< Kutoka 21 >

1 “Hizi ndizo sheria utakazoweka mbele ya Waisraeli:
Ето съдбите, които ще представиш пред тях.
2 “Kama ukimnunua mtumwa wa Kiebrania, atakutumikia kwa miaka sita. Lakini katika mwaka wa saba, atakuwa huru naye atakwenda zake pasipo kulipa chochote.
Ако купиш роб евреин, шест години ще работи, а в седмата ще излезе свободен, без откуп.
3 Kama akija peke yake, atakwenda huru peke yake, lakini kama akija na mke, ataondoka pamoja naye.
Ако е дошъл сам, сам да си излезе; ако е имал жена, то и жена му да излезе с него.
4 Kama bwana wake alimpatia mke naye akamzalia wana au binti, mwanamke pamoja na watoto wake watakuwa mali ya bwana wake na huyo mwanaume ataondoka peke yake.
Ако господарят му му е дал жена, и тя му е родила синове или дъщери, то жената и чадата й ще бъдат на гсподаря й, а той ще излезе сам.
5 “Lakini kama mtumishi akisema, ‘Ninampenda bwana wangu, mke wangu pamoja na watoto na sitaki kuwa huru,’
Но ако робът изрично каже: Обичам господаря си, жена си и чадата си; не желая да изляза свободен,
6 ndipo bwana wake atakapolazimika kumpeleka mbele ya waamuzi. Kisha atampeleka kwenye mlango au kizingiti na kutoboa sikio lake kwa shazia. Naye atamtumikia bwana wake maisha yake yote.
тогава господарят му ще го заведе пред съдиите, и, като го приведе при вратата, или при стълба на вратата, господарят му ще му промуши ухото с шило; и той ще му бъде роб за винаги.
7 “Kama mtu akimuuza binti yake kuwa mtumwa, hataachwa huru kama watumwa wa kiume waachiwavyo.
Ако някой продаде дъщеря си за робиня, тя няма да излезе така както излизат робите.
8 Kama hakumpendeza bwana wake aliyemchagua, huyo bwana atamwacha akombolewe. Hatakuwa na haki ya kumuuza kwa wageni, kwa sababu huyo bwana atakuwa amekosa uaminifu.
Ако не бъде угодна на господаря си, който се е сгодил за нея, то нека я остави да бъде откупена; той не ще има власт да я продаде на чужденци, тъй като й е изневерил.
9 Kama akimchagua aolewe na mwanawe, ni lazima ampe haki za kuwa binti yake.
Но ако я е сгодил за сина си, то нека постъпи с нея, както е обичайно с дъщерите.
10 Ikiwa huyo mwana aliyeozwa mtumwa mwanamke ataoa mwanamke mwingine, ni lazima aendelee kumtosheleza huyo mke wa kwanza kwa chakula, mavazi na haki zote za ndoa.
Ако си вземе още една жена, да не лиши оная от храната й, от дрехите й и от съпружеско съжитие с нея.
11 Iwapo hatamtosheleza kwa mambo hayo matatu, huyo mke wa kwanza ataondoka na kuwa huru bila malipo yoyote ya fedha.
И ако не й направи тия трите, тогава тя нека си излезе даром, без откуп.
12 “Yeyote ampigaye mtu na kumuua ni lazima auawe hakika.
Който удари човек смъртоносно, непременно да се умъртви.
13 Hata hivyo, kama hakumuua kwa makusudi, lakini Mungu akaruhusu itendeke, basi atakimbilia mahali nitakapomchagulia.
Но ако не го е причаквал, но Бог го е предал в ръката му, тогава Аз ще ти определя място гдето да побегне.
14 Lakini kama mtu akipanga na kumuua mwingine kwa makusudi, mwondoe katika madhabahu yangu na kumuua.
Ако, обаче, някой от злоба убие ближния си коварно, то и от олтара Ми ще го извадиш, за да се умъртви.
15 “Yeyote amshambuliaye baba yake au mama yake ni lazima auawe.
Който удари баща си или майка си непременно да се умъртви.
16 “Yeyote amtekaye nyara mwingine akamuuza au akamweka kwake, akikamatwa ni lazima auawe.
Който открадне човек и го продадеде, или ако откраднатият се намери в ръката му, той непременно да се умъртви.
17 “Yeyote atakayemlaani baba yake au mama yake ni lazima auawe.
Който хули баща си или майка си непременно да се умъртви.
18 “Kama watu wakigombana na mmoja akimpiga mwingine kwa jiwe au kwa ngumi yake na hakufa bali akaugua na kulala kitandani,
Когато се карат някои, ако единият удари другия с камък или с юмрука си, и той не умре, но пази легло;
19 yule aliyempiga ngumi hatahesabiwa kuwa na hatia kama mwenzake ataamka na kujikongoja kwa fimbo yake, lakini hata hivyo, ni lazima amlipe fidia ya muda wake aliopoteza na awajibike mpaka apone kabisa.
и ако последният се придигне и излиза макар с тояга, тогава оня, който го е ударил, ще бъде невинен, само ще плати за денгубата му и ще направи да бъде съвършено изцерен.
20 “Kama mtu akimpiga mtumwa wake wa kiume au wa kike kwa fimbo na mtumwa huyo akafa papo hapo, ni lazima aadhibiwe
Ако някой удари роба си или робинята си с тояга, та умре под ръката му, непременно да се накаже.
21 lakini ikiwa mtumwa ataamka baada ya siku moja au mbili, hataadhibiwa, kwa sababu yule mtumwa ni mali yake.
Обаче, ако удареният поживее един два дена, тогава да се не наказва, понеже той му е стока.
22 “Ikiwa watu wawili wanapigana na wakamuumiza mwanamke mjamzito, naye akazaa kabla ya wakati lakini hakuna majeraha makubwa, mhalifu atatozwa mali kiasi cha madai ya mume wa yule mwanamke, na jinsi mahakama itakavyoamua.
Ако се бият някои и ударят трудна жена, така щото да пометне, а не последва друга повреда, тогава оня, който я е ударил непременно да бъде глобен, според както мъжът й би му наложил, и да плати както определят съдиите.
23 Lakini kukiwa na jeraha kubwa, ni lazima ulipe uhai kwa uhai,
Но ако последва повреда, тогава да отсъдиш живот за живот,
24 jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu,
око за око, зъб за зъб, ръка за ръка, нога за нога,
25 kuchomwa moto kwa kuchomwa moto, jeraha kwa jeraha, mchubuko kwa mchubuko.
изгаряне за изгаряне, рана за рана, удар за удар.
26 “Ikiwa mtu atampiga mtumwa mwanaume au mwanamke kwenye jicho na kuliharibu, ni lazima amwache huru yule mtumwa kama fidia ya hilo jicho.
Ако някой удари роба си или робинята си в окото, и то се развали, поради окото му ще го освободи.
27 Kama akimvunja jino mtumwa wa kiume au wa kike, ni lazima amwache huru huyo mtumwa kwa kufidia hilo jino.
И ако избие някой зъб на роба си или някой зъб на робинята си, ще го освободи поради зъба му.
28 “Kama fahali akimuua mwanaume au mwanamke kwa kumpiga kwa pembe, fahali huyo ni lazima auawe kwa kupigwa mawe, na nyama yake haitaliwa. Lakini mwenye fahali huyo hatawajibika.
Ако вол убоде мъж или жена щото да умре, тогава да се убие с камъни, и да се не яде месото му; а стопанинът на вола ще бъде оправдан.
29 Lakini hata hivyo, ikiwa huyo fahali amekuwa na tabia ya kupiga kwa pembe, na mwenyewe ameonywa na hakutaka kumfungia naye akamuua mwanaume au mwanamke, huyo fahali ni lazima auawe kwa mawe na mwenye fahali pia auawe.
Но ако волът е бил бодлив от по-напред, и това е било известно на стопанина му, но той не го е ограничил, та е убил мъж или жена, то волът да се убие с камъни, още и стопанинът му да се умъртви.
30 Lakini ikiwa malipo yatatakiwa kwake, basi anaweza kulipa kinachodaiwa ili kuukomboa uhai wake.
Обаче, ако му се определи откуп, то за избавление на живота си нека даде, колкото му се определи.
31 Sheria hii pia itatumika ikiwa fahali atampiga kwa pembe mwana au binti.
Било че волът е убол мъж или е убол жена, според тая съдба ще му се направят.
32 Ikiwa fahali atampiga mtumwa wa kike au wa kiume, mwenye fahali atalipa shekeli thelathini za fedha kwa bwana mwenye mtumwa, na fahali ni lazima auawe kwa mawe.
Но ако волът убоде роб или робиня, стопанинът нека плати на господаря им тридесет сребърни сикли, и нека се убие волът с камъни.
33 “Kama mtu akiacha shimo wazi, ama akachimba shimo kisha asilifukie, na ngʼombe au punda akatumbukia ndani yake,
Ако отвори някой яма, или изкопае яма без да я покрие, и в нея падне вол или осел,
34 mwenye shimo ni lazima alipe hasara iliyotokea; ni lazima amlipe mwenye mnyama. Mnyama aliyekufa atakuwa wake.
притежателят на ямата ще заплати повредата; ще даде пари на стопанина им, а мършата ще бъде негова.
35 “Kama fahali wa mtu fulani atamuumiza fahali wa mtu mwingine na akafa, watamuuza yule aliye hai na wagawane sawa fedha pamoja na mnyama aliyekufa.
Ако волът на някого убоде вола на другиго, така щото умре, тогава да продадат живия вол и да си разделят стойността му, и мършата тоже да си разделят.
36 Hata hivyo, kama ikifahamika kwamba fahali huyo alikuwa na tabia ya kupiga kwa pembe na mwenyewe hakumfunga, ni lazima mwenye fahali alipe mnyama kwa mnyama, na mnyama aliyekufa atakuwa wake.
Но ако се е знаело от по-напред, че волът е бил бодлив, и стопанинът му не го е ограничил, то непременно ще плати вол за вол, а мършата ще бъде негова.

< Kutoka 21 >