< Kutoka 18 >

1 Basi Yethro, kuhani wa Midiani, baba mkwe wa Mose, akawa amesikia kila kitu Mungu alichomfanyia Mose na watu wake wa Israeli, pia jinsi Bwana alivyowatoa Israeli Misri.
When Jethro the priest of Midian, Moses's father-in-law, heard of all that God had done for Moses, and for Israel his people, [and] that the LORD had brought Israel out of Egypt:
2 Baada ya Mose kumrudisha mkewe Sipora, Yethro baba mkwe wake alimpokea
Then Jethro, Moses's father-in-law, took Zipporah Moses's wife, after he had sent her back,
3 pamoja na wanawe wawili. Jina la mmoja aliitwa Gershomu, kwa kuwa Mose alisema, “Nimekuwa mgeni katika nchi ya kigeni.”
And her two sons; of which the name of the one [was] Gershom; (for he said, I have been an alien in a strange land: )
4 Mwingine aliitwa Eliezeri, kwa kuwa alisema, “Mungu wa baba yangu alikuwa msaada wangu, akaniokoa kutoka upanga wa Farao.”
And the name of the other [was] Eliezer; (for the God of my father, [said he], [was] my help, and delivered me from the sword of Pharaoh: )
5 Yethro, baba mkwe wa Mose, pamoja na wana wawili wa Mose na mkewe, wakamjia Mose huko jangwani, mahali alipokuwa amepiga kambi karibu na mlima wa Mungu.
And Jethro, Moses's father-in-law, came with his sons and his wife to Moses into the wilderness, where he encamped at the mount of God:
6 Yethro alikuwa ametuma ujumbe kwake Mose, kusema, “Mimi Yethro baba mkwe wako ninakuja kwako pamoja na mke wako na wanao wawili.”
And he said to Moses, I thy father-in-law Jethro have come to thee, and thy wife, and her two sons with her.
7 Kwa hiyo Mose akatoka kumlaki baba mkwe wake, akainama na kumbusu. Wakasalimiana, kisha wakaingia hemani.
And Moses went out to meet his father-in-law, and did obeisance, and kissed him: and they asked each other of [their] welfare: and they came into the tent.
8 Mose akamwambia baba mkwe wake kuhusu kila kitu Bwana alichomfanyia Farao na Wamisri kwa ajili ya Israeli, na pia kuhusu shida zote walizokutana nazo njiani na jinsi Bwana alivyowaokoa.
And Moses told his father-in-law all that the LORD had done to Pharaoh, and to the Egyptians for Israel's sake, [and] all the travail that had come upon them by the way, and [how] the LORD delivered them.
9 Yethro akafurahishwa sana kusikia juu ya mambo yote mazuri Bwana aliyowatendea Waisraeli kuwaokoa kutoka mkono wa Wamisri.
And Jethro rejoiced for all the goodness which the LORD had done to Israel, whom he had delivered out of the hand of the Egyptians.
10 Yethro akasema, “Sifa na ziwe kwa Bwana, aliyekuokoa wewe kutoka mikononi mwa Wamisri na Farao, na aliyewaokoa watu kutoka mikononi mwa Wamisri.
And Jethro said, Blessed [be] the LORD, who hath delivered you out of the hand of the Egyptians, and out of the hand of Pharaoh, who hath delivered the people from under the hand of the Egyptians.
11 Sasa najua ya kuwa Bwana ni mkuu kuliko miungu mingine yote, kwa kuwa amewatendea hivi wale waliowatenda Israeli kwa ujeuri.”
Now I know that the LORD [is] greater than all gods: for in the thing in which they dealt proudly, [he was] above them.
12 Kisha Yethro, baba mkwe wa Mose, akaleta sadaka ya kuteketezwa na dhabihu nyingine kwa Mungu, naye Aroni pamoja na wazee wote wa Israeli wakaja kula chakula pamoja na baba mkwe wa Mose mbele za Mungu.
And Jethro, Moses's father-in-law, took a burnt-offering and sacrifices for God: and Aaron came, and all the elders of Israel to eat bread with Moses's father-in-law before God.
13 Siku iliyofuata, Mose akachukua nafasi yake kama hakimu wa watu, nao wakasimama kumzunguka kuanzia asubuhi hadi jioni.
And it came to pass on the morrow, that Moses sat to judge the people: and the people stood by Moses from the morning to the evening.
14 Baba mkwe wake alipoona yote Mose anayowafanyia watu, akasema, “Ni nini hiki unachowafanyia watu? Kwa nini wewe unakuwa mwamuzi wa watu hawa peke yako, wakati watu hawa wamesimama wakikuzunguka tangu asubuhi mpaka jioni?”
And when Moses's father-in-law saw all that he did to the people, he said, What [is] this thing that thou doest to the people? Why sittest thou thyself alone, and all the people stand by thee from morning to evening?
15 Mose akamjibu, “Kwa sababu watu wananijia kutaka mapenzi ya Mungu.
And Moses said to his father-in-law, Because the people come to me to inquire of God:
16 Kila wakiwa na shauri huletwa kwangu, nami huamua kati ya mtu na mwenzake na kuwajulisha juu ya amri na sheria za Mungu.”
When they have a matter, they come to me, and I judge between one and another, and I make [them] know the statutes of God, and his laws.
17 Baba mkwe wa Mose akamjibu, “Unachofanya sio kizuri.
And Moses's father-in-law said to him, The thing that thou doest [is] not good.
18 Wewe pamoja na watu hawa wanaokujia mtajichosha bure. Kazi ni nzito sana kwako, huwezi kuibeba mwenyewe.
Thou wilt surely wear away, both thou, and this people that [is] with thee: for this thing [is] too heavy for thee; thou art not able to perform it thyself alone.
19 Sasa nisikilize mimi, nitakupa shauri, naye Mungu na awe pamoja nawe. Yapasa wewe uwe mwakilishi wa watu mbele za Mungu na ulete mashauri yao kwake.
Hearken now to my voice, I will give thee counsel, and God shall be with thee: Be thou for the people toward God, that thou mayest bring the causes to God:
20 Uwafundishe amri na sheria, tena uwaonyeshe namna ya kuishi na kazi zinazowapasa wao kufanya.
And thou shalt teach them ordinances and laws, and shalt show them the way in which they must walk, and the work that they must do.
21 Lakini uchague watu wenye uwezo miongoni mwa watu wote, watu wanaomwogopa Mungu, watu waaminifu wanaochukia mali ya dhuluma, uwateuwe wawe maafisa juu ya maelfu, mamia, hamsini na makumi.
Moreover, thou shalt provide out of all the people, able men, such as fear God, men of truth, hating covetousness; and place [such] over them [to be] rulers of thousands, [and] rulers of hundreds, rulers of fifties, and rulers of tens:
22 Waweke wawe waamuzi wa watu kwa wakati wote, lakini waambie wakuletee kila shauri lililo gumu; yale yaliyo rahisi wayaamue wao wenyewe. Hii itafanya mzigo wako kuwa mwepesi, kwa sababu watashirikiana nawe.
And let them judge the people at all seasons: and it shall be, [that] every great matter they shall bring to thee, but every small matter they shall judge: So shall it be easier for thyself, and they shall bear [the burden] with thee.
23 Kama ukifanya hivi, na ikiwa Mungu ameagiza hivyo, utaweza kushinda uchovu, nao watu hawa wote watarudi nyumbani wameridhika.”
If thou shalt do this thing, and God command thee [so], then thou shalt be able to endure, and all this people shall also go to their place in peace.
24 Mose akamsikiliza baba mkwe wake na kufanya kila kitu alichosema.
So Moses hearkened to the voice of his father-in-law, and did all that he had said.
25 Mose akawachagua watu wenye uwezo kutoka Israeli yote, akawafanya kuwa viongozi wa watu, maafisa juu ya maelfu, mamia, hamsini na makumi.
And Moses chose able men out of all Israel, and made them heads over the people, rulers of thousands, rulers of hundreds, rulers of fifties, and rulers of tens.
26 Wakatumika kama waamuzi wa watu kwa wakati wote. Mashauri magumu wakayaleta kwa Mose, lakini yale yaliyo rahisi wakayaamua wenyewe.
And they judged the people at all seasons: the hard causes they brought to Moses, but every small matter they judged themselves.
27 Kisha Mose akaagana na Yethro baba mkwe wake, naye akarudi kwa nchi yake.
And Moses let his father-in-law depart; and he went his way into his own land.

< Kutoka 18 >