< Kutoka 19 >
1 Mnamo mwezi wa tatu baada ya Waisraeli kuondoka Misri, siku kama iyo hiyo, wakafika katika Jangwa la Sinai.
In the thridde monethe of the goyng `of Israel out of the lond of Egipt, in this dai thei camen in to the wildirnesse of Synai;
2 Baada ya kuondoka Refidimu, waliingia katika Jangwa la Sinai na Israeli wakapiga kambi pale jangwani mbele ya mlima.
for thei yeden forth fro Rafidym, and camen til in to deseert of Synai, and settiden tentis in the same place; and there Israel settide tentis, euen ayens the hil.
3 Kisha Mose akakwea kwenda kwa Mungu, naye Bwana akamwita kutoka kwenye ule mlima akasema, “Hivi ndivyo utakavyosema na nyumba ya Yakobo na utakachowaambia watu wa Israeli:
Forsothe Moises stiede in to the hil to God; and the Lord clepide hym fro the mount, and seide, Thou schalt seie these thingis to the hows of Jacob, and thou schalt telle to the sones of Israel,
4 ‘Ninyi wenyewe mmeona nililofanya huko Misri, jinsi nilivyowabeba kwenye mbawa za tai na kuwaleta kwangu.
Ye silf han seyn what thingis Y haue do to Egipcians, how Y bar you on the wengis of eglis, and took to me.
5 Sasa kama mkinitii kikamilifu na kutunza Agano langu, basi ninyi mtakuwa mali yangu ya thamani kubwa miongoni mwa mataifa yote. Ijapokuwa dunia yote ni mali yangu,
Therfor if ye schulen here my vois, and schulen kepe my couenaunt, ye schulen be to me in to a specialte of alle puplis; for al the lond is myn;
6 ninyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’ Haya ndiyo maneno utakayosema kwa wana wa Israeli.”
and ye schulen be to me in to a rewme of preesthod, and `ye schulen be an hooli folk; these ben the wordis whiche thou schalt speke to the sones of Israel.
7 Kwa hiyo Mose akarudi, akawaita wazee wa watu na kuwaambia maneno yote ambayo Bwana alikuwa amemwamuru ayaseme.
Moyses cam, and whanne the gretter men in birthe of the puple weren clepid to gidere, he expownede alle the wordis whiche the Lord comaundide.
8 Watu wote wakajibu kwa pamoja, “Tutafanya kila kitu Bwana alichokisema.” Naye Mose akarudisha majibu yao kwa Bwana.
And alle the puple answeride to gidere, We schulen do alle thingis whiche the Lord spak. And whanne Moises hadde teld the wordis of the puple to the Lord,
9 Bwana akamwambia Mose, “Nitakujia katika wingu zito, ili watu wanisikie nikinena nawe na kila mara waweke tumaini lao kwako.” Kisha Mose akamwambia Bwana yale ambayo watu walikuwa wamesema.
the Lord seide to hym, Riyt now Y schal come to thee in a derknesse of a cloude, that the puple here me spekynge to thee, and bileue to thee withouten ende. Therfor Moises telde the wordis of the puple to the Lord,
10 Naye Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa watu ukawaweke wakfu leo na kesho. Waambie wafue nguo zao
which seide to Moises, Go thou to the puple, and make hem holi to dai and to morewe, and waische thei her clothis,
11 na wawe tayari siku ya tatu, kwa sababu siku hiyo, Bwana atashuka juu ya mlima Sinai machoni pa watu wote.
and be thei redi in to the thridde dai; for in the thridde dai the Lord schal come doun bifore al the puple on the hil of Synai.
12 Weka mipaka kuzunguka mlima kwa ajili ya watu, uwaambie, ‘Mwe waangalifu, msije mkapanda mlimani au kuugusa. Yeyote atakayeugusa mlima hakika atauawa.
And thou schalt sette termes to the puple, bi cumpas; and thou schalt seie to hem, Be ye war, that ye `stie not in to the hil, nether touche ye the endis therof; ech man that schal touche the hil, schal die bi deeth.
13 Hakika atapigwa mawe au kupigwa mishale; mkono wa mtu hautamgusa. Akiwa mwanadamu au mnyama, hataruhusiwa kuishi.’ Ila tu wakati baragumu itakapopigwa kwa mfululizo, ndipo watu wote watakapopanda mlimani.”
Hondis schulen not touche hym, but he schal be oppressid with stoonus, ethir he shall be persid with dartis; whether it schal be a beest, ethir a man, it schal not lyue; whanne a clarioun schal bigynne to sowne, thanne `stie thei in to the hil.
14 Baada ya Mose kushuka kutoka mlimani akawaendea watu na kuwaweka wakfu, wakafua nguo zao.
And Moises cam doun fro the hil to the puple, and halewide it; and whanne thei hadden waischun her clothis,
15 Kisha akawaambia watu, “Jitayarisheni kwa ajili ya siku ya tatu. Mwanaume yeyote asimkaribie mwanamke.”
he seide to hem, Be ye redi in to the thridde dai, neiye ye not to youre wyues.
16 Asubuhi ya siku ya tatu kulikuwa na ngurumo na radi pamoja na wingu nene juu ya mlima na mlio mkubwa sana wa tarumbeta. Kila mmoja aliyekuwa kambini akatetemeka.
And now the thridde day was comun, and the morewetid was cleer; and, lo! thundris bigunnen to be herd, and leitis to schyne, and a moost thicke cloude to hile the mounteyn; and `the sownyng of a clarioun made noise ful greetli, and the puple dredde, that was in the castels.
17 Kisha Mose akawaongoza watu kutoka kambini kukutana na Mungu, nao wakasimama chini ya mlima.
And whanne Moises hadde led hem out in to the comyng of God, fro the place of castels, thei stoden at the rootis of the hil.
18 Mlima Sinai ulikuwa umefunikwa na moshi, kwa sababu Bwana alishuka juu yake katika moto. Moshi wa moto huo ulipanda juu kama moshi kutoka kwenye tanuru kubwa na mlima wote ukatetemeka kwa nguvu nyingi,
Forsothe al the hil of Synai smokide, for the Lord hadde come doun theronne in fier; and smoke stiede therof as of a furneis, and al the hil was ferdful;
19 nayo sauti ya tarumbeta ikawa kubwa zaidi na zaidi. Kisha Mose akazungumza na sauti ya Bwana ikamjibu.
and the `sown of a clarioun encreesside litil and litil, and was holdun forth lengere. Moises spak, and the Lord answeride to hym,
20 Bwana akashuka juu ya Mlima Sinai na akamwita Mose apande juu mlimani. Kwa hiyo Mose akapanda juu,
and the Lord cam doun on the hil of Synay, in thilke cop of the hil, and clepide Moises to the cop therof. And whanne he hadde stied thidur,
21 naye Bwana akamwambia Mose, “Shuka ukawaonye watu ili wasijipenyeze kutafuta kumwona Bwana na wengi wao wakafa.
the Lord seide to hym, Go thou doun, and witnesse thou to the puple, lest perauenture it wole passe the termes to se the Lord, and ful greet multitude therof perische;
22 Hata makuhani, watakaomkaribia Bwana ni lazima wajiweke wakfu, la sivyo Bwana atawaadhibu.”
also preestis, that neiyen to the Lord, be halewid, lest Y smyte hem.
23 Mose akamwambia Bwana, “Watu hawawezi kupanda mlima Sinai kwa sababu wewe mwenyewe ulituonya ukisema, ‘Wekeni mipaka kuuzunguka mlima na kuutenga kama patakatifu.’”
And Moises seide to the Lord, The comyn puple may not stie in to the hil of Synai; for thou hast witnessid, and hast comaundid, seiyinge, Sette thou termes aboute the hil, and halewe it.
24 Bwana akajibu, “Shuka ukamlete Aroni pamoja nawe. Lakini makuhani pamoja na watu wasije wakalazimisha kuja kwa Bwana, nisije nikawaadhibu.”
To whom the Lord seide, Go thou doun, and thou schalt stie, and Aaron with thee; forsothe the preestis and the puple passe not the termes, nethir stie thei to the Lord, lest perauenture he sle hem.
25 Basi Mose akashuka kwa watu na kuwaambia lile aliloambiwa.
Moises yede doun to the puple, and telde alle thingis to hem.