< Kutoka 19 >

1 Mnamo mwezi wa tatu baada ya Waisraeli kuondoka Misri, siku kama iyo hiyo, wakafika katika Jangwa la Sinai.
Le troisième mois après que les enfants d'Israël furent sortis du pays d'Égypte, ils arrivèrent ce même jour dans le désert de Sinaï.
2 Baada ya kuondoka Refidimu, waliingia katika Jangwa la Sinai na Israeli wakapiga kambi pale jangwani mbele ya mlima.
Ils partirent de Rephidim, et arrivèrent au désert de Sinaï; ils campèrent dans le désert, et là, Israël campa devant la montagne.
3 Kisha Mose akakwea kwenda kwa Mungu, naye Bwana akamwita kutoka kwenye ule mlima akasema, “Hivi ndivyo utakavyosema na nyumba ya Yakobo na utakachowaambia watu wa Israeli:
Moïse monta vers Dieu, et Yahvé l'appela de la montagne, en disant: « Voici ce que tu diras à la maison de Jacob et aux enfants d'Israël:
4 ‘Ninyi wenyewe mmeona nililofanya huko Misri, jinsi nilivyowabeba kwenye mbawa za tai na kuwaleta kwangu.
Vous avez vu ce que j'ai fait aux Égyptiens, et comment je vous ai portés sur des ailes d'aigle et amenés vers moi.
5 Sasa kama mkinitii kikamilifu na kutunza Agano langu, basi ninyi mtakuwa mali yangu ya thamani kubwa miongoni mwa mataifa yote. Ijapokuwa dunia yote ni mali yangu,
Maintenant, si vous écoutez ma voix et si vous gardez mon alliance, vous serez ma propriété entre tous les peuples, car toute la terre est à moi,
6 ninyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’ Haya ndiyo maneno utakayosema kwa wana wa Israeli.”
et vous serez pour moi un royaume de prêtres et une nation sainte ». Telles sont les paroles que tu adresseras aux enfants d'Israël. »
7 Kwa hiyo Mose akarudi, akawaita wazee wa watu na kuwaambia maneno yote ambayo Bwana alikuwa amemwamuru ayaseme.
Moïse vint appeler les anciens du peuple, et il exposa devant eux toutes ces paroles que l'Éternel lui avait commandées.
8 Watu wote wakajibu kwa pamoja, “Tutafanya kila kitu Bwana alichokisema.” Naye Mose akarudisha majibu yao kwa Bwana.
Tout le peuple prit la parole et dit: « Nous ferons tout ce que l'Éternel a dit. » Moïse rapporta à Yahvé les paroles du peuple.
9 Bwana akamwambia Mose, “Nitakujia katika wingu zito, ili watu wanisikie nikinena nawe na kila mara waweke tumaini lao kwako.” Kisha Mose akamwambia Bwana yale ambayo watu walikuwa wamesema.
Yahvé dit à Moïse: « Voici que je viens à toi dans une épaisse nuée, afin que le peuple entende quand je te parlerai, et qu'il te croie toujours. » Moïse rapporta à Yahvé les paroles du peuple.
10 Naye Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa watu ukawaweke wakfu leo na kesho. Waambie wafue nguo zao
Yahvé dit à Moïse: « Va vers le peuple, sanctifie-le aujourd'hui et demain, fais-lui laver ses vêtements,
11 na wawe tayari siku ya tatu, kwa sababu siku hiyo, Bwana atashuka juu ya mlima Sinai machoni pa watu wote.
et tiens-toi prêt pour le troisième jour, car le troisième jour, Yahvé descendra sur la montagne de Sinaï aux yeux de tout le peuple.
12 Weka mipaka kuzunguka mlima kwa ajili ya watu, uwaambie, ‘Mwe waangalifu, msije mkapanda mlimani au kuugusa. Yeyote atakayeugusa mlima hakika atauawa.
Tu fixeras des limites au peuple tout autour, en disant: « Prenez garde de ne pas monter sur la montagne et de ne pas toucher son bord. Celui qui touchera la montagne sera puni de mort.
13 Hakika atapigwa mawe au kupigwa mishale; mkono wa mtu hautamgusa. Akiwa mwanadamu au mnyama, hataruhusiwa kuishi.’ Ila tu wakati baragumu itakapopigwa kwa mfululizo, ndipo watu wote watakapopanda mlimani.”
Aucune main ne le touchera, mais il sera lapidé ou transpercé de balles, qu'il s'agisse d'un animal ou d'un homme, il ne vivra pas. Lorsque la trompette sonnera longuement, ils monteront sur la montagne. »
14 Baada ya Mose kushuka kutoka mlimani akawaendea watu na kuwaweka wakfu, wakafua nguo zao.
Moïse descendit de la montagne vers le peuple et sanctifia le peuple, qui lava ses vêtements.
15 Kisha akawaambia watu, “Jitayarisheni kwa ajili ya siku ya tatu. Mwanaume yeyote asimkaribie mwanamke.”
Il dit au peuple: « Soyez prêts le troisième jour. N'ayez pas de relations sexuelles avec une femme. »
16 Asubuhi ya siku ya tatu kulikuwa na ngurumo na radi pamoja na wingu nene juu ya mlima na mlio mkubwa sana wa tarumbeta. Kila mmoja aliyekuwa kambini akatetemeka.
Le troisième jour, comme c'était le matin, il y eut des tonnerres et des éclairs, une épaisse nuée sur la montagne, et le son d'une trompette extrêmement forte; et tout le peuple qui était dans le camp trembla.
17 Kisha Mose akawaongoza watu kutoka kambini kukutana na Mungu, nao wakasimama chini ya mlima.
Moïse conduisit le peuple hors du camp à la rencontre de Dieu, et ils se tinrent au bas de la montagne.
18 Mlima Sinai ulikuwa umefunikwa na moshi, kwa sababu Bwana alishuka juu yake katika moto. Moshi wa moto huo ulipanda juu kama moshi kutoka kwenye tanuru kubwa na mlima wote ukatetemeka kwa nguvu nyingi,
Toute la montagne de Sinaï fumait, car Yahvé y était descendu en feu; sa fumée montait comme la fumée d'une fournaise, et toute la montagne tremblait fortement.
19 nayo sauti ya tarumbeta ikawa kubwa zaidi na zaidi. Kisha Mose akazungumza na sauti ya Bwana ikamjibu.
Le son de la trompette devenant de plus en plus fort, Moïse parla, et Dieu lui répondit par une voix.
20 Bwana akashuka juu ya Mlima Sinai na akamwita Mose apande juu mlimani. Kwa hiyo Mose akapanda juu,
Yahvé descendit sur le mont Sinaï, au sommet de la montagne. Yahvé appela Moïse au sommet de la montagne, et Moïse y monta.
21 naye Bwana akamwambia Mose, “Shuka ukawaonye watu ili wasijipenyeze kutafuta kumwona Bwana na wengi wao wakafa.
L'Éternel dit à Moïse: « Descends, avertis le peuple, de peur qu'il ne s'introduise auprès de l'Éternel pour le regarder, et que beaucoup d'entre eux ne périssent.
22 Hata makuhani, watakaomkaribia Bwana ni lazima wajiweke wakfu, la sivyo Bwana atawaadhibu.”
Que les prêtres aussi, qui s'approchent de l'Éternel, se sanctifient, de peur que l'Éternel ne fasse irruption sur eux. »
23 Mose akamwambia Bwana, “Watu hawawezi kupanda mlima Sinai kwa sababu wewe mwenyewe ulituonya ukisema, ‘Wekeni mipaka kuuzunguka mlima na kuutenga kama patakatifu.’”
Moïse dit à Yahvé: « Le peuple ne peut pas monter sur le mont Sinaï, car tu nous as prévenus en disant: « Entourez la montagne et sanctifiez-la. »
24 Bwana akajibu, “Shuka ukamlete Aroni pamoja nawe. Lakini makuhani pamoja na watu wasije wakalazimisha kuja kwa Bwana, nisije nikawaadhibu.”
Yahvé lui dit: « Descends! Tu feras monter Aaron avec toi, mais ne laisse pas les prêtres et le peuple passer pour monter vers Yahvé, de peur qu'il ne se déchaîne contre eux. »
25 Basi Mose akashuka kwa watu na kuwaambia lile aliloambiwa.
Moïse descendit donc vers le peuple, et lui dit.

< Kutoka 19 >