< Kutoka 2 >
1 Basi mtu mmoja wa nyumba ya Lawi akaoa mwanamke Mlawi,
В това време отиде някой си човек от Левиевия дом та взе за жена една от Левиевите жени.
2 naye mwanamke huyo akapata mimba, akazaa mtoto wa kiume. Alipoona mtoto huyo ni mzuri, akamficha kwa miezi mitatu.
И жената зачна и роди син; и като видя, че беше красиво дете, кри го за три месеца.
3 Lakini alipoona hawezi kumficha zaidi, akamtengenezea kisafina cha mafunjo, akakipaka lami. Kisha akamweka huyo mtoto ndani yake, akakificha katikati ya matete kando ya ukingo wa Mto Naili.
Но понеже не можеше вече да се крие, взе му рогозен ковчежец и намаза го със смола и катран, тури детето в него и го положи в тръстиката край брега на реката.
4 Dada ya huyo mtoto akasimama mbali ili kuona kitakachompata mtoto.
А сестра му стоеше от далеч, за да види какво ще му се случи.
5 Ndipo binti Farao akateremka mtoni Naili kuoga, nao wahudumu wake wakawa wanatembea ukingoni mwa mto. Binti mfalme akaona kisafina katikati ya manyasi, akamtuma mmoja wa watumwa wake wa kike kukichukua.
И Фараоновата дъщеря слезе да се окъпе в реката, а слугините й ходеха по брега на реката; и когато съгледа ковчежеца в тръстиката, тя прати слугинята си за го донесе.
6 Alifungua kisafina akaona mtoto ndani yake. Mtoto alikuwa akilia, akamhurumia. Akasema, “Huyu ni mmoja wa watoto wa Kiebrania.”
Като го отвори, видя детето, и, ето малкото плачеше; и пожали го и каза: От еврейските деца е това.
7 Ndipo dada wa huyo mtoto akamuuliza binti Farao, “Je, niende nikakutafutie mmoja wa wanawake wa Kiebrania akulelee huyu mtoto?”
Тогава сестра му рече на Фараоновата дъщеря: Да отида ли да ти повикам доилка от еврейките, за да ти дои детето?
8 Binti Farao akamjibu, “Ndiyo, nenda.” Yule msichana akaenda akamleta mama wa mtoto.
И Фараоновата дъщеря й рече: Иди. И тъй, момичето отиде та повика майката на детето.
9 Binti Farao akamwambia, “Mchukue huyu mtoto unisaidie kumlea, nami nitakulipa.” Basi yule mwanamke akamchukua mtoto na kumlea.
И Фараоновата дъщеря й рече: Вземи това дете и ми го отдой, и аз ще ти заплатя. И жената взе детето и го доеше.
10 Mtoto alipokua, akampeleka kwa binti Farao, naye akawa mwanawe. Akamwita jina lake Mose akisema, “Nilimtoa kwenye maji.”
А когато порасна детето, донесе го на Фараоновата дъщеря, и то стана неин син. И наименува го Моисей: Понеже, каза тя, извлякох го от водата.
11 Siku moja, baada ya Mose kukua, akaondoka kwenda walikokuwa watu wake, na akachunguza jinsi walivyokuwa wakifanya kazi ngumu. Akamwona Mmisri akimpiga Mwebrania, mmojawapo wa watu wake.
А във времето, когато Моисей порасна, излезе при братята си и гледаше теглилата им. И видя някой си египтянин, че биеше един евреин, един от братята му;
12 Mose akatazama huku na huko asione mtu yeyote, akamuua yule Mmisri, akamficha mchangani.
и като поразгледа насам натам и видя, че няма никой, уби египтянина и го скри в пясъка.
13 Kesho yake akatoka, akaona Waebrania wawili wakipigana. Akamuuliza yule aliyekosa, “Mbona unampiga Mwebrania mwenzako?”
Излезе и на другия ден, и ето, двама евреи се препираха; и каза на обидника: Защо биеш другаря си?
14 Yule mtu akamjibu, “Ni nani aliyekufanya mtawala na mwamuzi juu yetu? Je, unataka kuniua kama ulivyomuua yule Mmisri?” Ndipo Mose akaogopa na kuwaza, “Jambo lile nililofanya lazima limefahamika.”
А той рече: Кой те постави началник и съдия над на? Искаш ли и мене да убиеш, както уби египтянина? Тогава Моисей се уплаши и си каза: Явно е, че това нещо стана известно.
15 Farao aliposikia jambo hili, alijaribu kumuua Mose, lakini Mose akamkimbia Farao na kwenda kuishi katika nchi ya Midiani, akaketi kando ya kisima.
А като чу това Фараон, търсеше случай да убие Моисея; но Моисей побягна от Фараоновото лице и се засели в Мадиамската земя. И седна до един кладенец.
16 Kuhani wa Midiani alikuwa na binti saba, nao wakaja kisimani ili kuchota maji na kujaza hori kwa ajili ya kunyweshea mifugo ya baba yao.
А Мадиамският жрец имаше седем дъщери, които дойдоха и наляха вода и напълниха коритата, за да напоят бащините си овци.
17 Baadhi ya wachungaji wakaja wakawafukuza hao wasichana. Ndipo Mose akainuka, akawasaidia na kunywesha mifugo yao.
Но овчарите дойдоха и ги изпъдиха; а Моисей стана та им помогна, и напои овците им.
18 Hao wasichana waliporudi nyumbani kwa Reueli baba yao, akawauliza, “Imekuwaje leo mmerudi mapema hivyo?”
И като дойдоха при баща си Рагуила, той им рече: Как дойдохте днес толкова скоро.
19 Wakamjibu, “Mmisri mmoja alituokoa kutoka mikononi mwa wachungaji. Pia mtu huyo alituchotea maji na kunywesha mifugo.”
А те казаха: Един египтянин ни избави от ръцете на овчарите, при това и вода ни наля та напои овците.
20 Akawauliza binti zake, “Yuko wapi? Mbona mmemwacha? Mkaribisheni ale chakula.”
И той рече на дъщерите си: А где е той? защо оставихте човека? повикайте го да яде хляб.
21 Mose akakubali kukaa kwa huyo mtu, ambaye alimpa Mose binti yake aliyeitwa Sipora amwoe.
И Моисей склони да живее при човека, който е даде на Моисея дъщеря си Сепфора за жена.
22 Sipora alizaa mtoto wa kiume, naye Mose akamwita Gershomu, akisema, “Nimekuwa mgeni katika nchi ya kigeni.”
И тя роди син; и той го наименува Герсам, защото думаше: Пришелец станах в чужда земя.
23 Baada ya muda mrefu, mfalme wa Misri akafa. Waisraeli wakalia kwa huzuni katika utumwa wao, walilia na kilio chao cha kutaka msaada kwa ajili ya utumwa kikamfikia Mungu.
Подир дълго време египетският цар умря; а израилтяните пъшкаха под робството и извикаха: и викат им от робството стигна до Бога.
24 Mungu akasikia kilio chao cha huzuni, akakumbuka Agano alilofanya na Abrahamu pamoja na Isaki na Yakobo.
Бог чу пъшканията им; и Бог спомни завета си с Авраама, с Исаака, и с Якова.
25 Kwa hiyo Mungu akawaangalia Waisraeli na kuwahurumia.
И Бог погледна на израилтяните, и Бог разбра положението им.