< Kutoka 19 >

1 Mnamo mwezi wa tatu baada ya Waisraeli kuondoka Misri, siku kama iyo hiyo, wakafika katika Jangwa la Sinai.
In the third month after the people of Israel had gone out from the land of Egypt, on the same day, they came to the wilderness of Sinai.
2 Baada ya kuondoka Refidimu, waliingia katika Jangwa la Sinai na Israeli wakapiga kambi pale jangwani mbele ya mlima.
After they left Rephidim and came to the wilderness of Sinai, they camped in the wilderness in front of the mountain.
3 Kisha Mose akakwea kwenda kwa Mungu, naye Bwana akamwita kutoka kwenye ule mlima akasema, “Hivi ndivyo utakavyosema na nyumba ya Yakobo na utakachowaambia watu wa Israeli:
Moses went up to God. Yahweh called to him from the mountain and said, “You must tell the house of Jacob, the people of Israel:
4 ‘Ninyi wenyewe mmeona nililofanya huko Misri, jinsi nilivyowabeba kwenye mbawa za tai na kuwaleta kwangu.
You have seen what I did to the Egyptians, how I carried you on eagles' wings and brought you to myself.
5 Sasa kama mkinitii kikamilifu na kutunza Agano langu, basi ninyi mtakuwa mali yangu ya thamani kubwa miongoni mwa mataifa yote. Ijapokuwa dunia yote ni mali yangu,
Now then, if you obediently listen to my voice and keep my covenant, then you will be my special possession from among all peoples, for all the earth is mine.
6 ninyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’ Haya ndiyo maneno utakayosema kwa wana wa Israeli.”
You will be a kingdom of priests and a holy nation for me. These are the words that you must speak to the people of Israel.”
7 Kwa hiyo Mose akarudi, akawaita wazee wa watu na kuwaambia maneno yote ambayo Bwana alikuwa amemwamuru ayaseme.
So Moses came and summoned the elders of the people. He set before them all these words that Yahweh had commanded him.
8 Watu wote wakajibu kwa pamoja, “Tutafanya kila kitu Bwana alichokisema.” Naye Mose akarudisha majibu yao kwa Bwana.
All the people answered together and said, “We will do everything that Yahweh has said.” Then Moses came to report the people's words to Yahweh.
9 Bwana akamwambia Mose, “Nitakujia katika wingu zito, ili watu wanisikie nikinena nawe na kila mara waweke tumaini lao kwako.” Kisha Mose akamwambia Bwana yale ambayo watu walikuwa wamesema.
Yahweh said to Moses, “I will come to you in a thick cloud so that the people may hear when I speak with you and may also believe you forever.” Then Moses told the people's words to Yahweh.
10 Naye Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa watu ukawaweke wakfu leo na kesho. Waambie wafue nguo zao
Yahweh said to Moses, “Go to the people. Today and tomorrow you must set them apart to me, and make them wash their garments.
11 na wawe tayari siku ya tatu, kwa sababu siku hiyo, Bwana atashuka juu ya mlima Sinai machoni pa watu wote.
Be ready for the third day, for on the third day Yahweh will come down to Mount Sinai.
12 Weka mipaka kuzunguka mlima kwa ajili ya watu, uwaambie, ‘Mwe waangalifu, msije mkapanda mlimani au kuugusa. Yeyote atakayeugusa mlima hakika atauawa.
You must set boundaries all around the mountain for the people. Say to them, 'Be careful that you do not go up the mountain or touch its border. Whoever touches the mountain will surely be put to death.'
13 Hakika atapigwa mawe au kupigwa mishale; mkono wa mtu hautamgusa. Akiwa mwanadamu au mnyama, hataruhusiwa kuishi.’ Ila tu wakati baragumu itakapopigwa kwa mfululizo, ndipo watu wote watakapopanda mlimani.”
No one's hand must touch such a person. Instead, he must certainly be stoned or shot. Whether it is a person or an animal, he must be put to death. When the trumpet sounds a long blast, they may come up to the foot of the mountain.”
14 Baada ya Mose kushuka kutoka mlimani akawaendea watu na kuwaweka wakfu, wakafua nguo zao.
Then Moses went down from the mountain to the people. He set apart the people to Yahweh and they washed their garments.
15 Kisha akawaambia watu, “Jitayarisheni kwa ajili ya siku ya tatu. Mwanaume yeyote asimkaribie mwanamke.”
He said to the people, “Be ready on the third day; do not go near your wives.”
16 Asubuhi ya siku ya tatu kulikuwa na ngurumo na radi pamoja na wingu nene juu ya mlima na mlio mkubwa sana wa tarumbeta. Kila mmoja aliyekuwa kambini akatetemeka.
On the third day, when it was morning, there were thunder and lightning bolts and a thick cloud on the mountain, and the sound of a very loud trumpet. All the people in the camp trembled.
17 Kisha Mose akawaongoza watu kutoka kambini kukutana na Mungu, nao wakasimama chini ya mlima.
Moses brought the people out of the camp to meet God, and they stood at the foot of the mountain.
18 Mlima Sinai ulikuwa umefunikwa na moshi, kwa sababu Bwana alishuka juu yake katika moto. Moshi wa moto huo ulipanda juu kama moshi kutoka kwenye tanuru kubwa na mlima wote ukatetemeka kwa nguvu nyingi,
Mount Sinai was completely covered with smoke because Yahweh descended on it in fire and smoke. The smoke went up like the smoke of a furnace, and the whole mountain shook violently.
19 nayo sauti ya tarumbeta ikawa kubwa zaidi na zaidi. Kisha Mose akazungumza na sauti ya Bwana ikamjibu.
When the sound of the trumpet grew louder and louder, Moses spoke, and God answered him in a voice.
20 Bwana akashuka juu ya Mlima Sinai na akamwita Mose apande juu mlimani. Kwa hiyo Mose akapanda juu,
Yahweh came down on Mount Sinai, to the top of the mountain, and he summoned Moses to the top. So Moses went up.
21 naye Bwana akamwambia Mose, “Shuka ukawaonye watu ili wasijipenyeze kutafuta kumwona Bwana na wengi wao wakafa.
Yahweh said to Moses, “Go down and warn the people not to break through to me to look, or many of them will perish.
22 Hata makuhani, watakaomkaribia Bwana ni lazima wajiweke wakfu, la sivyo Bwana atawaadhibu.”
Let the priests also who come near to me set themselves apart—prepare themselves for my coming—so that I do not attack them.”
23 Mose akamwambia Bwana, “Watu hawawezi kupanda mlima Sinai kwa sababu wewe mwenyewe ulituonya ukisema, ‘Wekeni mipaka kuuzunguka mlima na kuutenga kama patakatifu.’”
Moses said to Yahweh, “The people cannot come up to Mount Sinai, for you commanded us: 'Set boundaries around the mountain and set it apart to Yahweh.'”
24 Bwana akajibu, “Shuka ukamlete Aroni pamoja nawe. Lakini makuhani pamoja na watu wasije wakalazimisha kuja kwa Bwana, nisije nikawaadhibu.”
Yahweh said to him, “Go, get down the mountain, and bring up Aaron with you, but do not let the priests and the people break through the barrier to come up to me, or I will attack them.”
25 Basi Mose akashuka kwa watu na kuwaambia lile aliloambiwa.
So Moses went down to the people and spoke to them.

< Kutoka 19 >