< Kutoka 18 >

1 Basi Yethro, kuhani wa Midiani, baba mkwe wa Mose, akawa amesikia kila kitu Mungu alichomfanyia Mose na watu wake wa Israeli, pia jinsi Bwana alivyowatoa Israeli Misri.
And whanne Jetro, the prest of Madian, `the alye of Moises, hadde herd alle thingis which God hadde do to Moises, and to Israel his puple, for the Lord hadde led Israel out of the lond of Egipt,
2 Baada ya Mose kumrudisha mkewe Sipora, Yethro baba mkwe wake alimpokea
he took Sefora, `the wijf of Moises, whom he hadde sent ayen,
3 pamoja na wanawe wawili. Jina la mmoja aliitwa Gershomu, kwa kuwa Mose alisema, “Nimekuwa mgeni katika nchi ya kigeni.”
and hise twei sones, of which oon was clepid Gersan, for the fadir seide, Y was a comelyng in alien lond,
4 Mwingine aliitwa Eliezeri, kwa kuwa alisema, “Mungu wa baba yangu alikuwa msaada wangu, akaniokoa kutoka upanga wa Farao.”
forsothe the tother was clepid Eliezer, for Moises seide, God of my fadir is myn helpere, and he delyuerede me fro the swerd of Farao.
5 Yethro, baba mkwe wa Mose, pamoja na wana wawili wa Mose na mkewe, wakamjia Mose huko jangwani, mahali alipokuwa amepiga kambi karibu na mlima wa Mungu.
Therfor Jetro, `alie of Moises, cam, and the sones of Moises and his wijf camen to Moises, in to deseert, where Jetro settide tentis bisidis the hil of God;
6 Yethro alikuwa ametuma ujumbe kwake Mose, kusema, “Mimi Yethro baba mkwe wako ninakuja kwako pamoja na mke wako na wanao wawili.”
and sente to Moises, and seide, Y Jetro, thin alie, come to thee, and thi wijf, and thi twei sones with hir.
7 Kwa hiyo Mose akatoka kumlaki baba mkwe wake, akainama na kumbusu. Wakasalimiana, kisha wakaingia hemani.
And Moises yede out into the comyng of his alie, and worschipide, and kiste hym, and thei gretten hem silf to gidere with pesible wordis.
8 Mose akamwambia baba mkwe wake kuhusu kila kitu Bwana alichomfanyia Farao na Wamisri kwa ajili ya Israeli, na pia kuhusu shida zote walizokutana nazo njiani na jinsi Bwana alivyowaokoa.
And whanne he hadde entrid in to the tabernacle, Moises tolde to `his alie alle thingis whiche God hadde do to Farao, and to Egipcians, for Israel, and he tolde al the trauel which bifelle to hem in the weie, of which the Lord delyuerede hem.
9 Yethro akafurahishwa sana kusikia juu ya mambo yote mazuri Bwana aliyowatendea Waisraeli kuwaokoa kutoka mkono wa Wamisri.
And Jetro was glad on alle the goodis whiche the Lord hadde do to Israel, for he delyuerede Israel fro the hond of Egipcians.
10 Yethro akasema, “Sifa na ziwe kwa Bwana, aliyekuokoa wewe kutoka mikononi mwa Wamisri na Farao, na aliyewaokoa watu kutoka mikononi mwa Wamisri.
And Jetro seide, Blessid be `the Lord, that delyuerede you fro the hond of Egipcians, and fro `the hond of Farao, which Lord delyuered his puple fro the hond of Egipt;
11 Sasa najua ya kuwa Bwana ni mkuu kuliko miungu mingine yote, kwa kuwa amewatendea hivi wale waliowatenda Israeli kwa ujeuri.”
now Y knowe that the Lord is greet aboue alle goddis, for `thei diden proudli ayens hem.
12 Kisha Yethro, baba mkwe wa Mose, akaleta sadaka ya kuteketezwa na dhabihu nyingine kwa Mungu, naye Aroni pamoja na wazee wote wa Israeli wakaja kula chakula pamoja na baba mkwe wa Mose mbele za Mungu.
Therfor Jetro, `alie of Moises, offride brent sacrifices and offryngis to God; and Aaron, and alle the eldere men of Israel, camen to ete breed with hym bifore God.
13 Siku iliyofuata, Mose akachukua nafasi yake kama hakimu wa watu, nao wakasimama kumzunguka kuanzia asubuhi hadi jioni.
Forsothe in the tother dai Moises sat that he schulde deme the puple, that stood niy Moises, fro the morewtid til to euentid.
14 Baba mkwe wake alipoona yote Mose anayowafanyia watu, akasema, “Ni nini hiki unachowafanyia watu? Kwa nini wewe unakuwa mwamuzi wa watu hawa peke yako, wakati watu hawa wamesimama wakikuzunguka tangu asubuhi mpaka jioni?”
And whanne `his alie hadde seyn this, that is, alle thingis `whiche he dide in the puple, he seide, What is this that thou doist in the puple? whi sittist thou aloone, and al the puple abidith fro the morewtid til to euentid?
15 Mose akamjibu, “Kwa sababu watu wananijia kutaka mapenzi ya Mungu.
To whom Moises answeride, The puple cometh to me, and axith the sentence of God;
16 Kila wakiwa na shauri huletwa kwangu, nami huamua kati ya mtu na mwenzake na kuwajulisha juu ya amri na sheria za Mungu.”
and whanne ony strijf bifallith to hem, thei comen to me, that Y deme bitwixe hem, and schewe `the comaundementis of God, and hise lawis.
17 Baba mkwe wa Mose akamjibu, “Unachofanya sio kizuri.
And Jetro seide, Thou doist a thing not good,
18 Wewe pamoja na watu hawa wanaokujia mtajichosha bure. Kazi ni nzito sana kwako, huwezi kuibeba mwenyewe.
thou art wastid with a fonned trauel, bothe thou and this puple which is with thee; the werk is a boue thi strengthis, thou aloone maist not suffre it.
19 Sasa nisikilize mimi, nitakupa shauri, naye Mungu na awe pamoja nawe. Yapasa wewe uwe mwakilishi wa watu mbele za Mungu na ulete mashauri yao kwake.
But here thou my wordis and counseils, and the Lord schal be with thee; be thou to the puple in these thingis that perteynen to God, that thou telle the thingis that ben seid to the puple;
20 Uwafundishe amri na sheria, tena uwaonyeshe namna ya kuishi na kazi zinazowapasa wao kufanya.
and schewe to the puple the cerymonyes, and custom of worschipyng, and the weie bi which `thei owen to go, and the werk which `thei owen to do.
21 Lakini uchague watu wenye uwezo miongoni mwa watu wote, watu wanaomwogopa Mungu, watu waaminifu wanaochukia mali ya dhuluma, uwateuwe wawe maafisa juu ya maelfu, mamia, hamsini na makumi.
Forsothe puruey thou of al the puple myyti men, and dredynge God, in whiche is treuthe, and whiche haten auarice; and ordeyne thou of hem tribunes, and centuriouns, and quinquagenaries, and deenys,
22 Waweke wawe waamuzi wa watu kwa wakati wote, lakini waambie wakuletee kila shauri lililo gumu; yale yaliyo rahisi wayaamue wao wenyewe. Hii itafanya mzigo wako kuwa mwepesi, kwa sababu watashirikiana nawe.
whiche schulen deme the puple in al tyme; sotheli what ever thing is grettere, telle thei to thee, and deme thei ooneli lesse thingis, and be it esiere to thee, whanne the burthun is departid in to othere men.
23 Kama ukifanya hivi, na ikiwa Mungu ameagiza hivyo, utaweza kushinda uchovu, nao watu hawa wote watarudi nyumbani wameridhika.”
If thou schalt do this, thou schalt fille the comaundement of God, and thou schalt mowe bere hise comaundementis; and al this puple schal turne ayen with pees to her places.
24 Mose akamsikiliza baba mkwe wake na kufanya kila kitu alichosema.
And whanne these thingis weren herd, Moises dide alle thingis whiche Jetro counselide.
25 Mose akawachagua watu wenye uwezo kutoka Israeli yote, akawafanya kuwa viongozi wa watu, maafisa juu ya maelfu, mamia, hamsini na makumi.
And whanne noble men of al Israel weren chosun Moises ordeynede hem princis of the puple, tribunes, and centuriouns, and quinquagenaries, and denes,
26 Wakatumika kama waamuzi wa watu kwa wakati wote. Mashauri magumu wakayaleta kwa Mose, lakini yale yaliyo rahisi wakayaamua wenyewe.
whiche demeden the puple in al tyme; forsothe, whateuer thing was hardere, thei telden to Moises, and thei demeden esiere thingis oneli.
27 Kisha Mose akaagana na Yethro baba mkwe wake, naye akarudi kwa nchi yake.
And Moises lefte `his alie, which turnede ayen, and yede in to his lond.

< Kutoka 18 >