< Kutoka 19 >
1 Mnamo mwezi wa tatu baada ya Waisraeli kuondoka Misri, siku kama iyo hiyo, wakafika katika Jangwa la Sinai.
In the third month, when the children of Israel had gone forth from the land of Egypt, the same day they came [into] the wilderness of Sinai.
2 Baada ya kuondoka Refidimu, waliingia katika Jangwa la Sinai na Israeli wakapiga kambi pale jangwani mbele ya mlima.
For they had departed from Rephidim, and had come [to] the desert of Sinai, and had pitched in the wilderness; and there Israel encamped before the mount.
3 Kisha Mose akakwea kwenda kwa Mungu, naye Bwana akamwita kutoka kwenye ule mlima akasema, “Hivi ndivyo utakavyosema na nyumba ya Yakobo na utakachowaambia watu wa Israeli:
And Moses went up to God, and the LORD called to him from the mountain, saying, Thus shalt thou say to the house of Jacob, and tell the children of Israel;
4 ‘Ninyi wenyewe mmeona nililofanya huko Misri, jinsi nilivyowabeba kwenye mbawa za tai na kuwaleta kwangu.
Ye have seen what I did to the Egyptians, and [how] I bore you on eagles' wings, and brought you to myself.
5 Sasa kama mkinitii kikamilifu na kutunza Agano langu, basi ninyi mtakuwa mali yangu ya thamani kubwa miongoni mwa mataifa yote. Ijapokuwa dunia yote ni mali yangu,
Now therefore, if ye will obey my voice indeed, and keep my covenant, then ye shall be a peculiar treasure to me above all people: for all the earth [is] mine:
6 ninyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’ Haya ndiyo maneno utakayosema kwa wana wa Israeli.”
And ye shall be to me a kingdom of priests, and a holy nation. These [are] the words which thou shalt speak to the children of Israel.
7 Kwa hiyo Mose akarudi, akawaita wazee wa watu na kuwaambia maneno yote ambayo Bwana alikuwa amemwamuru ayaseme.
And Moses came and called for the elders of the people, and laid before their faces all these words which the LORD commanded him.
8 Watu wote wakajibu kwa pamoja, “Tutafanya kila kitu Bwana alichokisema.” Naye Mose akarudisha majibu yao kwa Bwana.
And all the people answered together, and said, All that the LORD hath spoken we will do. And Moses returned the words of the people to the LORD.
9 Bwana akamwambia Mose, “Nitakujia katika wingu zito, ili watu wanisikie nikinena nawe na kila mara waweke tumaini lao kwako.” Kisha Mose akamwambia Bwana yale ambayo watu walikuwa wamesema.
And the LORD said to Moses, Lo, I come to thee in a thick cloud, that the people may hear when I speak with thee, and believe thee for ever. And Moses told the words of the people to the LORD.
10 Naye Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa watu ukawaweke wakfu leo na kesho. Waambie wafue nguo zao
And the LORD said to Moses, Go to the people, and sanctify them to-day and to-morrow, and let them wash their clothes,
11 na wawe tayari siku ya tatu, kwa sababu siku hiyo, Bwana atashuka juu ya mlima Sinai machoni pa watu wote.
And be ready against the third day: for on the third day the LORD will come down in the sight of all the people upon mount Sinai.
12 Weka mipaka kuzunguka mlima kwa ajili ya watu, uwaambie, ‘Mwe waangalifu, msije mkapanda mlimani au kuugusa. Yeyote atakayeugusa mlima hakika atauawa.
And thou shalt set bounds to the people round about, saying, Take heed to yourselves, [that ye] go [not] up upon the mount, or touch the border of it: whoever toucheth the mount shall be surely put to death:
13 Hakika atapigwa mawe au kupigwa mishale; mkono wa mtu hautamgusa. Akiwa mwanadamu au mnyama, hataruhusiwa kuishi.’ Ila tu wakati baragumu itakapopigwa kwa mfululizo, ndipo watu wote watakapopanda mlimani.”
There shall not a hand touch it, but he shall surely be stoned or shot through: whether [it be] beast or man, it shall not live: when the trumpet soundeth long, they shall come up to the mount.
14 Baada ya Mose kushuka kutoka mlimani akawaendea watu na kuwaweka wakfu, wakafua nguo zao.
And Moses went down from the mount to the people, and sanctified the people; and they washed their clothes.
15 Kisha akawaambia watu, “Jitayarisheni kwa ajili ya siku ya tatu. Mwanaume yeyote asimkaribie mwanamke.”
And he said to the people, Be ready against the third day: come not at [your] wives.
16 Asubuhi ya siku ya tatu kulikuwa na ngurumo na radi pamoja na wingu nene juu ya mlima na mlio mkubwa sana wa tarumbeta. Kila mmoja aliyekuwa kambini akatetemeka.
And it came to pass on the third day in the morning, that there were thunders and lightnings, and a thick cloud upon the mount, and the voice of the trumpet exceeding loud; so that all the people that [were] in the camp trembled.
17 Kisha Mose akawaongoza watu kutoka kambini kukutana na Mungu, nao wakasimama chini ya mlima.
And Moses brought forth the people out of the camp to meet with God; and they stood at the nether part of the mount.
18 Mlima Sinai ulikuwa umefunikwa na moshi, kwa sababu Bwana alishuka juu yake katika moto. Moshi wa moto huo ulipanda juu kama moshi kutoka kwenye tanuru kubwa na mlima wote ukatetemeka kwa nguvu nyingi,
And mount Sinai was altogether in a smoke, because the LORD descended upon it in fire: and the smoke of it ascended as the smoke of a furnace, and the whole mount trembled greatly.
19 nayo sauti ya tarumbeta ikawa kubwa zaidi na zaidi. Kisha Mose akazungumza na sauti ya Bwana ikamjibu.
And when the voice of the trumpet sounded long, and grew louder and louder, Moses spoke, and God answered him by a voice.
20 Bwana akashuka juu ya Mlima Sinai na akamwita Mose apande juu mlimani. Kwa hiyo Mose akapanda juu,
And the LORD came down upon mount Sinai, on the top of the mount: and the LORD called Moses to the top of the mount; and Moses went up.
21 naye Bwana akamwambia Mose, “Shuka ukawaonye watu ili wasijipenyeze kutafuta kumwona Bwana na wengi wao wakafa.
And the LORD said to Moses, Go down, charge the people, lest they break through to the LORD to gaze, and many of them perish.
22 Hata makuhani, watakaomkaribia Bwana ni lazima wajiweke wakfu, la sivyo Bwana atawaadhibu.”
And let the priests also who come near to the LORD, sanctify themselves, lest the LORD break forth upon them.
23 Mose akamwambia Bwana, “Watu hawawezi kupanda mlima Sinai kwa sababu wewe mwenyewe ulituonya ukisema, ‘Wekeni mipaka kuuzunguka mlima na kuutenga kama patakatifu.’”
And Moses said to the LORD, The people cannot come up to mount Sinai: for thou chargedst us, saying, Set bounds about the mount, and sanctify it.
24 Bwana akajibu, “Shuka ukamlete Aroni pamoja nawe. Lakini makuhani pamoja na watu wasije wakalazimisha kuja kwa Bwana, nisije nikawaadhibu.”
And the LORD said to him, Away, go down, and thou shalt come up, thou, and Aaron with thee: But let not the priests and the people break through, to come up to the LORD, lest he break forth upon them.
25 Basi Mose akashuka kwa watu na kuwaambia lile aliloambiwa.
So Moses went down to the people, and spoke to them.