< Kutoka 19 >
1 Mnamo mwezi wa tatu baada ya Waisraeli kuondoka Misri, siku kama iyo hiyo, wakafika katika Jangwa la Sinai.
In the third month, after the children of Israel were gone forth out of the land of Egypt, the same day they came into the wilderness of Sinai.
2 Baada ya kuondoka Refidimu, waliingia katika Jangwa la Sinai na Israeli wakapiga kambi pale jangwani mbele ya mlima.
For they had departed from Rephidim, and they came to the desert of Sinai, and encamped in the wilderness; and Israel encamped there opposite the mount.
3 Kisha Mose akakwea kwenda kwa Mungu, naye Bwana akamwita kutoka kwenye ule mlima akasema, “Hivi ndivyo utakavyosema na nyumba ya Yakobo na utakachowaambia watu wa Israeli:
And Moses went up unto God, and the Lord called unto him from the mount, saying, Thus shalt thou say to the house of Jacob, and tell the children of Israel.
4 ‘Ninyi wenyewe mmeona nililofanya huko Misri, jinsi nilivyowabeba kwenye mbawa za tai na kuwaleta kwangu.
Ye have yourselves seen what I have done unto the Egyptians, and how I bore you on eagles' wings, and brought you unto myself.
5 Sasa kama mkinitii kikamilifu na kutunza Agano langu, basi ninyi mtakuwa mali yangu ya thamani kubwa miongoni mwa mataifa yote. Ijapokuwa dunia yote ni mali yangu,
Now therefore, if you will truly obey my voice, and keep my covenant, then shall ye be unto me a peculiar treasure above all nations; for all the earth is mine:
6 ninyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’ Haya ndiyo maneno utakayosema kwa wana wa Israeli.”
And ye shall be unto me a kingdom of priests, and a holy nation; these are the words which thou shalt speak unto the children of Israel.
7 Kwa hiyo Mose akarudi, akawaita wazee wa watu na kuwaambia maneno yote ambayo Bwana alikuwa amemwamuru ayaseme.
And Moses came and called for the elders of the people, and laid before them all these words which the Lord had commanded him.
8 Watu wote wakajibu kwa pamoja, “Tutafanya kila kitu Bwana alichokisema.” Naye Mose akarudisha majibu yao kwa Bwana.
And all the people answered unanimously, and said, all that the Lord hath spoken will we do; and Moses returned the words of the people unto the Lord.
9 Bwana akamwambia Mose, “Nitakujia katika wingu zito, ili watu wanisikie nikinena nawe na kila mara waweke tumaini lao kwako.” Kisha Mose akamwambia Bwana yale ambayo watu walikuwa wamesema.
And the Lord said unto Moses, Behold, I will come unto thee in a thick cloud, for the sake that the people may hear when I speak with thee, and that also in thee they shall believe for ever; and Moses told the words of the people unto the Lord.
10 Naye Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa watu ukawaweke wakfu leo na kesho. Waambie wafue nguo zao
And the Lord said unto Moses, Go unto the people, and sanctify them today and tomorrow, and let them wash their clothes.
11 na wawe tayari siku ya tatu, kwa sababu siku hiyo, Bwana atashuka juu ya mlima Sinai machoni pa watu wote.
And they shall be ready against the third day; for on the third day will the Lord come down, before the eyes of all the people, upon mount Sinai.
12 Weka mipaka kuzunguka mlima kwa ajili ya watu, uwaambie, ‘Mwe waangalifu, msije mkapanda mlimani au kuugusa. Yeyote atakayeugusa mlima hakika atauawa.
And thou shalt set bounds unto the people, round about, saying, Take heed to yourselves, that ye go not up into the mount, nor touch the border of it; whosoever toucheth the mount shall surely be put to death.
13 Hakika atapigwa mawe au kupigwa mishale; mkono wa mtu hautamgusa. Akiwa mwanadamu au mnyama, hataruhusiwa kuishi.’ Ila tu wakati baragumu itakapopigwa kwa mfululizo, ndipo watu wote watakapopanda mlimani.”
Yet not a hand shall touch him, but he shall surely be stoned, or shot through; whether it be beast or man, it shall not live; when the trumpet soundeth long, they may come up to the mount.
14 Baada ya Mose kushuka kutoka mlimani akawaendea watu na kuwaweka wakfu, wakafua nguo zao.
And Moses went down from the mount unto the people, and sanctified the people: and they washed their clothes.
15 Kisha akawaambia watu, “Jitayarisheni kwa ajili ya siku ya tatu. Mwanaume yeyote asimkaribie mwanamke.”
And he said unto the people, Be ready against the third day; approach not unto a woman.
16 Asubuhi ya siku ya tatu kulikuwa na ngurumo na radi pamoja na wingu nene juu ya mlima na mlio mkubwa sana wa tarumbeta. Kila mmoja aliyekuwa kambini akatetemeka.
And it came to pass on the third day when it was morning, that there were thunders and lightnings, and a heavy cloud was upon the mount, and the voice of the cornet was exceedingly loud; so that all the people that were in the camp trembled.
17 Kisha Mose akawaongoza watu kutoka kambini kukutana na Mungu, nao wakasimama chini ya mlima.
And Moses brought forth the people out of the camp to meet with God; and they placed themselves at the foot of the mount.
18 Mlima Sinai ulikuwa umefunikwa na moshi, kwa sababu Bwana alishuka juu yake katika moto. Moshi wa moto huo ulipanda juu kama moshi kutoka kwenye tanuru kubwa na mlima wote ukatetemeka kwa nguvu nyingi,
And mount Sinai smoked in every part, because the Lord had descended upon it in fire; and the smoke thereof ascended as the smoke of a furnace, and the whole mount quaked greatly.
19 nayo sauti ya tarumbeta ikawa kubwa zaidi na zaidi. Kisha Mose akazungumza na sauti ya Bwana ikamjibu.
And the voice of the cornet went on, and waxed louder and louder; Moses spoke, and God answered him with a loud voice.
20 Bwana akashuka juu ya Mlima Sinai na akamwita Mose apande juu mlimani. Kwa hiyo Mose akapanda juu,
And the Lord came down upon mount Sinai, on the top of the mount; and the Lord called Moses up to the top of the mount, and Moses went up.
21 naye Bwana akamwambia Mose, “Shuka ukawaonye watu ili wasijipenyeze kutafuta kumwona Bwana na wengi wao wakafa.
And the Lord said unto Moses, Go down, charge the people, lest they break through unto the Lord to gaze, and many of them might perish.
22 Hata makuhani, watakaomkaribia Bwana ni lazima wajiweke wakfu, la sivyo Bwana atawaadhibu.”
And the priests also, who come near to the Lord, shall sanctify themselves; lest the Lord break forth among them.
23 Mose akamwambia Bwana, “Watu hawawezi kupanda mlima Sinai kwa sababu wewe mwenyewe ulituonya ukisema, ‘Wekeni mipaka kuuzunguka mlima na kuutenga kama patakatifu.’”
And Moses said unto the Lord, The people cannot come up to mount Sinai; for thou hast charged us, saying, Set bounds about the mount and sanctify it.
24 Bwana akajibu, “Shuka ukamlete Aroni pamoja nawe. Lakini makuhani pamoja na watu wasije wakalazimisha kuja kwa Bwana, nisije nikawaadhibu.”
And the Lord said unto him, Go, get thee down, and then shalt thou come up, thou, and Aaron with thee; but the priests and the people shall not break through to come up unto the Lord, lest he break forth among them.
25 Basi Mose akashuka kwa watu na kuwaambia lile aliloambiwa.
So Moses went down unto the people, and spoke unto them.