall repay the price of the beasts, and what is dead will belong to him.
35 “Kama fahali wa mtu fulani atamuumiza fahali wa mtu mwingine na akafa, watamuuza yule aliye hai na wagawane sawa fedha pamoja na mnyama aliyekufa.
If the ox of a stranger wounds the ox of another, and it has died, then they shall sell the live ox and divide the price, but the carcass of the dead one they shall distribute between them.
36 Hata hivyo, kama ikifahamika kwamba fahali huyo alikuwa na tabia ya kupiga kwa pembe na mwenyewe hakumfunga, ni lazima mwenye fahali alipe mnyama kwa mnyama, na mnyama aliyekufa atakuwa wake.
But if he knew that his ox had pushed with its horns, yesterday and the day before, and its owner did not confine it, then he shall repay an ox for an ox, and he will receive the whole carcass.”

< Kutoka 21 >