< Kutoka 18 >
1 Basi Yethro, kuhani wa Midiani, baba mkwe wa Mose, akawa amesikia kila kitu Mungu alichomfanyia Mose na watu wake wa Israeli, pia jinsi Bwana alivyowatoa Israeli Misri.
Musa'nın kayınbabası Midyanlı Kâhin Yitro, Tanrı'nın Musa ve halkı İsrail için yaptığı her şeyi, RAB'bin İsrailliler'i Mısır'dan nasıl çıkardığını duydu.
2 Baada ya Mose kumrudisha mkewe Sipora, Yethro baba mkwe wake alimpokea
Musa'nın kendisine göndermiş olduğu karısı Sippora'yı ve iki oğlunu yanına aldı. Musa, “Garibim bu yabancı diyarda” diyerek oğullarından birine Gerşom adını vermişti.
3 pamoja na wanawe wawili. Jina la mmoja aliitwa Gershomu, kwa kuwa Mose alisema, “Nimekuwa mgeni katika nchi ya kigeni.”
4 Mwingine aliitwa Eliezeri, kwa kuwa alisema, “Mungu wa baba yangu alikuwa msaada wangu, akaniokoa kutoka upanga wa Farao.”
Sonra, “Babamın Tanrısı bana yardım etti, beni firavunun kılıcından esirgedi” diyerek öbürüne de Eliezer adını koymuştu.
5 Yethro, baba mkwe wa Mose, pamoja na wana wawili wa Mose na mkewe, wakamjia Mose huko jangwani, mahali alipokuwa amepiga kambi karibu na mlima wa Mungu.
Yitro Musa'nın karısı ve oğullarıyla birlikte Tanrı Dağı'na, Musa'nın konakladığı çöle geldi.
6 Yethro alikuwa ametuma ujumbe kwake Mose, kusema, “Mimi Yethro baba mkwe wako ninakuja kwako pamoja na mke wako na wanao wawili.”
Musa'ya şu haberi gönderdi: “Ben, kayınbaban Yitro, karın ve iki oğlunla birlikte sana geliyoruz.”
7 Kwa hiyo Mose akatoka kumlaki baba mkwe wake, akainama na kumbusu. Wakasalimiana, kisha wakaingia hemani.
Musa kayınbabasını karşılamaya çıktı, önünde eğilip onu öptü. Birbirinin hatırını sorup çadıra girdiler.
8 Mose akamwambia baba mkwe wake kuhusu kila kitu Bwana alichomfanyia Farao na Wamisri kwa ajili ya Israeli, na pia kuhusu shida zote walizokutana nazo njiani na jinsi Bwana alivyowaokoa.
Musa İsrailliler uğruna RAB'bin firavunla Mısırlılar'a bütün yaptıklarını, yolda çektikleri sıkıntıları, RAB'bin kendilerini nasıl kurtardığını kayınbabasına bir bir anlattı.
9 Yethro akafurahishwa sana kusikia juu ya mambo yote mazuri Bwana aliyowatendea Waisraeli kuwaokoa kutoka mkono wa Wamisri.
Yitro RAB'bin İsrailliler'e yaptığı iyiliklere, onları Mısırlılar'ın elinden kurtardığına sevindi.
10 Yethro akasema, “Sifa na ziwe kwa Bwana, aliyekuokoa wewe kutoka mikononi mwa Wamisri na Farao, na aliyewaokoa watu kutoka mikononi mwa Wamisri.
“Sizi Mısırlılar'ın ve firavunun elinden kurtaran RAB'be övgüler olsun” dedi, “Halkı Mısır'ın boyunduruğundan O kurtardı.
11 Sasa najua ya kuwa Bwana ni mkuu kuliko miungu mingine yote, kwa kuwa amewatendea hivi wale waliowatenda Israeli kwa ujeuri.”
Artık biliyorum ki, RAB bütün ilahlardan büyüktür. Çünkü onların gurur duyduğu şeylerin üstesinden geldi.”
12 Kisha Yethro, baba mkwe wa Mose, akaleta sadaka ya kuteketezwa na dhabihu nyingine kwa Mungu, naye Aroni pamoja na wazee wote wa Israeli wakaja kula chakula pamoja na baba mkwe wa Mose mbele za Mungu.
Sonra Tanrı'ya yakmalık sunu ve kurbanlar getirdi. Harun'la bütün İsrail ileri gelenleri, Musa'nın kayınbabasıyla Tanrı'nın huzurunda yemek yemeye geldiler.
13 Siku iliyofuata, Mose akachukua nafasi yake kama hakimu wa watu, nao wakasimama kumzunguka kuanzia asubuhi hadi jioni.
Ertesi gün Musa halkın davalarına bakmak için yargı kürsüsüne çıktı. Halk sabahtan akşama kadar çevresinde ayakta durdu.
14 Baba mkwe wake alipoona yote Mose anayowafanyia watu, akasema, “Ni nini hiki unachowafanyia watu? Kwa nini wewe unakuwa mwamuzi wa watu hawa peke yako, wakati watu hawa wamesimama wakikuzunguka tangu asubuhi mpaka jioni?”
Kayınbabası Musa'nın halk için yaptıklarını görünce, “Nedir bu, halka yaptığın?” dedi, “Neden sen tek başına yargıç olarak oturuyorsun da herkes sabahtan akşama kadar çevrende bekliyor?”
15 Mose akamjibu, “Kwa sababu watu wananijia kutaka mapenzi ya Mungu.
Musa, “Çünkü halk Tanrı'nın istemini bilmek için bana geliyor” diye yanıtladı,
16 Kila wakiwa na shauri huletwa kwangu, nami huamua kati ya mtu na mwenzake na kuwajulisha juu ya amri na sheria za Mungu.”
“Ne zaman bir sorunları olsa, bana gelirler. Ben de taraflar arasında karar veririm; Tanrı'nın kurallarını, yasalarını onlara bildiririm.”
17 Baba mkwe wa Mose akamjibu, “Unachofanya sio kizuri.
Kayınbabası, “Yaptığın iş iyi değil” dedi,
18 Wewe pamoja na watu hawa wanaokujia mtajichosha bure. Kazi ni nzito sana kwako, huwezi kuibeba mwenyewe.
“Hem sen, hem de yanındaki halk tükeneceksiniz. Bu işi tek başına kaldıramazsın. Sana ağır gelir.
19 Sasa nisikilize mimi, nitakupa shauri, naye Mungu na awe pamoja nawe. Yapasa wewe uwe mwakilishi wa watu mbele za Mungu na ulete mashauri yao kwake.
Beni dinle, sana öğüt vereyim. Tanrı seninle olsun. Tanrı'nın önünde halkı sen temsil etmeli, sorunlarını Tanrı'ya sen iletmelisin.
20 Uwafundishe amri na sheria, tena uwaonyeshe namna ya kuishi na kazi zinazowapasa wao kufanya.
Kuralları, yasaları halka öğret, izlemeleri gereken yolu, yapacakları işi göster.
21 Lakini uchague watu wenye uwezo miongoni mwa watu wote, watu wanaomwogopa Mungu, watu waaminifu wanaochukia mali ya dhuluma, uwateuwe wawe maafisa juu ya maelfu, mamia, hamsini na makumi.
Bunun yanısıra halkın arasından Tanrı'dan korkan, yetenekli, haksız kazançtan nefret eden dürüst adamlar seç; onları biner, yüzer, ellişer, onar kişilik toplulukların başına önder ata.
22 Waweke wawe waamuzi wa watu kwa wakati wote, lakini waambie wakuletee kila shauri lililo gumu; yale yaliyo rahisi wayaamue wao wenyewe. Hii itafanya mzigo wako kuwa mwepesi, kwa sababu watashirikiana nawe.
Halka sürekli onlar yargıçlık etsin. Büyük davaları sana getirsinler, küçük davaları kendileri çözsünler. Böylece işini paylaşmış olurlar. Yükün hafifler.
23 Kama ukifanya hivi, na ikiwa Mungu ameagiza hivyo, utaweza kushinda uchovu, nao watu hawa wote watarudi nyumbani wameridhika.”
Eğer böyle yaparsan, Tanrı da buyurursa, dayanabilirsin. Herkes esenlik içinde evine döner.”
24 Mose akamsikiliza baba mkwe wake na kufanya kila kitu alichosema.
Musa kayınbabasının sözünü dinledi. Söylediği her şeyi yerine getirdi.
25 Mose akawachagua watu wenye uwezo kutoka Israeli yote, akawafanya kuwa viongozi wa watu, maafisa juu ya maelfu, mamia, hamsini na makumi.
İsrailliler arasından yetenekli adamlar seçti. Onları biner, yüzer, ellişer, onar kişilik toplulukların başına önder atadı.
26 Wakatumika kama waamuzi wa watu kwa wakati wote. Mashauri magumu wakayaleta kwa Mose, lakini yale yaliyo rahisi wakayaamua wenyewe.
Halka sürekli yargıçlık eden bu kişiler zor davaları Musa'ya getirdiler, küçük davaları ise kendileri çözdüler.
27 Kisha Mose akaagana na Yethro baba mkwe wake, naye akarudi kwa nchi yake.
Sonra Musa kayınbabasını uğurladı. Yitro da ülkesine döndü.