< Kutoka 20 >
1 Ndipo Mungu akasema maneno haya yote:
And God spoke all these words, saying,
2 “Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekutoa Misri, kutoka nchi ya utumwa.
I am the LORD thy God, who brought thee out of the land of Egypt, out of the house of bondage.
3 Usiwe na miungu mingine ila mimi.
Thou shalt have no other gods before me.
4 Usijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote kilicho juu mbinguni, au duniani chini, au ndani ya maji.
Thou shalt not make to thee any graven image, or any likeness of any thing that is in heaven above, or that is in the earth beneath, or that is in the water under the earth:
5 Usivisujudie wala kuviabudu; kwa kuwa Mimi, Bwana Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, ninayewaadhibu watoto kwa ajili ya dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
Thou shalt not bow down thyself to them, nor serve them: for I the LORD thy God am a jealous God, visiting the iniquity of the fathers upon the children to the third and fourth generation of them that hate me;
6 lakini ninaonyesha upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.
And showing mercy to thousands of them that love me, and keep my commandments.
7 Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako, kwa kuwa Bwana hataacha kumhesabia hatia yeye alitajaye jina lake bure.
Thou shalt not take the name of the LORD thy God in vain; for the LORD will not hold him guiltless that taketh his name in vain.
8 Ikumbuke siku ya Sabato, uitakase.
Remember the sabbath day, to keep it holy.
9 Kwa siku sita utafanya kazi na kutenda shughuli zako zote,
Six days shalt thou labour, and do all thy work:
10 lakini siku ya saba ni Sabato kwa Bwana Mungu wako. Siku hiyo hutafanya kazi yoyote, wewe, wala mwanao au binti yako, wala mtumishi wako wa kiume au wa kike, wala wanyama wako, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.
But the seventh day is the sabbath of the LORD thy God: in it thou shalt not do any work, thou, nor thy son, nor thy daughter, thy male servant, nor thy female servant, nor thy cattle, nor thy stranger that is within thy gates:
11 Kwa kuwa kwa siku sita, Bwana aliumba mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo, lakini akapumzika siku ya saba. Kwa hiyo Bwana akaibariki siku ya Sabato na kuifanya takatifu.
For in six days the LORD made heaven and earth, the sea, and all that is in them, and rested the seventh day: therefore the LORD blessed the sabbath day, and hallowed it.
12 Waheshimu baba yako na mama yako, ili upate kuishi siku nyingi katika nchi anayokupa Bwana Mungu wako.
Honour thy father and thy mother: that thy days may be long upon the land which the LORD thy God giveth thee.
Thou shalt not commit adultery.
16 Usimshuhudie jirani yako uongo.
Thou shalt not bear false witness against thy neighbour.
17 Usiitamani nyumba ya jirani yako. Usimtamani mke wa jirani yako, wala mtumishi wake wa kiume au wa kike, wala ngʼombe wake au punda wake, wala chochote kile alicho nacho jirani yako.”
Thou shalt not covet thy neighbour’s house, thou shalt not covet thy neighbour’s wife, nor his male servant, nor his female servant, nor his ox, nor his donkey, nor any thing that is thy neighbour’s.
18 Watu walipoona ngurumo na radi, na kusikia mlio wa tarumbeta, na kuuona mlima katika moshi, walitetemeka kwa woga. Wakasimama mbali
And all the people saw the thunderings, and the lightnings, and the noise of the trumpet, and the mountain smoking: and when the people saw it, they trembled, and stood afar off.
19 na wakamwambia Mose, “Sema nasi wewe mwenyewe, nasi tutakusikiliza. Lakini usimwache Mungu aseme nasi, la sivyo tutakufa.”
And they said to Moses, Speak thou with us, and we will hear: but let not God speak with us, lest we die.
20 Mose akawaambia watu, “Msiogope! Mungu amekuja kuwajaribu, ili kwamba hofu ya Mungu iwakalie, msitende dhambi.”
And Moses said to the people, Fear not: for God is come to test you, and that his fear may be before your faces, that ye sin not.
21 Watu wakabaki mbali, wakati Mose alipolisogelea lile giza nene mahali pale Mungu alipokuwa.
And the people stood afar off, and Moses drew near to the thick darkness where God was.
22 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Waambie Waisraeli hivi: ‘Mmejionea wenyewe kwamba nimesema nanyi kutoka mbinguni:
And the LORD said to Moses, Thus thou shalt say to the children of Israel, Ye have seen that I have talked with you from heaven.
23 Msijifanyizie miungu yoyote na kuilinganisha nami, msijitengenezee miungu ya fedha wala miungu ya dhahabu.
Ye shall not make with me gods of silver, neither shall ye make to you gods of gold.
24 “‘Utanitengenezea madhabahu ya udongo, na juu yake utoe sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani, kondoo zako, mbuzi na ngʼombe zako. Popote nitakapofanya Jina langu liheshimiwe, nitakuja kwenu na kuwabariki.
An altar of earth thou shalt make to me, and shalt sacrifice on it thy burnt offerings, and thy peace offerings, thy sheep, and thy oxen: in all places where I record my name I will come to thee, and I will bless thee.
25 Ikiwa unanitengenezea madhabahu ya mawe, usiijenge kwa mawe ya kuchonga, maana mkitumia chombo cha kuchongea mtaitia unajisi.
And if thou wilt make me an altar of stone, thou shalt not build it of hewn stone: for if thou shalt lift up thy tool upon it, thou hast polluted it.
26 Msitumie ngazi kupandia kwenye madhabahu yangu, uchi wako usije ukadhihirika kwa chini.’
Neither shalt thou go up by steps to my altar, that thy nakedness be not discovered on it.